Hongera Rais Magufuli kwa kusema unachoamini, 2020 uwe hivyohivyo

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,794
71,211
Watu wamekusifu kuwa kule Bukoba umesema bila kuremba na kile unachokiamini. Hii ni style yako kila mahali, hukwepeshi kabisa. Hutajenga nyumba za waathirika hata kwa wale wasio na uwezo kabisa kwani sio kazi ya serikali (kwani sio Building contractor). Hupeleki chakula mahali penye njaa kama mvua ilinyesha na hawakulima, kwani serikali haina shamba.

Sio Bukoba tuu, bali kila mahali ulipo pata nafasi ya kuzungumza umeyazungumza hayo na kuwa kila mtu afanye kazi ili kujiletea maendeleo na kuwa msema kweli mpenzi wa Mungu. Safi sana.

Natumaini kuwa Chama chako kitakupendekeza (hata kama hakitakutaka) kugombea 2020 nafasi hiyo tena, tunakuomba wakati wa kampeni uwe hivyohivyo msema kweli mpenzi wa Mungu. Waambie hutatoa chakula kwenye njaa, au tetemeko,kimbunga na mafuriko yakitokea watajijua kwani hayo hayaletwi na CCM.

Usiseme tena kama kule Tabora kuwa wanafunzi wakipata sifa ya kuingia chuo wakikosa mikopo Bodi nzima haina kazi, bali uwaeleze wazazi kuwa kama mwanao hajafaulu daraja 1&2 tena sayansi utamlipia mwenyewe kama huwezi "wafwa". Ndio ni mtindo wa kusema Ukweli ili kuwa mpenzi wa Mungu.

Wananchi wameonyesha kukupenda sana kama tulivyo ona kule Bukoba jana, kwanini lakini? Ni kwa sababu unasimamia ukweli, na msema kweli mpenzi wa Mungu.

2015 Lubuva alikupa 52% ya ushindi kama sikosei, lakini baada ya kujua ukweli ulivyo na kwa vile Utawaambia ukweli Watanzania wakati wa kampeni 2020 basi nahakika hata bila "Lubava" lazima utazoa zaidi ya 95%
 
Nahisi kukuelewa ulicho maanisha lakini naamini hujamuelewa mtoa mada vyema hebu soma tena kwaumakin na tafakari kubwa uelewe ujumbe wake ulipo.
Actually, hii iko simply put kwa mtu yeyote anayefikirisha ubongo wake kidogo tu. Huyo aliyetoa comment ya ukuu wa wilaya sijui alikuwa anafikiria nini hadi akashindwa kuelewa alichomaanisha Chakaza
 
Tatizo hatuna Culture ya kuambiwa ukweli na Kuishi katika kweli
Si ndio maana tunampongeza mkuu kwa kuanzisha hiyo culture! Kwamba sasa 2020 ataendeleza huu ukweli, haya yaliyotokea Misenyi kuhusu chakula atayasema kila mahali, ya kule Bukoba na Shinyanga atakuwa wazi zaidi wakati wa kampeni na hata ya mikopo kwa vila..za nayo atawatwanga kuliko ule uongo wa Tabora.
Tunamsubiri msema kweli mpenzi wa Mungu atakapo kuja kusema kweli yake tena.
 
Actually, hii iko simply put kwa mtu yeyote anayefikirisha ubongo wake kidogo tu. Huyo aliyetoa comment ya ukuu wa wilaya sijui alikuwa anafikiria nini hadi akashindwa kuelewa alichomaanisha Chakaza
Mkuu wanapo sema watanzania wengi wana upeo mdogo sana wa mawazo ujue watu wamesha fanya utafiti mkuu wangu na hili linajidhihirisha kabisa kama mtu anashindwa kuelewa aya ndogo tu hiyo
 
Si ndio maana tunampongeza mkuu kwa kuanzisha hiyo culture! Kwamba sasa 2020 ataendeleza huu ukweli, haya yaliyotokea Misenyi kuhusu chakula atayasema kila mahali, ya kule Bukoba na Shinyanga atakuwa wazi zaidi wakati wa kampeni na hata ya mikopo kwa vila..za nayo atawatwanga kuliko ule uongo wa Tabora.
Tunamsubiri msema kweli mpenzi wa Mungu atakapo kuja kusema kweli yake tena.
Thubutu!

Mungu nipe uzima na afya niishuhudie kampeni ya kwanza yenye ukweli Tanzania
 
Si ndio maana tunampongeza mkuu kwa kuanzisha hiyo culture! Kwamba sasa 2020 ataendeleza huu ukweli, haya yaliyotokea Misenyi kuhusu chakula atayasema kila mahali, ya kule Bukoba na Shinyanga atakuwa wazi zaidi wakati wa kampeni na hata ya mikopo kwa vila..za nayo atawatwanga kuliko ule uongo wa Tabora.
Tunamsubiri msema kweli mpenzi wa Mungu atakapo kuja kusema kweli yake tena.[/QUO
Yapaswa tujue majukumu yetu ni yapi na ya serkali ni yapi, watu wakigundua wako responsible na maisha yao wataacha kutupia lawama wengine
 
Mtoa mada unamkebehi mtukufu.basi.sawaa...

Ila.2020 ukawa wakimweka tena lowasa

Napiga tiki kwa HASHIMU RUNGWE sijawai.jilaumu.kwa kura yangu
 
Mtoa mada unamkebehi mtukufu.basi.sawaa...

Ila.2020 ukawa wakimweka tena lowasa

Napiga tiki kwa HASHIMU RUNGWE sijawai.jilaumu.kwa kura yangu
Achana na habari ya Lowassa utaharibu thread, kwa nini hutampa tena msema ukweli mpenzi wa Mungu atakapo kuambia ukipata majanga sio swala lake? Au kama utapata ukame ukangoja chakula cha msaada wafwa! Kwani yeye serikali yake ina shamba? Yenyewe ina ndege, reli na barabara tuu. Au hupendi ukweli?
 
Watu wamekusifu kuwa kule Bukoba umesema bila kuremba na kile unachokiamini. Hii ni style yako kila mahali, hukwepeshi kabisa. Hutajenga nyumba za waathirika hata kwa wale wasio na uwezo kabisa kwani sio kazi ya serikali (kwani sio Building contractor). Hupeleki chakula mahali penye njaa kama mvua ilinyesha na hawakulima, kwani serikali haina shamba.

Sio Bukoba tuu, bali kila mahali ulipo pata nafasi ya kuzungumza umeyazungumza hayo na kuwa kila mtu afanye kazi ili kujiletea maendeleo na kuwa msema kweli mpenzi wa Mungu. Safi sana.

Natumaini kuwa Chama chako kitakupendekeza (hata kama hakitakutaka) kugombea 2020 nafasi hiyo tena, tunakuomba wakati wa kampeni uwe hivyohivyo msema kweli mpenzi wa Mungu. Waambie hutatoa chakula kwenye njaa, au tetemeko,kimbunga na mafuriko yakitokea watajijua kwani hayo hayaletwi na CCM.

Usiseme tena kama kule Tabora kuwa wanafunzi wakipata sifa ya kuingia chuo wakikosa mikopo Bodi nzima haina kazi, bali uwaeleze wazazi kuwa kama mwanao hajafaulu daraja 1&2 tena sayansi utamlipia mwenyewe kama huwezi "wafwa". Ndio ni mtindo wa kusema Ukweli ili kuwa mpenzi wa Mungu.

Wananchi wameonyesha kukupenda sana kama tulivyo ona kule Bukoba jana, kwanini lakini? Ni kwa sababu unasimamia ukweli, na msema kweli mpenzi wa Mungu.

2015 Lubuva alikupa 52% ya ushindi kama sikosei, lakini baada ya kujua ukweli ulivyo na kwa vile Utawaambia ukweli Watanzania wakati wa kampeni 2020 basi nahakika hata bila "Lubava" lazima utazoa zaidi ya 95%
mbona wamachinga hakuwaambia ukweli mkuu? nadhani huwa anajichanganya.
 
Labda hukua makini na kauli zake ila hata 2015 alisema alichokiamini!
 
2020 akirudi Tabora tunataka awaambie wale Wanyamwezi "Mikopo ya wanafunzi ni fadhila ya serikali, kama watoto wenu ni vila.za na hawasomi Chemistry na kupata div 1&2 shauri yenu kama mnadhani kuna cha mkopo mwafwa"
Si wanafunzi wote waliosoma sayansi na wakapata 1 & 2 wamepewa mikopo.....
Mi ninao mfano kijana kasoma PCM kaondoka na 2 hakupewa hata chapa kisa o'level kasoma kashule ka kulipia 800,000 kwa mwaka.
Binti kasoma PCB na kaondoka na 1 kapigwa chini sababu o'level baba yake alijichanga kasoma shule hiyohiyo ya 800,000 kwa mwaka. Na shule hiyo inaitwa Simba wa Yuda iko Magu mkoani Mwanza.
Nampenda rais wangu maana anatuambia ukweli kuwa serikali haiwezi kuwalipia wanafunzi wote. Ni sawa kabisa na 2020 lazima apate kura yangu japo sikumpigia kipindi kilichopita, Kwa ukweli huu,kura yangu anayo tuombe tu uzima.
 
Back
Top Bottom