Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Tarehe 12.3.2011 ni siku ya kumbukumbu kwa Padre John Chrisostom Ndimbo kutangazwa na Baba Mtakatifu kuwa Askofu mpya wa Jimbo la Mbinga.Anakuwa Askofu wa pili tangu kuanzishwa kwa Jimbo hilo mwaka 1986.Askofu wa kwanza amestaafu kwa mujibu wa sheria za kanisa katoliki.Alikuwa Dr Emmanuel Mapunda.
Hakika ni pongezi nyingi kwake kwani anastahili kushika nafas hii.Padre huyu ni mwana elimu mzuri aliyeapata kufundisha katika seminari ndogo ya Likonde tangu alipopata daraja la upadre mwaka 1989.Alikuwa mkuu wa seminari tangu mwaka 1995 hadi Octoba 2010 akiwa pia ni mwalimu wa Fizikia na Hesabu.Lakini pia katika miaka hii ya karibuni alikuwa akifundisha somo la Kiingereza kidato cha tatu na nne.Matunda ya somo hili yameonekana katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2010.
Sisi tuiliopata kufundishwa naye tunaamini ana uwezo wa kuwa kiongozi katika ngazi aliyopo.Binafsi nina mwona kama ndiye alinifungulia mafanikio yangu kielimu hata kimaadili.Nimeifahamu Fizikia na hesabu kupita kwake.Hakika na mwalimu wa kupongezwa sana.Japo nafas anayoshika ni nyeti na ngumu lakini naamin ataimudu kwa uwezo wa Mungu aliyemchagua.Mungu akupe mafanikio mema.
Hakika ni pongezi nyingi kwake kwani anastahili kushika nafas hii.Padre huyu ni mwana elimu mzuri aliyeapata kufundisha katika seminari ndogo ya Likonde tangu alipopata daraja la upadre mwaka 1989.Alikuwa mkuu wa seminari tangu mwaka 1995 hadi Octoba 2010 akiwa pia ni mwalimu wa Fizikia na Hesabu.Lakini pia katika miaka hii ya karibuni alikuwa akifundisha somo la Kiingereza kidato cha tatu na nne.Matunda ya somo hili yameonekana katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2010.
Sisi tuiliopata kufundishwa naye tunaamini ana uwezo wa kuwa kiongozi katika ngazi aliyopo.Binafsi nina mwona kama ndiye alinifungulia mafanikio yangu kielimu hata kimaadili.Nimeifahamu Fizikia na hesabu kupita kwake.Hakika na mwalimu wa kupongezwa sana.Japo nafas anayoshika ni nyeti na ngumu lakini naamin ataimudu kwa uwezo wa Mungu aliyemchagua.Mungu akupe mafanikio mema.