Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,628
- 218,059
Ile Taasisi pekee ya vijana ( BAVICHA ) ambayo ni Imara Kupita zote kwenye eneo la maziwa makuu na Africa , imepinga vikali sarakasi za RPC wa Dar es salaam ndugu Mambosasa ya kuwaachia huru wauaji halisi wa Akwilina , ikiwa ni katika kutengeneza njama za kishamba za kuwahusisha viongozi wa chadema na mauaji hayo.
Ikumbukwe kwamba Lazaro Mambosasa mara tu baada ya mauaji hayo ya kishenzi kutokea alikiri hadharani kuhusika kwa jeshi la polisi kwenye mauaji hayo ( ukiwa muongo usiwe msahaulifu ) , lakini ghafla amegeuka kwa mtindo wa U- TURN na kudai polisi hao hawahusiki tena na akadai kwenye maandamano yale kila kiongozi wa chadema alikuwa na silaha , na kwamba miongoni mwao anatafutwa aliyemfyatulia risasi Akwilina.
Mwenyekiti bora wa Taasisi za Vijana barani Afrika Mh Ole Sosopi amepinga vikali maelezo ya Mambosasa , na kudai kwamba polisi wameua , wamejikamata , wamejichunguza na hatimaye wamejiachia wenyewe , Sosopi amemuomba Rais wa Tanzania kuunda Tume ya Majaji kuchunguza uchafu huo , Tayari mpango wa Bavicha kusambaza waraka kwenye balozi zote zilizomo nchini umekamilika .
Mungu ibariki Bavicha .
Ikumbukwe kwamba Lazaro Mambosasa mara tu baada ya mauaji hayo ya kishenzi kutokea alikiri hadharani kuhusika kwa jeshi la polisi kwenye mauaji hayo ( ukiwa muongo usiwe msahaulifu ) , lakini ghafla amegeuka kwa mtindo wa U- TURN na kudai polisi hao hawahusiki tena na akadai kwenye maandamano yale kila kiongozi wa chadema alikuwa na silaha , na kwamba miongoni mwao anatafutwa aliyemfyatulia risasi Akwilina.
Mwenyekiti bora wa Taasisi za Vijana barani Afrika Mh Ole Sosopi amepinga vikali maelezo ya Mambosasa , na kudai kwamba polisi wameua , wamejikamata , wamejichunguza na hatimaye wamejiachia wenyewe , Sosopi amemuomba Rais wa Tanzania kuunda Tume ya Majaji kuchunguza uchafu huo , Tayari mpango wa Bavicha kusambaza waraka kwenye balozi zote zilizomo nchini umekamilika .
Mungu ibariki Bavicha .