Nimemsikia Mgombea wa CCM akinadi sera zake na kuahidi kuwa serikali inao mpango kabambe ya kubadili ukanda wa ziwa kuwa wa kiutalii ili kuiongezea Serikali mapato nikafurahi sana kama mwananchi. Ni wakati mwafaka sasa kusambaza utalii kanda ya magharibi na kusini ili kutekeleza Master Plan ya utalii Tanzania. Kanda za magharibi na kusini zina vivutio vipya na vya kipekee kuvutia watalii hivyo nashauri yafuatayo:
1. Kuboresha na kupanua miundo mbinu ya viwanja vya ndege maeneo haya kwa vile vilisahaulika muda mrefu
2. Kuhamasisha wawekezaji wa sekta ya utalii ili wajenge mahoteli na kuanzisha makampuni ya usafirishaji utalii
3. Kuboresha miundo mbinu ya mabarabara katika miji na hifadhi zilizoko maeneo hayo
4. Kutangaza utalii wa maeneo hayo
Haya ni machache yanayoweza kuchochea kukua kwa utalii maeneo hayo badala ya kutegemea utalii wa kaskazini pekee.Tumchague Magufuli atuletee maendeleo.
1. Kuboresha na kupanua miundo mbinu ya viwanja vya ndege maeneo haya kwa vile vilisahaulika muda mrefu
2. Kuhamasisha wawekezaji wa sekta ya utalii ili wajenge mahoteli na kuanzisha makampuni ya usafirishaji utalii
3. Kuboresha miundo mbinu ya mabarabara katika miji na hifadhi zilizoko maeneo hayo
4. Kutangaza utalii wa maeneo hayo
Haya ni machache yanayoweza kuchochea kukua kwa utalii maeneo hayo badala ya kutegemea utalii wa kaskazini pekee.Tumchague Magufuli atuletee maendeleo.