#COVID19 Hoja za Askofu Gwajima zimewaumbua wataalam wetu na waliomuingiza 'mkenge' Rais Samia kwenye chanjo ya Corona

Huyo gwajima aulizwe nae swali moja. Yeye si anafufua wafu. kwanini asimfufue mwwndazake? Au atupe jibu zile zilikuwa propaganda hazina ukweli.
 
Huyo gwajima aulizwe nae swali moja. Yeye si anafufua wafu. kwanini asimfufue mwwndazake? Au atupe jibu zile zilikuwa propaganda hazina ukweli.
Ingependeza ukajibu hoja zake kwanza ndipo na wewe ukauliza swali lako
 
Kwanini mtu akichanjwa anaendelea kuambukiza /kuambukizwa?

Kama chanjo ni kinga, kwanini mtu aliyechanjwa anaendelea kuvaa barakoa?

Kwanini kwenye vaccine form serikali imejitoa kuwajibika endapo mtu aliyechanjwa atapata madhara?

Toa majibu
Mwili wako una Kinga za Magonjwa mbalimbali au hauna? Kama unazo mbona Huwa unaugua na kuambukizwa hayo magonjwa?
 
Mimi nimeshachanja 09.08.2021.
Nasikitika nimeenda kituo kimoja nimeambiwa Sina kigezo Cha kuchanja nisubiri mpaka tamko jingine la serikali.Nikawambia watu si hawataki kuchanja mie nipo tayari nichanjeni,wapo tunaanza na makundi maalum.
 
Hatuna wataalamu, tuna wachumia tumbo. Wananchi wamefanywa majuha, jana wataalamu wanasema wazungu hawaaminiki, chanjo haziaminiki. Leo hao hao, akiwemo na Samia wamebadiri wimbo, wananchi mkachanjwe, chanjo ni bora kwa kinga ya corona. Hawana aibu, wanaongea kwenye majukwaa bila kupepesa macho.
Wataalam wetu wanaujua ukweli shida moja hawajapewa Uhuru was kueleza ukweli.Kila kitu kinaratibiwa na siasa
 
Hata mm sijawahi kupata majibu haya nikaridhika. Tujiulize kama kweli Samia kachanja kwanini anavaa barakoa? Yeye ana tofauti gani na mimi ambaye sijachanja? Kuna umuhimu gani wa chanjo kama utaendelea kuchukua tahadhari zile zile?
Ninachokumbuka ni kuwa wanasema chanjo inakuwa effective kabisa wiki mbili baada ya kuchanjwa yaani sio leo unachanjwa na kesho unakuwa na askari mwili mzima...kwa hiyo tunasubiri wiki mbili zipite tuone mwelekeo...Hata hivyo chanjo hazina ufanisi wa asilimia 100 ni kama 70 hivi kwa hiyo na kujikinga kimtindo sio mbaya hasa wale wa makundi maalum kama hao wa miaka 50 au 60 plus. nawasilisha
 
Huyo gwajima aulizwe nae swali moja. Yeye si anafufua wafu. kwanini asimfufue mwwndazake? Au atupe jibu zile zilikuwa propaganda hazina ukweli.
Kufufua watu na wengine kufa ni mtindo wa maisha. Hata wakati wa Yesu Kristo watu walikuwa wanakufa na kuumwa kama kawaida. Maana yake ni kwamba sio wafu wote waliopata bahati ya kufufuliwa na Yesu kadhalika sio wagonjwa wote waliopata bahati ya kuponywa na Yesu.

Haya kazi kwako. Najua huwezi kujibu maswali yote wa Gwajima, chukua lolote unaloweza kujibu kisha lete majibu.

My take# we need to attack issues not personalities
 
Ni sayansi gani ya chanjo inayosema ujikinge baada ya kupata chanjo? Wewe ulipopigwa ndui (ikiwemo chanjo ya TB) uliambiwa uvae barakoa?
Muwe na akili basi,kwa sasa chanjo iliyopatikana ni hiyo ya kukuongezea immunity!Sasa kama unasubiri kinga kamili basi subiri!
 
Nilitegemea wataalam wetu wa afya pamoja na washauri wa Rais waliomshauri kuagiza chanjo ya corona watakuwa mstari wa mbele kujibu hoja za askofu badala yake wamekuwa watu wa kumshambulia yeye binafsi na kumpa vitisho badala ya kujibu hoza zake kitaalam.

Katika hoja ya kwanza, Askofu gwajima ana hoji: Endapo mtu akichanjwa bado ataendelea kuambukiza na kuambukizwa virusi vya corona na kama ndivyo, kuna maana gani ya kuchanja?

Hoja ya pili Askofu anahoji endapo mtu amechanjwa bado atatakiwa kuchukua tahadhari zote ikiwemo kuvaa barakoa ili kujikinga na maambukizi. Askofu anataka kujua, kama kweli chanjo ya corona ni kinga kwanini mtu aliyechanjwa anatakiwa tena kuvaa barakoa?

Askofu anaendelea kuhoji, mataifa makubwa kama vile marekani yote yana chanjo zao. Kwa mfano, marekani wana chanjo ya jonhson&jonhson na moderna, china wana sinovac, uiongereza wana Astrazeneca, germany wana Pfizer, urusi wana ya kwao, Cuba pia wana ya kwao na mataifa mengine yana chanjo zao. Je ni kwanini haya mataifa yenyewe kwa yenyewe yanaogopana kutumia chanjo ya mwingine?

Gwajima ana hoji kwamba katika kipindi cha zaidi ya miezi sita iliyopita wataalam wetu wanaotaka tupambane na corona kwa njia ya chanjo ndio hawa hawa walisema tusiziamini chanjo kwamba zinaweza kuwa na madhara na kwamba tutumie njia za asili ikiwemo kujifukiza wakajenga hadi banda la kujifukizia pale muhimbili wengine wakafanya mahojiano TBC kuonyesha wasi wasi wao juu ya chanjo ya corona, kwanini leo wamebadilika?

Swali la nyongeza: kwenye fomu ya chanjo ya corona kuna kipengele kinasema serikali haitahusika kwa namna yoyote ile endapo mtu aliyechanjwa atapata maudhi ambayo kwa sasa hayafahamiki. Tunataka wataalam wetu watwambie kama hii chanjo wameifanyia utafiti wa kutosha kwanini wanasema tena kwamba mtu aliyechanjwa anaweza kupata maudhi ambayo hayafahamiki?

Napenda sana wataalam wajibu hoja za gwajima kwa sababu vile wanavyomshambulia badala ya kujibu hoja zake ni kudhihirisha kwamba hawana utaalam wa walichosomea kitu ambacho ni hatari kwa uhai na afya za watanzania.
Hoja ya kwanza:
Mtu akipata chanjo anaweza kuambukizwa kwa sababu zifuatazo:
a. Chanjo inachukua muda kuanza kukukinga kwa kikamilifu. Nyingi ni kati ya wiki mbili au tatu. Katika dirisha hili unaweza kuambukizwa.
b. Chanjo sio 100 % katika kuzuia maambukizi. Johnson and Johnson ni kama 80% na Pfizer 90% na Moderna 90%. Ila chanjo zote zinakaribia ubora wa 100% katika kukulinda usiathirike sana. Ndio maana sasa hivi Marekani 95% ya wanaopoteza maisha yao baada ya kuambukizwa ni wale ambao hawajachanjwa.

Hoja ya pili:
Barakoa zinasaidia zaidi kukuzuia kuambukiza kuliko kuambukiza. Ndio maana kama wote mkivaa maambukizi yanapungua sana. Lakini wakiwepo wabishi basi hao wanaweza kuwaambukiza hata waliovaa barakoa. Kwa vile aliyechanjwa anaweza kuambukizwa barakoa inasaidia kumzuia kuambukiza wale ambao hawajachanjwa na kuwaletea matatizo makubwa. Mkichanjwa wengi basi uwezekano wa kuambukizana unapungua sana na hivyo kufanya barakoa kutokua na umuhimu sana. Ila kama wengi hawajachanja basi barakoa ni muhimu hata kwa waliochanja. Mfano ni ingawa tunaoga ili tuwe wasafi lakini haimaanishi kuwa
hamna haja ya kufua taulo ambalo tunatumia kujikausha baada ya kuoga. Hii ni kwa sababu hata uoge vipi kuna uchafu unabaki, kuoga hakukuhakikishii kuwa wewe ni msafi 100 %. Hivyo hivyo kwa kinga.

Hoja ya tatu.
Katika nchi za magharibi chanjo hazitengenezwi na mataifa bali makampuni binafsi yaliyokuwa na uwezo wa kutengeneza. Serikali na watu binafsi wali invest katika haya makampuni ili kuyaongezea uwezo wao. Kwa vile hamna mtu alijua kampuni ipi itafanikiwa kwanza serikali ziliweka oda katika karibu makampuni yote. Umoja wa Ulaya walikubaliana kununua kwa pamoja. Kampuni hizi zilipofanikiwa zilitangulia kuwapa wale walioweka oda zao mapema. Ndio maana Marekani amejikuta ana chanjo nyingi kuliko anazohitaji na ugomvi ulilipuka kati ya EU na Uingereza baada ya Astrazeneca kusema atatimiza kwanza oda ya Uingereza kabla ya EU. Aidha, hizi nchi zote zina taasisi zao za kutoa kibali cha chanjo kutumika. Kibali hiki kinatolewa baada ya mtengenezaji kuomba. Kwa mfano, Astrazeneca haijaomba kibali Marekani kwa hiyo haitumiki Marekani bali inatumika Uingereza na EU ambako waliomba na kupata vibali (EU na Uingereza wanatumia pia za Pfizer na Moderna). Hivyo hivyo kwa chanjo za kichina, kirusi, Cuba n.k. Haziwezi kutumika nchi za magharibi kwa sababu hawawezi kuwaomba kibali adui zao maana wanaweza kuwakatalia ili kuwapakazia tu.

Hoja ya nne.
Hii siwezi kuijibu maana sikuhusika na uamuzi wa awali wa kupinga chanjo.

Hoja ya tano.
Kwa wenzetu fomu ya kibali cha kufanyiwa tiba ni kitu cha kawaida ( hasa Marekani) kwa sababu wenzetu wanatumia vizuri haki yao ya kumshitaki yeyote ambae amemkwaza kwa namna yeyote. Gharama za kutoa huduma yeyote kwa wenzetu zinakuwa juu kwa sababu wataalam wote inabidi wakate bima ( professional indemnity insurance) ambayo itawasaidia kama tatizo lolote litatokea kutokana na kazi walizofanya. Kwa wenzetu ukijikwaa na kuanguka mbele ya duka unaweza kumpeleka mahakamani mwenye duka kuwa hakukausha maji ya mvua mbele ya duka lake na hivyo kukusababishia maumivu makubwa ya kimwili na kisaikolojia kutokana na watu kukucheka ulipoanguka. Tabia hiyo hapa kwetu haipo. Lakini haimzuii mjanja mmoja ambae akijikuta anaharisha baada ya chanjo kumshitaki mtengenezaji katika mahakama za marekani kama pasingekuwa na clause hiyo.

Haya majibu yametolewa sana maana si Gwajima peke yake aliyekuwa na wasiwasi na hizi chanjo. Tofauti yetu ni kuwa hata baada ya kupewa majibu hatutayakubali kwa sababu imani yetu ya asili ( natural instinct) ni kuwaamini waganga na matapeli wanaojifanya ni watu wa Mungu.

Wenzetu wanaendelea kuchanja na kuna uwezekano kuwa hata zile tulizokuwa tunategemea tutapata zikachelewa kwa sababu sasa hivi wanazungumzia chanjo za ku boost hizi za mwanzo.

Mwisho wa siku ni uamuzi wako, hasa kama haujauguliwa au kufiwa na mtu kutokana na janga hili.

Amandla...
 
Kama inaongeza immunity kwa nini utumie barakoa? Ulipopigwa chanjo ya polio ulihitaji booster?
Mbona huelewi?Hii chanjo iliyopatikana so far ni kwa ajili ya kuongeza uwezo wa mwili kupambana na virus!Haizuii wewe kupata Corona ila inakusaidia ukipata uwe na chance kubwa ya kuishinda kuliko kama hujachanjwa!
Hiyo ndiyo iliyopatikana,kama unataka chanjo ambayo itazuia kabisa usipate Corona basi subiri,wataalamu bado wako wanapambana!
 
Mbona huelewi?Hii chanjo iliyopatikana so far ni kwa ajili ya kuongeza uwezo wa mwili kupambana na virus!Haizuii wewe kupata Corona ila inakusaidia ukipata uwe na chance kubwa ya kuishinda kuliko kama hujachanjwa!
Hiyo ndiyo iliyopatikana,kama unataka chanjo ambayo itazuia kabisa usipate Corona basi subiri,wataalamu bado wako wanapambana!
Unaielewa sayansi ya vaccine lakini?
 
Unaielewa sayansi ya vaccine lakini?
Usichanje kama unaona bado hujaridhika!Ila hao waliokufundisha ukajua vaccine ndio hao wamekuja na suluhisho la muda mfupi la Covid!Ukitaka hicho unachotaka basi subiri!
Sio case!
 
Back
Top Bottom