Hongera mke wangu siku yako ya kuzaliwa 28/01

funzadume

JF-Expert Member
Jan 28, 2010
13,559
21,036
kwako leo najitosa, yamoyoni kuyasema
nitajitenda makosa, kama nikikaa kimya
kwangu wazidi kipusa, wa-watoto wangu mama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

wazidi nipa hamasa, siku zinavyoyoyoma
Kwako mi nimenasa, siwezi kujitutuma
macho nilipepesa, kwako wewe yakakwama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Nakumbuka agosti, mwaka tisaina kenda
ukipita na mashosti, marafikizo mwaenda
moyo ulipigwa shoti, na kuzidi kunidunda
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

nilipojaribu kuita, sauti ilikatika
nilipatwa na utata, kwa kuona malaika
tamaa nikakata, ulipoenda hakika
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

siku zilijipitia, machoni sikukutia
ila nilijipa nia, la moyoni takwambia
mpaka napotea njia, nilipo kufukuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Andiko lilitimia, siku tulipokutana
la moyoni nikatoa, bila aibu kuona
nilitamani kulia, uliposema hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

kumbe hukumaanisha, ile yako hapana
ulitaka niondosha, utafakari kwa kina
baada ya wiki kwisha, ikawa ndio hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

nawashukuru wazazi, ua kunizalia
ya leo siku na mwezi, mke wangu kuzaliwa
kwa uwezo wa mwenyezi, anazidi nikuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Ningependa kukuenzi, kwa kukupa hii dunia
ila hilo siliwezi, uwezo haujatimia
ila takupa mapenzi, ufarahie malkia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Kaditama namaliza, sina cha kuongeza
zidi kuniliwaza, mapenzi yakupendeza
naahidi kukutunza, watoto kuwaongeza
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Funzadume mwana wa washawasha

Shairi ili nimemtungia mke wangu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa leo hii pamoja na shairi ili nimemnunulia zawadi nzuri sana na kilichoandikwa humu ni cha kweli kutoka moyoni mwangu

nimehamua kushare nanyi leo shairi ili kufuraia siku ya kuzaliwa mke wangu
 
kwako leo najitosa, yamoyoni kuyasema
nitajitenda makosa, kama nikikaa kimya
kwangu wazidi kipusa, wa-watoto wangu mama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

wazidi nipa hamasa, siku zinavyoyoyoma
Kwako mi nimenasa, siwezi kujitutuma
macho nilipepesa, kwako wewe yakakwama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Nakumbuka agosti, mwaka tisaina kenda
ukipita na mashosti, marafikizo mwaenda
moyo ulipigwa shoti, na kuzidi kunidunda
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

nilipojaribu kuita, sauti ilikatika
nilipatwa na utata, kwa kuona malaika
tamaa nikakata, ulipoenda hakika
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

siku zilijipitia, machoni sikukutia
ila nilijipa nia, la moyoni takwambia
mpaka napotea njia, nilipo kufukuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Andiko lilitimia, siku tulipokutana
la moyoni nikatoa, bila aibu kuona
nilitamani kulia, uliposema hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

kumbe hukumaanisha, ile yako hapana
ulitaka niondosha, utafakari kwa kina
baada ya wiki kwisha, ikawa ndio hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

nawashukuru wazazi, ua kunizalia
ya leo siku na mwezi, mke wangu kuzaliwa
kwa uwezo wa mwenyezi, anazidi nikuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Ningependa kukuenzi, kwa kukupa hii dunia
ila hilo siliwezi, uwezo haujatimia
ila takupa mapenzi, ufarahie malkia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Kaditama namaliza, sina cha kuongeza
zidi kuniliwaza, mapenzi yakupendeza
naahidi kukutunza, watoto kuwaongeza
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Funzadume mwana wa washawasha

Shairi ili nimemtungia mke wangu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa leo hii pamoja na shairi ili nimemnunulia zawadi nzuri sana na kilichoandikwa humu ni cha kweli kutoka moyoni mwangu

nimehamua kushare nanyi leo shairi ili kufuraia siku ya kuzaliwa mke wangu


shairi limetulia! Nitakuomba uniandikie nami nataka mtokea mtoto wa Kiarabu
 
Hongera sana FD kwa ushairi mzuri mpe salam sana wife na sherehe njema ya bday
 
kwako leo najitosa, yamoyoni kuyasema
nitajitenda makosa, kama nikikaa kimya
kwangu wazidi kipusa, wa-watoto wangu mama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

wazidi nipa hamasa, siku zinavyoyoyoma
Kwako mi nimenasa, siwezi kujitutuma
macho nilipepesa, kwako wewe yakakwama
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Nakumbuka agosti, mwaka tisaina kenda
ukipita na mashosti, marafikizo mwaenda
moyo ulipigwa shoti, na kuzidi kunidunda
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

nilipojaribu kuita, sauti ilikatika
nilipatwa na utata, kwa kuona malaika
tamaa nikakata, ulipoenda hakika
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

siku zilijipitia, machoni sikukutia
ila nilijipa nia, la moyoni takwambia
mpaka napotea njia, nilipo kufukuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Andiko lilitimia, siku tulipokutana
la moyoni nikatoa, bila aibu kuona
nilitamani kulia, uliposema hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

kumbe hukumaanisha, ile yako hapana
ulitaka niondosha, utafakari kwa kina
baada ya wiki kwisha, ikawa ndio hapana
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

nawashukuru wazazi, ua kunizalia
ya leo siku na mwezi, mke wangu kuzaliwa
kwa uwezo wa mwenyezi, anazidi nikuzia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Ningependa kukuenzi, kwa kukupa hii dunia
ila hilo siliwezi, uwezo haujatimia
ila takupa mapenzi, ufarahie malkia
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Kaditama namaliza, sina cha kuongeza
zidi kuniliwaza, mapenzi yakupendeza
naahidi kukutunza, watoto kuwaongeza
Hongera mke wangu, siku yako kuzaliwa

Funzadume mwana wa washawasha

Shairi ili nimemtungia mke wangu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa leo hii pamoja na shairi ili nimemnunulia zawadi nzuri sana na kilichoandikwa humu ni cha kweli kutoka moyoni mwangu

nimehamua kushare nanyi leo shairi ili kufuraia siku ya kuzaliwa mke wangu

Shairi zuri limesimama haswa

Hongera nyingi kwa siku ya kuzaliwa mke wako kipenzi.
 
shairi limetulia! Nitakuomba uniandikie nami nataka mtokea mtoto wa Kiarabu
poa mtu wako ila waarabu chapa halafu kula kona ndg zake wakikustukia wanakurushia kichomi, hawatakaki waolewe na ngozi nyeusi wale
 
Hongera sana FD kwa ushairi mzuri mpe salam sana wife na sherehe njema ya bday
asante naona mmepishana siku chache kuzaliwa na wife wangu halafu amezaliwa siku moja na Preta what a coincidence
 
Aiseeeee im proud of you man! mpaka nimehic uchozi fulani hivi! mpe hongera sana wifey
 
Happy Birthday Mrs ......
Mungu akupe maisha marefu yenye baraka tele,mafanikio na amani.
 
Kumbe mkeo Preta?

Tumewagundua humu humu.

Hongera Preta katika siku yako ya kuzaliwa.
sidhani kama ni Preta maana kuna kipindi nilimpigia akaniambia yuko njiani halafu preta huku anarusha tu msg nikajua sio yeye atakuwa pacha wake
 
Kudos kwa shairi zuri mkuu FD ; naamini utaniruhusu nami nilitumie siku ikifika! Mfikishie zetu salamu; Tunamwombea Maisha marefu kama Mlima Kilimanjaro!
 
Kudos kwa shairi zuri mkuu FD ; naamini utaniruhusu nami nilitumie siku ikifika! Mfikishie zetu salamu; Tunamwombea Maisha marefu kama Mlima Kilimanjaro!
ruksa kulitumia ila itabidi ulichakachue baadhi ya mistari maana ili la kwangu linaelezea vitu ambavyo vilitokea siku za nyuma na ni la kweli mwenyewe Mrs kalisoma mpaka machozi alipomaliza nikampa simu ya Samsung Touch Screen alichanganyikiwa zaidi
 
Back
Top Bottom