Hongera CCM Treni ya Moshi - Arusha yawa mkombozi kipindi hiki cha sikukuu hakuna mchaga atabaki DSM!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,616
141,447
Kiukweli kurejea kwa usafiri wa gari moshi kanda ya kaskazini imekuwa ni mkombozi mkubwa kwetu hasa nyakati hizi za sikukuu za kufungia mwaka.

Shukrani pekee ziwaendee viongozi wa CCM na hasa komredi Polepole kwa kuhakikisha usafiri wa gari Moshi unarejea.

2020 hakuna mchagga atakula Krismas na mwaka mpya Dar es salaam, sote tutakuwa nyumbani Kilimanjaro.

Karibuni wageni.

Maendeleo hayana vyama!
 
Wachaga tunaojielewa tutampongeza raisi kwa hili, na mengineyo mengi mazur aliyotufanyia ila wale wanaoshikiwa akili na kina Amsterdam na Lisu hawawezi kupongeza wala kushukuru kwa jema lolote linalofanywa na serikali hii ya CCM chini ya mwenyekiti wake raisi John P Magufuli
 
Wachaga tunaojielewa tutampongeza raisi kwa hili, na mengineyo mengi mazur aliyotufanyia ila wale wanaoshikiwa akili na kina Amsterdam na Lisu hawawezi kupongeza wala kushukuru kwa jema lolote linalofanywa na serikali hii ya CCM chini ya mwenyekiti wake raisi John P Magufuli
Wachaga halisi wamekuwa wakijitegemea hata kabla ya JPM.

Wachaga hawalambi mtu viatu.. hayo masuala ya kina amsterdam na lissu ni masuala ya kusadikika.

Ni siasa tu.
 
Wachaga halisi wamekuwa wakijitegemea hata kabla ya jpm.
Wachaga hawalambi mtu viatu.. hayo masuala ya kina amsterdam na lissu ni masuala ya kusadikika.

Ni siasa tu.
Serikali ya CCM chini ya mw/kiti wake raisi JPM kutimiza majukumu yake ktk mikoa yetu ya Kilimanjaro na Arusha, afu na sisi wenyeji wa mikoa hii ambao wengi ni wachaga kumpongeza, huko sio kulamba miguu. Bali ni kushukur kwa kile au yale mazuri yanayofanywa na serikali, tuache kujidanganya kwamb kila kitu tulifanya wenyewe
 
Kiukweli kurejea kwa usafiri wa gari moshi kanda ya kaskazini imekuwa ni mkombozi mkubwa kwetu hasa nyakati hizi za sikukuu za kufungia mwaka...
Leo mabasi yote yamejaa anayekata ni Kilimanjaro pekee! Watu wanahainga mno, pita Kilimanjaro pale uone foleni yake na wahudumu wana nyodo kama nini
 
Niko segera hapa,hizi gari zinazoelekea kaskazini zinavyoongozana utadhani ni msiba,halafu hakuna gari ya kinyonge!
 
Serikali ya CCM chini ya mw/kiti wake raisi JPM kutimiza majukumu yake ktk mikoa yetu ya Kilimanjaro na Arusha, afu na sisi wenyeji wa mikoa hii ambao wengi ni wachaga kumpongeza, huko sio kulamba miguu. Bali ni kushukur kwa kile au yale mazuri yanayofanywa na serikali, tuache kujidanganya kwamb kila kitu tulifanya wenyewe
Labda nikuulize ww unaejiita mchaga. Nani alikupa uwakilishi maana wachaga hawajahi kujikusanya wakatoa tamko?

Kama mkazi halisi sijawahi kusikia tamko lolote. Hilo ww umelitoa wapi na mwa mamlaka ya nani?
 
Kiukweli kurejea kwa usafiri wa gari moshi kanda ya kaskazini imekuwa ni mkombozi mkubwa kwetu hasa nyakati hizi za sikukuu za kufungia mwaka.

Shukrani pekee ziwaendee viongozi wa CCM na hasa komredi Polepole kwa kuhakikisha usafiri wa gari Moshi unarejea.

2020 hakuna mchagga atakula Krismas na mwaka mpya Dar es salaam, sote tutakuwa nyumbani Kilimanjaro.

Karibuni wageni.

Maendeleo hayana vyama!
Kupata hiyo ticket ni mtihani. Hamu yote ya tren inakuisha.
Naomba wanaohusika wafanye kama kukata ticket ya ndege.
Siku unayoamua unakata sio mtandao wao sijui wazee ndio wanaou operate . Yani ni kero
 
Back
Top Bottom