Wanabodi,
Nimekutana na bandiko hili
lenye tuhuma lukuki dhidhi ya kiongozi huyu..
Ukisikia majungu ndio haya. Ukituhumu humu, leta na uthibitisho.
Hapa umevurumisha tuhumu lukuki dhidi ya Biteko-
Tuhuma zenyewe ni hizi
Mode: JF tuweke standards za kulinda heshima na majina ya watu, dhidi ya mtu kuchafuliwa jina kwa chuki binafsi. Iongezwe kanuni, mtu ukileta tuhuma za mtu yoyote au kiongozi yoyote kwa jf as a whistleblower, lazima tuhuma hizo ziandamane na uthibitisho, ndipo jina la mtuhumiwa litajwe, kumtuhumu mtu kwa kumtaja kwa jina, bila ya uthibitisho wowote, ni kuchafua tuu bure majina ya watu.
- Dotto Biteko ameiba kiasi kikubwa cha pesa, kiasi gani?-Ni tuhuma tuu, hakuna uthibitisho!.
- Dotto Biteko ni mshirika usafirishaji madini ya Tanzanite kwa njia za panya kwa kushirikiana na wafanyabiashara. How?. Ni tuhuma tuu hazina uthibitisho wowote?.
- Dotto Biteko anaiba madini mengi, ameibaje, ameiba wapi, madini yapi, - Ni tuhuma tuu, hakuna uthibitisho wowote.
- Dotto Biteko ana percentage kwenye migodi kibao, percentage ngapi, migodi gani?-Ni tuhuma tuu hazina uthibitisho wowote!.
- Dotto Biteko ni jangili wa mwendazake!. Ujangili gani?, unamtukana marehemu na kumsingizia ujangili?!, hii ni dhambi!.
- Doto Biteko kila siku anashinda kwa waganga, waganga gani?, hili la mtu kushinda kwa waganga pia linaingilia the right to privacy ya mtu, kama watu wanaoshinda hospitali, makanisani, nyumba za ibada a makanisa ya walokole, haya ni mambo ya imani, Tanzania tuko huru kuamini lolote, waumini wa Mungu washinde makanisani, waumini wa tiba za kizungu washinde mahospitalini, waumini wa dini za asili, tushinde kwa mizimu na waganga wa kienyeji, tusiingilie privacy za watu!.
Najua JF as a whistleblower, imefanya kazi nzuri na inaendelea kufanya kazi nzuri, lakini na sisi sasa ni lazima tubadilike, kwenye tuhuma, lazima tufanye a due diligence kwa kuhakikisha tunafuata sheria, taratibu na kanunu, "the one who alleges, must prove", ukileta tuhuma zozote za hearsay bila uthibitisho, yes zilete, as a whistleblower, but don't mention names without proof. Yaani leta tuhuma, lakini usitaje majina bali taja tuu cheo na indications zote ambazo zita point kwa mhusika bila kumtaja jina na kumchafua bila uthibitisho wowote!.
Nimetokea kumfahamu mtuhumiwa huyu kupitia kazi yangu ya uandishi, kwa mambo anayoyafanya hadharani, huyu ni mmoja wa wazalendo wa kweli wa taifa hili.
Msikilize Dotto Biteko kwenye video hii.
Ukimsikiliza Biteko, utakubaliana na mimi, huyu ni mzalendo wa kweli wa nchi hii, kumtuhumu kwa tuhuma lukiki bila ushahidi wowote au uthibitisho wowote, sio kumtendea haki.
Hongera sana wana jf kwa kwa kazi kubwa nzuri ya Whistleblowing, ila sasa tubadilike, tukitoa tuhuma, tulete na uthibitisho kuepuka kuchafua bure majina ya watu.
Paskali.
P kwani wewe mtu wa usalama? Mtoa taarifa alikuwa na nia gani? Kumchafuwa waziri au ku alert umma na taasisi nyeti zenye mamlaka kufanya uchunguzi? Mimi nadhani mtoa taarifa mara zote hatoi full details ili msije kumtambuwa anatoa story fulani ambapo investigater akipewa anajuwa apite wapi. Mimi ningeshauri tukae kimya ukweli utajulikana. Kitendo cha wewe kuanza andika nakuchambuwa taarifa ya mtoa taarifa nikuonekana wazi umetumwa na hili laweza kukusumbuwa mbeleni. End