Honey kwanini hukuniambia mapema kama unakifafa?

GRAMAA

JF-Expert Member
Nov 1, 2014
1,155
3,399
Kabla sijaandika kitu chochote naomba nieleweke kwamba sio kwamba nalalamika kukutana na binti mwenye kifafa ila ninacholalamika kwanini hakuniambia mapema ili nijue na ili nijipange na yajayo. OK ilikuwa hivi.

JUMATATU YA TAREHE 2- 09- 2019.
Siku hii ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwenda kuwatembelea na kuwakagua wanafunzi wa chuo niliopangiwa waliokuwa kwenye mafunzo (field) ndani ya Ilala na Temeke. Baada ya kufika Temeke niliwakusanya wanafunzi wote ili tufahamiane kwanza maana nilikuwa siwajui japo kuwa wao walikuwa wananijua. Katika utambulisho ndipo nilipokutana na mwanafunzi mmoja mrembo sana wa mwaka wa pili na bahati nziri yeye ndiye aliyekuwa team leader wa lile kundi. Basi nikatoa namba kwa wanafunzi wote ili tuwe tunawasiliana.

JIONI YA TAREHE HIYO HIYO 2-09-2019.
Nilimpigia binti yule tukaongea kidogo kisha tukakubaliana tuonane. Ni kweli tulionana kwenye baa moja inayoitwa TETE BEACH palepale Temeke. Tukaongea kidogo. Mtu mzima nikaona bora nioe tu huyu binti kabisa maana alinivutia sana na nilikuwa nimeshachoka na mikasa ya kimapenzi nikaona bora nitulie sasa na mke kabisa kwani alikuwa anakila sifa ninayoihitaji. Nikamwambia dhamira yangu ya kumuita pale kuwa nina nina hitaji awe mchumba wangu kisha ndoa baadaye. Aliafiki haraka sana mpaka nikaguna mmmmh.

SIKU YA TAREHE 4- 9-2019.
Hii ni siku tuliyokubariana tukutane ili tufahamiane zaidi historia zetu na mambo mengine. Basi tukakubaliana tukutane mida ya saa kumi na mbili jioni ndani ya hotel moja pale pale Temeke. Tuliongea mengi sana ila cha ajabu hakunigusia kama ana matatizo ya kifafa na akipiga mihayo mdomo haurudi mara moja mpaka awepo mtu wa kumrudisha mdomo huo.

KIMBEMBE KINAANZA SAA SABA USIKU.
Kwanza alipiga mihayo, miayo au mwayo Mimi sijui jina sahihi. Baada ya kupiga mihayo hiyo mdomo wa binti ukabaki vilevile na akawa ananioneshea ishara ya kumsaidia kuurudishia. Kiukweli ilikata stim kinoma nikaona mmmh mimeo na ikaniogopesha sana. Na sikua na hamu ya kupiga gemu tena nikawa naomba pakuche tu. Aliniomba msamaha kwa kuto kuniambia mapema na akaomba nimvumilie tu.

KIMBEMBE CHA PILI NI SAA KUMI NA MOJA ASUBUHI.
Tukiwa tukelala nikasikia mtu pembeni yangu anafurukuta. Nilipostuka na kumuangalia nikamkuta anatoka povu mdomoni huku ameuma meno kwa nguvu na anatoka povu nyingi sana mdomono na macho yamemtoka huku mkojo ukimtoka. Mwanzo sikujua kama ni kifafa nikajua mtu ndio anakufa hivyo. Nikapanga nisepe ila nikakausha kidogo.

BAADA YA DAKIKA SABA HIVI KUPITA.
Binti akashusha pumzi kubwa sana na kisha akazinduka, na alikuwa ameumia kichwani kwani alikuwa anajigonga mwisho wa kitanda. Aliponiona akaanza Julia akiniomba nisimuache ila nimsaidie kumtibia tatizo lake maana linamnyima raha na amani. Muda wote huo nilikuwa kimya nikishikuru kimoyomoyo kwa kuzinduka kwake tu na sio kitu kingine chochote.

BAADA YA TUKIO ZIMA.
Nilimwambia tuonde tutakutana siku nyingine ndiyo tutaongea vizuri kuhusu matatizo yako. Tuliagana kila mtu akasepa na njia yake. Jana nilikutana nae kwenye kituo cha kazi kawa mnyonge sana na simu hanipigii tena na Mimi nimekaa kimya nikitafakari.

USHAURI KWA WAPENZI.
Please nawaomba muwe mnawaambia mapenzi wenu matatizo yenu ili wawajue mapema kuliko kuficha na baadaye wakaona wenyewe. Ina umiza sana.
 
Kabla sijaandika kitu chochote naomba nieleweke kwamba sio kwamba nalalamika kukutana na binti mwenye kifafa ila ninacholalamika kwanini hakuniambia mapema ili nijue na ili nijipange na yajayo. OK ilikuwa hivi.

JUMATATU YA TAREHE 2- 09- 2019.
Siku hii ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwenda kuwatembelea na kuwakagua wanafunzi wa chuo niliopangiwa waliokuwa kwenye mafunzo (field) ndani ya Ilala na Temeke. Baada ya kufika Temeke niliwakusanya wanafunzi wote ili tufahamiane kwanza maana nilikuwa siwajui japo kuwa wao walikuwa wananijua. Katika utambulisho ndipo nilipokutana na mwanafunzi mmoja mrembo sana wa mwaka wa pili na bahati nziri yeye ndiye aliyekuwa team leader wa lile kundi. Basi nikatoa namba kwa wanafunzi wote ili tuwe tunawasiliana.

JIONI YA TAREHE HIYO HIYO 2-09-2019.
Nilimpigia binti yule tukaongea kidogo kisha tukakubaliana tuonane. Ni kweli tulionana kwenye baa moja inayoitwa TETE BEACH palepale Temeke. Tukaongea kidogo. Mtu mzima nikaona bora nioe tu huyu binti kabisa maana alinivutia sana na nilikuwa nimeshachoka na mikasa ya kimapenzi nikaona bora nitulie sasa na mke kabisa kwani alikuwa anakila sifa ninayoihitaji. Nikamwambia dhamira yangu ya kumuita pale kuwa nina nina hitaji awe mchumba wangu kisha ndoa baadaye. Aliafiki haraka sana mpaka nikaguna mmmmh.

SIKU YA TAREHE 4- 9-2019.
Hii ni siku tuliyokubariana tukutane ili tufahamiane zaidi historia zetu na mambo mengine. Basi tukakubaliana tukutane mida ya saa kumi na mbili jioni ndani ya hotel moja pale pale Temeke. Tuliongea mengi sana ila cha ajabu hakunigusia kama ana matatizo ya kifafa na akipiga mihayo mdomo haurudi mara moja mpaka awepo mtu wa kumrudisha mdomo huo.

KIMBEMBE KINAANZA SAA SABA USIKU.
Kwanza alipiga mihayo, miayo au mwayo Mimi sijui jina sahihi. Baada ya kupiga mihayo hiyo mdomo wa binti ukabaki vilevile na akawa ananioneshea ishara ya kumsaidia kuurudishia. Kiukweli ilikata stim kinoma nikaona mmmh mimeo na ikaniogopesha sana. Na sikua na hamu ya kupiga gemu tena nikawa naomba pakuche tu. Aliniomba msamaha kwa kuto kuniambia mapema na akaomba nimvumilie tu.

KIMBEMBE CHA PILI NI SAA KUMI NA MOJA ASUBUHI.
Tukiwa tukelala nikasikia mtu pembeni yangu anafurukuta. Nilipostuka na kumuangalia nikamkuta anatoka povu mdomoni huku ameuma meno kwa nguvu na anatoka povu nyingi sana mdomono na macho yamemtoka huku mkojo ukimtoka. Mwanzo sikujua kama ni kifafa nikajua mtu ndio anakufa hivyo. Nikapanga nisepe ila nikakausha kidogo.

BAADA YA DAKIKA SABA HIVI KUPITA.
Binti akashusha pumzi kubwa sana na kisha akazinduka, na alikuwa ameumia kichwani kwani alikuwa anajigonga mwisho wa kitanda. Aliponiona akaanza Julia akiniomba nisimuache ila nimsaidie kumtibia tatizo lake maana linamnyima raha na amani. Muda wote huo nilikuwa kimya nikishikuru kimoyomoyo kwa kuzinduka kwake tu na sio kitu kingine chochote.

BAADA YA TUKIO ZIMA.
Nilimwambia tuonde tutakutana siku nyingine ndiyo tutaongea vizuri kuhusu matatizo yako. Tuliagana kila mtu akasepa na njia yake. Jana nilikutana nae kwenye kituo cha kazi kawa mnyonge sana na simu hanipigii tena na Mimi nimekaa kimya nikitafakari.

USHAURI KWA WAPENZI.
Please nawaomba muwe mnawaambia mapenzi wenu matatizo yenu ili wawajue mapema kuliko kuficha na baadaye wakaona wenyewe. Ina umiza sana.
Pole sana mkuu,ushawahi kufukiria kuanza utunzi wa vitabu? Maana una kipaji cha UTUNZI.
 
Amefanya vizuri hata mimi nisingekwambia mkuu, mapenzi ya haraka hivyo afunguke kila kitu?
 
I can't buy this lie
IMG_20190904_060855.jpeg
IMG_20190904_060849.jpeg
IMG_20190511_091701.jpeg
 
We Mzee tupumzishe kwanza Dah, Maana hata chai ya 7800 haijapoa unaleta gahawa chungu hvi
Kiukweli angepumzika kwanza, mkufunzi wa chuo analeta chai haina hata radha, ivi mtu umejuana nae Leo, siku hiyohiyo ushatongoza ushapeleka pepe beach, ushapeleka lodge,
We jamaa alimu yako haikusaidii, ivi magonjwa kam UKIMWI mmepima sangap?. Tupumzishe na chai zako.
Wewe huwezi kuwa baharia.
 
Kabla sijaandika kitu chochote naomba nieleweke kwamba sio kwamba nalalamika kukutana na binti mwenye kifafa ila ninacholalamika kwanini hakuniambia mapema ili nijue na ili nijipange na yajayo. OK ilikuwa hivi.

JUMATATU YA TAREHE 2- 09- 2019.
Siku hii ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwenda kuwatembelea na kuwakagua wanafunzi wa chuo niliopangiwa waliokuwa kwenye mafunzo (field) ndani ya Ilala na Temeke. Baada ya kufika Temeke niliwakusanya wanafunzi wote ili tufahamiane kwanza maana nilikuwa siwajui japo kuwa wao walikuwa wananijua. Katika utambulisho ndipo nilipokutana na mwanafunzi mmoja mrembo sana wa mwaka wa pili na bahati nziri yeye ndiye aliyekuwa team leader wa lile kundi. Basi nikatoa namba kwa wanafunzi wote ili tuwe tunawasiliana.

JIONI YA TAREHE HIYO HIYO 2-09-2019.
Nilimpigia binti yule tukaongea kidogo kisha tukakubaliana tuonane. Ni kweli tulionana kwenye baa moja inayoitwa TETE BEACH palepale Temeke. Tukaongea kidogo. Mtu mzima nikaona bora nioe tu huyu binti kabisa maana alinivutia sana na nilikuwa nimeshachoka na mikasa ya kimapenzi nikaona bora nitulie sasa na mke kabisa kwani alikuwa anakila sifa ninayoihitaji. Nikamwambia dhamira yangu ya kumuita pale kuwa nina nina hitaji awe mchumba wangu kisha ndoa baadaye. Aliafiki haraka sana mpaka nikaguna mmmmh.

SIKU YA TAREHE 4- 9-2019.
Hii ni siku tuliyokubariana tukutane ili tufahamiane zaidi historia zetu na mambo mengine. Basi tukakubaliana tukutane mida ya saa kumi na mbili jioni ndani ya hotel moja pale pale Temeke. Tuliongea mengi sana ila cha ajabu hakunigusia kama ana matatizo ya kifafa na akipiga mihayo mdomo haurudi mara moja mpaka awepo mtu wa kumrudisha mdomo huo.

KIMBEMBE KINAANZA SAA SABA USIKU.
Kwanza alipiga mihayo, miayo au mwayo Mimi sijui jina sahihi. Baada ya kupiga mihayo hiyo mdomo wa binti ukabaki vilevile na akawa ananioneshea ishara ya kumsaidia kuurudishia. Kiukweli ilikata stim kinoma nikaona mmmh mimeo na ikaniogopesha sana. Na sikua na hamu ya kupiga gemu tena nikawa naomba pakuche tu. Aliniomba msamaha kwa kuto kuniambia mapema na akaomba nimvumilie tu.

KIMBEMBE CHA PILI NI SAA KUMI NA MOJA ASUBUHI.
Tukiwa tukelala nikasikia mtu pembeni yangu anafurukuta. Nilipostuka na kumuangalia nikamkuta anatoka povu mdomoni huku ameuma meno kwa nguvu na anatoka povu nyingi sana mdomono na macho yamemtoka huku mkojo ukimtoka. Mwanzo sikujua kama ni kifafa nikajua mtu ndio anakufa hivyo. Nikapanga nisepe ila nikakausha kidogo.

BAADA YA DAKIKA SABA HIVI KUPITA.
Binti akashusha pumzi kubwa sana na kisha akazinduka, na alikuwa ameumia kichwani kwani alikuwa anajigonga mwisho wa kitanda. Aliponiona akaanza Julia akiniomba nisimuache ila nimsaidie kumtibia tatizo lake maana linamnyima raha na amani. Muda wote huo nilikuwa kimya nikishikuru kimoyomoyo kwa kuzinduka kwake tu na sio kitu kingine chochote.

BAADA YA TUKIO ZIMA.
Nilimwambia tuonde tutakutana siku nyingine ndiyo tutaongea vizuri kuhusu matatizo yako. Tuliagana kila mtu akasepa na njia yake. Jana nilikutana nae kwenye kituo cha kazi kawa mnyonge sana na simu hanipigii tena na Mimi nimekaa kimya nikitafakari.

USHAURI KWA WAPENZI.
Please nawaomba muwe mnawaambia mapenzi wenu matatizo yenu ili wawajue mapema kuliko kuficha na baadaye wakaona wenyewe. Ina umiza sana.
Umepata taarifa kuwa cutelove yupo mkoa wa mara?
 
Back
Top Bottom