Hongera Rais Magufuli kwa kupambana na Covid 19 na hongera Watanzania wenzagu

naxon

JF-Expert Member
Dec 6, 2014
367
199
Hodi jukwaani.
Hongera zangu kijana mtiifu wa CHADEMA kwa Mh. JPM na kwa sisi watanzania kwa ujumla.

Utanguli:
Awali ya yote, mimi ni kijana mtiifu wa chama kikuu cha upinzani Chadema na aghalabu nimekulia na bado ninaishi katika chama hiki kikuu cha upinzani.

Kwanini nipo huku; niliamua kujiunga na chama hiki takribani miaka kumi iliyopita, kwa sababu ya hoja na ajenda nzito zinazobebwa na Viongozi makini na wanachama kwa ujumla. Mungu ibariki Chadema.

Pia nilijiunga na JF takribani miaka 7 iliyopita hususani jukwaa hili la siasa na kwa wakati wote huo nimekuwa mtu wa kusoma nyuzi za watu na angalau marachache kuchangia kidogo tu au nisichangie kabisa. Lengo kubwa ilikuwa ni kujifunza na kuupata uzoefu kuhusu mijadala mbalimbali katika jukwaa hili. Leo nimeamua kutoa nyuzi hii kwa mara ya kwanza aghalabu hata Mungu atanichukua kilicho chake punde tu namaliza nukta ya mwisho na kuisubmit basi nisiondoke na huku nafsi inawashwa.

Basi baada ya kautangulizi kangu hako kenye njaa(kasikojitosheleza) naomba kujikita kwenye mada:

Pongezi zangu kwa Mh. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kupambana na Covid 19.
------------------------------------------
N:B pamoja na mambo mengine mengi yaliyofanywa na wewe hasa yanayohusu maendeleo, mada hii inahusu Covid19 pekee. MadaItajikita Katika mambo mawili tu (Imani na saikolojia)
Ndugu wanabodi nawasilimu na poleni na majukumu ya ujenzi wa taifa. Naweza nisiwe na maneno/uandishi mzuri kama manguli wa uandishi walipo humu hii ni kutoka na kutokuwa na uzoefu kwa kada ya uandishi(uvumilivu ni jambo jema pia).

Binafsi nakupongeza sana sana Rais wa Tanzania kwa msimamo wako kiimani na kisaikoljia.

Kwa mujibu wa baadhi ya maandiko ya kiimani(sitanukuu vifungu) kikristo yanasema" imani ni kuwa na hakika juu yale yatarajiwayo" na mengine yanasema "Hata ungalikuwa na imani ndogo hata kama chembe ya mbegu ya mti wa haradani, nawe ungaliuamuru mlima huu ng'oka ukajitose baharini nao ungali tii" (Naamini pia kwa upande wa Waislamu kunavifungu vizuri zaidi kuweza kutupa nguv zaidi).

Nikili wazi Covid19 imekuwa ni mlima mkubwa duniani huku ukichukua maefu ya maisha ya watu, na millions of people wakiwa wameembukizwa virusi hivi. Kama ilivyotabia ya janga lolote lile ni kuleta athari hasi, hili limevuruga uchumi wa kidunia, umepoteza ndugu, rafiki na jamaa duniani. Umeharibu taratibu zote za kiutawala na diplomasia za kidunia hasa kwa mataifa makubwa na tajiri, umewafanya kunyosheana vidole.

Kwa upande wa nchini ugonjwa huu ulileta taharuki na sintofahamu kubwa hata kabla ya kuingia nchini. Ukweli ni kwamba ulipoingia tu nchini HOFU KUU ilitamalaki hakuna kilichoweza kushikika/kufanyika bila kuiwazia Corona, kama kwamba hakuna ambacho kingeendelea. Tukitizama taarifa za vifo Italia, china, Irani, Hispania, USA na kwingineko basi mambo yalikuwa yanazidi kuwa mabaya zaidi. Ijapokuwa Wizara husika ilikuwa inaendelea kupambana kuokoa Maisha ya Watanzania (Mungu akubariki Ummy Mwalimu).
Ashukuliwe Mungu Tar. 10/April/2020 ukishiriki ibada uliongea na sisi watanzania ukitutaka kuondoa hofu na kuendelea kuchukua tahadhari juu ya hili.

Awali nilikuelewa mifano uliyoitoa kuhusu mazingira yanavyoweza kuufanya ugonjwa ukawa na athari ndogo au kubwa na kutolea mfano wa ugonjwa wa Malaria kwa kuwa na athari kubwa barani Afrika kuliko Ulaya ambako kuna baridi zaidi. Ukweli ulituasa kumtanguliza Mungu na kuondoa hofu. Kwa hili haukueleweka sana kutokana na kwamba ugonjwa huu ulizidi kuene na kuzua taharuki kiasi. Lakini ikafika kipindi kulikuwa na tahaluki kubwa tena ilijitokeza kiasi shughuli nyingi kusimama/kudolola hasa maeneo ya mijini. (Maduka, usafiri, ofisi, n. k). Hapa ilibaki kidogo

Pamoja na hali hii kukatokea sintofamu kubwa mpaka bungeni kiasi kwamba wabunge wa chama kikuu cha upinzani kuketi na kukubaliane wakae karantini kwa siku 14 wajisikilizie hali ya maambukizi ijapoo wengine waliendelea na vikao vya bunge (Askari shujaa hufia vitani).

Halikadharika Rais hukuchoka na hukukata tamaa uliendelea na mapambano( nilimsikia waziri akisema uliendelea kutoa maelekezo bila kuchoka na kumpigia simu zaidi mara nane kwa siku hata usiku (sisi watanzania hatuna cha kukulipa ila Mungu wetu wa mbinguni atazilipia juhudi hizi inshallah).

Katika ibada ya Tar. 17/May/2020 wakati ukishiriki ibada kanisa la KKKT Chato, Pamoja na mambo mengine, ni kama ulikuwa mitume ukituleta dawa mbadala nathabiti ya Corona ukiitaka itumiwe miyoni na akilini mwa watanzania (tiba ya kiimani/kisaikolojia). Kama sijakosea ulisema lazima watanzania tuviepuke vitu vitatatu navyo ni 1:HOFU 2:HOFU 3:HOFU, Nikajisemea moyoni hili neno ulilitamka awali lilitutibu kwa muda na hali ikarudi kuwa ya taharuki, iweje leo kalitoa tena? Nikajiuliza sasa neno leyewe ni moja tu " HOFU" kulikuwa na ulazima gani kulirudia mara kadhaa tena kwa kulipa namba. Wakati bado sijaamua kulipuuzia nikaamua kujirudisha Senti Kayumba huko nilikopita angalau kupata maarifa hata yale machache ya kuwa na uwezo binafsi wa kuvukia barabara za njia 2 huku mikoani au zile nane za hapo DSM(nini maana ya kurudia neno katika utumizi wa lugha=kusisitiza jambo). Basi jibu la haraka ikawa ni kusisitiza jambo.

Mtoto mwenye hekima humsikiliza babaye, bali mwana mpumbavu ni mzigo kwa mamaye. Nikilri wazi hapa sisi watanzania tulikusikiliza na kukuelewa vyema. 1 week later nimeona mabadiliko makubwa miongoni mwetu. Watu tumeondoa hofu na kuendelea na shughuli zetu kama kawaida huku tukichukua tahadhari. Vyombo vya usafiri, biashara, kilimo, maofisi n. k shulighuli zinafanyika bila hofu. Kwa kiasi kikubwa, tahaharuki hakuna tena nikama we 're backing to absolutely normal.

Umetumia nafasi kubwa kama Rais wa nchi, Mwalimu wa Saikolojia na kama mtu wa imani huku ukienda mbali ukiitolea mfano wa mwanao aliyeugua ugonjwa huu You went deeper and deeper Honorable!! (sisi watanzania hatukujua na pole kwa hilj) yote ni uchukngu kwa wenzako, kuwatia moyo watanzania tuone ni maradhi kama mengine tuu tulionayo ambayo huweza kusababisha kifo au kupona(jamani Mubgu atupe nini, haki labda atupe kifo hicho Pekee ndio no judgment) kwasababu tumezidi kuona vibanzi machoni mwa wengine huku boriti zilizopo machoni mwetu hatutaki kuziondoa.

Ndugu zangu watanzania, tazamo wangu juu ya maamuzi wa Rais haiumaanIshi kuwa Corona haipo/haiui La hasha. Bali nikuungana naye kuwa hofu inaua zaidi/inazua taharuki/inakatisha tamaa na mapambano kwani hudhoofisha mioyo na akili kutika kukabiliana na tatizo. Ukweli ni kwamba magonjwa yote huweza kusababisha vifo au kuugua na kupona(japo kuna yale hayaponi hadi umauti). Lakini ugonjwa huu wa hata kama hauna dawa wala kinga, kitakwimu umeonesha namba kubwa ya waathirika hupona duniani kuliko wanaokufa kulingana na kinga za mhusika (mimi sio mtaalamu wa afya). Ukweli ni kwamba hofu huchangia kuudhoofisha mwili hata kusabisha umaiti. Tunaweza kukabiliana na huu ugojwa huku tukichukua tahadhari na kuondoa hofu.

Hata kama watanzania wote milion 50+ tungeugua huu ugonjwa hakika hofu ingekuwa ni kitu cha kwanza kutuangamiza. Kumbe kinyume chake kwamba hata kama tungeugua kwa namba hiyo basi imani na ujasiriwa kuikataa hofu yangekuwa ndiyo matibabu ya awali kabisa/kinga kumshinda adui. Mungu atujaze imani zaidi tuendelee kuishinda hofu.

USHUHUDA nanma hofu inaweza kuondoa maisha ya mwanadamu.

Usiku wa J/mosi tar. 2/03/219 Kuamkia J/pili 03/03/2019 binafsi nilikuwa na siku ngumu sana kutokana kuugua ugonjwa nisioujua kabisa kiasi nalala na kuota ndoto nyingi za kutisha mfululizo. Na kila nikistuka basi presha na hofu kuu inapanda. Hali iliendelea kuwa mbaya zaidi na kulazimu kuwaita wazazi angalau kunitazamia kwa muda uliobaki kupambazuka. Ashukuriwe Mungu baada ya kukucha ilinbidi kuenda kupima nijue shida ambapo majibu ilikuwa -UTI, Damu ilizidi sana na maleria 7. Nilipewa masharii na madawa. Lakinini hali iliendeleaa zaidi kuwa mbaya damu ikazidi sana ingawa maleria ilipona. Hali hii ilinipa hofu kubwa na mwili uliendelea kudhoofu kwa kasi kiasi kujipimia mwendo sitaimaliza March. Mungu mwema kwa kujikongoja niliumaliza mwezi nikiwa dhaifu sana. Kutokana na hofu vilibuka vimaagonjwa vya ajabu, uvimbe, mwili kupooza baadhi ya maeneo. Hakika hapa nilijihesabia kuwa 2019 ndio mwaka pekee wa mimi kuondoka duniani huku nikijitabilia kuwa mwezi huu simalizi (nilijipa uungu jamani ugali nimtamu asikwaie mtu).

Maisha yaachage tu!! Nilijiona imara zaidi nilipokuwa mzima, hiki ndio kipindi pekee nilichotamani uzima wa watu wengine(akipita mtu unajisemea moyoni ningekuwa kama yule). Hakaka Izlaeli alikuwa busy na wengine akanisahau mimi, hivyo hofu na kudhoofu kulidumu toka March mpaka mwisho mwa June 2019. Hapa kwa hiari yangu mwenyewe bila kulazimishwa na mtu niliamua kumtafuta mtumishi kwa mambo mawili tu., 1: kunipa huduma kiroho niweze kupona ikishindikana 2: aniandalie njia yangu isiwe na Giza, mashimo na vigingi.

Mwache Mungu aitwe Mungu tu, He was like Magufuli, baada ya kunipa huduma ya kiroho, na maombezi alinipa Antidote ndogo sana na yenye kazi kubwa kiasi kurestore uzima. Baada ya kumpa background nzima akasema hivi "kwa chochote utafanya/utaota na kuweweseka/utaugua hata kwa upya jitahidi ondoa HOFU". Kweli hii ndio ilikuwa tiba kwangu mpaka leo nimeweza kusimama nyuma ya Keyboard na kuunganimusha herufi hizi.

Pengine nitumie fursa hii kuwaomba watanzaniania wenzangu kuungana na Rais kuondoa hofu mioyoni mwetu kwa imani kabisa kwani ni mbinu muhimu sana kuukabili ugonjwa huu na hata magonjwa mengine huku tukiendelea kuchukua tahadhari.

Mwanasaikolojia mmoja maarufu kwa jina Sigmud Freud alisema kuwa "binadamu anatabia ya kuficha na kuhamishia udhaifu wake kwa mtu mwingine" Haya yasikupotezee muda, nguvu na visions. Kwasababu macho huona kadoa kadogo keusi kwenye shati jeupe. Hivyo mtu huona 1% ya kuitilia kasoro na 99% rangi kusudiwa. Hii si nzuri kumfanya mtu alivue shati.

Jambo moja la kukutia moyo Mzee wangu na Rais wangu wewe fanya vile nafsi na Mungu wako anakutuma kwetu. Sisi tunaweza kuwa na maneno mengi ya kukuvunja moyo bila kujali waathirika nini sisi wenyewe na familia zetu. Mungu wetu wa mbinguni tunayemwabudu hatokaa kimya juu ya haya hata atakuzidishia kwa kuwa unayafanya kwa imani na kwa upendo.
Nimalize kwa kukumbusha maneno ya mwanafasafa mmoja anaitwa

Epicurus anasema "Skillful pilots gain their reputation from storms and tempest. Haya tunayopita yazidi kukuimarisha na kukutia moyo zaidi. Mungu akubariki wewe na kizazi chako chote.

N:B Tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya Covid19 kadiri tuvyoelekezwa na wataalamu.

Mungu awabariki nyote.

Naomba kuwasilisha.
 
Story ndeefu sana lkn kama haina mashiko zaidi ya kusifia tuuu, sidhani kama mtu anastahili sifa just kwa kukutia moyo ati ondoa hofu wakati jamaa zetu wamepukutika sana tu, tunajua huu ugonjwa bado upo na aya maneno yako ya ghiriba ni ya hatari sana kwan watu wanazidi kuangamia uko majumbani kwao kwani mahospitalini hapafai kuugulia hapo.

Tukumbuke serikali kutokana na kuwa na mamlaka iliamua kuficha taharifa juu ya ukweli wa haya maradhi na wajua kuwa hata taharifa za maambuzi mapya na vifo ilificha kuyatoa, na hata kupima walihacha japo tukadanganywa ati ooh mtoto wake jiwe alihugua COVID19 sijui alipimia wapi wakati twajua serikali wala haitangazi na ni kama imetuhacha wanamnchi tupambane na hali zetu wenyewe.

pia mahospitali hawa madaktari wakawanyanyapaa sana wagonjwa hata wagonjwa wakawa wanaogopa kwenda hospitali hapo serikali ikaje na jawabu kuwa wagonjwa wamepungua sana, huu ni utoto wa wazi.

sasa ebu tukumbushe alipambana na covid19 kama liugonjwa kivipi yeye kama yeye?? au unamaanisha kwa kwenda kubana chattles mpaka makali yalipo pungua?? Au aliliombea taifa hata covid19 ikafa??
hacheni arguments za kikinda na kuziwasilisha kwa watu wazima.

au wewe mleta hoja ni mama ntilie??
 
ahahahha jiwe anavyomwogopa bashite kampiga tu biti kwamba wale wote waliokimbia Dar watoke huko warudi mara moja maofisini mzee likajitokeza
 
Hodi jukwaani.
Hongera zangu kijana mtiifu wa CHADEMA kwa Mh. JPM na kwa sisi watanzania kwa ujumla.

Binafsi nakupongeza sana sana Rais wa Tanzania kwa msimamo wako kiimani na kisaikoljia.

Pengine nitumie fursa hii kuwaomba watanzaniania wenzangu kuungana na Rais kuondoa hofu mioyoni mwetu kwa imani kabisa kwani ni mbinu muhimu sana kuukabili ugonjwa huu na hata magonjwa mengine huku tukiendelea kuchukua tahadhari.
Mkuu Kijana wa Chadema, Naxon,
Naunga mkono hoja, unaonyesha wewe ni Chadema uliyejitambua, kilichobaki kwako mtoa mada ni kuunga tuu mkono juhudi, huko ndani ya hill jahazi ulimo siko!, jahazi hilo linazama, hivyo wahi kuhama chombo, vinginevyo utazama na jahazi lako!.

P
 
EY8co81XkAcuxWU.jpg
 
Kwani C-9 ineisha mbona bado wagonjwa wapya wenye homa ya mapafu makali wanapikelewa hospital na bado tunazika wapendwa.Hongera wanatakuwa wapewe nchi zenye green .Nenda worldometer/covid-19upate update ya CORONA na nchi zilizofanikiwa kutokuwa na mgonjwa kwa siku 30 siluzopita Ndio muanze kusifiana.Mkapa kasema acheni kusifia watu ,sifieni sera.Jikinge Corona ipo na inaua
 
Hodi jukwaani.
Hongera zangu kijana mtiifu wa CHADEMA kwa Mh. JPM na kwa sisi watanzania kwa ujumla.

Utanguli:
Awali ya yote, mimi ni kijana mtiifu wa chama kikuu cha upinzani Chadema na aghalabu nimekulia na bado ninaishi katika chama hiki kikuu cha upinzani.

Kwanini nipo huku; niliamua kujiunga na chama hiki takribani miaka kumi iliyopita, kwa sababu ya hoja na ajenda nzito zinazobebwa na Viongozi makini na wanachama kwa ujumla. Mungu ibariki Chadema.

Pia nilijiunga na JF takribani miaka 7 iliyopita hususani jukwaa hili la siasa na kwa wakati wote huo nimekuwa mtu wa kusoma nyuzi za watu na angalau marachache kuchangia kidogo tu au nisichangie kabisa. Lengo kubwa ilikuwa ni kujifunza na kuupata uzoefu kuhusu mijadala mbalimbali katika jukwaa hili. Leo nimeamua kutoa nyuzi hii kwa mara ya kwanza aghalabu hata Mungu atanichukua kilicho chake punde tu namaliza nukta ya mwisho na kuisubmit basi nisiondoke na huku nafsi inawashwa.

Basi baada ya kautangulizi kangu hako naomba kenye njaa(kasikojitosheleza) naomba kujikita kwenye mada:

Pongezi zangu kwa Mh. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kupambana na Covid 19.
------------------------------------------
N:B pamoja na mambo mengine mengi yaliyofanywa na wewe hasa yanayohusu maendeleo, mada hii inahusu Covid19 pekee. MadaItajikita Katika mambo mawili tu (Imani na saikolojia)
Ndugu wanabodi nawasilimu na poleni na majukumu ya ujenzi wa taifa. Naweza nisiwe na maneno/uandishi mzuri kama manguli wa uandishi walipo humu hii ni kutoka na kutokuwa na uzoefu kwa kada ya uandishi(uvumilivu ni jambo jema pia).

Binafsi nakupongeza sana sana Rais wa Tanzania kwa msimamo wako kiimani na kisaikoljia.

Kwa mujibu wa baadhi ya maandiko ya kiimani(sitanukuu vifungu) kikristo yanasema" imani ni kuwa na hakika juu yale yatarajiwayo" na mengine yanasema "Hata ungalikuwa na imani ndogo hata kama chembe ya mbegu ya mti wa haradani, nawe ungaliuamuru mlima huu ng'oka ukajitose baharini nao ungali tii" (Naamini pia kwa upande wa Waislamu kunavifungu vizuri zaidi kuweza kutupa nguv zaidi).

Nikili wazi Covid19 imekuwa ni mlima mkubwa duniani huku ukichukua maefu ya maisha ya watu, na millions of people wakiwa wameembukizwa virusi hivi. Kama ilivyotabia ya janga lolote lile ni kuleta athari hasi, hili limevuruga uchumi wa kidunia, umepoteza ndugu, rafiki na jamaa duniani. Umeharibu taratibu zote za kiutawala na diplomasia za kidunia hasa kwa mataifa makubwa na tajiri, umewafanya kunyosheana vidole.

Kwa upande wa nchini ugonjwa huu ulileta taharuki na sintofahamu kubwa hata kabla ya kuingia nchini. Ukweli ni kwamba ulipoingia tu nchini HOFU KUU ilitamalaki hakuna kilichoweza kushikika/kufanyika bila kuiwazia Corona, kama kwamba hakuna ambacho kingeendelea. Tukitizama taarifa za vifo Italia, china, Irani, Hispania, USA na kwingineko basi mambo yalikuwa yanazidi kuwa mabaya zaidi. Ijapokuwa Wizara husika ilikuwa inaendelea kupambana kuokoa Maisha ya Watanzania (Mungu akubariki Ummy Mwalimu).
Ashukuliwe Mungu Tar. 10/April/2020 ukishiriki ibada uliongea na sisi watanzania ukitutaka kuondoa hofu na kuendelea kuchukua tahadhari juu ya hili.

Awali nilikuelewa mifano uliyoitoa kuhusu mazingira yanavyoweza kuufanya ugonjwa ukawa na athari ndogo au kubwa na kutolea mfano wa ugonjwa wa Malaria kwa kuwa na athari kubwa barani Afrika kuliko Ulaya ambako kuna baridi zaidi. Ukweli ulituasa kumtanguliza Mungu na kuondoa hofu. Kwa hili haukueleweka sana kutokana na kwamba ugonjwa huu ulizidi kuene na kuzua taharuki kiasi. Lakini ikafika kipindi kulikuwa na tahaluki kubwa tena ilijitokeza kiasi shughuli nyingi kusimama/kudolola hasa maeneo ya mijini. (Maduka, usafiri, ofisi, n. k). Hapa ilibaki kidogo

Pamoja na hali hii kukatokea sintofamu kubwa mpaka bungeni kiasi kwamba wabunge wa chama kikuu cha upinzani kuketi na kukubaliane wakae karantini kwa siku 14 wajisikilizie hali ya maambukizi ijapoo wengine waliendelea na vikao vya bunge (Askari shujaa hufia vitani).

Halikadharika Rais hukuchoka na hukukata tamaa uliendelea na mapambano( nilimsikia waziri akisema uliendelea kutoa maelekezo bila kuchoka na kumpigia simu zaidi mara nane kwa siku hata usiku (sisi watanzania hatuna cha kukulipa ila Mungu wetu wa mbinguni atazilipia juhudi hizi inshallah).

Katika ibada ya Tar. 17/May/2020 wakati ukishiriki ibada kanisa la KKKT Chato, Pamoja na mambo mengine, ni kama ulikuwa mitume ukituleta dawa mbadala nathabiti ya Corona ukiitaka itumiwe miyoni na akilini mwa watanzania (tiba ya kiimani/kisaikolojia). Kama sijakosea ulisema lazima watanzania tuviepuke vitu vitatatu navyo ni 1:HOFU 2:HOFU 3:HOFU, Nikajisemea moyoni hili neno ulilitamka awali lilitutibu kwa muda na hali ikarudi kuwa ya taharuki, iweje leo kalitoa tena? Nikajiuliza sasa neno leyewe ni moja tu " HOFU" kulikuwa na ulazima gani kulirudia mara kadhaa tena kwa kulipa namba. Wakati bado sijaamua kulipuuzia nikaamua kujirudisha Senti Kayumba huko nilikopita angalau kupata maarifa hata yale machache ya kuwa na uwezo binafsi wa kuvukia barabara za njia 2 huku mikoani au zile nane za hapo DSM(nini maana ya kurudia neno katika utumizi wa lugha=kusisitiza jambo). Basi jibu la haraka ikawa ni kusisitiza jambo.

Mtoto mwenye hekima humsikiliza babaye, bali mwana mpumbavu ni mzigo kwa mamaye. Nikilri wazi hapa sisi watanzania tulikusikiliza na kukuelewa vyema. 1 week later nimeona mabadiliko makubwa miongoni mwetu. Watu tumeondoa hofu na kuendelea na shughuli zetu kama kawaida huku tukichukua tahadhari. Vyombo vya usafiri, biashara, kilimo, maofisi n. k shulighuli zinafanyika bila hofu. Kwa kiasi kikubwa, tahaharuki hakuna tena nikama we 're backing to absolutely normal.

Umetumia nafasi kubwa kama Rais wa nchi, Mwalimu wa Saikolojia na kama mtu wa imani huku ukienda mbali ukiitolea mfano wa mwanao aliyeugua ugonjwa huu You went deeper and deeper Honorable!! (sisi watanzania hatukujua na pole kwa hilj) yote ni uchukngu kwa wenzako, kuwatia moyo watanzania tuone ni maradhi kama mengine tuu tulionayo ambayo huweza kusababisha kifo au kupona(jamani Mubgu atupe nini, haki labda atupe kifo hicho Pekee ndio no judgment) kwasababu tumezidi kuona vibanzi machoni mwa wengine huku boriti zilizopo machoni mwetu hatutaki kuziondoa.

Ndugu zangu watanzania, tazamo wangu juu ya maamuzi wa Rais haiumaanIshi kuwa Corona haipo/haiui La hasha. Bali nikuungana naye kuwa hofu inaua zaidi/inazua taharuki/inakatisha tamaa na mapambano kwani hudhoofisha mioyo na akili kutika kukabiliana na tatizo. Ukweli ni kwamba magonjwa yote huweza kusababisha vifo au kuugua na kupona(japo kuna yale hayaponi hadi umauti). Lakini ugonjwa huu wa hata kama hauna dawa wala kinga, kitakwimu umeonesha namba kubwa ya waathirika hupona duniani kuliko wanaokufa kulingana na kinga za mhusika (mimi sio mtaalamu wa afya). Ukweli ni kwamba hofu huchangia kuudhoofisha mwili hata kusabisha umaiti. Tunaweza kukabiliana na huu ugojwa huku tukichukua tahadhari na kuondoa hofu.

Hata kama watanzania wote milion 50+ tungeugua huu ugonjwa hakika hofu ingekuwa ni kitu cha kwanza kutuangamiza. Kumbe kinyume chake kwamba hata kama tungeugua kwa namba hiyo basi imani na ujasiriwa kuikataa hofu yangekuwa ndiyo matibabu ya awali kabisa/kinga kumshinda adui. Mungu atujaze imani zaidi tuendelee kuishinda hofu.

USHUHUDA nanma hofu inaweza kuondoa maisha ya mwanadamu.

Usiku wa J/mosi tar. 2/03/219 Kuamkia J/pili 03/03/2019 binafsi nilikuwa na siku ngumu sana kutokana kuugua ugonjwa nisioujua kabisa kiasi nalala na kuota ndoto nyingi za kutisha mfululizo. Na kila nikistuka basi presha na hofu kuu inapanda. Hali iliendelea kuwa mbaya zaidi na kulazimu kuwaita wazazi angalau kunitazamia kwa muda uliobaki kupambazuka. Ashukuriwe Mungu baada ya kukucha ilinbidi kuenda kupima nijue shida ambapo majibu ilikuwa -UTI, Damu ilizidi sana na maleria 7. Nilipewa masharii na madawa. Lakinini hali iliendeleaa zaidi kuwa mbaya damu ikazidi sana ingawa maleria ilipona. Hali hii ilinipa hofu kubwa na mwili uliendelea kudhoofu kwa kasi kiasi kujipimia mwendo sitaimaliza March. Mungu mwema kwa kujikongoja niliumaliza mwezi nikiwa dhaifu sana. Kutokana na hofu vilibuka vimaagonjwa vya ajabu, uvimbe, mwili kupooza baadhi ya maeneo. Hakika hapa nilijihesabia kuwa 2019 ndio mwaka pekee wa mimi kuondoka duniani huku nikijitabilia kuwa mwezi huu simalizi (nilijipa uungu jamani ugali nimtamu asikwaie mtu).

Maisha yaachage tu!! Nilijiona imara zaidi nilipokuwa mzima, hiki ndio kipindi pekee nilichotamani uzima wa watu wengine(akipita mtu unajisemea moyoni ningekuwa kama yule). Hakaka Izlaeli alikuwa busy na wengine akanisahau mimi, hivyo hofu na kudhoofu kulidumu toka March mpaka mwisho mwa June 2019. Hapa kwa hiari yangu mwenyewe bila kulazimishwa na mtu niliamua kumtafuta mtumishi kwa mambo mawili tu., 1: kunipa huduma kiroho niweze kupona ikishindikana 2: aniandalie njia yangu isiwe na Giza, mashimo na vigingi.

Mwache Mungu aitwe Mungu tu, He was like Magufuli, baada ya kunipa huduma ya kiroho, na maombezi alinipa Antidote ndogo sana na yenye kazi kubwa kiasi kurestore uzima. Baada ya kumpa background nzima akasema hivi "kwa chochote utafanya/utaota na kuweweseka/utaugua hata kwa upya jitahidi ondoa HOFU". Kweli hii ndio ilikuwa tiba kwangu mpaka leo nimeweza kusimama nyuma ya Keyboard na kuunganimusha herufi hizi.

Pengine nitumie fursa hii kuwaomba watanzaniania wenzangu kuungana na Rais kuondoa hofu mioyoni mwetu kwa imani kabisa kwani ni mbinu muhimu sana kuukabili ugonjwa huu na hata magonjwa mengine huku tukiendelea kuchukua tahadhari.

Mwanasaikolojia mmoja maarufu kwa jina Sigmud Freud alisema kuwa "binadamu anatabia ya kuficha na kuhamishia udhaifu wake kwa mtu mwingine" Haya yasikupotezee muda, nguvu na visions. Kwasababu macho huona kadoa kadogo keusi kwenye shati jeupe. Hivyo mtu huona 1% ya kuitilia kasoro na 99% rangi kusudiwa. Hii si nzuri kumfanya mtu alivue shati.

Jambo moja la kukutia moyo Mzee wangu na Rais wangu wewe fanya vile nafsi na Mungu wako anakutuma kwetu. Sisi tunaweza kuwa na maneno mengi ya kukuvunja moyo bila kujali waathirika nini sisi wenyewe na familia zetu. Mungu wetu wa mbinguni tunayemwabudu hatokaa kimya juu ya haya hata atakuzidishia kwa kuwa unayafanya kwa imani na kwa upendo.
Nimalize kwa kukumbusha maneno ya mwanafasafa mmoja anaitwa

Epicurus anasema "Skillful pilots gain their reputation from storms and tempest. Haya tunayopita yazidi kukuimarisha na kukutia moyo zaidi. Mungu akubariki wewe na kizazi chako chote.

N:B Tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya Covid19 kadiri tuvyoelekezwa na wataalamu.

Mungu awabariki nyote.

Naomba kuwasilisha.
Mshukuru mungu , covid 19 katika la Africa ni Kama mvua za rasha rasha , Unaona kinachoendelea Brazil, Chile, .Jikumbushe hali ya Wuhan , Spain,na France kuhusu Corona
 
Dah! Mtoa mada bandiko lako ni refu mno!! Yaani kumpongeza tu Rais na sisi Watanzania wenzako ndiyo uandike maneno yote hayo! Mimi nimeishia kusoma hapo mwanzoni tu.

Ila tunashukuru kwa pongezi zako. Muda si mrefu tutaanza kutembea Vifua mbele bila shaka! Ila kuficha taarifa za Corona siyo ujanja kivile.
 
Back
Top Bottom