#COVID19 Hongera Rais Samia kwa maamuzi yako kwenye Corona

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,047
Amani iwe nawe Mama yetu!

Kwa mfululizo nimekuwa nikiandika mada mbalimbali za kukushauri juu ya mustakabali wa uchumi wetu sisi Tanzania kama nchi.

Leo badala ya kukushauri, napenda sana kukupongeza kwa hatua ulizochukua dhidi ya Corona.

Moja ya sifa kuu za kiongozi mzuri ni kuwa anatakiwa awe mtu anayejali uhai wa watu wake na maisha yao kwa ujumla! Anatakiwa kuwa mtu anayetizama kuokoa kwanza uhai wa watu wake huku akizingatia kwa kiwango cha juu.

Kwa wana JF ambao hamjui, kwa sasa, Corona ndo imebeba hoja za uchumi wa dunia. Corona kama ilivyobeba hoja za uchumi wa dunia, kwa sasa ndo imekuwa muelekeo wa dunia kiuchumi. Anayefanya masikhara na Corona uchumi wa dunia unamuacha kweli. Anayecheza na Corona uchumi wa Dunia unamchezea kweli.

Corona pia imetikisa familia nyingi tu hapa Tanzania. Mimi pia ni mmoja ya watu ambao tumetikiswa baada ya ndugu zangu 3 kuugua Corona na ndugu zangu 2 kufariki kwa corona.

Kiuchumi pia Corona imetikisa Tanzania Kwa sababu watu wengi wanepoteza ajira hasa kwenye kampuni za utalii na pia kwenye sekta zilizokuwa zinategemea kufanya biashara na Ulaya na pamoja na America yakiwemo makampuni mbalimbali.

Hatua alizochukua Mama Samia huku zikitangazwa na Media kubwa Duniani kama BBC na CNN zina faida kubwa sana kwa Tanzania kiuchumi na siku si nyingi hali ya ugonjwa huu inapoenda kutulia au kudhibitiwa kwa hatua alizochukua Mama Samia zinaenda kuirudisha kwa kiwango kikubwa sana Tanzania kwenye uchumi wa dunia Yaani utalii na Biashara za kimataifa.

Hatua hizi pia zina faida Kwa kuwaondoa watanzania wengi waliokuwa kwenye hatari ya kuangamizwa na huu ugonjwa hasa wenye magonjwa yasioambukizwa kama kisukari kuwa salama Kwa sababu endapo watapata chanjo watakuwa salama na kuendelea na shughuli za uzalishaji.

Kwa nini nasema haya?
1. Dunia saivi imeanza kujadili jinsi ya watu kuruhusiwa kutembea nje ya nchi zao wakiwa na uthibitisho wa kupokea chanjo. Hili litafanya nchi kuwahimiza raia wao kutembelea maeneo ambayo wanajua hayana threat za corona ikiwemo maeneo ambayo wana chanjo. Hivyo sekta yetu kuu tunayoitegemea katika kutupatia fedha za kigeni haitoweza kurudi kwenye haki yake na nchi kuendelea kufaidika endapo tungeendelea kushupaza shingo na kudai kuwa hatutaki chanjo.

2. Tunakoelekea hata biashara baina ya nchi na nchi zitafanyika kwa kuzingatia protocols ambazo dunia inaenda kuziweka kutokana na Corona. Hivyo tukiwa nyuma, ni kweli tutakuwa nyuma kweli! Dunia itatuacha na Tanzania tutakufa kibudu.

Napenda kukupongeza Mama Samia kwa hatua ulizichukua za kuipa thamani sayansi huku tukimtanguliza Mungu mbele. Napenda kukupongeza pia kwa kufanya maamuzi ya akili na sio tu magumu kwa mustakabali wa usalama na maendeleo ya Tanzania na watanzania kiafya na kiuchumi.
 
Kwani nchi ilipoingia uchumi wa kati Corona haikuwepo?

Mpotosheni tu mama watu watakapoanza kwisha mpate ajenda ya kumsulubisha.

Kwani hizo chanjo ni wapi zimezuia vifo au kupunguza?

Ni punguwani anaye amini chanjo ndo muarobaini wa corona.

Unafikiri wazungu wehu wamechanjwa na wamejifungia, wana vaa mask nk, leo nywele ngumu ameshiba makande anakenua meno,eti amefanya la maana. Visa vitakapo ongezeka kutokana na vipimo feki na kuambiwa aifunge miji mikubwa na miskiti na makanisa kufungwa,na shule hamtaongelea huo uchumi mtamgeuka.

Sasa anaye shauri vizuri mnawaita kila majina.

Swala ndege lilivyopotoshwa mliunga mkono kweli,wazalendo wakasimama imara sasa kimia,mmegeukia corona ambayo sasa haipo nchini,huku mkiomba mungu wenu alete wimbi la 3.

Hakika yupo Mungu aliyeiponya nchi atapambana,maana hamtaki hata kumtaja kana kwamba hamkuwepo tulipofunga na kuomba,ndo maana daladala zimejaa watu hawana hata barakoa wako salama.
 
Kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake bila kuvunja sheria.Hata hivyo kwa swala la C-19,ambalo ni swala la kitaaluma,anayetoa mawazo anapaswa kuwa na weledi muafaka. Kwa sababu hiyo, ili mimi binafsi niweze kuchukulia maoni na ushauri wako maanani,ningeomba vitu vifuatavyo:-

1. CV yako kama hutajali.
2. Maamuzi ambayo unadhani Rais, ameyafanya kwa kuzingatia sayansi,hekima na busara.

Mwisho, naomba nikufahamishe na niku-taharadhishe kwamba siku hizi wapo Wanasayansi ambao ni wachumia tumbo.Hawa maisha ya watu sio muhimu sana, jambo la msingi kwao ni matumbo yao. Tunawaita kwa lugha nyingine "compromised scientists," na wako wengi sana.
 
Kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake bila kuvunja sheria.Hata hivyo kwa swala la C-19,ambalo ni swala la kitaaluma,anayetoa mawazo anapaswa kuwa na weledi muafaka. Kwa sababu hiyo, ili mimi binafsi niweze kuchukulia maoni na ushauri wako maanani,ningeomba vitu vifuatavyo:-

1. CV yako kama hutajali.
2. Maamuzi ambayo unadhani Rais, ameyafanya kwa kuzingatia sayansi,hekima na busara.

Mwisho, naomba nikufahamishe na niku-taharadhishe kwamba siku hizi wapo Wanasayansi ambao ni wachumia tumbo.Hawa maisha ya watu sio muhimu sana, jambo la msingi kwao ni matumbo yao. Tunawaita kwa lugha nyingine "compromised scientists," na wako wengi sana.
CV yangu itakusaidia nini? Kwani kuwa na cv Kuna husiana nini na mawazo yangu. Wewe huoni corona ilivyoathili uchumi wa dunia?? Au hili hadi uone cv ya mtu ndo utaamini
 
Cha msingi maamuzi yake yasiguse kwa wananchi wa chini mibarakoa na mi social distance waishie nayo huko huko ikulu
Ikishuka huku chini uchumi utaporomoka kwa spidi ya 5G kwa mfano social distance ikitumika tu daladala watapata hasara ya kufa mtu na usafiri utakuwa mgumu wa kupindukia sababu daladala tu zilizopo kwa sasa hazitoshelezi mahitaji.

Magufuli aliliona hilo.Kwa wa juu yaweza onekana kama ni maamuzi sahihi lakini yakishuka chini hali itakuwa mbaya mno hizo hatua zao waishie nazo huko huko juu kwao kwa sababu viongozi wengi wakubwa huwa na magonjwa nyemelezi kibao peressure zao,visukari vyao nk magonjwa ya uswahilini makubwa ni kipindupindu, kifua kikuu na degedege ambayo Corona haiwawindi hao wa uswahilini inawinda hao wenye BP zao, kisukari nk ndio maana Corona Uswahilini haipo.
 
Cv yangu itakusaidia nini?? Kwani kuwa na cv Kuna husiana nini na mawazo yangu. Wewe huoni corona ilivyoathili uchumi wa dunia?? Au hili hadi uone cv ya mtu ndo utaamini
CV yako inanisaidia ku-ascertain kama una weledi wa kutosha wa kuweza kutoa mawazo kuhusu Corona mkuu, kwa kuwa hili ni swala la kitaalamu zaidi. Nadhani hili kiko wazi sana.
 
Back
Top Bottom