Hoja ya Spika Ndugai: Nitawafukuzaje wabunge ambao Rufaa zao hazijasikilizwa na Baraza kuu kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA?

Mimi nadhani Chadema wanajivuta kusikiliza rufaa kwa sababu watakapoisikiliza tu na uamuzi unaotegemewa ukatolewa, wakata rufaa wataweza kwenda Mahakamani na Mahakama ina mamlaka ya kuzuia utekelezaji wa hukumu yeyote. Kwa maneno mengine, inaweza kusema wakina Halima watabaki kuwa wanachama wa CHADEMA na viongozi wa Bawacha mpaka kesi yao itakapoamuliwa. Wakishindwa hapo wanapanda Mahakama ya Rufaa na mara tayari 2025 na uamuzi bado. Wakina Halima wanajiuzulu Chadema na kujiunga na CCM na wanapewa ubunge wowote wanaoutaka. Mchezo umekwisha. Kwa hii danadana ni vigumu kwa wakina Halima kwenda Mahakamani.

Amandla...

Maelezo yako yana mantiki, possibly ndicho Chadema wanacho kikwepa.

Maana mahakama ikizuia utekelezaji wa kuvuliwa uanachama, baadhi ya covid-19 ambao ni wajumbe wa kamati kuu waendelee kuhudhuria vikao vya chama kama kawaida huku wakiwa mguu mmoja CCM na mguu mwingine CDM.
 
Hoja kuu sio kufukuzwa. CHADEMA wanadai hawajawateua hao wabunge kupitia vikao vyao vya kikatiba. Hapo Mh Dugai mbona anapakwepa? Kufukuzwa likikuwa ni zao la kukiuka utaratibu za chama.

Chama chao kimesema hakijawateua kwa kuwa hakuna vikao vilivyokaa. Mbona hakikusikilizwa? Vikao vya rufaa ndio muhimu sasa?

Hata kama utaratibu wa kuwafukuza haukufuatwa, lakini hilo la kuteuliwa na vikao ama la ni factual issue. Kwa hivyo hoja kuu ni kuwa hawakuteuliwa na Chadema kama sheria inavyotaka, hiyo ya kutokuwa wanachama wa chama cha siasa ni nyongeza ambayo haina athari kwenye hoja kuu.

Pathetic!
Ndungai anajichanganya kwa kudai muhtasari wa kikao kilicho wasimamisha Halima na wenzake,lakini hazungumzii muhtasari wa kikao cha Chadema kilichowateua.
Aidha Ndungai anajulikana kwa dharau zake na upindishaje wa wazi wa sheria za nchi,sote ni mashahidi pale alipomrudisha bungeni mbunge Mwambe ambaye alikuwa amepoteza ubunge wake baada ya kujiunga na CCM akitokea Chadema.
 
Hao chadema wako very very selfish Yani wew mwanaume unapigania mwanamke afukuzwe kazi yake kisa wew huna that's very foolishness and stupidity, Spika kawajibu kwa hoja sana sana huwezi tu kumfukuza kazi mtu hivi hivi bila a fair justice never..
Wameshtuka sasa hivi wanatumika Bawacha ya Mbeya....wanasoma tamko lenye mwandiko wa kiume
 
Kipi kinatangulia kati ya kuvuliwa Ubunge na kusikilizwa rufaa?
Hapo kinachotangulia ni majina ya waliopendekezwa na kamati kuu ya Chadema kupelekwa kwenye Tume ya uchaguzi.
Kitu ambacho hakikufanyika,badala yake taasisi za serikali zikafanya uhuni wa kugushi nyaraka.
 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.

Kwa mujibu wa katiba ya Chadema Baraza kuu ndio lenye maamuzi ya mwisho ya kumvua mtu uanachama endapo hajaridhika na utaratibu wa awali.

Anachohoji Spika Ndugai ni kama wabunge hao akina Halima Mdee walipewa fursa ya kusikilizwa na kama ndio ameomba mihtasari ya vikao husika ili ajiridhishe na kuchukua maamuzi stahiki.

Ni vema JJ Mnyika akatoka na kuzijibu hoja za Spika Ndugai kwa mujibu wa katiba na siyo blah blah.

Mnyika aseme tu kwanini anasita kuitisha kikao cha baraza kuu ili kukata mzizi wa fitina?

Pia J J Mnyika aufahamishe Umma iwapo wabunge wote 19 hawakuridhika na maamuzi ya kamati kuu hivyo walikata rufaa au kuna baadhi waliridhika na maamuzi hayo kama alivyokiri mjumbe wa kamati kuu mh Jesca Kishoa.

Hili swala linatutia doa kama taifa ni vema likamalizwa sasa.

Tusisahau kufuatilia hotuba ya Rais Samia bungeni leo.

Kazi Iendelee!
Spika Ndugai yuko sahihi.

Moja ya Haki za Mwanachama kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA (2016):5.2.4 Kujitetea, kusikilizwa na kukata rufaa anaposhitakiwa ama kuchukuliwa hatua za kinidhamu kichama.

Wanaodaiwa kufukuzwa walikata rufaa ambayo hadi sasa haijasikilizwa. Na kwa kuzangatia Viongozi wa CHADEMA wamekuwa wakidai demokrasia, ni wakati mwafaka wa wao kuonyesha demokrasia ndani ya chama.

Kwa sababu hizo hao bado ni wanachama halali wa CHADEMA hadi hapo rufaa yao itakaposikilizwa.
 
Spika Ndugai yuko sahihi.

Moja ya Haki za Mwanachama kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA (2016):5.2.4 Kujitetea, kusikilizwa na kukata rufaa anaposhitakiwa ama kuchukuliwa hatua za kinidhamu kichama.

Wanaodaiwa kufukuzwa walikata rufaa ambayo hadi sasa haijasikilizwa. Na kwa kuzangatia Viongozi wa CHADEMA wamekuwa wakidai demokrasia, ni wakati mwafaka wa wao kuonyesha demokrasia ndani ya chama.

Kwa sababu hizo hao bado ni wanachama halali wa CHADEMA hadi hapo rufaa yao itakaposikilizwa.
Nimekuelewa bwashee!
 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.

Kwa mujibu wa katiba ya Chadema Baraza kuu ndio lenye maamuzi ya mwisho ya kumvua mtu uanachama endapo hajaridhika na utaratibu wa awali.

Anachohoji Spika Ndugai ni kama wabunge hao akina Halima Mdee walipewa fursa ya kusikilizwa na kama ndio ameomba mihtasari ya vikao husika ili ajiridhishe na kuchukua maamuzi stahiki.

Ni vema JJ Mnyika akatoka na kuzijibu hoja za Spika Ndugai kwa mujibu wa katiba na siyo blah blah.

Mnyika aseme tu kwanini anasita kuitisha kikao cha baraza kuu ili kukata mzizi wa fitina?

Pia J J Mnyika aufahamishe Umma iwapo wabunge wote 19 hawakuridhika na maamuzi ya kamati kuu hivyo walikata rufaa au kuna baadhi waliridhika na maamuzi hayo kama alivyokiri mjumbe wa kamati kuu mh Jesca Kishoa.

Hili swala linatutia doa kama taifa ni vema likamalizwa sasa.

Tusisahau kufuatilia hotuba ya Rais Samia bungeni leo.

Kazi Iendelee!
Bwasheee buku 7 tangu uzikose umekua hufikirii kabisa. Issue kubwa sio rufaa wala nini. Issue ni...walipelekwaje huko bungeni na kuapishwa. List ilitoka wapi? Walijichukulia uamuzi na kushirikiana na serekali dhaifu wakatengeneza list yao hao ma covid 19. Wamefukuzwa hasa hasa kwa hilo. Na huo ndio mzizi wa fitna. Nani aliwapitishaaaaaaaaa???? this is the stem of the problem in hand that led to their being fired.
 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.

Kwa mujibu wa katiba ya Chadema Baraza kuu ndio lenye maamuzi ya mwisho ya kumvua mtu uanachama endapo hajaridhika na utaratibu wa awali.

Anachohoji Spika Ndugai ni kama wabunge hao akina Halima Mdee walipewa fursa ya kusikilizwa na kama ndio ameomba mihtasari ya vikao husika ili ajiridhishe na kuchukua maamuzi stahiki.

Ni vema JJ Mnyika akatoka na kuzijibu hoja za Spika Ndugai kwa mujibu wa katiba na siyo blah blah.

Mnyika aseme tu kwanini anasita kuitisha kikao cha baraza kuu ili kukata mzizi wa fitina?

Pia J J Mnyika aufahamishe Umma iwapo wabunge wote 19 hawakuridhika na maamuzi ya kamati kuu hivyo walikata rufaa au kuna baadhi waliridhika na maamuzi hayo kama alivyokiri mjumbe wa kamati kuu mh Jesca Kishoa.

Hili swala linatutia doa kama taifa ni vema likamalizwa sasa.

Tusisahau kufuatilia hotuba ya Rais Samia bungeni leo.

Kazi Iendelee!
Spika aache blabla, Rufaa haitengui hukumu hadi hapo Rufaa itakapo elekeza vinginevyo.

Alipe GHARAMA ZA KIBURI CHA MADARAKA.
 
Spika wa bunge mh Job Ndugai hana tatizo na wabunge wa viti maalumu wa Chadema akina Halima Mdee na wenzake bali anachotaka ni utaratibu wa natural justice kufuatwa.

Kwa mujibu wa katiba ya Chadema Baraza kuu ndio lenye maamuzi ya mwisho ya kumvua mtu uanachama endapo hajaridhika na utaratibu wa awali.

Anachohoji Spika Ndugai ni kama wabunge hao akina Halima Mdee walipewa fursa ya kusikilizwa na kama ndio ameomba mihtasari ya vikao husika ili ajiridhishe na kuchukua maamuzi stahiki.

Ni vema JJ Mnyika akatoka na kuzijibu hoja za Spika Ndugai kwa mujibu wa katiba na siyo blah blah.

Mnyika aseme tu kwanini anasita kuitisha kikao cha baraza kuu ili kukata mzizi wa fitina?

Pia J J Mnyika aufahamishe Umma iwapo wabunge wote 19 hawakuridhika na maamuzi ya kamati kuu hivyo walikata rufaa au kuna baadhi waliridhika na maamuzi hayo kama alivyokiri mjumbe wa kamati kuu mh Jesca Kishoa.

Hili swala linatutia doa kama taifa ni vema likamalizwa sasa.

Tusisahau kufuatilia hotuba ya Rais Samia bungeni leo.

Kazi Iendelee!
Sehemu yoyote ile ya kazi, ukifukuzwa inabidi uondoke hapo sehemu ya kazi - iwe kufukuzwa kwako kumefuata utaratibu au la - na kama mhusika ataona utaratibu wa kufukuzwa haukufuatwa, atakata rufaa na kukata rufaa huwa hakuna maana kwamba mgogoro umeisha, bali ni fursa kwa mwathiriwa kujiridhisha kama ABC za kufukuzwa kwake zimefuata utaratibu au la. Siyo desturi ya mtu kufukuzwa sehemu na kung'ang'ania kubaki hadi hapo rufaa yake itakaposikilizwa. Kwa upande wa hao wabunge 19 waliofukuzwa na chama chao, ilibidi waheshimu uamuzi wa chama chao na wakate rufaa kama walivyofanya - na kukata rufaa ina maana kwamba wanakiri kuwa walishafukuzwa na kama walishafukuzwa na wamakiri hivyo kwa kukata rufaa, then wamekosa sifa za kuwa wabunge na ilibidi wasiwepo bungeni kama wabunge, otherwise hakuna mantiki ya wao kukata rufaa kama chama hakijawafukuza na hakuna mantiki ya kubaki bungeni kama walishafukuzwa na kuonyesha kwamba wamefukuzwa wamekata rufaa.
 
Hivi kwani Chadema wakiteua wabunge na kuwapeleka Bungeni badala ya waliopo kuna tatizo gani?
Je ni lazima kina Halima na kundi lake ndio lazima wawe wao tu ?
Ina maana kina Halima na kundi lake ni wakubwa kuliko Katiba ya Chadema?
Ina maana kanuni,taratibu za Bunge pamoja na katiba za vyama vya siasa ni kubwa /muhimu kuliko Katiba ya nchi?
 
Iblis namba moja ameshatangulia yy namba mbili hv punde tu atafuatia
hajawahi peleka hata medical report bungeni akataka tu spika aamini kuwa anaumwa!!! Bila documentary evidence alitaka spika afanyaje? kwa nini akina mbowr walikaa nairobi mwezi mzima kwa kujitia wanauguza wakati wao sio madaktari wala manesi kwa nini hawakupeleka medical report kwa spika?
 
Hivi kwani Chadema wakiteua wabunge na kuwapeleka Bungeni badala ya waliopo kuna tatizo gani?
Je ni lazima kina Halima na kundi lake ndio lazima wawe wao tu ?
Ina maana kina Halima na kundi lake ni wakubwa kuliko Katiba ya Chadema?
Ina maana kanuni,taratibu za Bunge pamoja na katiba za vyama vya siasa ni kubwa /muhimu kuliko Katiba ya nchi?
Unakuwa mbunge baada ya kuapishwa na Spika. Chadema hata wakiteua wengine na NEC wakayapeleka majina kwa Spika, Spika akigoma kuwaapisha ndio basi tena.

Ukimya wa NEC baada ya kukiri kuwa hawajapokea barua kutoka Chadema speaks volume. Wangekuwa huru wangeweza kumaliza mgogoro huu kwa kuweka wazi barua waliotumia kupeleka majina kwa Spika au wangesema hawajapeleka majina yeyote kwa Spika.

Amandla...
 
Hoja kuu sio kufukuzwa. CHADEMA wanadai hawajawateua hao wabunge kupitia vikao vyao vya kikatiba. Hapo Mh Dugai mbona anapakwepa? Kufukuzwa likikuwa ni zao la kukiuka taratibu za chama.

Chama chao kimesema hakijawateua kwa kuwa hakuna vikao vilivyokaa. Mbona hakikusikilizwa? Vikao vya rufaa ndio muhimu sasa?

Hata kama utaratibu wa kuwafukuza haukufuatwa, lakini hilo la kuteuliwa na vikao ama la ni factual issue. Kwa hivyo hoja kuu ni kuwa hawakuteuliwa na Chadema kama sheria inavyotaka, hiyo ya kutokuwa wanachama wa chama cha siasa ni nyongeza ambayo haina athari kwenye hoja kuu.

Pathetic!
Kuthibitisha km waliteuliwa ama hawakuteuliwa ni kazi ya tume na sii spika wala bunge,
 
Unakuwa mbunge baada ya kuapishwa na Spika. Chadema hata wakiteua wengine na NEC wakayapeleka majina kwa Spika, Spika akigoma kuwaapisha ndio basi tena.

Ukimya wa NEC baada ya kukiri kuwa hawajapokea barua kutoka Chadema speaks volume. Wangekuwa huru wangeweza kumaliza mgogoro huu kwa kuweka wazi barua waliotumia kupeleka majina kwa Spika au wangesema hawajapeleka majina yeyote kwa Spika.

Amandla...
CDM hawaelewi nini wanataka

Ukishindwa kudai haki yako kwa njia sahihi/ kufuata taratibu stahiki hutoipata na utajihisi unaonewa, kumbe wewe mwenyewe ndio unajionea pasipo kujua
 
Mnyikia ni mhuni halafu hajui kuwa mbowe anajuwa ishu yote ndiyo maana kakaa kimya amebakiyeye na BAWACHA.
Huu ni msigano wa makundi mawili hasimu ndani ya chadema. Kundi la mbowe ambalo ndilo liliridhia huo uteuzi kwa kulizunguka kundi la lisu ambalo lilitaka kila kitu kisusiwe baada ya matokeo ya uchaguzi. Mnyika yuko kundi la lisu!
 
CDM hawaelewi nini wanataka

Ukishindwa kudai haki yako kwa njia sahihi/ kufuata taratibu stahiki hutoipata na utajihisi unaonewa, kumbe wewe mwenyewe ndio unajionea pasipo kujua
Wanajielewa sana. Wanafanya hivi kutokana na experience yao. Wamefuata njia sahihi ya kumuandikia Spika nini kimetokea na wamepata nini?
Mara nyingi mtu ambae una uhakika amekudhulum akikuambia fuata njia fulani ili upate haki yako ujue kuwa hiyo njia anaimiliki na ana jua hutafika popote.

Ni bora waendelee kufanya wanachofanya kuliko kuingia gharama za kufungua mashtaka ambayo hatma yake wanaijua.

Amandla...
 
Wanajielewa sana. Wanafanya hivi kutokana na experience yao. Wamefuata njia sahihi ya kumuandikia Spika nini kimetokea na wamepata nini?
Mara nyingi mtu ambae una uhakika amekudhulum akikuambia fuata njia fulani ili upate haki yako ujue kuwa hiyo njia anaimiliki na ana jua hutafika popote.

Ni bora waendelee kufanya wanachofanya kuliko kuingia gharama za kufungua mashtaka ambayo hatma yake wanaijua.

Amandla...
hawajaambiwa wafungue mashtaka, wameambiwa wapeleke viambatanishi vya madai yao & hiyo ni kwa mujibu wa katiba yao
 
hawajaambiwa wafungue mashtaka, wameambiwa wapeleke viambatanishi vya madai yao & hiyo ni kwa mujibu wa katiba yao
Katiba ambayo Spika haijui maana ametaka apelekewe nakala? Hamna Katiba ya Chadema inayozungumzia viambatishi. Na Chadema hawajampelekea Spika madai bali wamempa taarifa. Wanachokidai sasa ni afuate Katiba ya nchi ( sio ya CDM) inavyosema kuhusu sifa ya mbunge.

Amandla..
 
Ndungai anajichanganya kwa kudai muhtasari wa kikao kilicho wasimamisha Halima na wenzake,lakini hazungumzii muhtasari wa kikao cha Chadema kilichowateua.
Aidha Ndungai anajulikana kwa dharau zake na upindishaje wa wazi wa sheria za nchi,sote ni mashahidi pale alipomrudisha bungeni mbunge Mwambe ambaye alikuwa amepoteza ubunge wake baada ya kujiunga na CCM akitokea Chadema.
Pia anashangaa wao kufukuzwa na chama wakati yeye alikuwa akiwafukuza baadhi yao bungeni na kutohudhuria vikao vya bunge miezi kadhaa.
 
Back
Top Bottom