Hongera Marando kwa kumpangua Masati:Vita ni Vita Muraa

Simple

JF-Expert Member
Feb 6, 2009
249
121
Pongezi zangu kwako Bwana Marando kwa kupangua hukumu ya kipambavu na ya uonevu aliyoitoa Jaji Masati kwenye kesi ya Nguza family.
Jaji Masati ni mtu makini, mwenye uzoefu mkubwa wa sheria, mcha Mungu na asiyekuwa biased. Lakini ilipofika kwenye kesi hii,,mzee huyu alichemsha mno kwa kutumia jazba, upendeleo kwa upande wa mashitaka na kutoa hukumu upesi upesi bila kuzingatia uzito wa kesi yenyewe.(Sijui alishinikizwa au utashi wake ndo uliishia pale)
Binafsi nilikuwepo Kisutu siku Nguza family wanahukumiwa jela ya maisha, niliingiwa na mshtuko mkubwa baada ya Jaji yule kumaliza kusoma hukumu yake kwa maneno ya jazba na chuki.

Pongezi zangu kwa Marando kwanza kabisa kwa kuisaidia familia ya Nguza kutendewa haki( vijana wawili wako nje sasa), pili kwa kuanisha upuuzi wa Jaji Masati.

Sijui Jaji huyu anajisikia hivi sasa, ukizingatia amewapotezea vijana wale wawili miaka saba, ambayo walifungwa. Wangekuwa wanawe sijui angejisikiaje?

Imefika kipindi sasa, waTanzania tuachane na sheria za jazba na uonevu na kuiacha haki isimame.
Aliyekosea aadhibiwe TU pale inapothibitika beyond reasonable doubt, sio kutumia mitazamo binafsi.

Mapambano yanaendelea Marando,,usikate tamaa...kama vipi wapeleke kina papii wakafungwe Congo maana hapo Bongo ngoma yao ishakuwa ingwe.
 
Huna uhakika na unachokiongea na pia huna ufahama wa kile unachokizungumza. Hiyo haitoshi bado wewe si mkweli. Unasema Jaji Masati ndio alimuhukum babu Seya? Km unakumbukumbu nzuri utakumbuka kuwa Jaji Masati alikuwa miongoni mwa majaji waliosikiliza rufaa ya kesi ya kina Seya.
 
Huna uhakika na unachokiongea na pia huna ufahama wa kile unachokizungumza. Hiyo haitoshi bado wewe si mkweli. Unasema Jaji Masati ndio alimuhukum babu Seya? Km unakumbukumbu nzuri utakumbuka kuwa Jaji Masati alikuwa miongoni mwa majaji waliosikiliza rufaa ya kesi ya kina Seya.

na wewe hujui .Jaji Masati alikuwa mwenyekiti wa jopo la majaji hao..
 
na wewe hujui .Jaji Masati alikuwa mwenyekiti wa jopo la majaji hao..

Na wewe pia huna unalolijua,kwenye mahakama ya rufaa JAJI NATALIA KIMARO ndio alikuwa mwenyekiti,jana nilisaidia kupost nakala ya hukumu hiyo,tafuta thread iliyoandikwa HUKUMU YA BABU SEYA HII HAPA usome,na wewe mwenye thread hii Jaji MASSATI hajamuhukumu Babu SEYA kule Kisutu aliyemhukumu ni hakimu anaitwa mama Lyamuya.,tena ujue hao jamaa hawawezi kupelekwa KONGO
 
Ndio sababu ya kuweka appellate machinery ili kuondoa matatizo kama haya. Mara nyingi interpretaion ya sheria na ushahidi sio straight forward hivyo na maamuzi ya majaji/mahakimu wawili yanaweza kuwa tofauti.
 
Na wewe pia huna unalolijua,kwenye mahakama ya rufaa JAJI NATALIA KIMARO ndio alikuwa mwenyekiti,jana nilisaidia kupost nakala ya hukumu hiyo,tafuta thread iliyoandikwa HUKUMU YA BABU SEYA HII HAPA usome,na wewe mwenye thread hii Jaji MASSATI hajamuhukumu Babu SEYA kule Kisutu aliyemhukumu ni hakimu anaitwa mama Lyamuya.,tena ujue hao jamaa hawawezi kupelekwa KONGO

mwenyekiti wa kijiji chenu au
 
Back
Top Bottom