Hongera Mh Rais; Umeonyesha kuwa unawajali wananchi wako

Mmhh!!!!!!!!!!!!!
icon8.png
 
Sawa basi, pamoja na hayo angalau muwe mnamkumbusha awe anaonyosha masikitiko, ikiwezekana muwe mnamlambisha hata ndimu ili itoe lile tabasamu aweke kahuzuni kidogo, l.o.l!
 
Watanzania tunapenda sana maneno. Sasa hapa tunampongeza kwa kuwajali, anawajalije mbona mimi sijaelewa. Kuwaahidi viwanja ni kauli tulizozizoea na kama mnabisha kuhusu kauli za serikali yanapotokea majanga waulizeni wa Mbagala.

Ni kwa akili hizi hizi tulimpongeza kwa kusema 'kila mwananchi atapata fursa ya kutoa maoni' bila kufikiri nini kitasaidia ukitoa maoni ambayo hayatafanyiwa kazi. Hata ukipewa pole mia 4 kamwe hazitarejesha nyumba yako iliyosombwa na maji. Hotuba ni maneno tu.

Kwa wale mnaoamini kuwa serikali haipaswi kulaumiwa kwa watu kuishi mabondeni: Kama mnaamini serikali haina jukumu la kuwalazimisha watu kuwa salama, mbona serikali hii hii imetukataza kuandamana mara kadhaa kwa kujifanya inatujali tusishambuliwe na Al-shabaab? Maandamano yakipigwa marufuku tunaambiwa kwa manufaa na usalama wetu, lkn watu wa mabondeni wanajenga hawakatazwi, au mwanzo ilifikiriwa kuwa ni salama?

Jibu hapa ni kuwa serikali haina uwajibikaji wa pamoja. Ningeamini kuwa ina nia ya dhati ya kuhakikisha watu hawaishi mabondeni kama nisingeona supply ya huduma za umeme na maji kwa wakazi wa mabondeni. Kuwapelekea huduma hizi ni kuhalalisha makazi na kama haitoshi serikali imezisajili zile nyumba na zina namba. Sasa mbona hazikunyimwa usajili kama ni haramu?

Tuache kushangilia ngonjera wanaume
 

Kweli kuna watu wana skills za biashara na ni wepesi wa kubaini Business Opportunities, hapa kwenye hii picha naona kuna ambulance ya kampuni binafsi ya ulinzi imekaa tayaru tayari kula kichwa incase Dokta kaanguka.
 
Wakati huu wanajamiiforums tunapochukua muda wetu kumpongeza au kumlaumu Mhe. Rais, yafaa pia tujue hili ni janga sawa na yale yaliaotokea mikoani sambamba na hili au kabla yake. Huku ni kuendelea kujadili matukio ambayo chanzo chake ni mpinduzi yanayofanywa na madaraka dhidi ya mamlaka taifani, bila ya kuangalia kiini chake. Miaka 50 ya uhuru tumekomaa, tuanze kujadili mada/fikra zenye utekelezaji utakaozuia majanga, lawama au pongezi hazitotufikisha tunakotarajia.

"fikra ndogo hujadili watu, fikra za kati za Ubinadam hujadili matukio na fikra kuu za Utu/Watu hujadili mada/fikra"
 
JK-Jangwani.jpg

kikwete-mafuriko.jpg

kikwete-darajani.jpg

Rais Jakaya Kikwete akiangalia athari ya mafuriko ya Msimbazi katika eneo la Jangwani, Dar es Salaam leo wakati alipofanya ziara ya kukagua athari za mafuriko yaliyosababishwa na mvua zilizonyesha kwa siku mbili mfululizo jijini humo. Amewataka wahame. (Picha: Ikulu)

Huku kwetu kumpungia mtu kwa mkono wa kushoto ni madharau.
 
Mbunge wa Mafia kwa moyo aliouonyesha,,,tunataka safu ya viongozi wa juu wenye moyo kama yeye ...Tafadhali sana afikiliwe kwa Uongozi wa juu! Sio viongozi wanaonekana pale JK anapotembelea Wahanga wa mafuriko basi matumbo mbele ili waonekane kwenye vyombo vya habari..BIG UP MH. Mbunge.
 
Ally Hasan Mwinyi aliwapa viwanja 105 ili wahame waligoma, Yusuf makamba akiwa mkuu wa mkoa wa Dar akawapa wakagoma, je Kikwete utaweza waliposhindwa waliokutangulia? jana Kamanda Kova kasema wamesema mvua zikiisha watarudi mabondeni. kazi kweli kweli
 
Wakati wa Utawala wa Mwinyi baadhi ya wakazi wa mabondeni walilipwa fidia ili wahame na kupewa viwanja wakasema hawataki kuhamia nje ya mji hadi leo wako mabondeni na fedha za fidia zimeliwa.
 
wakazi wa mabondeni hakuanza wakati wa kikwete wapo tangu enzi za Nyerere, awamu ya Mwinyi wakaongezeka, awamu yaMkapa wakaongezeka zaidi na Kikwete ndio yamemfika anabeba zigo utadhani makazi ya mabondeni yameanza awamu ya nne..... tutende haki.
 
Jk anawajibika kama Rais wa nchi lakini tutende haki kwani awamu ya nne imekuta mabonde yamejaa wakazi. Ni vema tukashauriana namna ya kumaliza tatizo na Tibaijuka alianza lakini mbunge Zungu kamsimamisha mama kuwahamisha pengine haya yote yasingewafika. Watu wa haki za binadamu nao wakapiga kelele ili mradi kila mtu anasema lake.
 
Mbunge wa Mafia Shah ni wa CCM wale wa upinzani kazi yao kulalamika tu na wengine kusaidia na wale wa CCM kuomba nyongeza ya posho. Shah asante kwa ubunifu wako binafsi. tunakupenda kama unavyotupenda

Mbunge wa Mafia kwa moyo aliouonyesha,,,tunataka safu ya viongozi wa juu wenye moyo kama yeye ...Tafadhali sana afikiliwe kwa Uongozi wa juu! Sio viongozi wanaonekana pale JK anapotembelea Wahanga wa mafuriko basi matumbo mbele ili waonekane kwenye vyombo vya habari..BIG UP MH. Mbunge.
 
apongezwe? Kwa Faraja ya mikono mitupu? Angefanya la maana kuwalinda kwa dakika hii. Angekuja na misaada kama mahema,chakula, magodoro ambavyo vitawalinda waathirika kwa sasa kisha ndo atoe na hzo ahadi hewa za viwanja. Tanzania, fungukaaaa....!


KWA nini asipongezwe? asingetokea mngesema katokea mnasema duuuu,binadamu haishi kulalama

"Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam tayari umeandaa eneo la ekari 200
lenye viwanja 2,800 katika wilaya ya Kinondoni"
 
Dr Slaa na Mbowe walishindwa kukodisha mitumbwi kusadiana na serikali kuokoa wananchi? Kipimo kimeanza mapema je tukiwapa Ikulu?
 
Big up JK zigo hilo wamekutwisha waliotangulia libebe wape viwanja kama watakubali kuhama ni jambo lingine

KWA nini asipongezwe? asingetokea mngesema katokea mnasema duuuu,binadamu haishi kulalama

"Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam tayari umeandaa eneo la ekari 200
lenye viwanja 2,800 katika wilaya ya Kinondoni"
 
Itifaki ya ulinzi wa afya ya Rais imechelewa sana hapa Tanzania wenzetu ulinzi wa afya ya Rais ipo mpaka kwenye ndege kama vile Airforce One ya Rais wa marekani lakini pia baadhi ya magari ya viongozi wa baadhi ya nchi tajiri duniani gari ya Rais kwa ndani ni ambulance pia kwa maana kwamba limejitosheleza kwa zana na vifaa mbalimbali endapo afya ya mkuu wa nchi itateteleka.


Kweli kuna watu wana skills za biashara na ni wepesi wa kubaini Business Opportunities, hapa kwenye hii picha naona kuna ambulance ya kampuni binafsi ya ulinzi imekaa tayaru tayari kula kichwa incase Dokta kaanguka.
 
Ukiona mtu analia sana msibani anaweza kuwa ndiye mchawi mwenyewe nani kasema mwenye kulia sana msibani ndiye mwenye uchungu kushinda wengine.

Sawa basi, pamoja na hayo angalau muwe mnamkumbusha awe anaonyosha masikitiko, ikiwezekana muwe mnamlambisha hata ndimu ili itoe lile tabasamu aweke kahuzuni kidogo, l.o.l!
 
Back
Top Bottom