Habari zenu waheshimiwa wote mliopo humu JF. Bila kupoteza muda naanza na mada straight. Kama ilivyo ada au desturi yetu waswahili tunapokutana popote nje ya mipaka yetu huwa tunaishi ki undugu kwa kushirikiana ktk mambo mbalimbali. Hapa kuna hawa ndug zetu mmoja anaitwa Chunya (sio jina halisi kutokan na maadili) ambae ana mke na mtoto mmoja, na mungine anaitwa Maumba (sio jina halisi) ambae ni best friend mkubwa wa Chunya. Kam nilivyoeleza hapo juu kwamba Chunya ni mtu mweny familia, ambapo Maumba anaishi kisela kwa madai kwamba eti yeye amekuja ukubwani kusaka maisha na sio kuanzisha familia, afu akishapata ndo badae arudi home kuowa na kuanza umpya "new life" akiwa na familia yake. Chunya aliishi vizuri san na familia yake. Chunya alishirikiana na home boy Maumba ktk mambo mbalimbali iwe shida au raha walishirikiana tu. Yan urafiki wao ulikuwa ni zaidi ya udugu mpk wengine mwanzon tulidhani ni familia moja. Chunya ni dereva na anafanya kazi ktk kampuni fulan (jina kampuni) kwahiy hutumia muda mwingi kuwa safarini, ila hilo halikuwa tatizo ktk siku za mwanzo za ndoa yao . Ndoa ya Chunya ikaanza kuingia doa taratibu. Inasemekana mke akaanza kukosa heshima kwa mumewe na kila alipoelezwa kuhusiana na swala hilo alikuja juu. Baada ya hali ile kuendelea kuwa mbaya huku hakuna maelewano ndan ya nyumba, ikabidi Chunya amshirikishe best wake Maumba ili aweze kusuluhisha ugomvi wao. Inasemekana Maumba akawa anajifanya kusuluhisha kinafki huku rohoni akifahamu chanzo cha tatizo. Akawa anasuluhisha lkn baada ya muda tatizo linajirudia. Mungu si athumani mke wa Chunya akashika mimba, Chunya hakukubaliana na mimba ile ikabidi waende kupima. Ambapo iligundulika kuwa mimba sio ya Chunya. Baada ya mwanamk kubanwa akaeleza ukweli kwamba mwenye mimba ni Maumba wakat huo Maumba hakuwepo Chunya kwa hasira akampigia simu kumuuliza ambapo Maumba alikataa kuhusika na mimba hiyo kwan ni shemeji yake so asingeweza kufanya uhuni huo. Jamaa hakuelewa wakaamua waende kwa Maumba kuupata ukweli wa swala hili ila kwa bahati mbaya wamemkuta Maumba ameshatoroka haijulikan alipo na nmb zake za sim hazipiti. Hapo ndo tukaamini kwamba msela Maumba kamega shemeji yake, kibaya zaidi mpk kamvimbisha tumbo. Dah ama kweli wema mtendee mbuzi utamnywa hata mchuzi, ila binadamu mwenzako.... Wema wote ule Chunya alimfanyia Maumba kamlipa ubaya dah.... Bado tunaendelea na msako wa kimya kimya mpk tutapomnasa jamaa, na tayar tushatoa taarifa ktk vyombo husika ili atapokamatwa sheria ichukue mkondo wake