Hongera Rais Samia kwa kufuata nyayo za mtangulizi wako japo gharama yake ni kubwa kwa taifa

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,489
40,999
Leo vyombo mbalimbali vya kimataifa vimetoa uzito wa hali ya juu kutekwa kwa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na kukamatwa na wasaidizi wake.

DW - Chadema yawaamuru wafuasi wake kumsaka Mbowe

Aljazeera - Tanzania’s Chadema party says leader Freeman Mbowe arrested

BBC - Chadema kwenda mahakamani kesho iwapo Freeman Mbowe hataachiliwa

VoA - Tanzania's Main Opposition Leader Freeman Mbowe Arrested

Africannews - Tanzanian opposition party says leader Freeman Mbowe, 10 others arrested | Africanews

AFP - Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Freeman Mbowe akamatwa

Si mara ya kwanza kwa viongozi wa upinzani, na hasa CHADEMA kutendewa unyama na Serikali ya CCM. Lakini matukio hayo mengi hayakupewa coverage kubwa kama hili tukio, ukiondoa lile la Tundu Lisu kushambuliwa kwa risasi 38, na 16 zikiingia mwilini mwake.

Wengi wanajiuliza, ni kwa nini?

Vyombo hivi vimetoa uzito wa hali ya juu, hasa kwa nia ya kuonesha undumilakuwili wa Rais Samia. Maana ni hivi karibuni, yeye mwenyewe kwa kauli yake, aliihakikishia jamii ya kimataifa kuwa ataheshimu misingi ya demokradia, utawala unaoheshima sheria na haki za raia. Hata kabla ya mwezi kupita, tunashuhudia matukio ya kidikteta yasiyoheshimu katiba, sheria na mikataba ya kimataifa ya kuheshimu haki za watu.

Mashaka yale ambayo Jumuia ya Kimataifa ilikuwa nayo juu ya utawala wa Serikali ya CCM, chini ya Rais Samia, sasa yanapata majawabu yasiyo na shaka.

Mtangulizi wake alikuwa na bahati. Aliingia madarakani wakati Jumuiya ya kimataifa ikiamini Tanzania inafuata misingi ya kidemokrasia kwa kiasi fulani. Taratibu, watawala wakaanza kuipa mashaka jamii ya kimataifa, na baadaye Jamii ya kimataifa ikatambua kuwa Tanzania inaongozwa kwa misingi ya kidikteta, na walichukua hatua kadhaa ikiwemo kutoa kauli kali dhidi ya utawala uliokuwepo, kupunguza na kufuta misaada mingi ambayo Tanzania ilikuwa ikiipokea.

Rais Samia, amechukua uongozi, nchi ikiwa katika udikteta, na jamii ya kimataifa ikimwangalia kwa ukaribu kama ana dhamira ya kubadilisha utawala wa nchi kutoka kwenye udikteta na kuifanya nchi iongozwe kwa ustaarabu wa Dunia. Naye akachombeza kuwa amedhamiria kufuata misingi ya haki na demokrasia. Kabla ya due diligence kukamilika, matukio ya kuthibitisha kuwa anachotamka na anachotenda ni tofauti, yanaendelea kutokea.

Gharama za kubadilika na kuwathibitishia wanadamu wastaarabu, hata wamwakini, zitakuwa kubwa zaidi sasa kuliko hapoalipoingia. CHADEMA walichofanya ni kuithibitishia Dunia kuwa Rais Samia, anaihadaa.

Kuongoza nchi kunahitaji upeo mkubwa na mpana, lakini pia inastahili kuzungukwa na wasaidizi wanaoweza kuiona kesho kabla ya kufika kesho, sio ambao uwezo wao wa kuona mambo unaishia mita moja.
 
Most likely wahafidhina ndani ya CCM walimuingiza chaka kumshauri aache kuwa kiongozi bali ageuke kuwa mtawala.

Mwanzo alifanya kazi nzuri yenye kuonyesha kuwa anaweza kuwa kiongozi mzuri, ila sasa na yeye ameanza kuvunja haki za wananchi zilizoko kikatiba.

Matokeo ndiyo haya anaanza kuwa dikteta kwa kasi ya airbus
 
Vyombo hivi vimetoa uzito wa hali ya juu, hasa kwa nia ya kuonesha undumilakuwili wa Rais Samia. Maana ni hivi karibuni, yeye mwenyewe kwa kauli yake, aliihakikishia jamii ya kimataifa kuwa ataheshimu misingi ya demokradia, utawala unaoheshima sheria na haki za raia. Hata kabla ya mwezi kupita, tunashuhudia matukio ya kidikteta yasiyoheshimu katiba, sheria na mikataba ya kimataifa ya kuheshimu haki za watu.
Inaelekea sasa kuwa wazi kwamba Samia hajui anachofanya; anauza tu maneno matamu bila ya kuwa na uelewa wa nini kinatakiwa kufanywa ili hayo anayoyasema yaonekane kuwa ya kweli.

Mama hawezi kazi. Matukio mengi yanaonyesha kwamba mama hana chembechembe za uongozi.
 
Hivyo vyombo vya kimataifa havijawahi report mema ya Samia hata siku mojamoja

Huyo mbowe yupo salama kabisa ila urais kwake ndio wasahau
 
Hivyo vyombo vya kimataifa havijawahi report mema ya Samia hata siku mojamoja

Huyo mbowe yupo salama kabisa ila urais kwake ndio wasahau
Toa hoja kama mwenye ukamilifu wa fikra.

Ni lini Mbowe alisema anautaka Urais? Mbowe aligombea Urais mara moja, mara nyingine zote hajawahi kugombea. Ataupataje Urais wakati hagombei?

Unasema vyombo vya kimataifa havijawahi report mema ya Samia. Ulitaka waripoti nini? Hivi wewe hapo ukitoka ukatembea uchi wa mnyama barabarani, vyombo vya habari vikaripoti hicho kituko chako, jibu lako litakuwa, mbona hamkuripoti siku nilipovaa gauni zuri?

Kukosekana kwa uongozi thabiti toka kwa Samia, ni hasara kwake binafsi, lakini ni hasara zaidi kwa Taifa.
 
Toa hoja kama mwenye ukamilifu wa fikra.

Ni lini Mbowe alisema anautaka Urais? Mbowe aligombea Urais mara moja, mara nyingine zote hajawahi kugombea. Ataupataje Urais wakati hagombei?

Unasema vyombo vya kimataifa havijawahi report mema ya Samia. Ulitaka waripoti nini? Hivi wewe hapo ukitoka ukatembea uchi wa mnyama barabarani, vyombo vya habari vikaripoti hicho kituko chako, jibu lako litakuwa, mbona hamkuripoti siku nilipovaa gauni zuri?

Kukosekana kwa uongozi thabiti toka kwa Samia, ni hasara kwake binafsi, lakini ni hasara zaidi kwa Taifa.

Mbowe ni mwenyekiti wa chadema anakiwakilisha chama chake
Samia ni mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT

Ukiwa unatafuta tuu uone mabaya ya mtu hata mazuri hutayaona
 
Back
Top Bottom