CHIETH
Senior Member
- Aug 15, 2011
- 179
- 67
Ndugu WanaJF,
Napenda kutumia jukwaa hii tena kuipongeza Chuo kikuu cha Udaktari Buagando Kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye ufundishaji. Kama Miezi miwili hivi iliyopita nilitumia jukwaa hili kuiarifu jamii na wamiliki wa chuo hiki kuwa hali ya ufundaishaji hapo si nzuri licha ya karo kubwa wanayolipa wazazi.
Baada ya post yangu hiyo nilisikia kuwa viongozi wa chuo hicho walihaha kutaka kujua ni nani aliyepost thread iliyokuwa inawaumbuwa kwa jamii. Walibaki kuwalaumu maskini wanafunzi kuwa ndiyo waliandika maneno hayo hapa JF. Wangejua kuwa mimi si mwanafunzi wa hapo ila nina interests na chuo hicho wasilaumu wanafunzi hao. Ningependa pia kuwa shauri kuwa JF ni sehemu ambapo kila mtu anaweza kutoa kero zake. Ukweli ni kwamba nilikuwa nafuatilia Mgogoro kati ya MD3 (2010/2011) na dean of faculty of medicine ndiyo maana niliamua kutoa kero hizo hapa ili wahusika na wenye interest na chuo hiki wawajibike kuwaokoa wanafunzi wale wasiharibiwe maisha na mtu mmoja.
Ninashukuru kwamba walikuwa wasikivu na kuweza kufanya marekebisho makubwa katika ufundishaji wa "MANAGEMENT OF DISEASES". Habari nilizopata kutoka Bugando ni kwamba wanafunzi wa MD3 (2011/2012) sasa wanafundishwa mpaka wanakubali kwamba medicine sio lele mama. Na hili ndiyo wananchi tulikuwa tunataka. Haiwezekani ukalaumu wanafunzi eti hawaingii darasani wakati walimu hawaingii pia darasani kufundisha. Hivi sasa hata mtihani ukitungwa mwanafunzi akafeli atajilaumu mwenyewe na hatapata kisingizio eti si kufundishwa.
Nilisikia sauti iliyorekodiwa ya mkutano iliyoitishwa na makamu mkuu wa chuo, katika rekodi hiyo nilisikia makamu mkuu msaidizi Taaluma ambaye pia ni profesa akiponda wanafunzi eti wasisubiri kufundishwa. Napenda kumshauri Profesa kwamba hii si sociology au open university ambapo wanafunzi wanaweza kujisomea tu na kufaulu mitihani. Medicine inahitaji mwalimu ili mtu awe daktari mzuri.
Hata hivyo napenda kuwapongeza kwa mabadiliko makubwa mlioanza nao. Vile ville wanafunzi wanaomba pia mabadiliko haya yaende idara ya surgery na gynaecology/obstetrics.
Tafadhali napenda kuomba uongozi wa chuo na walimu wasiwabughudhi wanafunzi kwa taarifa hizi kwa kuwa mimi si mwanafuzi ila ni mtu niko kwenye kazi zangu za kitaifa. Tunapenda kuona vijana wetu wanahitimu na kupunguza shida za watanzania waliowengi kukosa madaktari wazuri.
Mwisho nawapongeza maaskofu kwa huduma wanaotoa kwa watanzania bila ubaguzi wa kidini,rangi na ukabila. Kwa pamoja tutaweza
Nawasilisha.
Napenda kutumia jukwaa hii tena kuipongeza Chuo kikuu cha Udaktari Buagando Kwa kufanya mabadiliko makubwa kwenye ufundishaji. Kama Miezi miwili hivi iliyopita nilitumia jukwaa hili kuiarifu jamii na wamiliki wa chuo hiki kuwa hali ya ufundaishaji hapo si nzuri licha ya karo kubwa wanayolipa wazazi.
Baada ya post yangu hiyo nilisikia kuwa viongozi wa chuo hicho walihaha kutaka kujua ni nani aliyepost thread iliyokuwa inawaumbuwa kwa jamii. Walibaki kuwalaumu maskini wanafunzi kuwa ndiyo waliandika maneno hayo hapa JF. Wangejua kuwa mimi si mwanafunzi wa hapo ila nina interests na chuo hicho wasilaumu wanafunzi hao. Ningependa pia kuwa shauri kuwa JF ni sehemu ambapo kila mtu anaweza kutoa kero zake. Ukweli ni kwamba nilikuwa nafuatilia Mgogoro kati ya MD3 (2010/2011) na dean of faculty of medicine ndiyo maana niliamua kutoa kero hizo hapa ili wahusika na wenye interest na chuo hiki wawajibike kuwaokoa wanafunzi wale wasiharibiwe maisha na mtu mmoja.
Ninashukuru kwamba walikuwa wasikivu na kuweza kufanya marekebisho makubwa katika ufundishaji wa "MANAGEMENT OF DISEASES". Habari nilizopata kutoka Bugando ni kwamba wanafunzi wa MD3 (2011/2012) sasa wanafundishwa mpaka wanakubali kwamba medicine sio lele mama. Na hili ndiyo wananchi tulikuwa tunataka. Haiwezekani ukalaumu wanafunzi eti hawaingii darasani wakati walimu hawaingii pia darasani kufundisha. Hivi sasa hata mtihani ukitungwa mwanafunzi akafeli atajilaumu mwenyewe na hatapata kisingizio eti si kufundishwa.
Nilisikia sauti iliyorekodiwa ya mkutano iliyoitishwa na makamu mkuu wa chuo, katika rekodi hiyo nilisikia makamu mkuu msaidizi Taaluma ambaye pia ni profesa akiponda wanafunzi eti wasisubiri kufundishwa. Napenda kumshauri Profesa kwamba hii si sociology au open university ambapo wanafunzi wanaweza kujisomea tu na kufaulu mitihani. Medicine inahitaji mwalimu ili mtu awe daktari mzuri.
Hata hivyo napenda kuwapongeza kwa mabadiliko makubwa mlioanza nao. Vile ville wanafunzi wanaomba pia mabadiliko haya yaende idara ya surgery na gynaecology/obstetrics.
Tafadhali napenda kuomba uongozi wa chuo na walimu wasiwabughudhi wanafunzi kwa taarifa hizi kwa kuwa mimi si mwanafuzi ila ni mtu niko kwenye kazi zangu za kitaifa. Tunapenda kuona vijana wetu wanahitimu na kupunguza shida za watanzania waliowengi kukosa madaktari wazuri.
Mwisho nawapongeza maaskofu kwa huduma wanaotoa kwa watanzania bila ubaguzi wa kidini,rangi na ukabila. Kwa pamoja tutaweza
Nawasilisha.