Na Bwanku M Bwanku
Hekaheka na pilika za kampeni zinaendelea kutimua vumbi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi kwa wagombea wa Urais, wabunge na madiwani kunadi Sera na Ilani zao wanazoenda kuzitekeleza kwa miaka mitano ijayo kama wananchi wakiwapa ridhaa yao.
Kwa bahati nzuri sana nimeendelea kufuatilia kwa kila jambo linaloendelea kwenye kampeni hizi na leo kwa uchache kidogo nitazungumzia kwa uchache tabia ya upotoshaji inayotumiwa na kuota mabawa kwa baadhi ya wagombea wa vyama mbalimbali.
Ukiachana na baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani kuwakashfu kwa kutweza utu na heshima ya watumishi wetu wa umma wote wanaofanya kazi kubwa usiku na mchana kwa kuwaita watu waliokotwa majalalani lakini zaidi nimesikia mara kadhaa wagombea haohao wa vyama vya upinzani wakipotosha kuhusu maslahi ya watumishi wa umma na mambo mbalimbali yanayowahusu watumishi wetu.
Nimewasikia wakipotosha waziwazi kuhusu hoja ya maslahi kwa watumishi wa umma bila hata ya kuogopa kama maneno yao yanaweza kuichonganisha Serikali, jamii na watumishi wetu wanaofanya kazi kubwa sana. Sasa njia ya muongo ni fupi na wala hakawii kuumbuka.
Kimsingi Serikali ya awamu ya 5 chini ya Dkt. John Pombe Magufuli imeshughulikia maslahi ya watumishi wa umma kwa kiasi kikubwa sana tangu iingie madarakani Novemba 2015 hadi sasa.
Zifuatazo ni hatua mbalimbali na chache tu kati ya nyingi zilizochukuliwa na Serikali ya awamu ya 5 kushughulikia changamoto na maslahi ya watumishi wa umma wote nchini. Nayasema haya ili kuondoa huu upotoshaji wa wachache wasiolitakia mema Taifa letu. Twende pamoja.
1. Malipo ya malimbikizo ya mishahara.
Mpaka Novemba, 2020 Serikali imelipa Tsh. Billioni 137 kwa watumishi 76,332. Kati ya watumishi hao walimu ni 41,385 waliolipwa Tsh. Bil. 45.5 na watumishi wasio walimu ni 34, 947 waliolipwa Tsh. 91.6. Haya ni malimbikizo yaliyokuwa kero kwa watumishi kwa miaka na miaka. Halafu mtu anakuja kupotosha kuhusu maslahi ya watumishi hapa. Hapana! tutaongea ukweli.
Hiki ni kiwango cha juu kabisa cha malipo ya malimbikizo kufanyika kwa kipindi cha miaka mitano katika historia ya nchi yetu.
2. Watumishi kupandishwa vyeo na madaraja.
Serikali ya awamu ya tano hadi August, 2020 imewapandisha madaraja na vyeo watumishi wapatao 246,637. Kati ya watumishi hao, walimu 161,655 walipandishwa vyeo na kulipwa Tsh. Billioni 33.28, watumishi wasio walimu ni 91,982 waliolipwa Tsh. 27.47.
Serikali yoyote duniani ni lazima itambue watumishi wake, na kuwathamini kwani ndio nyenzo na kichocheo cha maendeleo katika nchi. Serikali imekusudia kuendelea kupandisha vyeo watumishi wake watakaokidhi vigezo kama inavyohitajika zaidi.
3. Nyongeza ya mwaka ya mshahara (Annual Increment).
Baada ya zoezi la uhakiki wa watumishi kukamilika Serikali ilitoa nyongeza ya mwaka ya mshahara kwa watumishi wa umma 505,985 kwa mujibu wa utaratibu. Jumla ya Tsh. bilioni 72.8 ziliongezeka, kati ya kiasi hicho Tsh. 37.2 zililipwa kwa walimu 270,878 na Tsh. bilioni 35.7 zililipwa kwa watumishi wasio walimu.
4. Ongezeko la mishahara kwa kiwango kisichotozwa kodi.
Pamoja na kupandisha vyeo watumishi wa Umma, kulipa malimbikizo yaliyorithiwa kutoka awamu ya nne, kutoa nyongeza ya mishahara na ajira vilevile Serikali ya awamu ya 5 imepandisha kiwango cha mshahara usiotozwa kodi.
Hatua hiyo imeongeza imeongeza pato halisi la mshahara (take home) kwa wastani wa Tsh. 100,000/= kwa kila mfanyakazi wa umma na sekta binafsi. Kwa kipindi cha mwezi July, 2020 hadi June, 2021 Serikali itatumia Tsh. billioni 517 kama ongezeko la pato halisi kwa watumishi wa umma. Hatua hii imeanza kutekelezwa kuanzia mwezi July, 2020. Halafu mtu aseme tofauti kwa maslahi ya watumishi wa umma.
5. Ajira mpya.
Serikali zote duniani haziwezi kuajiri watu wake wote peke yake isipokuwa ni lazima iwezesha na kuweka mazingira mazuri ya watu kuajiriwa na kujiajiri pia. Serikali ya awamu ya 5 imezalisha ajira nyingi kwa kuwezesha sekta binafsi kuajiri lakini pia Serikali yenyewe kuajiri jumla ya vijana 66,178. Jumla ya Tsh. billioni 54.9 zimeongezeka kila mwezi katika sekta ya ajira. Hapo unazungumza watumishi zaidi ya elfu 14 kwenye sekta ya afya, sekta ya ujenzi wa miradi ya kimkakati ambayo nayo imezalisha ajira nyingi sana. Kulipa madai yasiyo ya mishahara na kutoa mikopo isiyo na riba kwa watumishi wa umma.
Hadi kufikia Agost 2020, Serikali ya awamu ya tano imelipa madai ya watumishi yasiyo ya mishahara kiasi cha Tsh. billioni 358.1. Malipo hayo yamefanyika baada ya kuhakikiwa na kuondolewa malipo bandia yaliyokuwa yameghushiwa tu na wajanja.
Aidha, Serikali ya awamu ya 5 imefanikiwa kutoa mikopo isiyo na riba kwa watumishi wa umma. Jumla ya Tsh. billioni 54.8 zimetumika kwa ajili hiyo hadi sasa. Mambo yote haya yamefanyika na serikali kwa kutambua wajibu wake kwa watumishi wa umma na wa sekta binafsi.
7. Kulipa mishahara ya watumishi wa umma mapema na kwa wakati.
Leo kutoka kwenye kero ya watumishi kucheleweshewa mishaharo yao sasa watumishi wanateleza tu. Yani kabla ya mwezi haujaisha tarehe za mapema kabisa kuanzia Oktoba 23-27 mshahara unakua umeingia. Nani huyo anananga kazi kubwa ya kuboresha maslahi ya watumishi umma iliyofanyika?
8. Kudhibiti mfumuko wa bei na utulivu wa thamani ya shilingi ya Tanzania ili mshahara wa Mtumishi uendelee kuwa na nguvu.
Hili ni eneo ambalo Serikali ya awamu ya 5 imejitahidi sana kwa kuhakikisha hapawi na mfumuko wa bei ya bidhaa na huduma kwa kuendelea kubaki kuwa ndani ya wigo wa tarakimu 1 kwa wastani wa asilimia 4.4 toka mwaka 2016 hadi sasa na nguvu ya hela yenyewe hata ikiwa mia 1. Hii ni katika kuhakikisha hela anayopata mtumishi kwenye mshahara wake inaendelea kuwa na nguvu na imara zaidi. Sasa hawa wanaopotosha haya akina nani? Shubash!
#MITANO TENA.
Hekaheka na pilika za kampeni zinaendelea kutimua vumbi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi kwa wagombea wa Urais, wabunge na madiwani kunadi Sera na Ilani zao wanazoenda kuzitekeleza kwa miaka mitano ijayo kama wananchi wakiwapa ridhaa yao.
Kwa bahati nzuri sana nimeendelea kufuatilia kwa kila jambo linaloendelea kwenye kampeni hizi na leo kwa uchache kidogo nitazungumzia kwa uchache tabia ya upotoshaji inayotumiwa na kuota mabawa kwa baadhi ya wagombea wa vyama mbalimbali.
Ukiachana na baadhi ya wagombea wa vyama vya upinzani kuwakashfu kwa kutweza utu na heshima ya watumishi wetu wa umma wote wanaofanya kazi kubwa usiku na mchana kwa kuwaita watu waliokotwa majalalani lakini zaidi nimesikia mara kadhaa wagombea haohao wa vyama vya upinzani wakipotosha kuhusu maslahi ya watumishi wa umma na mambo mbalimbali yanayowahusu watumishi wetu.
Nimewasikia wakipotosha waziwazi kuhusu hoja ya maslahi kwa watumishi wa umma bila hata ya kuogopa kama maneno yao yanaweza kuichonganisha Serikali, jamii na watumishi wetu wanaofanya kazi kubwa sana. Sasa njia ya muongo ni fupi na wala hakawii kuumbuka.
Kimsingi Serikali ya awamu ya 5 chini ya Dkt. John Pombe Magufuli imeshughulikia maslahi ya watumishi wa umma kwa kiasi kikubwa sana tangu iingie madarakani Novemba 2015 hadi sasa.
Zifuatazo ni hatua mbalimbali na chache tu kati ya nyingi zilizochukuliwa na Serikali ya awamu ya 5 kushughulikia changamoto na maslahi ya watumishi wa umma wote nchini. Nayasema haya ili kuondoa huu upotoshaji wa wachache wasiolitakia mema Taifa letu. Twende pamoja.
1. Malipo ya malimbikizo ya mishahara.
Mpaka Novemba, 2020 Serikali imelipa Tsh. Billioni 137 kwa watumishi 76,332. Kati ya watumishi hao walimu ni 41,385 waliolipwa Tsh. Bil. 45.5 na watumishi wasio walimu ni 34, 947 waliolipwa Tsh. 91.6. Haya ni malimbikizo yaliyokuwa kero kwa watumishi kwa miaka na miaka. Halafu mtu anakuja kupotosha kuhusu maslahi ya watumishi hapa. Hapana! tutaongea ukweli.
Hiki ni kiwango cha juu kabisa cha malipo ya malimbikizo kufanyika kwa kipindi cha miaka mitano katika historia ya nchi yetu.
2. Watumishi kupandishwa vyeo na madaraja.
Serikali ya awamu ya tano hadi August, 2020 imewapandisha madaraja na vyeo watumishi wapatao 246,637. Kati ya watumishi hao, walimu 161,655 walipandishwa vyeo na kulipwa Tsh. Billioni 33.28, watumishi wasio walimu ni 91,982 waliolipwa Tsh. 27.47.
Serikali yoyote duniani ni lazima itambue watumishi wake, na kuwathamini kwani ndio nyenzo na kichocheo cha maendeleo katika nchi. Serikali imekusudia kuendelea kupandisha vyeo watumishi wake watakaokidhi vigezo kama inavyohitajika zaidi.
3. Nyongeza ya mwaka ya mshahara (Annual Increment).
Baada ya zoezi la uhakiki wa watumishi kukamilika Serikali ilitoa nyongeza ya mwaka ya mshahara kwa watumishi wa umma 505,985 kwa mujibu wa utaratibu. Jumla ya Tsh. bilioni 72.8 ziliongezeka, kati ya kiasi hicho Tsh. 37.2 zililipwa kwa walimu 270,878 na Tsh. bilioni 35.7 zililipwa kwa watumishi wasio walimu.
4. Ongezeko la mishahara kwa kiwango kisichotozwa kodi.
Pamoja na kupandisha vyeo watumishi wa Umma, kulipa malimbikizo yaliyorithiwa kutoka awamu ya nne, kutoa nyongeza ya mishahara na ajira vilevile Serikali ya awamu ya 5 imepandisha kiwango cha mshahara usiotozwa kodi.
Hatua hiyo imeongeza imeongeza pato halisi la mshahara (take home) kwa wastani wa Tsh. 100,000/= kwa kila mfanyakazi wa umma na sekta binafsi. Kwa kipindi cha mwezi July, 2020 hadi June, 2021 Serikali itatumia Tsh. billioni 517 kama ongezeko la pato halisi kwa watumishi wa umma. Hatua hii imeanza kutekelezwa kuanzia mwezi July, 2020. Halafu mtu aseme tofauti kwa maslahi ya watumishi wa umma.
5. Ajira mpya.
Serikali zote duniani haziwezi kuajiri watu wake wote peke yake isipokuwa ni lazima iwezesha na kuweka mazingira mazuri ya watu kuajiriwa na kujiajiri pia. Serikali ya awamu ya 5 imezalisha ajira nyingi kwa kuwezesha sekta binafsi kuajiri lakini pia Serikali yenyewe kuajiri jumla ya vijana 66,178. Jumla ya Tsh. billioni 54.9 zimeongezeka kila mwezi katika sekta ya ajira. Hapo unazungumza watumishi zaidi ya elfu 14 kwenye sekta ya afya, sekta ya ujenzi wa miradi ya kimkakati ambayo nayo imezalisha ajira nyingi sana. Kulipa madai yasiyo ya mishahara na kutoa mikopo isiyo na riba kwa watumishi wa umma.
Hadi kufikia Agost 2020, Serikali ya awamu ya tano imelipa madai ya watumishi yasiyo ya mishahara kiasi cha Tsh. billioni 358.1. Malipo hayo yamefanyika baada ya kuhakikiwa na kuondolewa malipo bandia yaliyokuwa yameghushiwa tu na wajanja.
Aidha, Serikali ya awamu ya 5 imefanikiwa kutoa mikopo isiyo na riba kwa watumishi wa umma. Jumla ya Tsh. billioni 54.8 zimetumika kwa ajili hiyo hadi sasa. Mambo yote haya yamefanyika na serikali kwa kutambua wajibu wake kwa watumishi wa umma na wa sekta binafsi.
7. Kulipa mishahara ya watumishi wa umma mapema na kwa wakati.
Leo kutoka kwenye kero ya watumishi kucheleweshewa mishaharo yao sasa watumishi wanateleza tu. Yani kabla ya mwezi haujaisha tarehe za mapema kabisa kuanzia Oktoba 23-27 mshahara unakua umeingia. Nani huyo anananga kazi kubwa ya kuboresha maslahi ya watumishi umma iliyofanyika?
8. Kudhibiti mfumuko wa bei na utulivu wa thamani ya shilingi ya Tanzania ili mshahara wa Mtumishi uendelee kuwa na nguvu.
Hili ni eneo ambalo Serikali ya awamu ya 5 imejitahidi sana kwa kuhakikisha hapawi na mfumuko wa bei ya bidhaa na huduma kwa kuendelea kubaki kuwa ndani ya wigo wa tarakimu 1 kwa wastani wa asilimia 4.4 toka mwaka 2016 hadi sasa na nguvu ya hela yenyewe hata ikiwa mia 1. Hii ni katika kuhakikisha hela anayopata mtumishi kwenye mshahara wake inaendelea kuwa na nguvu na imara zaidi. Sasa hawa wanaopotosha haya akina nani? Shubash!
#MITANO TENA.