Hongera boss wa Traffick Dar

Balile

Member
Oct 10, 2011
74
140
Leo nimefarijika sana baada ya Kamanda wa Usalama Barabarani Kanda Maalum ya Dar es Salaam (ZTO), ACP Awadhi Haji kusimamia Sheria na kumwamuru askari wa Usalama Barabarani WP Beatrice alipe faini ilipobainika kuwa alitaka kumbikia kosa la kupita kwenye taa nyekundu Dereva wa Gazeti la JAMHURI.

WP Beatrice alilazimisha kuwa Dereva Leonce Mujuruzi amepita taa nyekundu wakati alipita taa ya kijani baadaye akabadili kauli na kusema yeye alikuwa anaongoza magari hivyo Dereva Leonce hakupaswa kufuata ishara ya taa bali maelekezo ya WP Beatrice.

Katika kikao tulichofanya Ofisi ya ZTO Awadhi leo Aprili 28, 2017 Dar es Salaam, Afande Awadhi amesema amebaini ukweli kuwa WP Beatrice hakufuata utaratibu anaopaswa kufuata askari anaponkamata Dereva kwa kosa analomtuhumi nalo Barabarani.

Nitaandika kwa kina sakata hili kwenye safu yangu ya SITANII Jumanne ijayo katika Gazeti la JAMHURI, ila kwa ufupi amesema askari akimkamata Dereva anapaswa kufanya yafuatayo:-

1. Askari akimkamata Dereva anaangalia aina ya kosa. Adhabu ya kwanza ni ONYO.

2. Adhabu ya pili imegawanyika sehemu mbili. Dereva akikiri kosa, anapigwa faini. Akikataa anapelekwa Mahakamani pande mbili zisikilizwe na haki itendeke.

Katika shauri lililokuwa mbele yetu, WP Beatrice hakumpa fursa Dereva wetu Leonce ya ama onyo au kuchagua kati ya faini au kupelekwa Mahakamani.

In charge wa Police Msimbazi Inspekta Bihemo, alikuwa ameelekeza Dereva Leonce awekwe ndani na kufunguliwa mashtaka kwa kutokana na Leonce kulalamika kuwa WP Beatrice amemwonea.

ACP Awadhi amesema hayupo kutetea Polisi au Raia. Mwenye makosa anawajibika kwa makosa yake. Amebaini WP Beatrice amekiuka wajibu wake hivyo akamwagiza alipe faini aliyokuwa amemwandikia Leonce.

Nitaandika kwa kina kwenye safu yangu ila nampongeza ACP Awadhi. Sisi kama JAMHURI tumekuwa tukipokea malalamiko juu ya uonevu wa askari. Si kwamba hatukuwa na Sh 30,000 za kulipa faini, ila tumejiuliza kama askari ana uwezo wa kutubambikia kesi sisi, inakuwaje kwa wasio na kuwasemea?

Ilitubidi tusimame kutetea haki. Tunamshujuru ACP Awadhi kwa kutetea na kusimamia haki bila uonevu. Tunaamini WP Beatrice na Inspekta Bihemo kuanzia sasa watafanya kazi kwa weledi na kitenda haki kwa kila mmoja.

Asante ACP Awadhi na Mungu akubariki uendelee kusimamia haki, leo, kesho na baadaye.

Balile
 
Msamiati wa Onyo haupo siku hizi. Ukifanya kosa lolote hata liwe dogo vipi, hawa "wakusanya mapato" wanachojua ni 30,000/= tu. Tena zile machine walizowapa siku hizi zimewatia kibri ya ajabu sana. Mwambieni hivyo huyo Boss wao

Issue ya kwenda Mahakamani nayo watu wengi wanaweza kukwepa ili kuokoa muda. I am sure ukikomaa upelekwe mahakamani, wale jamaa wataconfiscate driving licence yako, gari utaambiwa ukalipark police nk. So, wengi wanaona nafuu wateme thirty tu yaishe.
 
Si kwasababu wanawajua nyinyi ni WADAKU sisi tulishazoea anakuvuta pembeni unampa hela ya kubrashia viatu..alafu anakuambia nina pea nne,unazama mfukoni munamalizana.
 
Awadh namjua ni muadilifu sana haonei mtu nilishawahi kumshtakia nilinyanyaswa mataa ya veta kuna traffic aliniambia nenda popote nikampigia akaamua kesi vzr
 
Huyo ACP Awadhi naona kachoka kazi, akumbuke geshi hilo wiki hii walitutangazia kukusanya milioni 888 kwa siku 5 tu ktk jiji la Der, sasa kama anataka kupunguza speed ya ujenzi wa treni ya mwendokasi basi ajue atapunguzwa yeye speed.
Geshi hili ni chanzo kizuri cha mapato kwa awamu hii ya gwara baada ya wafanyabiashara kuvunjwavunjwa uti wa mgongo.
 
mimi walinikamata eti kwenye 50 nimezidisha nimeendesha 53. ni hatari !!!!
 
mimi walinikamata eti kwenye 50 nimezidisha nimeendesha 53. ni hatari !!!!
Mkuu siku nyingine komaa nao. Kamanda Mpinga aliyoandika ufafanuzi kuwa ikiwa speed inayooneshwa kibali ni 50 basi ili uwe umevunja sheria ni uwe juu ya 55. Speedometer zinasoma 40 inayofuata ni 60, hivyo ku balance katika ya 40 na 50 ni mtihani, aisha uendeshe kwa speed 40 tu.
 
sawa mkuu, ila nililipa kwa sababu afande alikua demu alafu ni figure no. 8 nilijikuta nimempa 40000 akanirudishia 10000, nikamwambia keep change. lakini baadae hela yangu iliniuma !!!
 
Huyu huyu Awadh aliyeambiwa nataka jamaa waongezwe mara 10. Point moja Askari 10 kweli tutafika.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom