Son of Gamba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2012
- 4,358
- 6,073
Tumemaliza mwaka mmoja sasa tangu Rais Magufuli aapishwe na kuwa Rais wa tano wa nchi yetu Tanzania. Tokea Rais Magufuli aingie madarakani, amekuwa akichukua hatua mbali mbali za kusafisha nchi kwa kutumia mtindo alioupachika jina la "kutumbua majipu".
Wote tumeshuhudia Rais akichukua maamuzi "magumu" na bila uwoga wala kupepesa macho amefanya mambo ambayo watangulizi wake hawakuthubutu kufanya ama hata hawakuota kufanya hivyo. Mambo yote aliyoyafanya Rais Magufuli wote tunayafahamu na sina haja ya kuyarudia kuandika hapa sababu nitajaza tu page bila sababu. Sasa twende kwenye hoja yenyewe.
Kumekuwa na malalamiko mengi sana, hasa kwenye vyombo vya habari, hasa vile ambavyo vinamilikiwa na watu ambao naweza kusema wako "mlengo wa kushoto" na pia kwenye mitandao ya kijamii hasa humu JF, kuwa Rais Magufuli amelitumbukiza taifa kwenye "ukata" mkubwa sana wa fedha. Malalamiko mengi ni kuwa eti, Wananchi hawana pesa mifukoni, biashara zinashindwa kujiendesha, mabenki yanafilisika, watu wanafukuzwa kazi, mzunguko wa pesa umekuwa mdogo na mengine mengi.
Nafikiri umefika wakati sasa kila mmoja aliyemo humu JF "afunguke" bila woga na atueleze ni jinsi gani na kwa namna gani ameathirika moja kwa moja na maamuzi yaliyokwisha chukuliwa na Rais Magufuli. Nataka tufunguke na kila mtu anayelalamika humu JF aseme namna alivyoguswa na Mheshimiwa Rais, kiasi kwamba sasa anaona "maisha ni machungu". Tusilalamike kijumla jumla tu, kila mmoja, "as an individual" aseme kilichomsibu kama ni kutumbuliwa yeye au kama ni kutumbuliwa mtu aliyekuwa anamtegemea. Na sio lazima iwe kutumbuliwa, labda kuna kodi fulani imekuwa mzigo kwako, labda biashara imeyumba, tuwe wawazi ili tujue kama ni kweli malalamiko ya watu ni "genuine".
Binafsi naweza kusema mimi sijaathirika na hatua zote zote alizochukua Rais na maamuzi yake hayajanigusa kwa namna yoyote ile. Nathubutu kusema kuwa maisha yangu hayana tofauti kabla na baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani. Zaidi sana naona kama bidhaa zimeshuka bei na upatikanaji wa vyakula, viwanja vya kujenga nyumba, na huduma zimeboreka zaidi.
Naomba sasa kila mmoja aseme yake ya moyoni na tujadili bila matusi, wala kashfa.
Wote tumeshuhudia Rais akichukua maamuzi "magumu" na bila uwoga wala kupepesa macho amefanya mambo ambayo watangulizi wake hawakuthubutu kufanya ama hata hawakuota kufanya hivyo. Mambo yote aliyoyafanya Rais Magufuli wote tunayafahamu na sina haja ya kuyarudia kuandika hapa sababu nitajaza tu page bila sababu. Sasa twende kwenye hoja yenyewe.
Kumekuwa na malalamiko mengi sana, hasa kwenye vyombo vya habari, hasa vile ambavyo vinamilikiwa na watu ambao naweza kusema wako "mlengo wa kushoto" na pia kwenye mitandao ya kijamii hasa humu JF, kuwa Rais Magufuli amelitumbukiza taifa kwenye "ukata" mkubwa sana wa fedha. Malalamiko mengi ni kuwa eti, Wananchi hawana pesa mifukoni, biashara zinashindwa kujiendesha, mabenki yanafilisika, watu wanafukuzwa kazi, mzunguko wa pesa umekuwa mdogo na mengine mengi.
Nafikiri umefika wakati sasa kila mmoja aliyemo humu JF "afunguke" bila woga na atueleze ni jinsi gani na kwa namna gani ameathirika moja kwa moja na maamuzi yaliyokwisha chukuliwa na Rais Magufuli. Nataka tufunguke na kila mtu anayelalamika humu JF aseme namna alivyoguswa na Mheshimiwa Rais, kiasi kwamba sasa anaona "maisha ni machungu". Tusilalamike kijumla jumla tu, kila mmoja, "as an individual" aseme kilichomsibu kama ni kutumbuliwa yeye au kama ni kutumbuliwa mtu aliyekuwa anamtegemea. Na sio lazima iwe kutumbuliwa, labda kuna kodi fulani imekuwa mzigo kwako, labda biashara imeyumba, tuwe wawazi ili tujue kama ni kweli malalamiko ya watu ni "genuine".
Binafsi naweza kusema mimi sijaathirika na hatua zote zote alizochukua Rais na maamuzi yake hayajanigusa kwa namna yoyote ile. Nathubutu kusema kuwa maisha yangu hayana tofauti kabla na baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani. Zaidi sana naona kama bidhaa zimeshuka bei na upatikanaji wa vyakula, viwanja vya kujenga nyumba, na huduma zimeboreka zaidi.
Naomba sasa kila mmoja aseme yake ya moyoni na tujadili bila matusi, wala kashfa.