Hongera mh. Waziri sitta

Tule

New Member
Dec 2, 2010
1
0
Kama watanzania wengi, nilikua napata wasiwasi kwa mh. Sitta kupelekwa wizara ya afrika mashariki. Hotuba aliyoitoa juzi hasa kipengele alichopendekeza kuwepo kugawana nafasi za kazi(quota system) katika jumuiya ya afrika mashariki (eac) kwa kweli kilionyesha mapenzi makubwa kwa watanzania na wengine wa jumuiya hiyo kwani imekuwa ni ya wakenya na waganda hasa nafasi nzuri na hili limekua lalamiko la watu wengi hasa arusha.

Hongera mh. Sitta, kweli wewe ni mtetezi wa watu. Kuingia kwako wizara hii sasa nimeona ni faraja na tumaini na usiachie hewani hakikisha hii jumuiya inakua ni ya manufaa kwa wote.

Hongera mh. Jakaya kikwete kwa kumteua mtu sahihi naamini hapa kazi itakwenda.
 
Ile nayo WIZARA gani? Kilipaswa kuwa kitengo tu pale Mambo ya Nje.

Kweli WC, sioni Tija ya hii wizara ingetakiwa iunganiswhe na wizara ya mambo ya Nje na awepo mtu competent kuimanage.
 
Kilipaswa kuwa moja ya kitengo cha EA na hakikuwa. Kwahiyo huyo aliyepewa kama anafanya kazi murua ni wajibu wa Wtz kumpa moyo.
Kwani Kenya na Uganda hawana wizara kama hii? Kama zipo, kwanini baadhi yetu hapo juu mlitaka hii iwe ni idara tu ya EA?
 
Back
Top Bottom