Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,690
- 20,445
Nimemfuatilia mtangazaji wa ITV bi. Farhia Middle mara kadhaa, nimeona pale anapokuwa amemaliza kusoma taarifa za habari za michezo amekuwa akiwabana vilivyo watangazaji wenzake wanazi wa vyura kama akina Kivuyo, ambao wamekuwa wakisoma habari za michezo bila kuzingatia uzito wa habari ya mjini kwa siku husika.
Mfano leo, Kivuyo amekomaa na habari za mashabiki wa Liverpool waishio Dodoma, wakati kuna tukio zito nchini la fainali ya Kombe la FA ambalo mshindi wake ataiwakilisha nchi katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Farhia amembana Kivuyo aizungumzie mechi ya leo, ila Kivuyo aliendelea kukwepakwepa lakini Simba ni kama maji, utayaoga usipoyanywa
Mfano leo, Kivuyo amekomaa na habari za mashabiki wa Liverpool waishio Dodoma, wakati kuna tukio zito nchini la fainali ya Kombe la FA ambalo mshindi wake ataiwakilisha nchi katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Farhia amembana Kivuyo aizungumzie mechi ya leo, ila Kivuyo aliendelea kukwepakwepa lakini Simba ni kama maji, utayaoga usipoyanywa