funzadume
JF-Expert Member
- Jan 28, 2010
- 13,559
- 21,036
kwako leo najitosa, yamoyoni kuyasema
nitajitenda makosa, kama nikikaa kimya
kwangu wazidi kipusa, wa-watoto wangu mama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
wazidi nipa hamasa, siku zinavyoyoyoma
Kwako mi nimenasa, siwezi kujitutuma
macho nilipepesa, kwako wewe yakakwama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Nakumbuka agosti, mwaka tisaina kenda
ukipita na mashosti, marafikizo mwaenda
moyo ulipigwa shoti, na kuzidi kunidunda
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
nilipojaribu kuita, sauti ilikatika
nilipatwa na utata, kwa kuona malaika
tamaa nikakata, ulipoenda hakika
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
siku zilijipitia, machoni sikukutia
ila nilijipa nia, la moyoni takwambia
mpaka napotea njia, nilipo kufukuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Andiko lilitimia, siku tulipokutana
la moyoni nikatoa, bila aibu kuona
nilitamani kulia, uliposema hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
kumbe hukumaanisha, ile yako hapana
ulitaka niondosha, utafakari kwa kina
baada ya wiki kwisha, ikawa ndio hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
nawashukuru wazazi, ua kunizalia
ya leo siku na mwezi, mke wangu kuzaliwa
kwa uwezo wa mwenyezi, anazidi nikuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Ningependa kukuenzi, kwa kukupa hii dunia
ila hilo siliwezi, uwezo haujatimia
ila takupa mapenzi, ufarahie malkia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Kaditama namaliza, sina cha kuongeza
zidi kuniliwaza, mapenzi yakupendeza
naahidi kukutunza, watoto kuwaongeza
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Funzadume mwana wa washawasha
Shairi ili nimemtungia mke wangu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa leo hii pamoja na shairi ili nimemnunulia zawadi nzuri sana na kilichoandikwa humu ni cha kweli kutoka moyoni mwangu
nimehamua kushare nanyi leo shairi ili kufuraia siku ya kuzaliwa mke wangu
nitajitenda makosa, kama nikikaa kimya
kwangu wazidi kipusa, wa-watoto wangu mama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
wazidi nipa hamasa, siku zinavyoyoyoma
Kwako mi nimenasa, siwezi kujitutuma
macho nilipepesa, kwako wewe yakakwama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Nakumbuka agosti, mwaka tisaina kenda
ukipita na mashosti, marafikizo mwaenda
moyo ulipigwa shoti, na kuzidi kunidunda
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
nilipojaribu kuita, sauti ilikatika
nilipatwa na utata, kwa kuona malaika
tamaa nikakata, ulipoenda hakika
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
siku zilijipitia, machoni sikukutia
ila nilijipa nia, la moyoni takwambia
mpaka napotea njia, nilipo kufukuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Andiko lilitimia, siku tulipokutana
la moyoni nikatoa, bila aibu kuona
nilitamani kulia, uliposema hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
kumbe hukumaanisha, ile yako hapana
ulitaka niondosha, utafakari kwa kina
baada ya wiki kwisha, ikawa ndio hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
nawashukuru wazazi, ua kunizalia
ya leo siku na mwezi, mke wangu kuzaliwa
kwa uwezo wa mwenyezi, anazidi nikuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Ningependa kukuenzi, kwa kukupa hii dunia
ila hilo siliwezi, uwezo haujatimia
ila takupa mapenzi, ufarahie malkia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Kaditama namaliza, sina cha kuongeza
zidi kuniliwaza, mapenzi yakupendeza
naahidi kukutunza, watoto kuwaongeza
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa
Funzadume mwana wa washawasha
Shairi ili nimemtungia mke wangu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa leo hii pamoja na shairi ili nimemnunulia zawadi nzuri sana na kilichoandikwa humu ni cha kweli kutoka moyoni mwangu
nimehamua kushare nanyi leo shairi ili kufuraia siku ya kuzaliwa mke wangu