Hongera Naibu Waziri wa Elimu kwa tamko la kudhibiti viboko mashuleni

Regnatus Cletus

JF-Expert Member
May 26, 2018
1,114
958
Ndugu wanabodi,

Salaam!

Nimpongeze ndugu Naibu Waziri wa Elimu, Mheshimiwa WILLIAM OLE NASHA kwa kutoa tamko lenye malengo ya kuendelea kufanya shule kuwa sehemu salama kwa wanafunzi, watoto, na wadogo zetu kupata elimu kwa amani na utulivu wa mwili na akili, ambapo kuanzia sasa NI MARUFUKU KWA WALIMU KUTEMBEA NA BAKORA MAENEO YA SHULE.

Nikushukuru ndugu Naibu Waziri kwa kusikiliza makaripio ya wananchi dhidi ya walimu WASIO NA MAADILI hususani baada ya mauaji ya kikatili ya mtoto Sperius Eradius yaliyofanywa na mwalimu wa nidhamu kwa shutuma batili za wizi wa mkoba.

Marufuku hii isitafsiriwe kama amri za kisiasa, isipokuwa ieleweke kama namna ya kusimamia SHERIA YA UTOAJI WA ADHABU YA VIBOKO, YAANI SHERIA YA ELIMU SURA YA 353 MAREJEO YA 2002, NA CORPORAL PUNISHMENT REGULATIONS G. N 294 2002 ; ZINAZOTAKA ADHABU YA VIBOKO VISIVYOZIDI VINNE ITOLEWE NA MWALIMU MKUU TU, AU MWALIMU MWINGINE KWA RUHUSA YA MWALIMU MKUU, NA SI VINGINEVYO.

Sheria na kanuni za utoaji wa adhabu za viboko zina malengo ya kuwaadabisha wanafunzi kwa kiwango sahihi bila kuongozwa na mihemko na hisia.

Nikiwa kama mdau wa sheria, hasa mtu anayependa kujitoa kupigania haki za watoto, SIPENDEZWI KABISA NA ADHABU YA VIBOKO.

Yangekuwa ni mamlaka yangu ningesisitiza KUFUTWA kwa adhabu za kinyama na kitumwa za viboko, na badala yake, wanafunzi watovu wa nidhamu wapewe adhabu kali za mikono, wasimamishwe masomo, au wafukuzwe shule.

Adhabu ya viboko ni kielelezo cha jamii inayoamini na kuhusudu katika ukatili kama nyenzo ya kuadabishana.

UKATILI DHIDI YA WATOTO NA WANAFUNZI HAUKUBALIKI.

PUMZIKA KWA AMANI MTOTO MWEMA SPERIUS ERADIUS.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu wanabodi,

Salaam!

Nimpongeze ndugu Naibu Waziri wa Elimu, Mheshimiwa WILLIAM OLE NASHA kwa kutoa tamko lenye malengo ya kuendelea kufanya shule kuwa sehemu salama kwa wanafunzi, watoto, na wadogo zetu kupata elimu kwa amani na utulivu wa mwili na akili, ambapo kuanzia sasa NI MARUFUKU WALIMU KUTEMBEA NA BAKORA MAENEO YA SHULENI.

Nikushukuru ndugu Naibu Waziri kwa kusikiliza makaripio ya wananchi dhidi ya walimu WASIO NA MAADILI hususani baada ya mauaji ya kikatili ya mtoto Sperius Eradius yaliyofanywa na mwalimu wa nidhamu kwa shutuma batili za wizi wa mkoba.

Marufuku hii isitafsiriwe kama amri za kisiasa, isipokuwa ieleweke kama namna ya kusimamia SHERIA YA UTOAJI WA ADHABU YA VIBOKO, YAANI SHERIA YA ELIMU SURA YA 353 MAREJEO YA 2002, NA CORPORAL PUNISHMENT REGULATIONS G. N 294 2002, ZINAZOTAKA ADHABU YA VIBOKO VISIVYOZIDI VINNE ITOLEWE NA MWALIMU MKUU TU, AU MWALIMU MWINGINE KWA RUHUSA YA MWALIMU MKUU, NA SI VINGINEVYO.

Sheria na kanuni za utoaji wa adhabu za viboko zina malengo ya kuwaadabisha wanafunzi kwa kiwango sahihi bila kuongozwa na mihemko na hisia.

Nikiwa kama mdau wa sheria, hasa mtu anayependa kujitoa kupigania haki za watoto, SIPENDEZWI KABISA NA ADHABU YA VIBOKO.

Yangekuwa ni mamlaka yangu ningesisitiza KUFUTWA kwa adhabu za kinyama na kitumwa za viboko, na badala yake, wanafunzi watovu wa nidhamu wapewe adhabu kali za mikono, wasimamishwe masomo, au wafukuzwe shule.

Adhabu ya viboko ni kielelezo cha jamii inayoamini na kuhusu katika ukatili kama nyenzo ya kuadabishana.

UKATILI DHIDI YA WATOTO NA WANAFUNZI HAIKUBALIKI KABISA.

PUMZIKA KWA AMANI MTOTO MWEMA SPERIUS ERADIUS.


Sent using Jamii Forums mobile app
Je na wale wanaopewa adhabu ya viboko mahakamani nayo itolewe??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera yako inatokana na kitu gani alichokifanya cha maana?? Hivi wewe una mtoto anayesoma shule ya kata?? Hivi wewe ulisoma shule gani??
Nadhani mngeweza kutenganisha siasa na maisha yetu ya kila siku tungelifika mbali. Nadhani sasa huyu waziri ndio kaleteleza maasi kule shuleni. Ushauri wangu, wakuu wa shule watengeneze ratiba ya kutoa mboko huko mashuleni hadi nidhamu isimame. Kila mtoto kichwa maji, alundikiwe makosa na kila kosa alimwe fimbo hizo 4 na makosa yasipungue 20 kwa siku ili alimwe mboko 80.
Mzazi asiyetaka mwanaye alimwe mboko amweke mfukoni mwake asije tuharibia watoto wetu mashuleni. Litoto la form 2 linavutia bangi darasani halafu useme asitandikwe?? Litoto linamtukana mwalimu wake matusi ya nguoni mbele ya darasa halafu useme nikamtafute mwalim mkuu aje kumwadhibu?? Msiwafanye watoto wetu wawe maharamia mchana jamani. Simpi hongera huyo waziri.
Hakuna aliyesoma na kuongoza darasani ambaye hakuonja mboko kwanza. Fimbo haiuiiii bali hukuza ufahamu. Hakuna mwalimu asiyempenda mwanafunzi wake hivyo hawatawaua.
 
Watoto watukutu wapo kila sehemu ya jamii ila ambacho huwa nakifikiria mara zote ni hiki; laiti serikali ingeliangalia kwa umakini swala la Maslahi duni ya waalimu wakayaboresha maradufu, walimu wakawa marafiki wa wanafunzi sidhani kama jamii yetu ingekuwa na tabu kiasi hiki. Angalia shule za kishua, hukuti watoto wakichapwa wala kupewa adhabu za visiki, ila wale jamaa wanacheza tu na saikolojia ya mwanafunzi kiasi kwamba akizingua atahudumiwa kitaalam kuondolewa pale alipokwama. Haya mengine yangejiseti yenyewe tu
 
Hongera yako inatokana na kitu gani alichokifanya cha maana?? Hivi wewe una mtoto anayesoma shule ya kata?? Hivi wewe ulisoma shule gani??
Nadhani mngeweza kutenganisha siasa na maisha yetu ya kila siku tungelifika mbali. Nadhani sasa huyu waziri ndio kaleteleza maasi kule shuleni. Ushauri wangu, wakuu wa shule watengeneze ratiba ya kutoa mboko huko mashuleni hadi nidhamu isimame. Kila mtoto kichwa maji, alundikiwe makosa na kila kosa alimwe fimbo hizo 4 na makosa yasipungue 20 kwa siku ili alimwe mboko 80.
Mzazi asiyetaka mwanaye alimwe mboko amweke mfukoni mwake asije tuharibia watoto wetu mashuleni. Litoto la form 2 linavutia bangi darasani halafu useme asitandikwe?? Litoto linamtukana mwalimu wake matusi ya nguoni mbele ya darasa halafu useme nikamtafute mwalim mkuu aje kumwadhibu?? Msiwafanye watoto wetu wawe maharamia mchana jamani. Simpi hongera huyo waziri.
Hakuna aliyesoma na kuongoza darasani ambaye hakuonja mboko kwanza. Fimbo haiuiiii bali hukuza ufahamu. Hakuna mwalimu asiyempenda mwanafunzi wake hivyo hawatawaua.
Mwalimu umejaa hasira tu dhidi ya wanafunzi.

Wanafunzi wanapaswa kuongozwa, kushauriwa na kuelekezwa.

Kwa maandishi yako haya naamini kabisa wewe ndiye MVUTA BANGI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makosa madogo madogo ambayo walimu walikuwa wanatumia fimbo kumalizana na wanafunzi
Uchelewaji shuleni
Kutoandika notes
Kutochomekea sare
Kutofanya usafi wa mazingira
Kelele darasani
Utoro mdogo
Swahili speaker
N.K

Sasa haya yote yanahamishiwa kwenye adhabu za nje, zikiwemo
Kulima
Kuchimba shimo la taka
Kufagia
Kudeki chooni
Kufyeka
N.K
Adhabu hizi zitapoteza muda mwingi wa mtoto kutohudhuria masomo darasani. Kwa wale nundaz wasiopenda kipindi cha somo fulani, akijua muda huu ni kipindi kile nisichokipenda, anachomoa sare halafu huyoooo anajipitisha mbele ya walimu. Si anajua hatochapwa, atapewa eneo afyeke wakati kipindi kinateketea. Kama unaamini wale vibaka wa ubungo na mateja wala unga nao pia kwa nyakati tofauti waliwahi kuwa wanafunzi, gonga like kuwatia moyo walimu. Kama mwanao nunda #pelekagereji.
 
Makosa madogo madogo ambayo walimu walikuwa wanatumia fimbo kumalizana na wanafunzi
Uchelewaji shuleni
Kutoandika notes
Kutochomekea sare
Kutofanya usafi wa mazingira
Kelele darasani
Utoro mdogo
Swahili speaker
N.K

Sasa haya yote yanahamishiwa kwenye adhabu za nje, zikiwemo
Kulima
Kuchimba shimo la taka
Kufagia
Kudeki chooni
Kufyeka
N.K
Adhabu hizi zitapoteza muda mwingi wa mtoto kutohudhuria masomo darasani. Kwa wale nundaz wasiopenda kipindi cha somo fulani, akijua muda huu ni kipindi kile nisichokipenda, anachomoa sare halafu huyoooo anajipitisha mbele ya walimu. Si anajua hatochapwa, atapewa eneo afyeke wakati kipindi kinateketea. Kama unaamini wale vibaka wa ubungo na mateja wala unga nao pia kwa nyakati tofauti waliwahi kuwa wanafunzi, gonga like kuwatia moyo walimu. Kama mwanao nunda #pelekagereji.
Mwanafunzi mtovu wa nidhamu atapatiwa viboko visivyozidi vinne na mwalimu mkuu tu, au mwalimu wa kawaida kwa ruhusa ya mwalimu mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu wanabodi,

Salaam!

Nimpongeze ndugu Naibu Waziri wa Elimu, Mheshimiwa WILLIAM OLE NASHA kwa kutoa tamko lenye malengo ya kuendelea kufanya shule kuwa sehemu salama kwa wanafunzi, watoto, na wadogo zetu kupata elimu kwa amani na utulivu wa mwili na akili, ambapo kuanzia sasa NI MARUFUKU KWA WALIMU KUTEMBEA NA BAKORA MAENEO YA SHULE.

Nikushukuru ndugu Naibu Waziri kwa kusikiliza makaripio ya wananchi dhidi ya walimu WASIO NA MAADILI hususani baada ya mauaji ya kikatili ya mtoto Sperius Eradius yaliyofanywa na mwalimu wa nidhamu kwa shutuma batili za wizi wa mkoba.

Marufuku hii isitafsiriwe kama amri za kisiasa, isipokuwa ieleweke kama namna ya kusimamia SHERIA YA UTOAJI WA ADHABU YA VIBOKO, YAANI SHERIA YA ELIMU SURA YA 353 MAREJEO YA 2002, NA CORPORAL PUNISHMENT REGULATIONS G. N 294 2002 ; ZINAZOTAKA ADHABU YA VIBOKO VISIVYOZIDI VINNE ITOLEWE NA MWALIMU MKUU TU, AU MWALIMU MWINGINE KWA RUHUSA YA MWALIMU MKUU, NA SI VINGINEVYO.

Sheria na kanuni za utoaji wa adhabu za viboko zina malengo ya kuwaadabisha wanafunzi kwa kiwango sahihi bila kuongozwa na mihemko na hisia.

Nikiwa kama mdau wa sheria, hasa mtu anayependa kujitoa kupigania haki za watoto, SIPENDEZWI KABISA NA ADHABU YA VIBOKO.

Yangekuwa ni mamlaka yangu ningesisitiza KUFUTWA kwa adhabu za kinyama na kitumwa za viboko, na badala yake, wanafunzi watovu wa nidhamu wapewe adhabu kali za mikono, wasimamishwe masomo, au wafukuzwe shule.

Adhabu ya viboko ni kielelezo cha jamii inayoamini na kuhusudu katika ukatili kama nyenzo ya kuadabishana.

UKATILI DHIDI YA WATOTO NA WANAFUNZI HAUKUBALIKI.

PUMZIKA KWA AMANI MTOTO MWEMA SPERIUS ERADIUS.


Sent using Jamii Forums mobile app
Siungi mkono hoja Tumeku na nidham mpaka tumefika hapa ctaki kua kijana wangu ni sehem ya taifa hilo kunamakosa ya kumuonya mtoto na kuna makosa ya viboko taratibu naona heshima ya mwalimu inapoteaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom