Hoja ya Moto: Hakuna dharau mbaya kama ya kudharauliwa akili

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Na. M. M. Mwanakijiji

Mtu anaweza kukudharau kwa vitu vingi sana; anaweza kukudharau kwa sababu huvai nguo kama za kwake, huna gari kama lake, unaishi maisha duni, au hata huzungumzi kwa ufasaha kama yeye. Dharau kubwa walizonazo watu dhidi ya wengine zinahusiana hasa na hadhi (status), mali (material wealth) na hali ya kijamii (social condition). Dharau hizi kubwa tatu zinawafanya wenye hadhi ya juu, au wenye mali zaidi au wenye kuonekana juu katika jamii wakati mwingine kuwaona wale wasio kama wao kama watu walio "chini yao". Inapuzungumzwa chini yao si kama mtu ambaye anakufikia kwa chini labda miguuni au magotini; la hasha ni kuwa 'beneath you" yaani kama ni chini ya soli zako.

Lakini dunia imejawa na mifano ya watu waliodhaniwa wako chini ambao kutokana na juhudi zao au mchanganyiko wa vitu mbalimbali wakajikuta na wao wananyanyuka kutoka huko "chini" na kupanda ngazi na kuwa juu. Wakati mwingine ni hawa hawa ambao waliwahi kuwa chini ndio ambao nao wakishafika juu huanza kuonesha dharau kwa walio chini yao. Bila ya shaka wengine ambao wametoka chini na kufika juu huwa na mtazamo wa huruma na simanzi kwa walio chini na hujitahidi kuwanyanyua.

Wakati mwingine mtu mwenye dharau hizi kubwa tatu hawezi kuridhika anapoona aliye chini naye ameanza kunyanyuka. Wapo ambao wanaweza kutumia njia mbalimbali ili kuhakikisha wale walio chini wanaendelea kuwa chini iwe kihadhi, hali au mali. Na hawa hutumia njia nyingi sana kuhakikisha wale walio chini hawawafikii pale juu. Hivyo, huwekwa vikwazo viwe vya sheria au kanuni kuhakikisha kuwa aliye chini anaendelea kuwa chini.

Tawala nyingi duniani zimejengwa kwa msingi huo. Kwamba wale ambao wanatawala huamini kuwa wanapasa kutawala au wana haki ya kutawala na hivyo huwaona watawaliwa wao kuwa wako chini. Matokeo yake watawala wa aina hii duniani hufanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa watawaliwa hawainuki na kutaka kuwa juu ya watawala. Kwa muda - hasa kama watawaliwa hawajafunguka kifikra - hali hii (status quo) hukubalika na yumkini hata kwa vizazi na vizazi. Vipo vizazi vya watu katika jamii mbalimbali duniani ambao wamekubali hali hiyo kuwa ni haki au stahiki yao.

Hata hivyo utaona kuwa jamii ya watu yenye kutawaliwa kwa msingi huo kwa kweli kabisa haidharauliwi kwa mambo hayo matatu bali jambo moja tu - akili. Kuna hisia kwa watawala kuwa wao wana "akili sana" kiasi kwamba ndio maana wanatawala na wale watawaliwa hawana "akili kihivyo" ndio maana wanatawaliwa. Matokeo yake watawala huanza kuwaangalia watawaliwa kwa dharau; dharau ya kuwaona kuwa hawastahili hata kuwahoji, kuwauliza au kuwakatalia. Watawala hao huamini kuwa wanaweza kufanya lolote, vyovyote na kwa yeyote na watawaliwa waliokubali hilo huamini wanaweza kufanyiwa lolote, vyovyote na yeyote kutoka kona za watawala.

Ni hili ambalo hatimaye huwa msingi wa mgongano kati ya watawala na watawaliwa. Kwamba watawaliwa ambao "wamefunguka" wanapoamua kukataa au kuwakatalia watawala. Hakuna kitu ambacho kinawashangaza watawala kama watawaliwa wasiokubali hadhi, hali na mali yao duni. Inawashangaza kwa sababu hawaamini kama watawaliwa wanaweza kuwa na "akili" za kujitambua kuwa wao ni nani. Tena watawala wanaweza hata kuzungumza kwa dharau; utasikia wanasema "wananchi wetu hawajui" au "inabidi tuwaelimishe kwanza wananchi" au "wananchi wanadanganywa na upinzani"; kimsingi wanaona wananchi hawana akili ya kuweza kufikiria wenyewe na kuamua kutenda kutokana na matokeo ya fikara zao.

Ni dharau inayoshangaza sana kwani hawa watawala wanawadharau watu wale ambao wamewapoa wao madaraka. Yaani, walipowapa madaraka (kwa kuwachagua na kufanya kazi kulipa mishahara yao) wananchi hawana hawana akili za kutambua wanapoburuzwa au kudanganywa au kuuziwa maneno na ahadi hewa! Walikuwa na akili walipopiga kura lakini walipotaka kujua kura zao zinafanyaje kazi wananchi hawa hawaaminiwi!

Sasa, wananchi ambao wanaamini kuwa watawala ndio wana akili zaidi kuliko wao hawawezi kamwe kuwahoji watawala wao. Watathubutu vipi wakati watawala ndio "elite"? Wananchi ambao wameambiwa "hawajui" au "hawana uwezo wa kujua" wataweza vipi kuhoji watawala kuhusu fedha, utendaji, au sera fulani fulani. Mara nyingi wananchi wanaojaribu kufanya hivyo hunyamazishwa kwa kuambiwa "serikali imejizatiti" au "serikali inajipanga" au "serikali iko mbioni"! Mtu ambaye ana akili akiuliza "mbona mmekuwa mkisema mnajizatiti, kujipanga na kuwa mbioni tangu mwaka elfu mia tisa kweusi?" watawala hapo hucharuka na kumuona huyo mtu kama mleta majungu, anachonganisha watu na "anajifanya anajua sana" wengine wanamuita "kimanyi"

Ndugu zangu, kwa nchi yetu hapa ndipo ilipochangamoto ya kizazi kipya cha Watanzania. Je wataendelea kuambiwa na kupigishwa stori na watawala mpaka lini? NI kwa muda gani wananchi wenye akili wataendelea kuambiwa visingizio na sababu zisizo na kichwa wala miguu na wao wakakubali? Ni jinsi gani waandishi wa habari wanaweza kukaa chini na kusikiliza masimulizi ambayo hayaingii kichwani lakini wanashindwa kuhoji au kukataa kwa sababu wanaogopa labda wataonekana wanakimbelembele. Au mtu anaweza kuelezea vipi waandishi ambao wanaenda kusikiliza "mkutano wa waandishi wa habari" na kushika kalamu na vinasa sauti zao na baadaye wanaondoka bila hata kutaka kuuliza maswali? Mtu akishakudharau akili anaweza kukuambia lolote!

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema lile neno maarufu - mtu mweye akili akikushauri jambo la kipumbavu akijua kuwa na wewe una akili halafu na wewe ukakubali atakudharau. Ni kweli; lakini mimi naweza kusema mtu mwenye akili akifikiria kuwa wewe huna akili halafu akakuambia jambo la kipumbavu na wewe ukakubali basi amethibitisha kukudharau kwake. Ndio maana mojawapo ya maneno tuliyojifunza wakati wa kupigania huru bado yanarindima kiukweli - tumedharauliwa kiasi cha kutosha! Lakini ukiangalia sana utaona kuwa Watanzania bado hawajachoshwa kudharauliwa; walichoshwa kudharauliwa na wazungu tu! Leo hii wanapodharauliwa na watawala weusi hawawezi hata kuhoji; hawawezi kukataa na kwa hakika hawawezi hata kuonesha kuwa wanatambua wamedharauliwa!

Mpaka kizazi cha watakaokataa kudharauliwa na watawala kitakapoinuka. Kwa mbali naweza kukiona kizazi hicho kikichukua nafasi yake taratibu. Angalia vijana, angalia madaktari, angalia wafanyakazi - wapo kati yao kundi la wale wasiokubali kudharauliwa na watawala. Je waweza kujua kama wewe hujali kudharauliwa na unakubali kudharauliwa? Naam!

Jiulize ukisikia "serikali imesema" mwitikio wako ni nini? je unahoji? Je unapima kama inaingia akilini? je unaona kuna vitu haviko sawa? au unafunga mjadala na kukubali bila kuhoji?

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
 
Niliwahi kuweka uzi jukwaa la Intelligence nikiuliza maana ya akili ni nini.Je akili ni hewa(vacuum)_,ni kitu kigumu(yabisi)au kimiminika?Do we measure it in quantity or in quality?.Hata hivyo uzi wangu Mods kwa sababu wanazojua wao waliutupilia mbali.
 
Niliwahi kuweka uzi jukwaa la Intelligence nikiuliza maana ya akili ni nini.Je akili ni hewa(vacuum)_,ni kitu kigumu(yabisi)au kimiminika?Do we measure it in quantity or in quality?.Hata hivyo uzi wangu Mods kwa sababu wanazojua wao waliutupilia mbali.

Inawezekana kwa wengine ni swali la kifilosofia wakati kwa wengine hili ni swali la kisaikolojia wakati wengine wanaliangalia kama swali la Kibiolojia. Hata hivyo siyo lengo la mada hii.
 
MMM.
Ni kweli tumedharauliwa sana sana, tumefanywa wajinga kiasi Cha kutosha, Na hii inakera mno.
Tatizo ni kwamba, wapi tutahoji? Hata Kama tukihoji tutaambiwa yaleyale ya upumbavu, Tutaendelea kudharauliwa. Labda kuwe Na move zaidi ya kuhoji, mass strike itakuwa dawa, but who has the guts? We have fear and we are the loosers.
 
Tunahitaji mapinduzi ya kutodharauliwa na watawala. Binafsi nachukulia kuwa mtu/serikali inayotawala huku ikidharau na kuwalazimisha kwa kutumia dola kuwa hawana akili, huo ni udikteta of high level.
 
Mwanakijiji umenena vema. Ila sisi tunatawaliwa badala ya kuongozwa. Mabadiliko ya akili kwa mwanadamu mpaka kuleta mabadiliko ya kimaendeleo huchukua muda. Wanatupa elimu darasani duni ila hawajui elimu dunia kwa sasa ikoje kwenye vichwa vyetu. Nishakutana na mtu hajui kuandika hata kusoma vizuri lakini upeo wake wa kuchambua mambo utadhani alipita chuo. Elimu ya uraia inasambaa kwa haraka sana ndio njia ya ukombozi pekee.
 
Kwanini msiijadili hii hoja kama ilivyo bila kuhusisha siasa?
Unapoonewa, si lazima anaekuonea akudharau kuwa huna akili. Na unapotoa maelezo (explanation) ya kitu fulani, ni wewe ndiye unayeamini hiyo explanation hata kama unadanganya. Kuamini kupo kwa aina nyingi.

Ni sawa na mhubiri akikwambia utaponywa upofu ilhali akijua kuwa haijawahi kutokea mtu kupona upofu kwa maombi, lakini ndivyo anavyoamini either kiuhakika au kwa kusadikika.

Mtu akijua kuwa huna akili (intelligence), hakudharau bali mara nyingi hutumia muda wake mwingi kukuonyesha anachojua au kukuonyesha usichojua.
 
Mfalme anamasikio kama ya punda,Tolwa akala gizani na sizitaki mbichi hizi.

Je tamu ziko wapi?

"Not every white man is your enemy and not every black man is your brother"~Lucky DUBE
 
Kwanini msiijadili hii hoja kama ilivyo bila kuhusisha siasa?
Unapoonewa, si lazima anaekuonea akudharau kuwa huna akili. Na unapotoa maelezo (explanation) ya kitu fulani, ni wewe ndiye unayeamini hiyo explanation hata kama unadanganya. Kuamini kupo kwa aina nyingi.

Ni sawa na mhubiri akikwambia utaponywa upofu ilhali akijua kuwa haijawahi kutokea mtu kupona upofu kwa maombi, lakini ndivyo anavyoamini either kiuhakika au kwa kusadikika.

Mtu akijua kuwa huna akili (intelligence), hakudharau bali mara nyingi hutumia muda wake mwingi kukuonyesha anachojua au kukuonyesha usichojua.

Kumbe watawala wanatumia muda wao mwingi kutuonesha watawaliwa vitu gani tusivyovijua na vitu gani wanajua.

Nanikweli even KOVA amedhihirisha hilo,amejaribu kutuonyesha kile anachodhani sisi hatukijui,kumbe tunauelewa wa kung'amua, kunahaja gani ya kuwa na watu wa aina yake kama mtawala?

Kule zanzibar kuna maukumbi ya sanaa za majukwaani,nadhani panafaa sana kwa muigizaji kama yeye.
 
Nimelala nikitafakari kauli ya Kova na kung'amua kuwa yeye na viongozi wengine wana tudharau watanzania kwa viwango vya dahari za kale!
Ona hii kauli "Mtu huyo ni mkenya aliye kodiwa na mtu ambae hamfahamu vizuri ili kumteka na kumtesa Ulimboka...., mtu huyo ni mkenya alie enda kutubu dhambi kanisani, (kanisa la gwajima) baada ya kutenda dhambi hiyo...... Wanakundi lao huko kenya...".
Hawa jamaa wametudharau viwango vya kutosha na hakika wanadhani kuwa akili zetu ndogo na zinatawala akili kubwa.
Kwa nini watu wawe na imani na hivi vyombo kwa kauli hizi?
 
Mara nyingi mwenye dharau anapata kiburi cha kuendelea kumdharau mtu, kwa kuwa mdharauliwa amekubali kudharauliwa, "amejidunisha" anajiona si kitu!
Nasema sio wote, ila zaidi ya 75% ya watanzania maamuzi yao huangalia upepo wa vipenzi vyao aidha katika siasa au dini, pasi kuhoji "critically" kwa vile Lowassa, au Slaa, au Kikwete, au Simba, au Pengo, au Kakobe, au Mbowe, au Lipumba, au Sitta, au Lema,nk amesema hivi, basi na mimi ndio hivyo hivyo! Pumbavu! Hata Mungu ameruhusu kumdharau mtu huyu, lakini ole wake atumiaye ujinga wake kujinufaisha binafsi (kama wafanyavyo wote tajwa hapo juu)
Tusiukimbie ukweli, "watanzania hatupendi kuumiza vichwa".
TUKIENDELEA KUJIDHARAU kamwe HAWATAACHA KUTUDHARAU.
Ni hayo tu Mwanakijiji.
Mungu wetu anaita!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom