MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Wanafunzi zaidi ya laki 8 wa darasa la 7 wataanza mitihani yao kesho. wanafunzi hao ni kutoka zaidi ya shule za msingi elfu 13 kote nchini.
Hatua ya walimu wa sekondari kutumika kusimamia mtihani huo ni ya kupongezwa kwani inaboresha usimamizi makini. Mwanafunzi bora wa elimu ya msingi anatendengeneza mwanafunzi bora wa sekondari. Natumaini walimu wa sekondari watakuwa makini ili wapate wanafunzi bora watakaochaguliwa kwenda sekondari.
Hatua ya mitihani kusahihishwa kwa kompyuta kama ilivyo kwa nchi zingine kama Ghana na Afrika kusini kutapunguza ' human errors' hasa malalamiko ya upendeleo. Wakati wa kusahihisha mtihani walikuwa wanahitajika waalimu zaidi ya 3000 kuwekwa kwenye kituo kimoja na kulipwa posho kwa siku 60 lakini sasa mtihani utasahihishwa kwa siku 21 tu kwa komptuta.
Kila jambo lina changamoto zake lakini huu ni mwanzo mzuri.
source: Naibu waziri wa Elimu Mh. Mulugo, Radio One na Baadhi ya magazeti ya leo.
Mods: wameondoa thread hii kwenye jukwaa la siasa lakini siasa ndizo zimetufikisha kulalamiko kwenye mambo ya msingi na waliozungumza haya ni wanasiasa. kuna wanaotumia jukwaa la kisiasa kuomba kura za wananchi kwa kuzungumza mapungufu ya serikali likiwemo suala la mitihani.
Hatua ya walimu wa sekondari kutumika kusimamia mtihani huo ni ya kupongezwa kwani inaboresha usimamizi makini. Mwanafunzi bora wa elimu ya msingi anatendengeneza mwanafunzi bora wa sekondari. Natumaini walimu wa sekondari watakuwa makini ili wapate wanafunzi bora watakaochaguliwa kwenda sekondari.
Hatua ya mitihani kusahihishwa kwa kompyuta kama ilivyo kwa nchi zingine kama Ghana na Afrika kusini kutapunguza ' human errors' hasa malalamiko ya upendeleo. Wakati wa kusahihisha mtihani walikuwa wanahitajika waalimu zaidi ya 3000 kuwekwa kwenye kituo kimoja na kulipwa posho kwa siku 60 lakini sasa mtihani utasahihishwa kwa siku 21 tu kwa komptuta.
Kila jambo lina changamoto zake lakini huu ni mwanzo mzuri.
source: Naibu waziri wa Elimu Mh. Mulugo, Radio One na Baadhi ya magazeti ya leo.
Mods: wameondoa thread hii kwenye jukwaa la siasa lakini siasa ndizo zimetufikisha kulalamiko kwenye mambo ya msingi na waliozungumza haya ni wanasiasa. kuna wanaotumia jukwaa la kisiasa kuomba kura za wananchi kwa kuzungumza mapungufu ya serikali likiwemo suala la mitihani.