Nimekuwa nikifuatilia sana siasa za ndani ya nchi yetu. Katika kipindi hiki hadi tarehe 12-11-2012 siku ambayo itakuwa ni mwisho wa uchaguzi wa ndani wa CCM(kama ratiba inavyoonesha), mengi yamesemwa juu ya hatma ya CCM na baadhi ya wagombea.
Kama kuna mgombea aliyesemwa sana katika mchakato huu, si mwingine bali ni mbunge wa Monduli Mhe. Edward Lowassa. Wapo waliokuwa wanasema, mabadiliko ya katiba ya CCM yalikuwa na lengo la kumwondoa/ kumzibia njia Lowassa. Waswahili wana msemo wao wa busara kabisa kuwa "wa mbili ni wa mbili, havai moja" na wengine husema "lililopangwa na Mungu, binadamu hawezi kulipangua" na pia "asiyekuwemo haingii, na aliyemo hatoki". Kusemwa kwa Lowasa ni muendelezo wa siasa za CCM kuelekea 2015. Binafsi hajaweka wazi kama atagombea urais 2015, na kila anapoulizwa husema "tutavuka daraja pindi tutakapoufikia mto"
Vikao vya uamuzi vya CCM vimemalizika. Jina la Lowassa limepitishwa kugombea nafasi ya U-NEC kupitia wilaya yake ya Monduli. Pamoja nae wapo Dr Salash Toure na kijana Nanai Konani. Mi si mtabiri wa kujua nani atafanikiwa kuwa M-NEC kutoka Monduli, ila ninachoweza kusema ni kuwa CCM wamekata ngebe za watu waliokuwa wanavumisha taarifa za uongo kuwa mwisho wa Lowasa katika siasa za CCM umefikia, kwa kuwa hataruhusiwa kugombea ujumbe wa NEC. Wapo wanaosema kuwa CCM imekata majina ya wagombea U-NEC wengi waliokuwa wanamtandao wa Lowasa. Inawezekana habari hii ikawa kweli, maana wanaojua ni CCM wenyewe. Ila tukumbuke kuwa: KAMA IPO, IPO TU
Nimalizie kusema kuwa "chochote tulicho nacho, hatujapata kwa ujanja wetu, bali ni makusudi ya Mungu". Kama Mungu amepanga Lowasa kuwa M-NEC atakuwa tu. Na kama amepanga Lowasa kuwa Rais, atakuwa tu. Hakuna wa kuzuia mipango ya Mungu.
Kama kuna mgombea aliyesemwa sana katika mchakato huu, si mwingine bali ni mbunge wa Monduli Mhe. Edward Lowassa. Wapo waliokuwa wanasema, mabadiliko ya katiba ya CCM yalikuwa na lengo la kumwondoa/ kumzibia njia Lowassa. Waswahili wana msemo wao wa busara kabisa kuwa "wa mbili ni wa mbili, havai moja" na wengine husema "lililopangwa na Mungu, binadamu hawezi kulipangua" na pia "asiyekuwemo haingii, na aliyemo hatoki". Kusemwa kwa Lowasa ni muendelezo wa siasa za CCM kuelekea 2015. Binafsi hajaweka wazi kama atagombea urais 2015, na kila anapoulizwa husema "tutavuka daraja pindi tutakapoufikia mto"
Vikao vya uamuzi vya CCM vimemalizika. Jina la Lowassa limepitishwa kugombea nafasi ya U-NEC kupitia wilaya yake ya Monduli. Pamoja nae wapo Dr Salash Toure na kijana Nanai Konani. Mi si mtabiri wa kujua nani atafanikiwa kuwa M-NEC kutoka Monduli, ila ninachoweza kusema ni kuwa CCM wamekata ngebe za watu waliokuwa wanavumisha taarifa za uongo kuwa mwisho wa Lowasa katika siasa za CCM umefikia, kwa kuwa hataruhusiwa kugombea ujumbe wa NEC. Wapo wanaosema kuwa CCM imekata majina ya wagombea U-NEC wengi waliokuwa wanamtandao wa Lowasa. Inawezekana habari hii ikawa kweli, maana wanaojua ni CCM wenyewe. Ila tukumbuke kuwa: KAMA IPO, IPO TU
Nimalizie kusema kuwa "chochote tulicho nacho, hatujapata kwa ujanja wetu, bali ni makusudi ya Mungu". Kama Mungu amepanga Lowasa kuwa M-NEC atakuwa tu. Na kama amepanga Lowasa kuwa Rais, atakuwa tu. Hakuna wa kuzuia mipango ya Mungu.