Hongera kwa Rais kwa kuwaziba mdomo wapinzani kuhusu kuungua kwa Soko la Karume

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Apr 19, 2021
1,502
4,408
Binafsi nimeshangazwa na ukimya wa wapinzani baada ya tukio la kuungua moto soko la Karume. Sijasikia pole yoyote kutoka kwa upinzani si CHADEMA wala ACT walioneshwa kusikitishwa na jambo hilo. Ni kimya kikuu kimetanda.

Ni wapinzani hawa hawa ambao polisi wakidhibiti mikusanyiko yao haramu wanapiga kelele na pengine hao waliounguliwa wakiwashawishi kushiriki lakini walipounguliwa soko wapo kimya. Kwa nini?

Kinachonishangaza, Mwenyekiti wa CCM alipoonesha yupo pamoja nao wamejazwa mitandaoni kuonesha hakuwa pamoja nao toka mwanzo kitu ambacho si kweli.

Je, kulikuwa na mpango gani uliopangwa na kuungua kwa soko la karume? Je, ni kwa nini maamuzi ya Mwenyekiti wa CCM yameonesha kuwakera wapinzani? Je, ni kwa nini hawajaonesha kusikitishwa na kuungua kwa soko la karume?

Wapinzani walikuwa wanataka sababu ya kusema wamekosa. Wapinzani walitengenezea jamii mtazamo hasi juu ya kuungua kwa masoko kwamba ni kazi ya 'kupangwa kutokea ndani' ili kuwaondosha. Wapinzani walisambaza taarifa za uzushi na uongo kwamba karume amepewa mwekezaji.

Wapinzani walifanya hayo yote kwa mtazamo wa kutengeneza chuki. Walitaka wasikie taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wetu kwamba wamachinga hawatakiwi tena karume lakini haikuwa hivyo.

Walifurahi kuona wakiandamana lakini haikuwa hivyo, ukimya wa upinzani ulikuwa na mengi yasiyoelezeka ila yote kwa yote Mungu amemjalia hekima Rais wetu kwa kuamua kwa utashi.

Tunampongeza sana Rais wetu kwa maamuzi ya hekima na busara iliyotumika kufika muafaka. Ameonesha kuwa ni mfariji katika mengi. Ametufariji na kututia moyo.
 
Binafsi nimeshangazwa na ukimya wa wapinzani baada ya tukio la kuungua moto soko la Karume. Sijasikia pole yoyote kutoka kwa upinzani si CHADEMA wala ACT walioneshwa kusikitishwa na jambo hilo. Ni kimya kikuu kimetanda...
Nadhani bado hujitambui au unatudanganya hujui.Inaelekea ndio unaamka usingizini unatafuta shuku,ulipopiga jicho dirishani ukakuta pamekucha.

Umeandika machapisho mareeefu, yasiyokuwa na chochote, kama unajua kuandika,jua pia na kusoma ujue.Vyote vinaenda pamoja. Hata kama hutaki kusoma,omba upitishwe haraka haraka kwenye mitandao ili uone kelele za vyama vya upinzani na masikitiko yao na pole nyingi kwa waliounguziwa vitu vyao.

Kama sio hizo kelele na matamshi yao hili la soko la Karume lingepita hivi hivi. Ilipoonekana tayari kwenye negative hakuna picha kumbe tayari filim ilishaungua.

Baada ya kuungua hiyo filim ukatafutwa utaratibu wa kuua ukweli wa jambo lenyewe.Ilisikitisha sana na watanzania wakatambua ni kweli maviatu hayajui PGO. Just imaging mmachinga kapoteza kila kitu,kaomba msaada mdogo kwa ndugu na marafiki zake,kaanza kuweka nguzo kwa gharama zake halafu anafukuzwa eneo hilo tena kwa mabomu ya machozi, utu wa mtanzania uko wapi.

Hili tukio waliohusika kuwapiga mabomu ya machozi wachukuliwe hatua wamemisuse kodi za watanzania.Ni vizuri kuwapa misaada ili warudi walipokuwa.Ila hili lilipashwa kufanyika kabla ya watu kupiga kelele wakisaidiwa na vyama vya upinzani na wanaharakati mbalimbali.

Huu uwe mwendelezo pia wa kukomesha matendo mengine maovu kama ya vijana wetu 5 ambao mpaka sasa serikali haijasema waliko hawa vijana wetu.

Mtoa mada asidhani kuwa, kila anayetoa mawazo au anaye comment kinyume na mawazo yake humu ni CHADEMA, Ukifanya vibaya unaambiwa wazi siku hizi bila kujali yupo chama gani.Ila akitaka aendelee kukipaaisha Chama chake cha CHADEMA.

Ahsanteni sana kwa kelele zenu zimezaa kilichotokea.Ila isijeonekana ni matayarisho ya 2025.Hizo fedha ni kodi za watanzania,ni fedha za maafa ndio kazi zake.Hazijatoka mfukoni kwa mtu.Ni sawa na mtu aliyeweka akiba sasa anaitumia.Hiyo siyo....................
 
Back
Top Bottom