Hoja za Fatma Karume baada ya Mahakama kufuta kesi ya Freeman Mbowe na wenzake

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Kauli za Wakili Fatma Karume kuhusu hatua ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kufutiwa mashitaka yake katika Mahakama Kuu, Machi 4, 2022 ambapo alikuwa yeye pamoja na wenzake watatu ambao wote wamefutiwa mashitaka yaliyokuwa yakiwakiabili.

"Ukitazama historia ya siasa, haijawahi kutokea hata siku moja njia ya kutumia fikra au mfumo wa kuendesha mashtaka ya makosa ya jinai kukomoa wanasiasa wenzako, njia hii haijawahi kufanya kazi, mfano ni Nelson Mandela alikaa jela miaka 27 na akaja kuwa Rais.

"Niliona tu itafika mahali kwamba Freeman Mbowe ni lazima wamtoe tu, kwa sababu hatokoma. Kama walitaka kumvunja moyo, sasa wamemzidisha kuwa shujaa.

"Kazi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) ni kuendesha mashtaka hadi mwisho, anapoendesha mashtaka ni kwamba ameangalia ana ushahidi wa kutosha, kinachonishangaza ni kwamba DPP amemaliza ushahidi wake na Jaji amesema Mbowe ana kesi ya kujibu, kisha DPP anajitoa.

"Katika kesi ya Freeman Mbowe, mahakama na Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) wote wamejivua nguo, ni fedheha pia kwa sababu hawakufuata utaratibu wowote wa kisheria ninaoujua mimi.

"Jaji alipaswa kutoa sababu mara baada ya kusikiliza ushahidi na kisha kusema Mbowe na wenzake wana kesi ya kujibu, kwamba ushahidi wote aliousikiliza na kuwasilishwa ulikuwa umefika lengo la kutokuwa na shaka yoyote.

"Niliwahi kumuuliza Jaji Mkuu mmoja kwamba, wewe huna kinga ya kutoshtakiwa, je ukishtakiwa uko tayari kushtakiwa katika mahakama zako hizi? Je, una imani na mfumo unatokana nao utakutendea haki?”


Source: Dar Mpya
 
Screenshot_20220305-115333.png
 
"Katika kesi ya Freeman Mbowe, mahakama na Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) wote wamejivua nguo, ni fedheha pia kwa sababu hawakufuata utaratibu wowote wa kisheria ninaoujua mimi.
Ndiyo sisi hao na ndivyo tulivyolelewa, tunasigida uwekezaji mkubwa elimu tuliyoijenga kwa miaka 60
 
Kauli za Wakili Fatma Karume kuhusu hatua ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kufutiwa mashitaka yake katika Mahakama Kuu, Machi 4, 2022 ambapo alikuwa yeye pamoja na wenzake watatu ambao wote wamefutiwa mashitaka yaliyokuwa yakiwakiabili.

"Ukitazama historia ya siasa, haijawahi kutokea hata siku moja njia ya kutumia fikra au mfumo wa kuendesha mashtaka ya makosa ya jinai kukomoa wanasiasa wenzako, njia hii haijawahi kufanya kazi, mfano ni Nelson Mandela alikaa jela miaka 27 na akaja kuwa Rais.

"Niliona tu itafika mahali kwamba Freeman Mbowe ni lazima wamtoe tu, kwa sababu hatokoma. Kama walitaka kumvunja moyo, sasa wamemzidisha kuwa shujaa.

"Kazi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) ni kuendesha mashtaka hadi mwisho, anapoendesha mashtaka ni kwamba ameangalia ana ushahidi wa kutosha, kinachonishangaza ni kwamba DPP amemaliza ushahidi wake na Jaji amesema Mbowe ana kesi ya kujibu, kisha DPP anajitoa.

"Katika kesi ya Freeman Mbowe, mahakama na Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) wote wamejivua nguo, ni fedheha pia kwa sababu hawakufuata utaratibu wowote wa kisheria ninaoujua mimi.

"Jaji alipaswa kutoa sababu mara baada ya kusikiliza ushahidi na kisha kusema Mbowe na wenzake wana kesi ya kujibu, kwamba ushahidi wote aliousikiliza na kuwasilishwa ulikuwa umefika lengo la kutokuwa na shaka yoyote.

"Niliwahi kumuuliza Jaji Mkuu mmoja kwamba, wewe huna kinga ya kutoshtakiwa, je ukishtakiwa uko tayari kushtakiwa katika mahakama zako hizi? Je, una imani na mfumo unatokana nao utakutendea haki?”


Source: Dar Mpya
Huyu dada anafaa kuwa Jaji mkuu
 
Nilichokiandika kwenye uzi wangu hakitofautiani sana na alichokisema Fatma.

Katika ulingo wa kisheria kilichofanyika ni makosa kwa mwendesha mashtaka na mbowe pia.

I hope ipo siku hawa vilaza wa Chadema wakijifunza kuacha matusi watatuelewa.
 
Miaka yote ya uhai wangu nimekuwa nikisikia juu ya "Banana Republics" Nilikerwa sana kusikia nchi yangu ikitajwa kuwa kwenye kundi la nchi zisizoweza kujiendesha zenyewe hata kama zina uhuru. Nilikerwa zaidi na kauli ya Rais wa Marekani Donald Trump ambaye pia aliwahi kuusema ukweli mchungu kuhusu nchi za kiafrika..... Hakukose hata kidogo!!!

🤒 Ukweli ni kuwa Tanzania bado tuna safari ndefu sana kufikia utawala halisi.
 
Nilichokiandika kwenye uzi wangu hakitofautiani sana na alichokisema Fatma.

Katika ulingo wa kisheria kilichofanyika ni makosa kwa mwendesha mashtaka na mbowe pia.

I hope ipo siku hawa vilaza wa Chadema wakijifunza kuacha matusi watatuelewa.
Mbowe kakosa nini
 
Waliokuwa wanatoa maagizo wameachia njiani kwa hiyo mwanasheria alikuwa hana njia nyingine zaidi ya kutii kulinda kitumbua chake.
 
JKT waliojenga ukuta wa Mererani na Ikulu ya Dodoma waachwe wakiteseka mitaani
Niliwahi Kwenda kwenye idara Fulani ya Jeshi kufanya shughuli Fulani za kiufundi.Wanajeshi niliokutana nao waliniambia,"Jeshini hakuna haki,anachoongea mkuu ndio sahihi hata kama hakina mantic,Bora kuwa gerezani kule Kuna haki zaidi kuliko jeshini".Hii Ina maana kwamba jeshini ukiondoa mshahara,maisha mengine ni magumu kuliko gerezani,hasa kwa wale private wasio na Cheo chochote ambao ndio majority!🤔
 
Nilichokiandika kwenye uzi wangu hakitofautiani sana na alichokisema Fatma.

Katika ulingo wa kisheria kilichofanyika ni makosa kwa mwendesha mashtaka na mbowe pia.

I hope ipo siku hawa vilaza wa Chadema wakijifunza kuacha matusi watatuelewa.
Sasa ukilaza wao upo wapi???
Nyie mlikuwa mnawaita timu gaid leo gaidi kaitwa ikulu ya magogoni na mkuu wa nchi kilaza nani kati yako wewe na hao chadema??
 
Wenzao tulifunga 40 mara mbili tukimlilia Mungu.

I don't care hata kama sitambuliki huko juu ila niliomba
 
Nilichokiandika kwenye uzi wangu hakitofautiani sana na alichokisema Fatma.

Katika ulingo wa kisheria kilichofanyika ni makosa kwa mwendesha mashtaka na mbowe pia.

I hope ipo siku hawa vilaza wa Chadema wakijifunza kuacha matusi watatuelewa.
Kwa hiyo unajifananisha na Fatma?!
 
Back
Top Bottom