Hongera dk. Joyce ndarichako, wizara ya elimu walimu wa sekondari kusimamia mtihani darasa la 7

MAMA POROJO

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
4,974
785
Wanafunzi zaidi ya laki 8 wa darasa la 7 wataanza mitihani yao kesho. wanafunzi hao ni kutoka zaidi ya shule za msingi elfu 13 kote nchini.

Hatua ya walimu wa sekondari kutumika kusimamia mtihani huo ni ya kupongezwa kwani inaboresha usimamizi makini. Mwanafunzi bora wa elimu ya msingi anatendengeneza mwanafunzi bora wa sekondari. Natumaini walimu wa sekondari watakuwa makini ili wapate wanafunzi bora watakaochaguliwa kwenda sekondari.

Hatua ya mitihani kusahihishwa kwa kompyuta kama ilivyo kwa nchi zingine kama Ghana na Afrika kusini kutapunguza ' human errors' hasa malalamiko ya upendeleo. Wakati wa kusahihisha mtihani walikuwa wanahitajika waalimu zaidi ya 3000 kuwekwa kwenye kituo kimoja na kulipwa posho kwa siku 60 lakini sasa mtihani utasahihishwa kwa siku 21 tu kwa komptuta.

Kila jambo lina changamoto zake lakini huu ni mwanzo mzuri.

source: Naibu waziri wa Elimu Mh. Mulugo, Radio One na Baadhi ya magazeti ya leo.

Mods: wameondoa thread hii kwenye jukwaa la siasa lakini siasa ndizo zimetufikisha kulalamiko kwenye mambo ya msingi na waliozungumza haya ni wanasiasa. kuna wanaotumia jukwaa la kisiasa kuomba kura za wananchi kwa kuzungumza mapungufu ya serikali likiwemo suala la mitihani.
 
Atakayefeli na ashindwe kihalali, wala hakuna kutafuta sababu!! Kilaza kilaza, anazo anazo.
 
Kumpyuta inasahihisha namba sio helufi kwa mujibu wa Waziri.

My take: Kompyuta haisahihishi majina, kabila wala dini ya mwanafunzi hii itapunguza malalamiko tuliyozoea kusikia lakini sasa mwanafunzi dhaifu hatakuwa na kimbilio kwamba amefelishwa na binadamu..... nadhani itapunguza malalamiko ingawa kwa hatua ya awali haiwezi kuondoa malalamiko yote.
 
Atakayefeli na ashindwe kihalali, wala hakuna kutafuta sababu!! Kilaza kilaza, anazo anazo.


Itapunguza sana visingizio lakini pia itatupatia wanafunzi bora. hatua hii imekuja wakati wake na itatoa majibu ya malalamiko ya nyuma kama yalikuwa sahihi au hapana.
 
Kumpyuta inasahihisha namba sio helufi kwa mujibu wa Waziri.

My take: Kompyuta haisahihishi majina, kabila wala dini ya mwanafunzi hii itapunguza malalamiko tuliyozoea kusikia lakini sasa mwanafunzi dhaifu hatakuwa na kimbilio kwamba amefelishwa na binadamu..... nadhani itapunguza malalamiko ingawa kwa hatua ya awali haiwezi kuondoa malalamiko yote.


Ha ha ha ha ha! Nasubiri kuona wale jamaa wa dini itakuwaje safari hii. Sijui kompyuta na mfumo utawaonea tena? Matokeo haya yatazua tena maandamano? Yetu macho.
 
Kompyuta imekuja duniani kupunguza ' human errors' ni wakati sasa na sisi kuingia kwenye mfumo huo.

Kwa miaka mingi tumekuwa tunaangalia matokeo ya mtihani bila kuangalia namna bora ya kuandaa wanafunzi hao. Dawa ya kusahihisha imepatikana sasa turudi nyuma je wanafunzi watapata kisingizio kipi?

Waziri kasema wale wanafunzi walifutiwa mitihani mwaka jana zaidi ya elfu 9 watafanya mtihani mwaka huu lakini hii itakuwa mara ya mwisho kurudia mitihani kwa wanafunzi wezi wa mitihani kwani wizi ni dhamira hivyo haitawezekana kila mwaka wezi hao wapatikane na kurudia mitihani na waalimu watakaoshiriki wizi wataathibiwa.
 
Itapunguza sana visingizio lakini pia itatupatia wanafunzi bora. hatua hii imekuja wakati wake na itatoa majibu ya malalamiko ya nyuma kama yalikuwa sahihi au hapana.

Pengine mwanafunzi bora atatoka shule za wale jamaa kwani visingizio vya mfumo vitakuwa vimekwisha. Subiri uone watoto waliopewa malezi bora ya kiroho, kimwili, na kisaikolojia wanavyochana pepa ile mbaya.
 
Ha ha ha ha ha! Nasubiri kuona wala jamaa wa dini itakuwaje safari hii. Sijui kompyuta na mfumo utawaonea tena? Matokeo haya yatazua tena maandamano? Yetu macho.
Mkuu kompyuta ni kipokea amri tu na kufanya kama amri zinavyosema kwa hiyo unaweza kulitegemea kompyuta kumbe limepewa amri sivyo ndivyo!! Tusubiri tujionee!!
 
Mkuu kompyuta ni kipokea amri tu na kufanya kama amri zinavyosema kwa hiyo unaweza kulitegemea kompyuta kumbe limepewa amri sivyo ndivyo!! Tusubiri tujionee!!

Asante Mkuu. Hata kama ni amri, hilo likompyuta limepewa amri ya kuonea wengine na kupendelea wengine tu? Hiyo kali.
 
Ha ha ha ha ha! Nasubiri kuona wale jamaa wa dini itakuwaje safari hii. Sijui kompyuta na mfumo utawaonea tena? Matokeo haya yatazua tena maandamano? Yetu macho.
Kwani huwa wanakosa la kusema?? Kujikubali ni kazi kuliko kwenda kazini haswa linapokuja swala la kuukubali udhaifu ulio nao.
 
Miaka yote namba ndizo zinatumika kusahihisha mtihani na kila msahihishaji anasahihisha swali moja tu katika karatasi la mwanafunzi mmoja kabla ya kufika mikononi mwa 'checkers' ambao kazi yao ni kupitia kama kuna kasoro yoyote na kimsingi wanapanga maksi ni wengine sio wale walisahihisha.

Ni marufuku kwa mwalimu kusahihisha mtihani wa shule yake. Kuja kwa mfumo wa kompyuta unakazia zaidi kuthibiti upendeleo kama ulikuwepo.
 
Malalamiko hayakuwa upande mmoja tu bali hata kutoka kwenye shule husika au upande mmoja wa Muungano. Ni jitihada mpya za kupunguza malalamiko..... tuwapongeze sana kwa uamuzi huo.
 
Mkuu kompyuta ni kipokea amri tu na kufanya kama amri zinavyosema kwa hiyo unaweza kulitegemea kompyuta kumbe limepewa amri sivyo ndivyo!! Tusubiri tujionee!!


Ndio maana nimetumia neno kupunguza malalamiko sio kuondoa kabisa.... uko sahihi ni sisi binadamu tunaosimamia kompyuta ingawa ukicheza na kompyuta unaweza kukamatwa kama mfumo wake ni mathubuti kuliko ujanja wa binadamu.
 
Malalamiko hayakuwa upande mmoja tu bali hata kutoka kwenye shule husika au upande mmoja wa Muungano. Ni jitihada mpya za kupunguza malalamiko..... tuwapongeze sana kwa uamuzi huo.

Huo upande wa pili wa Muungano ndio balaa kabisa safari hii.
 
mbona ma prof na lecturers wanasimamia pepa na watu wana desa kama kawa ishindikane hawa!!!!
 
Hao walimu waliokuwa wanasahihisha izo paper wasije subotage izo system ili turudi kwenye system za mkono tena
Otherwise big up maana naona litasidia kupunguza malalamiko na upendeleo
Jamaa zangu wa Ijumaa naona mtakuwa na imani sasa maana otherwise lawama zote kwa Bill Gates sasa oh sorry kwa watengeneza iyo software
 
Mkuu kompyuta ni kipokea amri tu na kufanya kama amri zinavyosema kwa hiyo unaweza kulitegemea kompyuta kumbe limepewa amri sivyo ndivyo!! Tusubiri tujionee!!

Yaani ungekuwa karibu ningekupa BIG FIVE! tuna uhakika gani kama hizo computer hazotojazwa madudu? computer ni GIGO ! GABBAGE IN GABBAGE OUT! isiwe ndio kumalizwa kabisa huku! halafu tukaambiwa kiko wapi! halafu sijaelewa ! hiyo computer insahihisha vipi mitihani iloandikwa kwa mwandiko tofauti ! HAPA NAPATA SHAKA! labda kwa multiple choice nakubali lakini kwa kusahihisha muandiko NITAKATAA MPAKA KUFA! ngoja na tuone kituko cha dunia hiki!
 
.................ebu tusubiri na hii nayo tuone ila kwa ulalamishi wa watu wa ile imani ya kilalamishi matokeo akiwa vile vile lazima watasema computer zilizotumika ni za Kikatoliki.
 
Yaani ungekuwa karibu ningekupa BIG FIVE! tuna uhakika gani kama hizo computer hazotojazwa madudu? computer ni GIGO ! GABBAGE IN GABBAGE OUT! isiwe ndio kumalizwa kabisa huku! halafu tukaambiwa kiko wapi! halafu sijaelewa ! hiyo computer insahihisha vipi mitihani iloandikwa kwa mwandiko tofauti ! HAPA NAPATA SHAKA! labda kwa multiple choice nakubali lakini kwa kusahihisha muandiko NITAKATAA MPAKA KUFA! ngoja na tuone kituko cha dunia hiki!
Msiwe na hofu walalamishi, safari hii Baraza la Mitihani wamepanga kum-consult Ponda azifanyie programming computer zote halafu pia yeye ndo atakuwa msimamizi mkuu wakati wa usahihishaji.
 
Back
Top Bottom