Hoja za Lula-Maridhiano ya Zanzibar yatokane na kanuni

Ninachofahamu ni kwamba huko Butiama walikuwepo Wazanzibari vile vile (Karume, Nahodha, et al) na kama waliona hilo wazo la Wabara (kama waliolianzisha ni wabara anyway, maana hujatoa ushahidi kuhusu hili) wangelikataa! Hapa nako unawaweka Wazanzibari waliokuwepo Butiama kuwa si lolote kama ilivyokuwa kwenye BLW! Anyway, kama nilivyosema tangu mwanzo, ikitokea hitilafu mahali fulani, Wazanzibari wanawekwa pembeni, hata kama walikuwa ni wenyewe watupu kama ilivyokuwa kwenye BLW, "mzigo mzito anabebeshwa Mnyamwezi!" Sasa hivi mmekaa mkao wa lawama kuhusu kura za maoni, ikitokea Wazanzibari wakakataa Serikali ya Mseto (Umoja wa Kitaifa?) Your hypocricy (undumilakuwili, ukinyonga, etc) will come to light soon!

Tusiandikie mate na wino upo...chama cha CCM cha Nyerere, hakiwakilishi matakwa ya wazanzibari.Ni chama kilichopo ulingoni kutekeleza sera za Bara au zake binafsi yake kama chama.

Ndio sababu ya msingi ya kufeli chama hicho huku visiwani.Na hii haijaanza leo, tokea shina la ASP likiitwa TAA (if im right bout history).Hiki chama kitoto kilikuwa ni chama cha Nyerere behind doors, ndicho chama hichi hichi kilicho shiriki kupindua Zanzibar.

Na baada ya Mapinduzi, chama hicho kikiongozwa na Nyerere ndio kilichopoteza muelekeo mzima wa Zanzibar hadi ikapoteza mamlaka yake yote.Hapa sio tuu Mapinduzi, bali nguvu za ziada zilitumika kuuwa na kufumba wazanzibari wasipige hata chafya.

Hapa western walivyoleta vyama vingi Africa, walikuwa washasahau maasi yao katika historia au tuseme mungu hawatupi waja wake...ndio sasa unaona CUF imeanzishwa 1992, 3 years later imepanda juu na kufika kileleni kuwakilisha wazanzibari walio wengi ambao walikuwa hawana la kufanya ndani ya CCM (chama cha mafia's).

Sasa ndugu yangu mie nikisema ukweli usiumie, bali uvumilie....sawa na mimi ukipiga kelele za utumwa na uchafu wote mwengine....inanibidi nivumilie maana huo ndio ukweli.

Sometimes ukweli hata ukisababisha machozi kudondoka...lakini tutafanyaje?Ukweli ndio huo, Zenji ishachoka kuburuzwa....tusubirie hiyo kura ya maoni....sisi wengine ni waumini, tunaomba dua zetu hili la GNU lipite ili vibabu vyetu huko visiwani vipate kupunga upepo wa karafuu BADALA WA MABOMU YA KUWASHA :D
 
Kiranga, I hate your signature: "There is no god, and Kiranga is his prophet."

Hate is a poison that will only consume you.

There is no god, and Kiranga is his prophet. Let us not derail this thread.If you really want a showdown start a special thread on this.
 
Tusiandikie mate na wino upo...chama cha CCM cha Nyerere, hakiwakilishi matakwa ya wazanzibari.Ni chama kilichopo ulingoni kutekeleza sera za Bara au zake binafsi yake kama chama.

Ndio sababu ya msingi ya kufeli chama hicho huku visiwani.Na hii haijaanza leo, tokea shina la ASP likiitwa TAA (if im right bout history).Hiki chama kitoto kilikuwa ni chama cha Nyerere behind doors, ndicho chama hichi hichi kilicho shiriki kupindua Zanzibar.

Na baada ya Mapinduzi, chama hicho kikiongozwa na Nyerere ndio kilichopoteza muelekeo mzima wa Zanzibar hadi ikapoteza mamlaka yake yote.Hapa sio tuu Mapinduzi, bali nguvu za ziada zilitumika kuuwa na kufumba wazanzibari wasipige hata chafya.

Hapa western walivyoleta vyama vingi Africa, walikuwa washasahau maasi yao katika historia au tuseme mungu hawatupi waja wake...ndio sasa unaona CUF imeanzishwa 1992, 3 years later imepanda juu na kufika kileleni kuwakilisha wazanzibari walio wengi ambao walikuwa hawana la kufanya ndani ya CCM (chama cha mafia's).

Sasa ndugu yangu mie nikisema ukweli usiumie, bali uvumilie....sawa na mimi ukipiga kelele za utumwa na uchafu wote mwengine....inanibidi nivumilie maana huo ndio ukweli.

Sometimes ukweli hata ukisababisha machozi kudondoka...lakini tutafanyaje?Ukweli ndio huo, Zenji ishachoka kuburuzwa....tusubirie hiyo kura ya maoni....sisi wengine ni waumini, tunaomba dua zetu hili la GNU lipite ili vibabu vyetu huko visiwani vipate kupunga upepo wa karafuu BADALA WA MABOMU YA KUWASHA :D

Poleni sana kwa kulialia kila wakati kama watoto wadogo!
 
Hate is a poison that will only consume you.

There is no god, and Kiranga is his prophet. Let us not derail this thread.If you really want a showdown start a special thread on this.

Sure, let's leave it, at least 4 now, because there is God who created you (and all things) and will judge you (and others, including me) in the day of judgment when all men's secrets will put to light and evildoers will be eternally condemned!
 
Sure, let's leave it, at least 4 now, because there is God who created you (and all things) and will judge you (and others, including me) in the day of judgment when all men's secrets will put to light and evildoers will be eternally condemned!


Is this the logic that made you believe in a nonexistent god?

First you say "let's leave it" and then you continue to comment?

If god created all things, who created him?

How can god judge me if he created everything, even my ability to do what he will judge me for.

How can a just god condemn his own creation eternally? For wrongs that were done in a short span of time?

C'mon man, take the god mythology elsewhere kwa watu wasiojua A wala BE.
 
Guys those God stuffs better be off the thread...otherwise ni MSETO
...sorry bout that.
 
Pumba za Lula-Maridhiano ya Zanzibar yatokane na kanuni
MrFroasty
user_online.gif
Yesterday, 01:04 PM
Huyu mwandishi kasomea uandishi au basi ni mwana maskani aliepewa kalamu na kuanza kudumaza akili za jamii?

Kwa waandishi kama hawa kazi tunayo kweli kweli
...:confused:

Maridhiano ya Zanzibar yatokane na kanun
- Sometimes JF nayo huwa tunakuwa kama kichwa cha mwendawazimu, sasa exactly ni nani hasa mwenye pumba? anayedai kuwepo kanuni katika Muungano au anayembeza meaning anataka Muungano wa kiholela holela, dhana ya pumba ambayo imeufikisha huo muungano hapa ulipo?

- Huwa inasikitisha sana!


Es!
 
- Sometimes JF nayo huwa tunakuwa kama kichwa cha mwendawazimu, sasa exactly ni nani hasa mwenye pumba? anayedai kuwepo kanuni katika Muungano au anayembeza meaning anataka Muungano wa kiholela holela, dhana ya pumba ambayo imeufikisha huo muungano hapa ulipo?

- Huwa inasikitisha sana!


Es!

Kuna watu wanataka mawazo yao ndio yatumike kama "marking scheme" ndugu yangu! Mmojawao alidai eti hakuna mtu wa kumhoji Prof Issa G. Shivji simply kwa sababu ni Profesa! Cha kushangaza ni kwamba BLW liliyapiga chini mawazo hayo ya Profesa ambaye alitoa "maelekezo" ya kuundwa kwa Serikali ya mseto!
 
anayedai kuwepo kanuni katika Muungano au anayembeza meaning anataka Muungano wa kiholela holela, dhana ya pumba ambayo imeufikisha huo muungano hapa ulipo?
!

Huyo mwandishi ameonesha wazi kuwa ni some sort of dictator....kwanza ameonesha ana hofu kubwa kama wananchi watapewa nafasi ya referendum juu ya muungano.

Pili ameonesha wazi tokea mwanzoni mwa mchakato wake na maridhiano, kuwa hakuyasupport.Alichokifanya amejaribu kukimbia hoja na kuanza kuzua critical comments kuhusiana na utumwa, na kujaribu kumtia Seif kama ndie aliekuwa Master of all Slaves in the world, but now he is just hiding those stuffs.Wakati mimi nafahamu lengo ambalo Seif ameskip hizo slavery issues kwenye ile hotuba.

Seif alichokuwa anajaribu kuonesha ni kuweka hoja yake kuwa chaguzi ni masuala ambayo yamezorotesha uchumi na maendeleo ya Zanzibar.Sasa labda tumuulize Lula na wengine hapa JF, ni vipi angeliweza kujenga hoja yake kama angepoteza 1-2hrs kuzungumzia historia ya utumwa.

Mwisho, mwandishi mwenye akili zake timamu hapotezi muda wake kujibizana na wasomaji wake...sijawahi kuona gazeti la majibizano mwandishi akijibu watu kwenye magazeti.

All in all Nahodha wa SMZ ameshatowa mwaliko kuwa kila mwenye mawazo mengine ya kuleta amani anakaribishwa.Hayo ya Seif na Karume yalikuwa ni aina moja ya mawazo (ambayo yanaonesha mafanikio)....Sasa yeye katika hilo pumba lake lote ameonesha njia gani inaweza kutumika kuleta amani ya kudumu visiwani humo?
 
Lula wa Ndali-Mwananzela
Februari 3, 2010

KATIKA sehemu ya kwanza ya mfululizo wa makala hizi, tuliangalia kwa karibu ni jinsi gani Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Shariff Hamad, alifanya jaribio la kuandika upya historia ya Zanzibar huku akiyang’arisha yaliyo mazuri na kuyakana yaliyo na machungu.

Katika makala ya pili nilijenga hoja kuwa mambo ya Zanzibar yanawagusa Watanzania wote, na hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuia Watanzania wasijadili mambo ya Zanzibar kwa sababu wao si Wazanzibari.

Lakini vile vile nilidokeza kuwa ni rahisi zaidi kutafuta kuridhishana kuliko kupatana. Nasikitikia kuona kuwa viongozi wa CCM na CUF (Bara na Visiwani) wamechagua kuridhiana kuliko kupatana.

Ninatambua ugumu wa kupatana; kwani katika kupatana ni lazima kwanza mkubali kuelewana tofauti zenu, mitazamo yenu na maono yenu ya kila mnachokitaka. Katika mazungumzo ya mapatano kila mmoja anakuja na hasira zake, uchungu wake, furaha zake, matamanio yake, n.k na kuviweka mezani.

Katika kufanya hivyo, kila mmoja anamuelewa mwenzake na anajifunua hata yale ambayo angependa yasitambulike. Mazungumzo ya mapatano ni magumu zaidi kuliko kupiga kura za maoni!

Vikorombwezo vya msingi katika mapatano

Ili kuweza kuwa na mazungumzo ya mapatano mambo makubwa matatu yanahitajika. Kwanza kabisa ni usawa. Wanaokuja katika kuzungumza ni lazima waje wakiwa sawa; yaani asiwepo kati yake anayejiona yuko juu ya mwingine au mwingine anayekuja akiwa anajiona duni.

Bila kuwa na usawa ni rahisi sana kuendeleza kutuhumiana. Pili, ni ukweli. Mazungumzo yote ya mapatano ni lazima yajikite katika ukweli. Huwezi kuwa na mapatano ambayo msingi wake ni ulaghai, uongo au ukanaji wa ukweli. Tatu, mapatano ya kweli yana msingi katika utayari wa kukubali kubadilika au kubadilisha msimamo. Anayekwenda kwenye mazungumzo tayari akiwa ameshaamua anachotaka na chochote nje ya hicho, hafai.

Nitatoa mfano ambao unaeleweka vizuri sana. Mojawapo ya mambo yanayokwaza upatanisho wa Waisraeli na Wapalestina ni hadhi ya mji wa Yerusalemu. Waisraeli wanasema Yerusalemu ni mji mkuu usiogawanyika wa taifa la Waisraeli. Wapalestina wanasema Yerusalemu Mashariki uwe mji mkuu wa Taifa la Wapalestina. Hakuna aliye tayari kubadilika au kubadilisha msimamo! Je, ni kitu gani kinaweza kuwafanya wakubaliane? Hakuna.

Mgongano wa Zanzibar haukuanza 1964.

Naomba nirudi nyuma kidogo tena kwenye historia. Kuna baadhi ya watu ambao wanajitahidi sana, tena sana, kuwabambikizia watu wa Bara mzigo wa matatizo ya Zanzibar. Wapo ambao kwa kutokujua historia wamefikia mahali pa kulaumu tofauti za Zanzibar kuwa zinatokana na watu wa Bara.

Na wapo ambao wanaamini kabisa kuwa Zanzibar imegawanyika sababu ya Muungano. Mwanahistoria yeyote (awe Mzanzibari au mtu mwingine) anajua ukweli (kikorombwezo cha pili).

Tofauti za Zanzibar hazikupandwa na Muungano wala na Mapinduzi. Hivyo vyaweza kuwa vimechangia kwa kiasi kikubwa tofauti ambayo tayari ilikuwepo. Na wanafanya makosa wanaodhania kuwa ati Muungano ukivunjika basi tofauti zao nazo zitatoweka kama ukungu wa alfajiri.

Kanuni za mapatano

Ni lazima kutambua tofauti;

hivyo mapatano ni lazima tayambue Kanuni ya kwanza: Tutambue tofauti zetu. Je vyama vya ASP, ZPPP, na ZNP vilisimamia misingi gani wakati vinaundwa? Je ajenda zao za uchaguzi ziliwakilisha maslahi gani.

Je masalia ya wafuasi wake leo wanaamini nini? Je tunaweza kuona mwelekeo wa sera za vyama vilivyopo sasa kama vimebeba itikadi na sera za vyama hivyo vya zamani?

Bila kujua tofauti zetu za msingi ni rahisi sana kuendeleza utawala wa woga na wa kutokuaminiana. Tofauti hizi za kimtazamo, kiitikadi na kimwelekeo ndizo zilisababisha kuwe na mgongano Zanzibar na kuendeleza mgawanyiko katika chaguzi zote za 1957, 1961 (mara zote mbili) na hata 1963. Kujaribu kutafuta maridhiano bila kutambua kiini cha tofauti hizo ni kujaribu kukana historia.

Zipo tofauti za msingi zinazowagawa watu wa Zanzibar na tofauti hizo hazitafutika kwa sababu wanasiasa wameamua kuitisha kura ya maoni kuhusu serikali ya Mseto! Anayefikiria kuwa serikali ya Mseto itafuta matatizo yote ya Zanzibar na tofauti za wananchi wake ni mkanaji wa historia.

Kutambua yale yanayounganisha

Haitoshi peke yake kutambua tofauti za watu mbalimbali na makundi mbalimbali lakini ni muhimu zaidi kutambua kile kinachowaunganisha. Leo hii kitu kibaya kinawaunganisha Zanzibar na ninaamini wao wenyewe wanaamini ni kitu kizuri.

Kitu hicho ni chuki ya baadhi ya watu dhidi ya Tanzania Bara. Ukweli huu ni lazima usemwe. Tangu nimeanza kuandika juu ya somo hili wiki chache zilizopita nimepokea maneno ambayo hata nikiamua kuyaandika hapa kuwa ni mawazo ya watu ambao ninaamini ni Watanzania wenzangu (sikuzaliwa Tanganyika!) huwezi kuamini.

Chuki hii kwa upande mmoja inachangiwa na ukweli kuwa Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 yasingefanikiwa na kusimama kama Tanganyika isingejiunga na Zanzibar miezi michache baadaye.

Kwamba Muungano wa Tanzania ulizuia kwa kiasi cha kushangaza umwagikaji damu mkubwa zaidi katika visiwa hivyo endapo serikali ya Sultani wa Oman aliyeng’olewa ingeweza kujiandaa kurudi madarakani. Naogopa kukisikia kile ambacho kingetokea endapo mashabiki na wafuasi wa Sultani wangepata muda wa kujiandaa kuiangusha Serikali ya Mapinduzi.

“Kosa” hili la Muungano halijasamehewa na baadhi ya watu, na ni kutokana na hilo wapo ambao wana kisirani na kinyongo na Bara kwa sababu hiyo tu.

Lakini hata hivyo, kipo kizazi kipya ambacho kimezaliwa katika Tanzania (siyo Jamhuri ya Zanzibar) ambao leo nao wanaamini kabisa kuwa Muungano ni kitu kibaya na kuwa watu wa Bra hawataki maendeleo ya Zanzibar. Mtu mmoja ameniandikia hivi:

“Ni kweli kuwa kura ya maoni tunayotaka isiishie maridhiano, tu lakini hata Muungano kwa vile hili pia ni jambo zito na watu hawakuwahi kuulizwa wakati Watanganyika walipovimeza visiwa hivi. Ni bahati tu kuwa havimezeki. Kashindwa Mreno na Mwarabu atakuwa Mtanganyika mjukuu wa watumwa zetu?” – Mkombe

Binafsi, naamini Wazanzibari wanapaswa kuunganishwa na mambo makubwa zaidi kama tulivyoshuhudia siku za karibuni. La kwanza ni suala la matumizi ya raslimali zake na uhuru wake kujiendeshea mambo yake ya kisiasa.

Mimi ni mmoja wa watu ambao tunaamini kabisa kuwa suala la mafuta yanayopatikana Zanzibar lisimamiwe na Zanzibar yenyewe. Zanzibar kama kisiwa ina vikwazo vingi vya nafasi ya kujiendeleza kiuchumi na kama mafuta yatapatikana, basi, itakuwa heri.

Na ninaamini kabisa kuwa mafuta yakichimbwa Zanzibar hakutadhuru Bara wala kusababisha matatizo makubwa ya kiuchumi. Haya ndiyo mambo ya kuunganisha.

Lakini wale wanaofikiria kuwa udugu wa watu wa bara na Zanzibar utakoma kwa sababu watu walichukizwa na Muungano, hawa wanaota. Udugu na damu ya watu wa Zanzibar na Bara vimechanganyika katika miili ya Wazanzibari kiasi kwamba usishangae watu wakipimwa vinasaba (DNA) wakajikuta wana damu zaidi ya watu wa Bara kuliko ya Uarabuni; japo wao wenyewe wanajiita Waarabu, Washirazi nk.

Tume ya Ukweli na Mapatano (Truth and Reconciliation Commission)

Lakini kuna mambo ambayo kwa kadri ya vizazi vya watu vinaishi yataendelea kuwa sumu katika maisha yao na kuwatofautisha Wazanzibari. Lakini ninaamini ili kuweza kufikia mapatano ya kweli, naamini ipo haja ya kuundwa kwa tume huru ya Ukweli na Mapatano.

Ni tume ya ukweli kwa sababu jukumu lake la kwanza lapaswa kukusanya ukweli wote kwa watu wote bila ya kuogopa matokeo ya ukweli huo. Tume iwe tayari kutoa msamaha kwa wote watakaokubali kusimama na kutoa ushahidi wa ukweli.

Tume hiyo iongozwe na mtu mwenye kaliba ya kimataifa, anayejulikana kwa weledi wake katika mambo ya sheria na haki za binadamu na ambaye yeye mwenyewe hatokuwa mtu wa kugawanya.

Tume hiyo ipewe jukumu la kufuatailia, kukusanya na hatimaye kuweka hadharani mambo yafuatayo.

* Ikusanye historia kabla na baada ya ujio wa Sultani. Historia hii inajulikana na imeandikwa kwa kiasi kikubwa na imepokelewa vya kutosha. Jukumu ni kuhakikisha historia hii inaandikwa kwa ukweli na kwa uwazi tena ikijibu maswali muhimu ya maisha ya watu wa Zanzibar.

* Pasipo kuogopa kuwaudhi watu au kuwakera tume ipewe nafasi ya kuchambua hali ya maisha ya matabaka mbalimbali wakati wa utawala wa Sultani na kutolea maoni kama hali hiyo ingeweza kuendelea na kukubaliwa kizazi na kizazi.

* Iangalie hali ya kisiasa Zanzibar chini ya Usimamizi wa Uingereza hadi kuelekea harakati za Uhuru.

* Iangalie historia ya kisiasa na kimaisha ya wakati wa Uhuru na kuchambua kwanini tayari kulitokea migongano ya kisiasa 1957, 1961, na 1963.

Hii ni katika kuelewa kiini cha tofauti za kisiasa za Zanzibar bila kuona haya. Historia ya vyama vya ZNP, ZPPP, ASP na Umma na makundi mengine yaliyokuwa na mirengo ya kisiasa yaangaliwe kwa uwazi na ukweli. Kwa vile baadhi ya watu waliokuwepo wakati huo bado wa hai ni vizuri kukusanya historia hiyo kutoka kwao vile vile.

* Tume iangalie matukio yaliyofuatia uchaguzi wa 1963 ulioingiza Serikali ya Mseto ya Shamte na hatimaye matukio yaliyosababisha mapinduzi ya 1964. Katika hili ni lazima kuangalia gharama kubwa ya maisha na vitu ambayo visiwa hivyo vililipia katika mapinduzi hayo.

* Tume iangalie nafasi ya Sultani katika Zanzibar huru na kama kwa namna yoyote uzao wa Sultani wa sasa wapaswa kushirikishwa katika kuleta mapatano ya kweli. Ni wazi kuwa Sultani wa Zanzibar hajakana kiti chake cha Usultani wala watoto wake kukana haki yao ya kurithi kiti hicho. Kwa kadri ya kwamba bado wanadai haki hiyo, ni wazi kuwa mapatano ya kweli hayawezi kufikiwa.

* Tume iangalie mtiririko wa uamuzi wa Zanzibar kuungana na Tanganyika na kuangalia kama makubaliano yale ya Muungano yalifuatwa ipasavyo.

* Tume iangalie vile vile mauaji ya Mzee Karume na matukio yaliyochangia hilo.

* Tume ichunguze mambo yote ambayo ni muhimu katika kuleta maridhiano na mapatano ya kweli.

Tume ikishamaliza kazi yake ni LAZIMA itoe Mapendekezo ya mambo gani yafanyike kwa upande wa Zanzibar na kwa upande wa Serikali ya Muungano katika kuleta umoja na mshikamano ndani ya tofauti za kisiasa visiwani humo na vile vile kudumisha Muungano.

Aidha, ripoti yake yote ITOLEWE hadharani ili kila Mzanzibari na kila Mtanzania apate nafasi ya kuangalia ripoti hiyo. Na ni kutoka hapo ndipo mazungumzo ya kutekeleza mapendekezo hayo yafanyike.

Na ni kutoka hapo ndio kwa mara ya kwanza Zanzibar na Tanzania, kwa ujumla, tutakuwa tumepiga hatua ya kwanza ya mapatano ya kweli.
 
Mie namuunga mkono Lula ila katika jambo la historia ya zanzibar na watu wake. Na historia hiyo iandikwe na tume kutoka nje ya zanzibar na Africa kwa ujumla yaani waje historian wenye authority kutoka America, EU waiandike (pesa inapatikana ikiandikwa proposal nzuri kwa UN).

La pili watu wanabishana kila siku humu JF waruhusuni zanzibar waichague serikali waipendayo. Hili litachangia mwamko wa maendeleo otherwise hakuna jambo la maendeleo litafanyika zanzibar hata ikija mseto haitasaidia
 
Haya ya Bw.Lula kweli ni Pumba. Kwa ufupi Watanzania wa Bara hawajakatazwapo kuzungumza yale ya Zanzibar wala kuyatolea ushauri. Kinachokataliwa na kupingwa kwa nguvu zote ni wao kutoa maaumzi kuhusu mambo hayo. Wanaweza kutoa ushauri, na Wazanzibari wanahaki ya kuukataa na kuamua vyengine dhidi ya ushauri huo -kuhusu yale majambo yao.
 
MrFroasty.. hii nayo ina matatizo gani?

Hiyo makala iko poa kabisa, sema huyo Lula na wasomi wengine kutoka Bara wana matatizo ya kiakili au ni wabinafsi.

Hivi chaguzi zote za Zanzibar sijawahi kuwaona kutoa data za ukweli, badala yake utawasikia kimya na vitu kama hivyo.Mimi kupata scientific data za Zanzibar elections, inanibidi nichakure report za International Observers kupata picha kama wapinzani wameibiwa au wanapenda kupiga kelele pekee.

Sasa Lula hana tofauti kubwa, na wazanzibari wengi watafumba masikio yao na kutokumsikiliza....sio kwamba anaandika pumba, bali amechelewa kutoa maelekezo ya nini Maridhiano na Mapatano.

Alitakiwa kuonesha njia na kuonesha kusumbuliwa na vurugu hizo za uchaguzi, kabla ya attempts za Seif na Karume.Sio asubiri Seif na Karume akijaribu kuleta amani, halafu yeye ndio awe mstari wa mbele kufahamisha na kukosoa nini maana ya Maridhiano na Mapatano....huku akifahamisha hotuba ya Seif iwe vipi.Huu kwangu ndio naita pumba.

Na Lula anaonesha wazi kuwa haijuwi historia ya Zanzibar wala ground situation ya visiwani humo, nitajaribu kudokoa vipande viwili vitatu:

Chuki hii kwa upande mmoja inachangiwa na ukweli kuwa Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 yasingefanikiwa na kusimama kama Tanganyika isingejiunga na Zanzibar miezi michache baadaye.
Hapa anajaribu kuikosha Tanganyika, mimi naamini kabisa kuwa Mapinduzi hayo vyovyote iwavyo Nyerere hawezi kuwa excluded kama ni prime suspect.Rukeni watanganyika mukitoja, huo ndio ukweli.Evidence zote zinaonesha wazi kuwa Nyerere aliogopa Zanzibar interms of cold war na sababu zengine.Sasa sio muungano ulituliza Mapinduzi, ni Tanganyika ndio iliosababisha Mapinduzi na kuyatuliza kwa muungano.

Mimi ni mmoja wa watu ambao tunaamini kabisa kuwa suala la mafuta yanayopatikana Zanzibar lisimamiwe na Zanzibar yenyewe.
Nakupongeza kwa msimamo wako huo wa kuwa mkweli na kutetea haki ya wazanzibari.Hapa narudia tena hoja yangu ile ile, wakati mafuta haya yakiingizwa kwenye muungano kinyemela...wale wasomi wetu mabingwa wa Bara waliosimama kidete kuilinda katiba walikuwa wapi?

Ni wazi kuwa Sultani wa Zanzibar hajakana kiti chake cha Usultani wala watoto wake kukana haki yao ya kurithi kiti hicho. Kwa kadri ya kwamba bado wanadai haki hiyo, ni wazi kuwa mapatano ya kweli hayawezi kufikiwa.
Hii sijuwi niite nini, hakuna sultani wala muarabu anaetaka kurudi Zanzibar.Hizi ni kasumba za CCM wakipiga propaganda wakati wa kampeni kutisha wazanzibari wasichague CUF watarudisha ukoloni na waarabu.Sisi vijana wa leo hatuoni sababu yoyote ya mtu wa Oman kukimbilia Zanzibar tuliyonayo sasa...Oman kuna maisha mazuri zaidi kuliko Zanzibar kimaendeleo.Tofauti na miaka hiyo, ambapo Zanzibar kulikuwa ni bora kuliko Oman.

Tume iangalie mtiririko wa uamuzi wa Zanzibar kuungana na Tanganyika na kuangalia kama makubaliano yale ya Muungano yalifuatwa ipasavyo.
Lula soma chapisho lenye kichwa cha habari "Karume na harakati za kujinasua na muungano".Utaona kila kitu kama muungano huu Zanzibar imelazimishwa, na aliefanya mbinu zote za kumtisha Karume kwa kupitia CIA ni Nyerere.


Tume iangalie vile vile mauaji ya Mzee Karume na matukio yaliyochangia hilo.

Nyerere ndio genius wa assisination ya Karume, pia rudia chapisho lenye kichwa cha habari "Karume na harakati za kujinasua na muungano".

P:S
**Chapisho hilo pia limo humu JF limejibu kila kitu.
 
Huyo mwandishi ameonesha wazi kuwa ni some sort of dictator....kwanza ameonesha ana hofu kubwa kama wananchi watapewa nafasi ya referendum juu ya muungano.

Pili ameonesha wazi tokea mwanzoni mwa mchakato wake na maridhiano, kuwa hakuyasupport.Alichokifanya amejaribu kukimbia hoja na kuanza kuzua critical comments kuhusiana na utumwa, na kujaribu kumtia Seif kama ndie aliekuwa Master of all Slaves in the world, but now he is just hiding those stuffs.Wakati mimi nafahamu lengo ambalo Seif ameskip hizo slavery issues kwenye ile hotuba.

Seif alichokuwa anajaribu kuonesha ni kuweka hoja yake kuwa chaguzi ni masuala ambayo yamezorotesha uchumi na maendeleo ya Zanzibar.Sasa labda tumuulize Lula na wengine hapa JF, ni vipi angeliweza kujenga hoja yake kama angepoteza 1-2hrs kuzungumzia historia ya utumwa.

Mwisho, mwandishi mwenye akili zake timamu hapotezi muda wake kujibizana na wasomaji wake...sijawahi kuona gazeti la majibizano mwandishi akijibu watu kwenye magazeti.

All in all Nahodha wa SMZ ameshatowa mwaliko kuwa kila mwenye mawazo mengine ya kuleta amani anakaribishwa.Hayo ya Seif na Karume yalikuwa ni aina moja ya mawazo (ambayo yanaonesha mafanikio)....Sasa yeye katika hilo pumba lake lote ameonesha njia gani inaweza kutumika kuleta amani ya kudumu visiwani humo?

- Mkuu kweli mwandishi asiye na akili timamu, amekufanya uache shuguli zako muhimu na kuja hapa kumjibu tena na maelezo makali makali kama haya, na umemuandama thred nzima?

- What is the agenda mkuu? JF unajua we are very good at reading between the lines!


Respect.

FMEs!
 
- Mkuu kweli mwandishi asiye na akili timamu, amekufanya uache shuguli zako muhimu na kuja hapa kumjibu tena na maelezo makali makali kama haya, na umemuandama thred nzima?

- What is the agenda mkuu? JF unajua we are very good at reading between the lines!


Respect.

FMEs!

Sasa unanifukuza kiujanja au?:rolleyes:
 
Sasa unanifukuza kiujanja au?:rolleyes:

- Hapana ndugu yangu, wewe weka vitu hapa wengi tunakusoma sana, ila acha personal na muandishi maana inapunguza utamu wa dataz nyingi unazozitoa, tupingane kwa hoja tu mkuu unazo hoja nzito sana ila unaharibu kidogo tu na personal, ushauri wangu kidogo tu na wa bure!

Respect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom