Hongera kamanda Mpinga

Sep 4, 2016
44
28
Jamani wadau ni kwamba napenda kumpongeza kamanda w kikosi cha usalama barabarani kamanda Mpinga. Naomba tu atupe statistics za ajari barabarani hasa za mwezi December kwa miaka kumi hivi. Ni wazi kabisa mwaka jana 2016 utakuwa ni mwaka ambao umekuwa na matukio machache ya ajari barabarani kwa mwezi december kuliko miaka yote iliyopita (base line ni miaka kumi iliyopita). Hii ni kutokana na uongozi mzuri sana wa huyu kamanda.

Pili nataka kulipongeza Jeshi la polisi kwa kazi nzuri maana matukio ya wizi au kuuwawa kwa albino hayasikiki, hii ni kutokana na uongozi mzuri na wenye kujituma kwa kweli mnahitaji pongezi kwa mafanikio ya mwaka 2016.

Rushwa pia imepungua sana ingawa rushwa ni tabia ya mtu mmoja mmoja lakini polisi wanajitahidi kutoomba rushwa, wako vichwa ngumu ambao wanaendelea kudai rushwa lakini generally wengi kwa asilimia 99% wanajiheshimu na kuridhika na mishahara yao.

Maoni yangu ni kwamba naomba wakuu wa vituo vya polisi wawe innovators, wavipende vituo vyao vya kazi na wajitahidi kuviendeleza. Unakuta kituo kichafu utazani kazi inaisha kesho. Tandabui, vumbi kibao, mabenchi wanayokalia yamevunjika vunjika, hawana hata saa za ukutani za kumjulisha mahabusu ameletwa mda gani kituoni. Jamani hee, tuipende kazi yetu na tuithamini. Kama mkuu tafuta hela hata kwa kuchangisha kwa wafanyakazi ili mnunue saa za ukutani, changisha upate viti na kadhalika. Weka mahitaji muhimu kwenye budget ya kwaka, pia kuna vimiladi vidogo vidogo anzisheni ili mboleshe mazingira ya kazi. Msitegemee serikali, serikali ina mambo mengi.

Mwisho niwapongeze viongozi wote wa nchi hii wa awamu hii ya hapa kazi tu. Msiwe na hofu tunawaombea jamani. Msiangalie upepo hamtapanda nyie piga kazi. Kazi kwanza vyama baadae. Hapendwi mtu ila kazi. Kama hufanyi kazi hutapendwa hata uwe nani, hapa is job only
 
Back
Top Bottom