Hoja ya Corona Wabunge wetu mjitambue nyinyi ni wawakilishi wa Wananchi na sio wataalamu

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Nimesikiliza baadhi ya michango ya wabunge wetu juu ya Corona nikabaki na maswali mengi najiuliza hawa wanaongea bungeni kama watu gani?

Anasimama mbunge bungeni anachangia mjadala kwa kuelezea Corona ni nini? Inasambaa vipi? na kibaya zaidi anahitimisha kwa kutoa wito kwa wananchi ni kitu gani wafanye.

Hizi kweli mbunge ndivyo anavyotakiwa kufanya? Yawezekana hujaona tatizo lakini ngoja nikuelezee mtizamo wangu.

Yaani ukimsikiliza mtaalamu wa wizara ya afya anavyofafanua Corona na kushauri nini cha kufanya, ndivyo mbunge naye unavyomsikia akijadili korona bungeni, ndivyo unavyomsikia layman akijadili Corona mtaani.

Hii inaonyesha tatizo maana wataalamu, wawakilishi wa wananchi na wananchi ni lazima aongee kwa nafasi yake.

Tukiwa mtaani kuna mengi yanasemwa juu ya Corona, wananchi tumesikia mengi hasa kupitia mitandao ya kijamii:

1. wapo wanaosema ugonjwa huu umetengezwa na watu kwa ajili ya biashara kwa madai kwamba wametengeneza wadudu wakaletwa na kutengeneza panic alafu wakaenda kuleta suluhisho la tatizo walilolitengeneza wao wenyewe kutuuzia.

2. wapo wanaosema Corona imetokana na wachina kula popo.

3. wapo wanaosema ugonjwa huu hutokea kila baada ya miaka 100 kwani huko nyuma yalishatokea kama "spanish flue".

4. Yapo mengi yametokea mfano kuna wengine wametengeneza dawa zao huko nje na wanataka kila mtu atumie hizo hizo hizo

5. Yapo mengi yameibuliwa juu ya dawa hizo kwa wengine kusema hiyo siyo dawa na kuhoji uhallali wake kwani technolojia ilitumika haijawahi kuruhusiwa kutumika kwa binadamu.

6. wapo wanaosema mda wa kuzalisha chanjo haikufuatwa na kuhoji iweje tufanyie majaribio kwa binadamu na kuhoji ikiwa kunaweza kutokea madhara makubwa.

7. kwa upande mwingine serikali yetu imetoa taarifa juu ya utafiti unaoendelea nchini kwa kutumia miti shamba na kufanikiwa kuzalisha baadhi ya tiba ambazo imesema zimeonyesha mafanikio mazuri.

8. serikali imeenda mbali zaidi na kutoa msimamo wake kwamba itaendelea kutumia tiba zilizozalishwa nyumbani na haina mpango wa kugiza chanjo nje.

9. taarifa hii imeonekana kupelekewa tofauti na mataifa ya nje kwani shirika la afya Dunia lilianza kwa kusema tanzania ijiandae kupokea tiba, mara ukitazama vyombo vya habari vya kimataifa mfano bbc imeandika makala yenye kichwa Conona Tanzania na kuishambulia kwa kukataa chanjo.

Mwananchi anasikia mengi na waswahili walisema miluzi mingi humpoteza mbwa, na huyu mwananchi ndiye amemtuma mbunge wake kwenda kumuwakilisha katika kuongea na serikali yake.

Wananchi tulitegemea kusikia wawakilishi wetu wakieleza changamoto iliyopo kwa mwananchi kutokana na taarifa nyingi zilizoko mtaani na kwa kutoa mfano yanayoelezwa na kuiomba kuiuliza serikali mfano yafuatayo:

1. Yapo mengi yanahusishwa na chimbuko la virusi vya Corona ikiwemo uhalifu juu ya binadamu, je serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inajiridhisha na chimbuko la ugonjwa huu kabla ya kuingia kwenye mfumo wa biashara ili kama kweli ni uhalifu kuhakikisha haisapoti uhalifu kwa namna yoyote ile.

2. Yapo mengi yanazunguzwa juu ya techolojia iliyotumika kutengeneza chanjo na kudai haifai kwa matumizi ya binadamu kwa sasa, je serikali imefanya juhudi gani za kufuatilia kinachofanyika ili kubaini manufaa na madhara kwa binadamu. tukumbuke serikali ilitunga sheria ya kuzuia matumizi ya GMO katika kilimo na technolojia iliyotumika inahusishwa kwa ukaribu na technolojia hii, je kama serikali ilipiga marufuku kwenye kilimo ni nini msimamo wa serikali juu ya matumizi ya technojia kama hizi kwa wananchi wetu

3. ni jitihada gani serikali inazozifanya kujenga uwezo wa ndani katika kutafiti na kuzalisha kinga, tiba na vifaa, pamoja na wataalamu wa kukabiliana na changamoto kama hizi na nyingine za kiafya.

Na sio mbunge kusoma makala fulani anaikalili hiyo na akipewa mda wa kuchangia basi yeye ndiye anayekuwa kama mtaalamu akiwaelekeza watanzania kilichopo ni kitu gani na nini cha kufanya. Waeleze waliyoyasikia kwa mantiki ya kujenga hoja ya kushauri na kuielekeza serikali katika nini cha kufanya.

Huo ni mtizamo wangu karibu kwa maoni
 
Wabunge wanacheza kulingana na beat wanatoa hoja ambazo wanaamini zitaifurahisha mamlaka ya uteuzi and bad enough Hii awamu inaamini juu ya ile formula takatifu ya malaika isemayo "kwanza mimi mtu akinishauri ndiyo anaharibu kabisa"
 
WaTaz mnasahau za haraka sana,hivi mnajitoa ufahamu kwanini lakini ? Hawa wabunge hawana uchungu wala hasira na wananchi kwani hapo wamechomekwa kimagumashi na wao wanajuwa sasa ,ukimletea habari za kutetea wananchi kwenye mitandao ,wanahisi kama hamuelewi kilichopita na mnaamini kama walipigiwa kura hawana tofauti na wale covid 19 waChadema,msiweke kabisa matumaini kwao,hilo lifuteni na wekeni akili zenu sawa,mkielewe kilichopita.

Halafu waTz mnadharau sana misemo yetu...kuna ule msemo unaonena... akili ni nywele kila mtu ana zake...na pia raisi aliemaliza muda wake Jakaya wa Kikwete nae alituongezea msemo ....akili za kuchangiwa ongeza na zako....,jamani sasa unangojea Mheshimiwa Magufuli aje akuvishe barakowa .....mna vichaa au mmezugwa ? eei hata mimi ukinikuta nitakwambia Tanzania hakuna korona.
 
Umenena yaliyo kweli. Wanasiasa wanajifanya wataalam wa tiba kwa kumufurahisha aliyewapa nafasi hiyo. Hawawajibiki kwa wananchi tena kwa kuwa hawakuwachagua. Kwa mzaha huu; Corona itatumaliza.
 
Corona ipo nchini na itatuathiri sana.kama nchi ambayo imepiga hatua kubwa kimaendeleo hadi kufikia uchumi wa kati taarifa ya WHO kuwa hatutokuwa miongoni mwa nchi ambazo hazijaomba chanjo,ni jambo la kushangaza.serikali yetu sikivu,washauri wa afya waingilie kati suala hili kwani in a long run litatuathiri kiuchumi.jamani hata watalii wataogopa kuja,wawekezaji nao vivyo hivyo.kifupi tutaathirika kiuchumi.
 
Corona ipo nchini na itatuathiri sana.kama nchi ambayo imepiga hatua kubwa kimaendeleo hadi kufikia uchumi wa kati taarifa ya WHO kuwa hatutokuwa miongoni mwa nchi ambazo hazijaomba chanjo,ni jambo la kushangaza.serikali yetu sikivu,washauri wa afya waingilie kati suala hili kwani in a long run litatuathiri kiuchumi.jamani hata watalii wataogopa kuja,wawekezaji nao vivyo hivyo.kifupi tutaathirika kiuchumi.
Wengine wanasema kwa kawaida chanjo ikitolewa mwenye chanjo hapati ugonjwa, sasa bado watu wanajiuliza watalihi wenye chanjo wataogopaje kuja kwetu wakati wao wamechanjwa hawawezi kupata ugonjwa?

Mimi sijui ila natamani hawa wabunge wetu wahoji haya kwa wataalamu wa wizara ya afya ili watuchambulie mbichi na mbivu
 
Ila inategermea ni mbunge wa chama gani.

Wabunge 95% huko bungeni wameingia kwa maagizo ya Magufuli, hivyo lazima waongee anachotaka Magufuli. Sasa kama 95% wako kwa maagizo ya Rais, kuna cha kutegemea ni mbunge wa chama gani hapo?
 
Wengine wanasema kwa kawaida chanjo ikitolewa mwenye chanjo hapati ugonjwa, sasa bado watu wanajiuliza watalihi wenye chanjo wataogopaje kuja kwetu wakati wao wamechanjwa hawawezi kupata ugonjwa?

Mimi sijui ila natamani hawa wabunge wetu wahoji haya kwa wataalamu wa wizara ya afya ili watuchambulie mbichi na mbivu

Kwanza sio kila mzungu ameshapata chanjo, na isitoshe akipata chanjo sio lazima aje Tanzania kutalii.
 
Wabunge 95% huko bungeni wameingia kwa maagizo ya Magufuli, hivyo lazima waongee anachotaka Magufuli. Sasa kama 95% wako kwa maagizo ya Rais, kuna cha kutegemea ni mbunge wa chama gani hapo?
Ndio maana nikasema inategemea na chama,hao wabunge unaowasema hawawezi kuongea kitu tofauti na Magufuli maana Magufuli ndio chama chenyewe sasa hivi na hata hao wengine nao pia hawawezi kueleza yenye kutofautiana na vyama vyao.

Na sisi wananchi tunapima hoja za wabunge kwa kuangalia vyama vyao na ndio imekuwa hivyo miaka yote.
 
Ni lini tumefanya utafiti wa ugonjwa wowote na kujaribu kutengeneza vaccine yake? Malaria eradication imetushinda, hata kwa kufanya usafi. Viongozi wangepunguza matumizi ya magari ya kifahari hiyo hela ikafanyia research. Tutabaki kuwalaumu wazungu ila sisi hatujawekeza kwenye research. Taaluma zitumike tuache siasa kwenye kila kitu
 
Nani kakuambia hao wajumbe wa mkutano wa CCM ni wawakilishi wa wananchi?
Mwananchi gani mwenye akili timamu aliwachagua?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom