Hongera Rais Samia kwa kufuata nyayo za mtangulizi wako japo gharama yake ni kubwa kwa taifa

N

Hivi uimara wa kiongozi wa Tanzania ni kukandamiza uhuru wa raia kujumuika, uhuru wa mawazo, haki za kiraia, haki za binadamu, kuendekeza ubaguzi na kutumia dola kufanikisha hayo yote? Huu ni ujima mtupu.
Hakuna alipokandamizwa raia katika kujumuika au kutoa mawazo yake. Na wala hakuna haki za kiraia na haki za binadamu zilizovunjwa na kiongozi yeyote wa Tanzania. Hayo mawazo siyo yenu, mmekuwa brainswashed kutumia vimisamiati vya kibeberu hivyo ili kupenyeza ajenda zao ambazo kwa bahati mbaya zimekuwa zenu.

Na ajenda za kibeberu zinajulikana. Wanataka nchi na watu wetu wafuate model yao ya kimaisha ili iwe rahisi kwao kufanya wanachokitaka bila upinzani wowote. Na wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupitia programmes nyingi, walizowekeza fedha nyingi, za muda mrefu, za kuformat namna ya kufikiria kwa watu wetu.

Sisi tunamtaka kiongozi wa Tanzania afanye mambo haya yafuatayo, akusanye kodi, asimamie pesa yetu vizuri iisipotee hata senti kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu na watu wake, ahakikishe usalama wa nchi na watu wake, alinde na kuisimamia amani ya nchi yetu.

Akifanikiwa hayo who cares about vimisamiati vya kibeberu. Frankly speaking ni lini hivi nimekatazwa kutoa mawazo yangu?

Kuhusu kukamatwa Mbowe na lile genge lake, kwanza anatumiwa ujumbe kwamba who is the boss katika nchi hii. Mama ndiye boss kwa sasa akisema no ni no, akisema yes ni yes. Hata mimi hapa nikiwaambia walio chini yangu kwamba hiki hapana wananisikiliza, seuze Rais wa nchi. Kwa kauli ya Rais hakuna cha haki zya kufanya unachojisikia, and there is a good reason kwa nini imewekwa hivyo.
 
Leo vyombo mbalimbali vya kimataifa vimetoa uzito wa hali ya juu kutekwa kwa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na kukamatwa na wasaidizi wake.

DW - Chadema yawaamuru wafuasi wake kumsaka Mbowe

Aljazeera - Tanzania’s Chadema party says leader Freeman Mbowe arrested

BBC - Chadema kwenda mahakamani kesho iwapo Freeman Mbowe hataachiliwa

VoA - Tanzania's Main Opposition Leader Freeman Mbowe Arrested

Africannews - Tanzanian opposition party says leader Freeman Mbowe, 10 others arrested | Africanews

AFP - Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Freeman Mbowe akamatwa

Si mara ya kwanza kwa viongozi wa upinzani, na hasa CHADEMA kutendewa unyama na Serikali ya CCM. Lakini matukio hayo mengi hayakupewa coverage kubwa kama hili tukio, ukiondoa lile la Tundu Lisu kushambuliwa kwa risasi 38, na 16 zikiingia mwilini mwake.

Wengi wanajiuliza, ni kwa nini?

Vyombo hivi vimetoa uzito wa hali ya juu, hasa kwa nia ya kuonesha undumilakuwili wa Rais Samia. Maana ni hivi karibuni, yeye mwenyewe kwa kauli yake, aliihakikishia jamii ya kimataifa kuwa ataheshimu misingi ya demokradia, utawala unaoheshima sheria na haki za raia. Hata kabla ya mwezi kupita, tunashuhudia matukio ya kidikteta yasiyoheshimu katiba, sheria na mikataba ya kimataifa ya kuheshimu haki za watu.

Mashaka yale ambayo Jumuia ya Kimataifa ilikuwa nayo juu ya utawala wa Serikali ya CCM, chini ya Rais Samia, sasa yanapata majawabu yasiyo na shaka.

Mtangulizi wake alikuwa na bahati. Aliingia madarakani wakati Jumuiya ya kimataifa ikiamini Tanzania inafuata misingi ya kidemokrasia kwa kiasi fulani. Taratibu, watawala wakaanza kuipa mashaka jamii ya kimataifa, na baadaye Jamii ya kimataifa ikatambua kuwa Tanzania inaongozwa kwa misingi ya kidikteta, na walichukua hatua kadhaa ikiwemo kutoa kauli kali dhidi ya utawala uliokuwepo, kupunguza na kufuta misaada mingi ambayo Tanzania ilikuwa ikiipokea.

Rais Samia, amechukua uongozi, nchi ikiwa katika udikteta, na jamii ya kimataifa ikimwangalia kwa ukaribu kama ana dhamira ya kubadilisha utawala wa nchi kutoka kwenye udikteta na kuifanya nchi iongozwe kwa ustaarabu wa Dunia. Naye akachombeza kuwa amedhamiria kufuata misingi ya haki na demokrasia. Kabla ya due diligence kukamilika, matukio ya kuthibitisha kuwa anachotamka na anachotenda ni tofauti, yanaendelea kutokea.

Gharama za kubadilika na kuwathibitishia wanadamu wastaarabu, hata wamwakini, zitakuwa kubwa zaidi sasa kuliko hapoalipoingia. CHADEMA walichofanya ni kuithibitishia Dunia kuwa Rais Samia, anaihadaa.

Kuongoza nchi kunahitaji upeo mkubwa na mpana, lakini pia inastahili kuzungukwa na wasaidizi wanaoweza kuiona kesho kabla ya kufika kesho, sio ambao uwezo wao wa kuona mambo unaishia mita moja.
Dunia ipo bize na korona. Unajua kinachotokea Palestina? Unaona anachofanya Abiy Ethiopia? Siasa za kimataifa ni mchezo wa kimaslahi. Magufuli alifanya aliyofanya kwa miaka mitano mfululizo, na international media ikafanya coveage ya kutosha tu. What happened?
 
Sisi hatumtegemei mtu wala nini. Tunachoangalia ni misingi tu. Tulimtahadharisha mapema mama kwamba hii nchi haina ubia na taifa au mataifa mengine, itajengwa kwa mikono yetu wenyewe tu. Watakaotaka kutusaidia watusaidie kwa nia safi sio kwa ajili ya ajenda zao. Vinginevyo mama atapata tabu sana kuiongoza hii nchi maana wale wanaotaka awe dhaifu ni vibaraka, sisi tunaotaka awe na nguvu na kufanikiwa ndio tunaomtaka aangalie maslahi ya nchi kwanza na asicheke na kima yeyote mwenye vipaumbele vingine zaidi ya maendeleo ya nchi yetu.

Wanaotaka katiba mpya watwambie kipengele gani kwenye katiba ya sasa kinakwamisha maendeleo ya nchi na watu wake. Baba wa Taifa alituambiwa mwenyewe kuwa katiba yetu ilikuwa inampa nafasi ya kutosha kuwa dikteta.
Baba wa Taifa mwenyewe alituhakishia kuwa katiba yetu ilikuwa inamwezesha kuwa dikteta! Pamoja na hayo hakuwa dikteta kwa sababu mbali na kuwa na elimu nzuri pia alikuwa na karama kubwa ya uongozi. Waliomfuata nao walikuwa na elimu nzuri, karama ya kutosha ya uongozi na pia kwa sababu walifanya kazi na Baba wa Taifa waliendelea kutumia fikra zake katika uongozi. Awamu ya tano tulipopata kiongozi asiyekuwa na karama ya uongozi asiyejua historia ya nchi hii kisiasa na asiyejua maana ya dhamana ya uongozi wa kisiasa, ndipo udhaifu wa katiba yetu ulipodhihirika kwa kila mwenye macho. Nchi nzima pamoja na Hazina ya taifa ikawa mali ya kiongozi! Vipaumbele vyake binafsi vikawa ndiyo mipango ya taifa. Rasimali za taifa zikaelekezwa kama alivyotaka yeye mwenyewe badala ya kuzingatia mpango mkakati wa kitaifa. Nchi ikawa kama iliyopata uhuru jana! Vipaumbele vyake binafsi ni pamoja na kutoa upendeleo usioelezeka kwa kijiji chake! Mbali na hayo, sera za uchumi, uwekezaji, siasa, nk zilivurugika sana na kuathiri kasi ya ukuaji wa uchumi. Kwa mfano uwekezaji kutoka nje ulipungua kwa 50% na mauzo nje ya nchi yaliporomoka. Yote haya yaliwezekana kwa sababu ya katiba ya nchi inayompa kiongozi mkuu mamlaka yasiyo na mipaka. Kiongozi huyo kama anao upungufu wake kiafya, kielimu, kiuzoefu, kimaadili, kiuongozi, kisiasa, nk bila shaka yoyote madhara yatakayotokea yatakuwa yamesababishwa na hiyo katiba. Hayo yalitokea hapa kwetu miaka mitano iliyopita. Tulirudi nyuma kiuchumi kwa sababu ya kuongozwa na akili ya mtu mmoja badala ya taasisi na katiba.
 
Baba wa Taifa mwenyewe alituhakishia kuwa katiba yetu ilikuwa inamwezesha kuwa dikteta! Pamoja na hayo hakuwa dikteta kwa sababu mbali na kuwa na elimu nzuri pia alikuwa na karama kubwa ya uongozi. Waliomfuata nao walikuwa na elimu nzuri, karama ya kutosha ya uongozi na pia kwa sababu walifanya kazi na Baba wa Taifa waliendelea kutumia fikra zake katika uongozi. Awamu ya tano tulipopata kiongozi asiyekuwa na karama ya uongozi asiyejua historia ya nchi hii kisiasa na asiyejua maana ya dhamana ya uongozi wa kisiasa, ndipo udhaifu wa katiba yetu ulipodhihirika kwa kila mwenye macho. Nchi nzima pamoja na Hazina ya taifa ikawa mali ya kiongozi! Vipaumbele vyake binafsi vikawa ndiyo mipango ya taifa. Rasimali za taifa zikaelekezwa kama alivyotaka yeye mwenyewe badala ya kuzingatia mpango mkakati wa kitaifa. Nchi ikawa kama iliyopata uhuru jana! Vipaumbele vyake binafsi ni pamoja na kutoa upendeleo usioelezeka kwa kijiji chake! Mbali na hayo sera za uchumi, uwekezaji, siasa, nk zilivurugika sana na kuathiri kasi ya ukuaji wa uchumi. Yote haya yaliwezekana kwa sababu ya katiba ya nchi inayompa kiongozi mkuu mamlaka yasiyo na mipaka. Kiongozi huyo kama anao upungufu wake kiafya, kielimu, kiuzofu, kimaadili, kiuongozi, kisiasa, nk bila shaka yoyote madhara yatakayotokea yatakuwa yamesababishwa na hiyo katiba.
Yote hayo unayoyasema kuhusu kiongozi wa awamu ya tano kuna baadhi yetu tunayaona ni chuki dhidi yake isiyo na maana. Kiongozi wa awamu ya tano hakuenda Ikulu kula bata na kuimba kumbaya. Alienda kufanya kazi kwa mujibu wa nguvu na uwezo ailiopewa na katiba. Nguvu hiyo ilimpa uwezo wa kubadilisha maono yake makubwa kwa nchi yetu kuwa halisi. Kama alikuuumiza kwa namna moja au nyingine wakati akitekeleza majukumu yake, pole. Hata mimi ashawahi kuniumiza.

Unamtaka Rais ambaye atacheka na kima eti asionekane mbaya?
Unamtaka Rais atakeyeenda Ikulu na kila siku awe kiguu na njia kwenda Ulaya kutembeza bakuli?
Unamtaka Rais atakayesema kila kitu ruksa?

Baba mwenyewe wa taifa alipewa nguvu na katiba na alikuwa na nguvu kweli kweli. Kama ambavyo baadhi yenu hamkumpenda JPM ndivyo hata baadhi ya wale walioishi enzi za baba wa taifa hawakumpenda na walimwona dikteta. Usitake kupendwa na kila mtu, We fanya lile lililo sahihi.
 
Back
Top Bottom