Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Bibi Elsie Kanza, Mshauri wa Uchumi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa na Taasisi ya World Economic Forum (WEF) kuingia katika kundi dogo la heshima la vijana waliothibitisha vipaji vya uongozi la Viongozi Vijana Duniani (Young Global Leader- YGL)) kwa mwaka huu wa 2011.
Bibi Kanza ni mmoja wa kinamama wawili Watanzania vijana waliotangazwa na WEF mjini Geneva, Uswisi, leo, Jumatano, Machi 9, 2011, kujiunga na kundi la YGL ambalo linashirikisha Waafrika 14 miongoni mwa vijana 190 waliochaguliwa kutoka nchi 65 duniani kujiunga na kundi la vijana la Young Global Leaders kwa mwaka huu wa 2011.
Mtanzania mwingine aliyechaguliwa ni Susan Mashibe, Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni mawili TanJet na Kilimanjaro Aviation Loegistic Centre - ambayo yanashughulika na usafiri wa anga.
Mabibi Kanza na Mashibe wamechaguliwa kutoka miongoni mwa viongozi vijana 5,000 waliopendekezwa kutoka duniani pote na hatimaye kuchaguliwa kwenye mchujo mkali na Kamati Maalum chini ya uenyekiti wa Malikia Rania Al Abdullah wa Ufalme wa Hashemite wa Jordan.
YGL wa mwaka huu wanajiunga katika kundi la viongozi vijana wengine 668 walioteuliwa miaka ya nyuma, na miongoni mwao yumo aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bwana Lawrence Masha.
Kila mwaka WEF hutoa heshima hiyo ya YGL ili kutambua vipaji vya uongozi vya vijana kutoka pote duniani kwa mchango wao katika uongozi, mafanikio ya kitaaluma ana ari yao ya kuleta mabadiliko katika jamii na huchaguliwa kutoka nyanja zote za maisha ikiwemo biashara, serikali, vyuo vikuu, habari na mawasiliano, taasisi zisizokuwa za kiserikali, utamaduni na sanaa.
Bibi Kanza aliteuliwa kuwa Mshauri wa Uchumi wa Rais Kikwete tokea Machi mwaka 2006. Kabla ya hapo alifanya kazi katika Wizara ya Fedha (2002-2006) na Benki Kuu ya Tanzania (1997-2002).
Anayo Shahada ya BSc katika Uongozi wa Biashara za Kimataifa kutoka United States International University-Africa (USIA-A), Shahada ya Uzamili ya MSc katika Fedha kutoka Chuo Kikuu cha Strathclyde cha Uingereza na Shahada nyingine ya Uzamili katika Uchumi wa Maendeleo kutoka Williams College, Marekani.
Bibi Kanza ndiye alikuwa Mratibu wa Taifa wa Mkutano wa WEF-Afrika uliofanyika kwa mafanikio makubwa mjini Dar es Salaam Mei, mwaka jana, 2010 na pia ametunukiwa Tuzo la Uongozi la Askofu Mkuu Desmond Tutu wa Afrika Kusini.
Wengine waliojiunga na YGL mwaka huu ni pamoja na Makamu wa Rais (Uhandisi) wa Kampuni ya Google kutoka Ukraine, mwanahewa mmoja kutoka Japan, mtangazaji mmoja wa habari wa televisheni ya CNN, mwandishi mmoja wa habari kutoka Nigeria, msanii wa filamu kutoka China, Meya wa Jiji la Calgary, Canada.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
DAR ES SALAAM.
Bibi Kanza ni mmoja wa kinamama wawili Watanzania vijana waliotangazwa na WEF mjini Geneva, Uswisi, leo, Jumatano, Machi 9, 2011, kujiunga na kundi la YGL ambalo linashirikisha Waafrika 14 miongoni mwa vijana 190 waliochaguliwa kutoka nchi 65 duniani kujiunga na kundi la vijana la Young Global Leaders kwa mwaka huu wa 2011.
Mtanzania mwingine aliyechaguliwa ni Susan Mashibe, Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni mawili TanJet na Kilimanjaro Aviation Loegistic Centre - ambayo yanashughulika na usafiri wa anga.
Mabibi Kanza na Mashibe wamechaguliwa kutoka miongoni mwa viongozi vijana 5,000 waliopendekezwa kutoka duniani pote na hatimaye kuchaguliwa kwenye mchujo mkali na Kamati Maalum chini ya uenyekiti wa Malikia Rania Al Abdullah wa Ufalme wa Hashemite wa Jordan.
YGL wa mwaka huu wanajiunga katika kundi la viongozi vijana wengine 668 walioteuliwa miaka ya nyuma, na miongoni mwao yumo aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Bwana Lawrence Masha.
Kila mwaka WEF hutoa heshima hiyo ya YGL ili kutambua vipaji vya uongozi vya vijana kutoka pote duniani kwa mchango wao katika uongozi, mafanikio ya kitaaluma ana ari yao ya kuleta mabadiliko katika jamii na huchaguliwa kutoka nyanja zote za maisha ikiwemo biashara, serikali, vyuo vikuu, habari na mawasiliano, taasisi zisizokuwa za kiserikali, utamaduni na sanaa.
Bibi Kanza aliteuliwa kuwa Mshauri wa Uchumi wa Rais Kikwete tokea Machi mwaka 2006. Kabla ya hapo alifanya kazi katika Wizara ya Fedha (2002-2006) na Benki Kuu ya Tanzania (1997-2002).
Anayo Shahada ya BSc katika Uongozi wa Biashara za Kimataifa kutoka United States International University-Africa (USIA-A), Shahada ya Uzamili ya MSc katika Fedha kutoka Chuo Kikuu cha Strathclyde cha Uingereza na Shahada nyingine ya Uzamili katika Uchumi wa Maendeleo kutoka Williams College, Marekani.
Bibi Kanza ndiye alikuwa Mratibu wa Taifa wa Mkutano wa WEF-Afrika uliofanyika kwa mafanikio makubwa mjini Dar es Salaam Mei, mwaka jana, 2010 na pia ametunukiwa Tuzo la Uongozi la Askofu Mkuu Desmond Tutu wa Afrika Kusini.
Wengine waliojiunga na YGL mwaka huu ni pamoja na Makamu wa Rais (Uhandisi) wa Kampuni ya Google kutoka Ukraine, mwanahewa mmoja kutoka Japan, mtangazaji mmoja wa habari wa televisheni ya CNN, mwandishi mmoja wa habari kutoka Nigeria, msanii wa filamu kutoka China, Meya wa Jiji la Calgary, Canada.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu
DAR ES SALAAM.