Hoja ya zuio la wagombea uchaguzi Zanzibar ni mizengwe dhidi ya Maalim Seif Sharrif Hamad, haina mashiko

Shoctopus

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
3,434
1,985
Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi Hamza Juma, amejitokeza kutaka kupeleka hoja binafsi ili Baraza la Wawakilishi litunge sheria kuzuia wagombea ambao hawajtimiza miaka miwili ya uanachama wa chama cha siasa, wasigombee katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Hii ni hoja mbovu isiyo na mantiki. Ukimchunguza huyu mtu ni kama yule Jecha wa November 2015. Ametumwa.

Yote hii ni moja ya mambo yanayofanywa na CCM kuvuruga uchaguzi.

Hoja ya Hamad Juma haina tofauti na ubadilishaji wa ramani za majimbo ya uchaguzi ili kudhoofisha nguvu za wagombea wa upinzani, kama ulivyofanywa maeneo ya Segerea Tabata, Temeke/Kigamboni, Ubungo/Kibamba nk.kabla ya uchaguzi 2015. (Hii inaitwa Gerrymandering)

Bahati nzuri huyu mwakilishi ameongea kupitia DW leo mchana kwa kujiamini kabisa kwamba amesema kitu ambacho ulimwengu utamwona ana busara sana! Na hii ndiyo tabia ya baadhi ya wanasiasa wengi upande wa watawala.

Ni juzi tu dunia imeshuhudia mbinu chafu za POTUS DT dhidhi ya mtarajiwa mgombea mwenzake Joe Biden; hadi Congress kufikia hatua ya kupitisha hoja ya kumfukuza kazi.

Halafu leo anajitokeza mtu hapa nchini kutaka ulimwengu ujue kwamba tunao watu kama Trump wanaoandaa kuvuruga Uchaguzi Mkuu ujao kwa makusudi tu?

Imefika sasa hata baadhi tuliokuwa tunavumilia madudu ya muungano tunaanza kukata tamaa. Kwasababu kitu alichosema huyu mwakilishi kinahusu vyama kwanza kabla ya kuingizwa ktk sheria ya uchaguzi, ambayo ni ya Jamhuri mzima.

Kiutaratibu angeanzia kwenye katiba za vyama. Kwasababu kikatiba kila mtu ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa. Pendekezo lake linapingana na Katiba ya JMT, ingawa kwa CCM ataungwa mkono na hoja yake kupitishwa katika Baraza la Wawakilishi.

Ni wazi hizi ni njama za kuvuruga Uchaguzi Mkuu wa November huko visiwani na lengo lao liko wazi mno.
Lakini yote kwa yote tusubiri tuone kama wataendelea?

Sent from my XT1097 using JamiiForums mobile app
 
Wanamuogopa 'Simba' Maalim Seif

Sent using tecno tochi
MWALIMU SEIFU NI CCM, wanaomuunga mkono hawajui hilo masikini!
Ni kama Mzee Mrema. Na wapemba hawatalijua hilo mpaka siku Mwalimu Sefu atakapo tangulia mbele ya haki, utakapo somwa wasifu wake ndipo watakaa midomo wazi.

Wasifu wake utafanana sana na wa Bwana Sumaye, utakuwa na maneno - kwamba walikuwa watiifu kwa CCM na wamekitumikia nje na ndani ya chama kwa uadilifu mkubwa.

Ref. Maneno na ahadi za Mwalimu Sefu baada ya kutoka ughaibuni, kwamba ataapishwa!
 
Hiyo hoja ina mashiko, ili mtu awe na sifa za kupiga kura kwa Zanzibar ni lazima awe mkaazi wa eneo hilo kwa miezi 36,
Wakati sheria hii inapitishwa, CUF ilikuwa ndani ya SUK na wakaipitisha.

1581427395611.png

Anachofanya huyo mbunge ni kuhesabu kuwa mgombea akihama chama, amehamia ukaazi wa chama hicho hivyo anahitaji muda wa kutosha kupata ukaazi wa chama kingine.
P
 
Shoctopus,
Asante kwa hili chapisho. Bahati nzuri hili jambo halitakwenda mbele kwani hili halitafumbiwa macho kama walivyofanya kwa Jecha. Nawashauri wasijisumbue, yanini kujiletea taabu isiyokuwa na sababu?
 
Hiyo hoja ina mashiko, ili mtu awe na sifa za kupiga kura kwa Zanzibar ni lazima awe mkaazi wa eneo hilo kwa miezi 36,
Wakati sheria hii inapitishwa, CUF ilikuwa ndani ya SUK na wakaipitisha.

View attachment 1354521
Anachofanya huyo mbunge ni kuhesabu kuwa mgombea akihama chama, amehamia ukaazi wa chama hicho hivyo anahitaji muda wa kutosha kupata ukaazi wa chama kingine.
P

"lazima awe mkaazi wa eneo hilo kwa miezi 36" Seif hajawahi kuhama Zanzibar hivyo kuhama Chama sio kuhama makazi. Makazi (sehemu unayo kaa) ni tofauti na Kazi yako (job). Kwa kigezo hicho basi wanaobadilisha vyama wasingekuwa wakazi. Kisheria haiwezi ku stand kabisa. Seif atagombea na kumzuia ni kuharakisha vurugu tu kule mwaka huu nipagumu sana kule. Kibaya sasa kila mtu hata wa nje wote wanajua game nzima.
 
"lazima awe mkaazi wa eneo hilo kwa miezi 36" Seif hajawahi kuhama Zanzibar hivyo kuhama Chama sio kuhama makazi. Makazi (sehemu unayo kaa) ni tofauti na Kazi yako (job). Kwa kigezo hicho basi wanaobadilisha vyama wasingekuwa wakazi. Kisheria haiwezi ku stand kabisa
Hamjawahi kusikia kitu kama hicho huku bara ili kumzuia Lissu?. Kwa mijibu wa sheria, ni sheria ya ukaazi, lakini sasa ndio Mwakilishi huyo, anataka kuitroduce sheria ya ukaazi wa kisiasa!.
P
 
Hamjawahi kusikia kitu kama hicho huku bara ili kumzuia Lissu?. Kwa mijibu wa sheria, ni sheria ya ukaazi, lakini sasa ndio Mwakilishi huyo, anataka kuitroduce sheria ya ukaazi wa kisiasa!.
P

Lissu ni kitu tofauti huyu mzee anakaa sehemu hiyo kwa miaka 40, hajatoaka nje ya nchi. Lissu hayupo Tanzania wala bungeni kwa miaka zaidi ya miwili. Hizi kesi hazina uhusiano wowote. Seif hajabadilisha makazi yake. Kubadili Chama sio kubadili makazi ina maana watu wasio na chama hawana makazi. Tukienda kwenye vitambulisho na evidence Je kwenye vitambulisho vya kura vya serikali kabadili makazi, je analipa kodi sehemu hiyo. Je kwa sheria hiyo mawaziri kama Mwinyi ambao wamekaa bara kuliko seif na makamu wa Raisi na wenyewe sio wakazi! Hii sheria itakula kwa CCM zaidi. Watanzania ndiyo haya mambo yanaturudisha nyuma cha kujiuliza CCM ni kwanini wananchi hawataki kuwapigia kura? dawa ni kuweka sera za kutatua matatizo hizi mbinu hazibadilishi watu imefika wakati sasa maji yamechemka. Nashauri tusikokuwa makini uongozi wa zanzibar wote utaingizwa kwenye list pamoja na makonda na watalii kukatazwa kwenda huko tuwe waaangalifu na ku support sera ambazo hazisaidii nchi bali watu na manufaa yao ya matumbo. Kama kuna sheria ni kwanini waende tena bungeni? vilevile kwanini sheria imesubiri mpaka miezi 7 kabla ya uchaguzi. Yaani hii yenyewe inatosha Zanzibar kuwekewa vikwazo.
 
Wanasheria naombeni mtueleweshe kuhusu "retrospectivity" endapo sheria mpya ama kifungu kipya cha sheria kinapoanza kutumika, kuhusiana na hoja binafsi ambayo inataka kuwasilishwa barazani. Je! Upya huu wa sheria utaanza kuwabana viongozi waliohamia ACT Wazalendo mara tu itakapopitishwa ama la.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MWALIMU SEIFU NI CCM, wanaomuunga mkono hawajui hilo masikini!
Ni kama Mzee Mrema. Na wapemba hawatalijua hilo mpaka siku Mwalimu Sefu atakapo tangulia mbele ya haki, utakapo somwa wasifu wake ndipo watakaa midomo wazi.

Wasifu wake utafanana sana na wa Bwana Sumaye, utakuwa na maneno - kwamba walikuwa watiifu kwa CCM na wamekitumikia nje na ndani ya chama kwa uadilifu mkubwa.

Ref. Maneno na ahadi za Mwalimu Sefu baada ya kutoka ughaibuni, kwamba ataapishwa!
Wacha izo wewe zungumza facts usitoe porojo

Inamaana wewe ndio unamjua Seif kuliko watu wake wa karibu waliomzunguka?

Na hata kama ni ccm mwenzao mbona hawataki kumpa madaraka

WACHA IZO BHANA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo hoja ina mashiko, ili mtu awe na sifa za kupiga kura kwa Zanzibar ni lazima awe mkaazi wa eneo hilo kwa miezi 36,
Wakati sheria hii inapitishwa, CUF ilikuwa ndani ya SUK na wakaipitisha.

View attachment 1354521
Anachofanya huyo mbunge ni kuhesabu kuwa mgombea akihama chama, amehamia ukaazi wa chama hicho hivyo anahitaji muda wa kutosha kupata ukaazi wa chama kingine.
P
Mwambieni JPM maneno haya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom