Home of AC Milan, Official Thread

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,302
4,681
1FEE6A91-A88E-4053-835D-71A05C5CC3CF.jpeg
ac-milan.jpg

jina kamili: Associazione Calcio Milan.
a.k.a: Rossoneli ''red & black'', Diavolo ''the Devil''.
Kuanzishwa: 16/dec/1899.
Uwanja: Sansiro Meazza.
Uwezo: unabeba watu 80,074...
President: Paolo Scaloni.
Kocha: Stefano Pioli.
Nahodha; David Calabria.
Daktari: Mauro Gevi.
Ac Milan ni klabu kubwa na yenye mafanikio ya kimataifa zaidi ya timu yoyote ile hapa Duniani.
AC Milan ilianzishwa na waingereza wawili Alfred Edward na Albert kilpin ktk mwaka huo wa 1899 ambapo makao makuu ya klabu yalikuwa Fiaschetteria Toscana ktk Barabara ya Beschet hapahapa Milan
Mpaka sasa Milan ndio klabu inayoongoza kwa mafanikio ya kimataifa ikiwa imekusanya
Intercontinental cup mara 4
European super cups mara 5
Cup winner cup mara 2
UEFA champions league mara 7.

Pia Milan imebeba ndoo 18 za ligi kuu ya Italia maarufu kama Scudeto.
for more info visit www.acmilan.com
....................................................................
Hah hah ha hah ahaaah dah nianze kwa kicheko kilichojaa dharau na kebehi kisha nashushia na Bia aina ya Peroni inayopatikana kila Bar au Night Club au sehemu yoyote ya anasa katika jiji la Milan.

kikubwa kinachonichekesha ni kitendo cha makusudi cha washabiki wa soka wa siku hizi kujitia uzezeta na kutoa maneno ya kipumbavu ambayo kwa siku za karibuni wamezidi kuambukizana hivyo matapishi hayo wanayoongea yanatapakaa kila kona.

mwanzo niliposikia nikasema labda niliemsikia alitoka chooni bila kuchamba, lakini kwa sasa mambo ni tofauti.

soka lina misingi yake, soka lina sheria zake, lakini soka lina kitu kimoja muhimu mno ambacho hicho ndio kinaleta ladha halisi, kitu kicho ni historia.

unapozungumzia Historia ya Soka kwa ngazi za vilabu basi hutaacha kuitaja klabu yenye mafanikio zaidi hapa ulimwenguni, hapa naizungumzia AC Milan, ambayo pia ndio klabu iliochezewa na nyota wengi zaidi kuliko klabu yoyote mpaka sasa.

basi wakati nafungua Peroni ya 4 huku nikivuta shisha nikawa navuta kumbukumbu huku natafakari kauli kauli za wakurupukaji hawa wanaodai eti AC Milan ni katimu kadoogo sana, tena huwa wanakwenda mbali zaidi kwa kusema eti katimu haka hakana lolote.

ukiwauliza vilaza hawa watakwambia kwao timu bora ni Barcelona, Manchester, Madrid, Chelsea eti na hata Arsenal nayo imo sasa wakati nilipokuwa na Peroni ya 9 huku moshi wa Fleva ya Minti ukiingia mpaka kwenye Bandama na kupanda hadi kwenye mishipa midogo inayoingia ndani ya Ubongo nikarejea tukio la kusisimua na kuchekesha ndani yake.

nilikumbuka tukio la tarehe 19/04/1989 mwendo wa saa mbili na na nusu usiku, katika usiku huu usiosahaulika na Los blancos ulikuwa ni wa mechi ya nusu fainali ya marudiano ya AC Milan dhidi ya Real Madrid, ikumbukwe ktk mechi ya kwanza iliofanyika katika dimba la El Santiago Bernabeu, Madrid walilazimisha suluhu ya goli 1-1.

na ktk mechi iliofuata sasa na kushuhudiwa na washabiki 73112 waliofurika Sansiro, Real Madrid walicharazwa goli 5-0 huku magoli ya Milan yakifungwa na Carlo Ancelotti, Frank Rijkaard, Ruud Gulitt, Marco Van Basten na Roberto Donadoni na hatimae Milan kutinga fainali.

kama hio haitoshi May/24/1989 milango ya saa mbili na robo usiku ktk dimba la Camp Nou ambapo mashuhuda wapatao 97,000 walishuhudia Milan wakiifunga Steau Bucharesti kwa jumla ya magoli 4-0 magoli yaliowekwa kimiani na Ruud Gullit aliefunga 2 na Marco Van Basten alietupia goli mbili pia na kuchukua tuzo ya mfungaji bora akiwa na jumla ya magoli 10.

eti watu wanajisahaulisha hayo pamoja na kujitoa akili kabisaa na kuishi bila kukumbuka kuwa hata msimu uliofuata baada ya hapo ilikuwa ni AC Milan pia iliobeba ndoo hio na rekodi hio hakuna alieweka mpaka sasa.

hivi leo hii nani hajui kuwa Milan ilitengeneza timu bora ambayo haitakuja kutokea ktk historia ya Soka?

hivi ni strikers gani wangeweza kupita beki imara ilioongozwa na Franco Baresi huku akisaidiwa na Alesandro Billy Costacurta, Paolo Maldini na Mauro Tasotti?
hivi ni nani alietimamu ambae anaweza kusahau kipigo cha Mbwa koko ndani ya uzio walichokipata Barcelona iliowahi kuwa bora kuliko Barcelona yoyote ile katika mechi ya fainali ya ligi hiohio ya mabingwa mwaka 1994?
kama mnajisaulisha well naomba kesho muanze kuvaa suruali kisha juu mvae chupi. ila mimi nawakumbusha kuwa Milan waliwasasambua Barca jumla ya goli 4-0 goli zilizopachikwa na Savicevic, Daniele Masaro, Roberto Donadoni na mkoba Marcel Desailly ktk mechi iliopigwa tarehe 18/04/1994 ktk dimba la Olimpico hapo Athens jumla ya watazamaji 70000 walishuhudia Pep Guardiola na Romalio wakishindwa kugusa mpira takriban dakika 30 za mwisho.

cha kuchekesha zaidi Milan walicheza bila top striker Van basten wala nahodha Franco Baresi na bila mchezaji ghali duniani kwa wakati huo yaani Gianluigi Lentini...hivi ni kipi Milan wafanye ili muwashimu?
je mlikuwa wadogo kipindi George Wear anatwaa tuzo ya mwanasoka bora wa Dunia, Ulaya na Africa? je hamkumbuki alikuwa striker wa timu gani?

hivi kweli mnajisahaulisha ukuta bora kwa karne hii umeundwa na Dida, Cafu, Maldini, Stam na Nesta?

niwaweke kundi gani kama mnashindwa kuheshimu triple R toka Brazil yaani Rivaldo, Ronaldo na Ronaldinho kuwa wote walicheza Milan?

sawa Seedorf, Rui Costa, Boban na Pirlo hamuwaheshimu, basi hata Redondo?

eti mtu alieitwa Super pipo hamumtambui, je Mtakatifu Baggio nae? au mnataka Mbwana Samatta acheze Milan ndio muiheshimu?

Bayern walishapigwa goli 4 Sansiro wakaonekana hawajui, je nani asiekumbuka kuwa washabiki wa Man UTD waligoma kurudia kuangalia kipindi cha pili baada ya wachezaji wao kuusaka mpira takriban dakika 45 za mwanzo huku Gatusso akibweka na kumficha Christiano?
[/QUOTE]
TO BE CONTINUA...
 
GREAT TEAM NEED A GREAT COACH...
AC Milan imewahi kufundishwa na makocha kama Gippo Viani, Nereo rocco, Niels Liedholm, Arrigo Sacchi, Fabio Capelo, Alberto Zacheroni, Fatih Terim, Carlo Ancelotti, Leonaldo na Massimiliano Allegri.
 
Dinho kuikimbia Milan Kongwe!

Ronaldinho holds Gremio talks

January 2, 2011

Ronaldinho's departure from AC Milan now appears certain after he left the club's training camp to negotiate a return to Brazil.

ronaldinhotraining20101228_275x155.jpg

GettyImagesRonaldinho has now left the AC Milan training camp in Dubai

Ronaldinho, 30, is discussing a move to Gremio with officials from both clubs.
"He will arrive in Porto Alegre today in order to negotiate with Gremio, but nothing is decided yet," agent Roberto De Assis said. "Everything depends on how these negotiations go.
"If we don't reach an agreement with a club in Brazil then he will return to Milan, as he is still a Milan player. We are not ruling anything out."
Milan's €8 million price tag could prove a stumbling block, but Flamengo and Palmeiras have also expressed interest and his coach, Massimiliano Allegri, appears resigned to losing the player.
"There is a great deal of disappointment and I am sorry that we couldn't get him back to his best," Allegri told Sky Sport Italia. "Potentially he is the best in the world. I hoped for a great year from him."
Zlatan Ibrahimovic added: "I'm disappointed Ronaldinho is no longer with us.
"In my view, he is one of the greatest champions of all time and it was an honour to play alongside him. It's true that recently he wasn't very happy on the field, but the important thing is that he's happy now. Dinho knows what he wants from his career and must follow it."

AC Milan star Ronaldinho in negotiations with Gremio - ESPN Soccernet
 
Companelo hii Habari ya Dinho inaniumiza sana moyo kiasi kwamba hata kuigusia hapa sijathubutu......inaniuma sana moyoni yani
 
Companelo hii Habari ya Dinho inaniumiza sana moyo kiasi kwamba hata kuigusia hapa sijathubutu......inaniuma sana moyoni yani
Usiumie, AC Milan is still there, Dinho ni jina tu kama majina mengi makubwa yaliyokuwepo hapo. Welcome to the forum Rossoneri Milan.
 
San Sirro stadium is very beautful...kwa walioko Italy its a must visit. Inter Milan 4eva.

 
Blackburn Rovers confirm Ronaldinho bid
08:30 PM 03 January, 2011
nographicsLarge.jpg

Despite earlier denying an interest in the Brazilian, Blackburn Rovers Football Club have now confirmed they have in fact made an offer for Ronaldinho.

The 30-year-old is set to leave Milan this month, and although he had been heavily linked with a move to Ewood Park, club director Venkatesh Rao earlier denied an interest.

However, the Lancashire side have now performed a staggering u-turn on the matter, and have confirmed they have in fact made a bid for the forward.

It is believed the Premier League side have tabled a bid of £6.2million for Ronaldinho, who is also expected to receive offers from his homeland in the coming days.
 
Blackburn Rovers confirm Ronaldinho bid
08:30 PM 03 January, 2011
nographicsLarge.jpg

Despite earlier denying an interest in the Brazilian, Blackburn Rovers Football Club have now confirmed they have in fact made an offer for Ronaldinho.

The 30-year-old is set to leave Milan this month, and although he had been heavily linked with a move to Ewood Park, club director Venkatesh Rao earlier denied an interest.

However, the Lancashire side have now performed a staggering u-turn on the matter, and have confirmed they have in fact made a bid for the forward.

It is believed the Premier League side have tabled a bid of £6.2million for Ronaldinho, who is also expected to receive offers from his homeland in the coming days.

Blackburn Owner insist they have no interest @ all in signing soccer super star Ronaldo de Assis Morreira ''Dinho''
 
IMEKWISHA:
Milan President silvio Berlusconi:
I am sorry Ronaldinho is Leaving, but it was his choice....
 
Blackburn blow as Ronaldinho signs for Gremio

Former twice world player of the year Ronaldinho has signed a deal to join Brazilians
Gremio from AC Milan, according to the Gazzetta dello Sport on Tuesday.


ronaldinho_1796771c.jpg

Brazil bound: Ronaldinho has reportedly signed a deal to join Brazilians Gremio from AC Milan Photo: AFP

By Telegraph staff and agencies 9:15PM GMT 04 Jan 2011

The sports newspaper claims Ronaldinho's brother and agent Roberto
de Assis has reached an agreement with Gremio, where the 30-year-old
began his career in 1998 in his home town of Porto Alegre.

Gazzetta claims the official news will be announced in a few hours.

Should that be the case it will scupper Blackburn's bid to bring the former
Barcelona and Paris St Germain forward to the Premier League.
 
na taarifa zilizojiri hivi punde zinasema ukimya umetawala sehemu kubwa ya wilaya ya Sansiro kufuatia habari za kuhuzunisha kuwa mteule toka Mbinguni aliyekuja kuutia radha mpira Ronaldo de Assis Morreira al-maaruf kama Ronaldinho Gaucho muda wowote itatangazwa kuwa ameihama AC Milan.

Wanaume kwa wanawake waishio maeneo ya valese, Carnago, Cassano na Magnago wameonekana wakiwa na hudhuni mitaani huku kila mmoja akiwa kalishika bango lake kuuubwa lenye maneno ya kitaliano ambayo kwa kiswahili yanasomeka ''Usituache Dinho, tunaamini ktk wewe uliyeshushwa kwa ajili ya Mpira''

Nao wakazi wa Cairate, Malpensa airport, Como Chiasso, na Lollentaggio wameonekana wakiwa wamekaa pembezoni mwa Barabara huku baadhi yao wakionekana wakiwa na hudhuni mithiri ya msiba.

Na pembezoni mwa uwanja wa Sansiro Meazza, kilo eneo kuna makundi ya washabiki wa AC Milan ambao wengi wao wamevalia jezi zenye jina Gaucho na wengine wakiwa na mabango ya kumtukuza Dinho.

Mlango mkuu wa kuingia uwanjani Polisi wamesimama imara kuhakikisha hakuna vurumai yoyote kwani tangu Asubuhi ya tarehe 4 washabiki weengi wenye jazba wamekuwa wakivurumusha nyimbo za Matusi, kebehi na maneno makali kwa kocha wao Max Allegri kwa kile walichodai kuwa hakukuwa na sababu ya kumuweka Dinho nje na kumdhalilisha.

Aidha washabiki hao ambao wengine walishindwa kuongea na kubakia wanalia kwa uchungu walisikika wakisema kama mpira anaochezea Gaucho ungekuwa Na Mdomo basi kila dakika ipitayo uwanjani ungeomba upelekwe kwa Dinho kwani kwa kufanya hivyo wenyewe utafurahi na mashabiki woote Duniani watafurahi...

Hatima ya mikusanyiko hii mpk sasa haijajulikana na taarifa za mapema wiki hii zilisema kuwa Dinho yuko Brazil.

To b continua
 
January Signings tayari, nendeni sokoni na ushawishi mkubwa, mtawapata wachezaji wa kuing'arisha Milan. Milan ni timu kubwa,kila mchezaji angetamani kwenda pale, kikubwa ni kuwavuta waje hapo.
 
Gang tatizo ni nini hasa? Si ulidai Dinho alikuwa bora mwaka jana? Sasa ina maana Robinho na Ibrahimovich + Cassano wamemzidi?
 
companero Huyu Alegri ana mapungufu mengi sana.
Keshamuweka Dinho benchi mara kadhaa na muda anaomtumbukiza uwanjani basi ni lazma Dinho amsute.

Jamaa anahisi kwa kumuweka star kama Mt Dinho nje halafu Timu ikashinda basi Dunia nzima itaamini kuwa yeye ana uwezo.

Yaani hatofautiani Falsafa zake na yule sakala aliyemuacha Dinho ktk kombe la Dunia lililofanyika South, matokeo yake timu ikatolewa na kisha akafanya kombe kutokuwa na radha hata ya kulitazama
 
Leo huyu Msierra Leone Sidney Strasser ametutoa kwa goli lake ktk ushindi wa 1-0 dhidi ya Cagliari. Goli hili limepikwa na supa straika Antonio Cassano. Sasa tunapeta ktk msimamo wa ligi kwa tofauti ya pointi 5.

Sforza Rossoneri
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom