Hongera Prof Muhongo/Maswi kwa uzalendo, ingekuwa Ngeleja/Jairo ingekuwaje?

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,171
HawA maafisa waandamizi wa Wizara ya Nishati na Madini wanastahili pongezi kwa kuonyesha kibri ya Kitanzania ambaya kwa siku za hivi karibuni imekuwa nadra.
Prof Muhongo, Waziri wa Nishati na Madini, pamoja na Katibu Mkuu wake wameweza kuhimili majaribu ya kuhongwa na kuhongeka, na hivyo kutunza heshima zao na Watanzania kwa ujumla.

Makampuni makubwa kimataifa ya nishati na madini, huo kwao ni mchezo wa kila siku na wa kawaida.

Nawasikitikia tu wale wabunge na maofisa wa Seriikali waliotongozwa na kuhongeka na hatimaye sasa wanaonekana hawana faida mbele ya umma wa Kitanzania.

Nabaki najiuliza je? Wangekuwepo bado wale machalii wawili Ngeleja na Jairo, leo hali ingekuwaje?
 
kama kawaida yetu
tushabikia siasa mno

sio kazi ya waziri wala katibu mkuu
kuendesha shirika la umma kama Tanesco

mpaka kufikia kuwapangia gharama za kuunganisha umeme
na kuzipunguza kisiasa zaidi
bila kujali gharama halisi

kama tatizo ni Mhando

dawa si kwa waziri kuingilia utendaji

dawa ni kutafuta better CEO
na apewe nafasi
 
kama kawaida yetu
tushabikia siasa mno

sio kazi ya waziri wala katibu mkuu
kuendesha shirika la umma kama Tanesco

wewe huna jipya! kibalaka wa mafisadi. waziri na katibu wake wamefanya kazi kubwa na yakizalendo. ngeleja na jairo wangeshapiga dili hapo huku shilika linakufa!
 
Na Kikwete aliyewateua, huna habari nae?

Tunamshurukuru Kikwete kwa kuwateu pia. Binafsi niseme kuwa hivi sasa Kikwete ana washauri wazuri wa karibu akiwemo katibu mkuu kiongozi ambaye ni mzalendo na mchapakazi pia. Pia Kikwete kuwa mbali kwake na akina RA na EL kumesaidia kwa kiasi kikubwa ndo leo tuna watu kama hawa bila kuwasahau Magufuli kurudishwa wizara ya ujenzi na Mwakyembe kupewa wizara kamili. Nirudie kusema kuwa kwa kiasi kikubwa jamaa wa Mara ni waadilifu.
 
kama kawaida yetu
tushabikia siasa mno

sio kazi ya waziri wala katibu mkuu
kuendesha shirika la umma kama Tanesco

mpaka kufikia kuwapangia gharama za kuunganisha umeme
na kuzipunguza kisiasa zaidi
bila kujali gharama halisi

kama tatizo ni Mhando

dawa si kwa waziri kuingilia utendaji

dawa ni kutafuta better CEO
na apewe nafasi

Mkuu hebu tuambie gharama halisi za kuunganisha umeme unazozifahamu wewe. Hujuwi kuwa gharama zinakuwa kubwa kwa sababu ya kile cha juu wanachogawiwa mafisadi? Tanesco lazima serikali iingilie kati kwani kila wakati Tanesco wanategemea ruzuku toka serikalini. Na Tanesco ni mali ya serikali.
 
Tunamshurukuru Kikwete kwa kuwateu pia. Binafsi niseme kuwa hivi sasa Kikwete ana washauri wazuri wa karibu akiwemo katibu mkuu kiongozi ambaye ni mzalendo na mchapakazi pia. Pia Kikwete kuwa mbali kwake na akina RA na EL kumesaidia kwa kiasi kikubwa ndo leo tuna watu kama hawa bila kuwasahau Magufuli kurudishwa wizara ya ujenzi na Mwakyembe kupewa wizara kamili. Nirudie kusema kuwa kwa kiasi kikubwa jamaa wa Mara ni waadilifu.

...................Na vile vile Kikwete ameshachukua chake cha kutosha hana haja tena ya kuchukua zaidi.
 
Mimi bado siwaamini viongozi wetu kabisaaa. Mwalimu alisema "kiongozi akisema atailinda katiba, na tukimuangalia machoni tuone kweli atailinda katiba". Sasa hawa jamaa nikiwaangalia machoni, sioni wanachokisema. Mara nyingi huwa wamekorofishana kwenye maslahi binafsi ya hizo wizara ndiyo wanaamuwa kuumbuwana bungeni. Wananchi mnashangilia mkidhania mnatetewa. Imeshatokea mara nyingi na ndivyo ilivyo. Sijaona na hakuna kiongozi anayeogelea kwenye mfumo mchafu halafu yeye akatoka akiwa msafi. Hakuna, nasisitiza, NEVER EVER.
 
kama kawaida yetu
tushabikia siasa mno

sio kazi ya waziri wala katibu mkuu
kuendesha shirika la umma kama Tanesco

mpaka kufikia kuwapangia gharama za kuunganisha umeme
na kuzipunguza kisiasa zaidi
bila kujali gharama halisi

kama tatizo ni Mhando

dawa si kwa waziri kuingilia utendaji

dawa ni kutafuta better CEO
na apewe nafasi

Huwajui Waafrika? hata usafi wa majumbani mwetu mpaka Rais aingilie.

Miafrika Ndivyo Ilivyo - Nyani Ngabu
 
Tunamshurukuru Kikwete kwa kuwateu pia. Binafsi niseme kuwa hivi sasa Kikwete ana washauri wazuri wa karibu akiwemo katibu mkuu kiongozi ambaye ni mzalendo na mchapakazi pia. Pia Kikwete kuwa mbali kwake na akina RA na EL kumesaidia kwa kiasi kikubwa ndo leo tuna watu kama hawa bila kuwasahau Magufuli kurudishwa wizara ya ujenzi na Mwakyembe kupewa wizara kamili. Nirudie kusema kuwa kwa kiasi kikubwa jamaa wa Mara ni waadilifu.

Kuna mama mmoja ambae amerudi kutoka katika kazi za Umoja wa Mataifa hivi karibuni (siyo Asha Rose).

Huyo mama ni kichwa na aliporudi tu Kikwete akamwambia hakuna kwenda kokote kaa hapa Ikulu unisaidie kazi, huyo mama ni kichwa hapana mchezo, zamani wakati wa Nyerere aliwahi kuwa Katibu Mkuu wizara fulani (siikumbiki jina kwa sasa).

Toka kuwepo kwake huyo mama pale Ikulu mambo yanakwenda vizuri sana anaitwa Z. Nuru. Anachonifurahisha hataki publicity kabisa wala hajulikani kama yupo. Yeye anachapa kazi tu.
 
Mkuu hebu tuambie gharama halisi za kuunganisha umeme unazozifahamu wewe. Hujuwi kuwa gharama zinakuwa kubwa kwa sababu ya kile cha juu wanachogawiwa mafisadi? Tanesco lazima serikali iingilie kati kwani kila wakati Tanesco wanategemea ruzuku toka serikalini. Na Tanesco ni mali ya serikali.

Mashauri,
You are absolutely right! Watanzania ni Mazuzu haya sio maneno yangu aliyasema Baba wa Taifa.

Hata hizo shilling laki moja na sabini elfu bado ni nyingi sana . Bei ya kuunganisha umeme inapaswa kuwa bure na hili linawezekana!

Yes let us make a simple calculation kuonyesha wizi wa Tanesco kwa wateja.
Gharama ya vifaa vya kuunganisha umeme :
1.Meter ya single phase Usd 50 sawa na Tshs 80,000 ( Hii ni Mali ya Tanesco)
2. Waya za umeme 25 sq.mm mita 60 Kila mita moja Tshs 1500 = Tshs 90,000 ( Mali ya Tanesco)
3. Vikombe 4 @ 1500 = Tshs 6000 (Mali ya Tanesco )
4. Waya wa Umeme 16mm sq mita 10 @ Tshs 4,000 = Tshs 40, 000 ( Mali ya tanesco)
5. Bolts and nuts pamoja na kazi ya kuijenga service line Tshs 50,000 ( include transport) : (mteja)

Mantiki ya kutokulipa ni kwamba those are the investment costs which Taneso has to incurr so that they can sell power to a customer period!
Kwa kifupi hata Kama wangekuwa hawana pesa za kuwekeza kwenye biashara Yao then Mteja angepaswa kuchangia zisizozidi Tshs 140, 000 ambazo it has to be recovered from power sales .

Ni lazima tuwapongeze Prof. Mhongo na Katibu Mkuu kwa kuanzia we should expect more from them wapatiwe muda and space!

Madudu yote haya ni kutokana na kuwaweka madarakani watu ambao uwezo wao kufikiria ni mdogo.
They
 
Mkuu hebu tuambie gharama halisi za kuunganisha umeme unazozifahamu wewe. Hujuwi kuwa gharama zinakuwa kubwa kwa sababu ya kile cha juu wanachogawiwa mafisadi? Tanesco lazima serikali iingilie kati kwani kila wakati Tanesco wanategemea ruzuku toka serikalini. Na Tanesco ni mali ya serikali.

Mashauri,
You are absolutely right! Watanzania ni Mazuzu haya sio maneno yangu aliyasema Marehemu Baba wa Taifa.

Hata hizo shilling laki moja na sabini elfu bado ni nyingi sana . Bei ya kuunganisha umeme inapaswa kuwa bure na hili linawezekana!

Yes let us make a simple calculation kuonyesha wizi wa Tanesco kwa wateja.
Gharama ya vifaa vya kuunganisha umeme :
1.Meter ya single phase Usd 50 sawa na Tshs 80,000 ( Hii ni Mali ya Tanesco)
2. Waya za umeme 25 sq.mm mita 60 Kila mita moja Tshs 1500 = Tshs 90,000 ( Mali ya Tanesco)
3. Vikombe 4 @ 1500 = Tshs 6000 (Mali ya Tanesco )
4. Waya wa Umeme 16mm sq mita 10 @ Tshs 4,000 = Tshs 40, 000 ( Mali ya tanesco)
5. Bolts and nuts pamoja na kazi ya kuijenga service line Tshs 50,000 ( include transport) : (Labda anaweza kuchangia Mteja ))

Mantiki ya kutokulipa ni kwamba those are the investment costs which Taneso has to incurr so that they can sell power to a customer period!
Kwa kifupi hata Kama wangekuwa hawana pesa za kuwekeza kwenye biashara Yao then Mteja angepaswa kuchangia zisizozidi Tshs 140, 000 ambazo it has to be recovered from power sales .

Ni lazima tuwapongeze Prof. Mhongo na Katibu Mkuu kwa kuanzia we should expect more from them wapatiwe muda and space!

Madudu yote haya ni kutokana na kuwaweka madarakani watu ambao uwezo wao kufikiria ni mdogo.
A good MD should sit down prepare a business plan and show how he can operate the company to generate income and make sure there is a return on Investment (ROI) make profit for the share holders and not otherwise . Hawa wapuuzi wanaotaka kuendelea kupata Ruzuku kutoka Serikalini then they can go to hell?

Of course pamoja na nia nzuri ya Prof na Katibu Mkuu they have inherited a dead body( Tanesco) with huge debts a product of grand and corporate corruption.
Bila kufuta mikataba mibovu ya Songas, IPTL , Symbion , na Aggreko pamoja na deni la Tshs 300 billion aliloacha Dr. Idris Rashid hata ashuke malaika Gabriel you can turn out Taneso.

Prof na Katibu Mkuu wataendelea kutumia pesa za walipa kodi kulipa Ufisadi uliooteshwa Tanesco over the past 20 years. Kuna haja ya kuanza alifu kwa kijiti na wahusika wote dead or alive tuwaanike hadharani of Jakaya Mrisho Kikwete in person has nowhere to hide ??.!
 
uzalendo unaanza kurudi Tanzania,hawa jamaa ni majembe ya uhakika,ila tukubali pia inachangiwa na kuwa na katibu mkuu kiongozi mzalendo!na hakika tutegemee mabadiliko makubwa kwa mawaziri,manaibu waziri na maktibu wakuu walio wengi maana bosi wao mpya ni kisiki kwa mafisadi!sasa iwapo viongozi wa wizara watakuwa wanashirikiana na mafisadi,katibu mkuu kiongozi hatawavumilia,hivyo ni wazi itawabidi viongozi wa wizara wabadilike waendane nae sambamba katika kulitumikia taifa kwa uadilifu!
 
Maafisa/watu wengi sana wameishindwa hii wizara kwasababu whatever you decide unagusa maslahi wa wachache, na ndio maana unakuwa kwenye high risk ya kuharibiwa na mwishowe kunyofolewa....mi sikuwahi hata kuimagine kwamba mgao wa umeme unapangwa makusudi ili fisadiz watukamue...LOL..this country ina wenyewe.
 
Tunamshurukuru Kikwete kwa kuwateu pia. Binafsi niseme kuwa hivi sasa Kikwete ana washauri wazuri wa karibu akiwemo katibu mkuu kiongozi ambaye ni mzalendo na mchapakazi pia. Pia Kikwete kuwa mbali kwake na akina RA na EL kumesaidia kwa kiasi kikubwa ndo leo tuna watu kama hawa bila kuwasahau Magufuli kurudishwa wizara ya ujenzi na Mwakyembe kupewa wizara kamili. Nirudie kusema kuwa kwa kiasi kikubwa jamaa wa Mara ni waadilifu.

Rmashauri naungana na wewe kabisa katika sentensi yako ya mwisho kwamba watu wa mara ni waadilifu. Lakini kumbukakuwa RA na EL ni marafiki wa damu na EL ni msanii by professional ana Masters ya maigizo na JK ni tegemezi sana hawezi kujisimamia yeye kama yeye hebu nambie nini kinaendelea ndiyo yaleyale kukumbuka shuka asubuhi na kuingiza siasa katika mambo ya kitaalam.
 
Kuna mama mmoja ambae amerudi kutoka katika kazi za Umoja wa Mataifa hivi karibuni (siyo Asha Rose).

Huyo mama ni kichwa na aliporudi tu Kikwete akamwambia hakuna kwenda kokote kaa hapa Ikulu unisaidie kazi, huyo mama ni kichwa hapana mchezo, zamani wakati wa Nyerere aliwahi kuwa Katibu Mkuu wizara fulani (siikumbiki jina kwa sasa).

Toka kuwepo kwake huyo mama pale Ikulu mambo yanakwenda vizuri sana anaitwa Z. Nuru. Anachonifurahisha hataki publicity kabisa wala hajulikani kama yupo. Yeye anachapa kazi tu.

?????? Mh!
 
Na Kikwete aliyewateua, huna habari nae?
Mkuu Zomba, kwa Rais wangu Kikwete pongezi nazihold kwanza.

Hao ambao wana elements za ufisadi kama Ngeleja na Jairo aliwateua yeye mweyewe.
Si picha nzuri sana kuteua viongozi kwa trial and error katika positions sensitive kama za Nishati na Madini.

Na kwa hakika suala lenyewe la kuukubali au kuukataa ufisadi inaelekea siku hizi ni msimamao wa mtu mwenyewe, na ndio maana wengi wanatuhumiwa ufisadi lakini bado wanapeta.
Na hapo ndo maana nawapongeza hao viongozi wawili Prof Muhongo na Ng Maswi.

Sasa turudi kwenye kukata mzizi wa fitna,

Wawekezaji wakubwa tunawapigia magoti ama hatuna akili nzuri.
Wanadiriki kuhonga MAWAZIRI HADI WABUNGE!!!
This is serious.

Kama kampuni ya nje ikaweza kuwa honga viongozi wa cadre hiyo basi hatuna Nchi!

Zomba, kama uko karibu na Kikwete na anataka nimpe senks, naomba tu awa blaclklist hayo makampuni yaliyodiriki kuhonga viongozi wake na wachukuliwe hatua zifaazo na ikiwezekana wanyang'nywe hizo kandarasi au tenda.
 
Mashauri,
You are absolutely right! Watanzania ni Mazuzu haya sio maneno yangu aliyasema Baba wa Taifa.

Hata hizo shilling laki moja na sabini elfu bado ni nyingi sana . Bei ya kuunganisha umeme inapaswa kuwa bure na hili linawezekana!

Yes let us make a simple calculation kuonyesha wizi wa Tanesco kwa wateja.
Gharama ya vifaa vya kuunganisha umeme :
1.Meter ya single phase Usd 50 sawa na Tshs 80,000 ( Hii ni Mali ya Tanesco)
2. Waya za umeme 25 sq.mm mita 60 Kila mita moja Tshs 1500 = Tshs 90,000 ( Mali ya Tanesco)
3. Vikombe 4 @ 1500 = Tshs 6000 (Mali ya Tanesco )
4. Waya wa Umeme 16mm sq mita 10 @ Tshs 4,000 = Tshs 40, 000 ( Mali ya tanesco)
5. Bolts and nuts pamoja na kazi ya kuijenga service line Tshs 50,000 ( include transport) : (mteja)

Mantiki ya kutokulipa ni kwamba those are the investment costs which Taneso has to incurr so that they can sell power to a customer period!
Kwa kifupi hata Kama wangekuwa hawana pesa za kuwekeza kwenye biashara Yao then Mteja angepaswa kuchangia zisizozidi Tshs 140, 000 ambazo it has to be recovered from power sales .

Ni lazima tuwapongeze Prof. Mhongo na Katibu Mkuu kwa kuanzia we should expect more from them wapatiwe muda and space!

Madudu yote haya ni kutokana na kuwaweka madarakani watu ambao uwezo wao kufikiria ni mdogo.
They


hebu nielekeze wapi nitanunua mita kwa dollar 50?
nina shida na mita nyiingi saana
 
Wasi sifiwe sana bali ndivyo wanavyotakiwa kufanya siku zote! kumbuka wako hapo kwa kazi hiyo!
 
Back
Top Bottom