Hongera Dkt. Charles Msonde, mbinu ulizotumia katika mitihani hii ya darasa la 7 ni zaidi ya TISS

Kajeba

JF-Expert Member
Oct 15, 2020
820
1,961
Wakuu,

Leo watoto wetu wa darasa la saba wamehitimu elimu yao ya msingi kwa kufanya mitihani ya taifa kama ilivyo kawaida chini ya NECTA inayoongozwa na katibu wake Dkt Charles Msonde.

Picha lilianza siku ya jumatatu ambapo iliripotiwa kwamba kuna watu wawili walikamatwa kwa tuhuma za kusambaza mtihani ambao ulitakiwa kufanyika siku ya jumatano na biti kali sana likatolewa dhidi ya wale wote ambao watajihusisha na vitendo vya udanganyifu

Zaidi hii ndio nimeiona ni zaidi ya mbinu za kiTISS, inasemekana kwamba mithani wa somo la kiswahili ulikuwa wa aina mbili
Yaani mkondo A ulifanya mtihani tofauti na mkondo B! Hakika hapa umekusudia kufanya na kubaini jambo fulani la udanganyifu endapo litajitokeza. Hii taarifa nimeipata baada ya kuuliza watoto kutoka shule tofauti na mikondo A na B

Lakini pia naiona NECTA ya Msonde ikijidhatiti zaidi kukomesha udanganyifu katika maswala ya mitihani kwani Msonde alienda mabali zaidi na kuanzisha kamati ya mitihani kwa ngazi ya kila wilaya na mkoa huku zikiongozwa na maafisa elimu, maafisa wa jeshi la polisi na maafisa usalama wa taifa kwa lengo la kuhakikisha usalama wa uandaaji, usambazaji na ufanyikaji wa mitahani hapa nchini katika level mbalimbali

Pia ile hali ya kuchanganya wasimamizi wa Primary na Secondary umetia fora nashauri uendelezwe ili kupunguza mazoea miongoni mwa wasimamizi kitu ambacho hupelekea kuvuja kwa mitihani.

Natumia jukwaa hili kukupongeza Dkt Charles Msonde kwa kazi yako nzuri ndani ya baraza la mitihani la taifa NECTA!
 
Kuna jamaa alifanya u FBI form six sitamsahau.

Kuna ile kasumba makaratasi ya kujibia maswali yanawekwa kwenye meza kabla ya watahiniwa kuingia kwenye chumba cha mtihani.

Mnapoingia tu, anachukua karatasi ya kujibia maswali kutoka kwenye meza yeyote. Mkisha tulia karatasi za maswali zinafunguliwa, mnagawiwa, baada ya kama dakika 10 au 15 anaomba ruhusa kwenda msalani, hapo anatoka na karatasi ya maswali na ile ya kujibia akiwa amezificha.

Akifika huko anaziacha, kisha vijana wa kidato cha tano walioko bwenini wanazichukua na wanajibu huku wakitumia rejea za vitabu kwa kuwa hawana ulinzi. Wakimaliza, wanairudisha pale pale maliwatoni.

Jamaa muda ukikaribia kwisha, anaomba ruhusa tena, anaenda kuchukua karatasi yake yenye majibu anakuja kuikusanya.

Alifanya hivyo mitihani yote akaambulia Div 2 ya PCB. Na hapo alikua amepigwa adhabu ya kutokuonekana shule arudi siku ya mtihani tu, hayo ndio mandingo aliyokuja nayo.

Nimesoma hii habari ya NECTA nikajikuta namkumbuka huyo mwamba...
 
Kuna jamaa alifanya u FBI form six sitamsahau.

Kuna ile kasumba makaratasi ya kujibia maswali ysnawekwa kwenye viti vya watahiniwa kabla ya watahiniwa kuingia...
kuna mbinu mmoja zamani shuleni kwetu tulitumia kujibu maswali ya kuchagua A,B,C,D,E.

Tuliongea kama hujui jibu gani uchague unanyooyoosha kidole msimamizi akusomee,mfano hujui swali la 7 utasema naomba unisomee swali la 7,akimaliza anayejua jibu ananyoosha kidole na kusema "naomba nisomee swali la 7 C " hapo jibu ndo C halafu na msimamizi anakusomea.
 
Kiukweli hata kama kuna mapungufu basi ni ya kibidamu. Kuna shule fulani fulani hapa mjini maafisa usalama ngazi ya wilaya na mkoa walikuwa hawakauki.

Ni jambo jema katika kuongeza umakini wa zoezi lenyewe na kupunguza ubadhilifu.

Pia ile hali ya kuchanganya wasimamizi wa Primary na Secondary umetia fora nashauri uendelezwe ili kupunguza mazoea miongoni mwa wasimamizi kitu ambacho hupelekea kuvuja kwa mitihani.
 
kuna mbinu mmoja zamani shuleni kwetu tulitumia kujibu maswali ya kuchagua A,B,C,D,E.

Tuliongea kama hujui jibu gani uchague unanyooyoosha kidole msimamizi akusomee,mfano hujui swali la 7 utasema naomba unisomee swali la 7,akimaliza anayejua jibu ananyoosha kidole na kusema "naomba nisomee swali la 7 C " hapo jibu ndo C halafu na msimamizi anakusomea.

Hapo ndio hua nachoka, akili kubwa inatumika kutatua tatizo dogo...unajiuliza kama mtu ameweza kukaa akapanga huu mpango kabambe wa kimkakati namna hii, anaogopa nini mtihani, hiyo akili akisoma si anajibu bila shida?
 
Kwani kuiba mitihani ni sifa? hili taifa sijui linaelekea wapi.

Halafu wageni wakija kuajiriwa kwenye nafasi nyeti tunapiga kelele wazawa wanaonewa, kama wazawa wenyewe ndio hawa wanabuniwa mbinu wasiibe mitihani bora wageni wapewe hizo kazi.
 
Hapo ndio hua nachoka, akili kubwa inatumika kutatua tatizo dogo...unajiuliza kama mtu ameweza kukaa akapanga huu mpango kabambe wa kimkakati namna hii, anaogopa nini mtihani, hiyo akili akisoma si anajibu bila shida?
ni uvivu tu halafu mfumo wetu wa elimu kuna masomo mengi yote mtu anatakiwa ayafahamu na pia hata wasahihishaji ni watu wa kukariri majibu
 
Hii pia ngoja niiongeze mkuu
Kiukweli hata kama kuna mapungufu basi ni ya kibidamu. Kuna shule fulani fulani hapa mjini maafisa usalama ngazi ya wilaya na mkoa walikuwa hawakauki.

Ni jambo jema katika kuongeza umakini wa zoezi lenyewe na kupunguza ubadhilifu.

Pia ile hali ya kuchanganya wasimamizi wa Primary na Secondary umetia fora nashauri uendelezwe ili kupunguza mazoea miongoni mwa wasimamizi kitu ambacho hupelekea kuvuja kwa mitihani.
 
Back
Top Bottom