Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,592
- 29,721
Nampongeza kwa dhati Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kuiweka Tanzania upya kwenye ramani ya nchi zinazosimamia na kulinda Utu.
Tangu ameingia madarakani siku 109 zilizopita amekuwa akikemea kwa wazi matendo ya aibu yanayofanywa na mamlaka za nchi hususani polisi na ofisi ya DPP bila kuwasahau TRA na TAKUKURU kwa kuwaasa kuacha kubambikiza watu kesi na kuondoa mahakamani kesi zote zilizoundwa kwa kigezo cha kisiasa na kiuonevu.
Masheikh wa Uamsho ambao walisota ndani tangu enzi za Kikwete wamefutiwa kesi kwani inaonekana walishtakiwa kama kutolewa kafara kwa matukio ya kipuuzi yaliyotokea Zanzibar.
Mtaani kwetu kuna wananchi wawili ambao walikuwa mahabusu dhidi ya kesi za uhujumu uchumi nao wametoka na kufutiwa kesi zao za kubumba.
Leo tunaona Mahakama ikimfutia mashtaka Mdude Nyagali kesi ya kubambika ya madawa ya kulevya na utakatishaji.
Naamini mengi mazuri yanakuja na Watanzania tuungane kujenga nchi yetu.
Pia nikiwa kama MwanaCCM ndakindaki ninawaomba radhi wote niliowahi kuwakwaza humu kupitia hoja na misimamo yangu kisiasa.
Nimegundua kwamba, chama changu cha CCM kiliamua kuunda propaganda za kutusadikisha waumini wake kwamba kipo mstari sahihi.
Naunga mkono mashtaka dhidi ya yule DC wa Hai na ikiwezekana kwa wengine iwe funzo kwa viongozi wengine kuheshimu dhamana walizopewa.
Tuungane kumpongeza mama Samia Suluhu Hassan
Tangu ameingia madarakani siku 109 zilizopita amekuwa akikemea kwa wazi matendo ya aibu yanayofanywa na mamlaka za nchi hususani polisi na ofisi ya DPP bila kuwasahau TRA na TAKUKURU kwa kuwaasa kuacha kubambikiza watu kesi na kuondoa mahakamani kesi zote zilizoundwa kwa kigezo cha kisiasa na kiuonevu.
Masheikh wa Uamsho ambao walisota ndani tangu enzi za Kikwete wamefutiwa kesi kwani inaonekana walishtakiwa kama kutolewa kafara kwa matukio ya kipuuzi yaliyotokea Zanzibar.
Mtaani kwetu kuna wananchi wawili ambao walikuwa mahabusu dhidi ya kesi za uhujumu uchumi nao wametoka na kufutiwa kesi zao za kubumba.
Leo tunaona Mahakama ikimfutia mashtaka Mdude Nyagali kesi ya kubambika ya madawa ya kulevya na utakatishaji.
Naamini mengi mazuri yanakuja na Watanzania tuungane kujenga nchi yetu.
Pia nikiwa kama MwanaCCM ndakindaki ninawaomba radhi wote niliowahi kuwakwaza humu kupitia hoja na misimamo yangu kisiasa.
Nimegundua kwamba, chama changu cha CCM kiliamua kuunda propaganda za kutusadikisha waumini wake kwamba kipo mstari sahihi.
Naunga mkono mashtaka dhidi ya yule DC wa Hai na ikiwezekana kwa wengine iwe funzo kwa viongozi wengine kuheshimu dhamana walizopewa.
Tuungane kumpongeza mama Samia Suluhu Hassan