Hoja kuu mbili kuhusu taarifa iliyosambazwa na ubalozi wa Marekani, Tanzania

blix22

JF-Expert Member
Jun 23, 2013
213
645
Na, Ibrahim Haroub Geveva

Nikiwa katika shughuli za kikazi za Umoja wa Mataifa hapa Geneva, nimefadhaishwa na namna Ubalozi wa Marekani Tanzania ulivyotoa taarifa ya UZUSHI huko Tanzania.

Mwaka 1998, hao ndugu walipigwa na hawakutoa tahadhari yoyote Dar es Salaam wala Nairobi. Nakumbuka nilikuwa Sudan wakati huo katika shughuli za Kanda ya Mashariki ya UN.

Hakukuwa na taarifa zozote za tahadhari kama huu uzushi. Jiulize kwa nini leo wametoa, tena siku ya Bajeti ya Nchi inapojadiliwa, Siku ambazo Watalii wengi wanakwenda kwa makundi makubwa Tanzania, Kuna nini hapo kimefichika?

Nimemuuliza Mtoto wa Shemeji yangu anayefanya kazi Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam, amethibitisha hata Ubalozi wenyewe umeshangazwa na aliyechapisha taarifa hiyo katika mitandao ya kijamii bila kujiridhisha.

Wanahojiana, hivi walishindwa hata kuwapatia Polisi Oysterbay wachunguze? Au hata wale walinzi wa pale FFU au G4S ambao wanalinda Ubalozi wao?

Walishindwa kuwapa JWTZ? Walishindwa kuwapa Usalama wa Taifa waseme wanayojua? Je huu sio ujasusi uliopindukia katika nchi za wenzao?

Hayo maswali lazima yawasukume Wamarekani kuwaomba radhi washirika wao katika masuala ya Kiusalama. Kuna Mikataba ya Kimataifa inayowataka kushirikiana na vyombo vya ndani ya nchi husika wanapofuatilia mambo yanayohusu masuala ya ndani ya nchi.

Wamarekani hadi wanatoa kauli, walituma wachunguzi wao Masaki?Je, waliomba kibali Wizara ya Mambo ya Nje Tanzania au hata Umoja wa Mataifa? Wanatumia njia gani kuchunguza mambo nchini Tanzania hadi kutoa kauli ya namna hiyo?

Nani amewathibitishia huko mitaani hizo taarifa hadi kuchapisha katika tovuti yao? Tujiulize sote haya maswali.

Hivi Balozi wa Tanzania nchini Marekani hata akiwa na taarifa yoyote ya nchi hiyo ndio atoke kwa umma pale Washington DC kutangaza anachojua kuhusu Marekani? Sisi watu wa Diplomasia tunahoji, hiyo ni diplomasia ya wapi?

Basi ukiona hivi kuna jambo wanatengeneza kwa makusudi, si vinginevyo. Watanzania AMKENI.

Marekani, waombeni RADHI Watanzania na lazima mjenge tabia ya kufanya kazi na vyombo vya dola vya Tanzania katika kazi zenu. Umoja wa Mataifa unafuatilia jambo hili kwa karibu
 
Mkuuu kweliii kwa wataalam ya mambo ya usalama naomba watufafanulie....maaana hata mimi sijui kituu kuhusiana na maswala ya usalama naona kunatatizo sehem...
 
Na, Ibrahim Haroub Geveva

Nikiwa katika shughuli za kikazi za Umoja wa Mataifa hapa Geneva, nimefadhaishwa na namna Ubalozi wa Marekani Tanzania ulivyotoa taarifa ya UZUSHI huko Tanzania.

Mwaka 1998, hao ndugu walipigwa na hawakutoa tahadhari yoyote Dar es Salaam wala Nairobi. Nakumbuka nilikuwa Sudan wakati huo katika shughuli za Kanda ya Mashariki ya UN.

Hakukuwa na taarifa zozote za tahadhari kama huu uzushi. Jiulize kwa nini leo wametoa, tena siku ya Bajeti ya Nchi inapojadiliwa, Siku ambazo Watalii wengi wanakwenda kwa makundi
makubwa Tanzania, Kuna nini hapo kimefichika?

Nimemuuliza Mtoto wa Shemeji yangu anayefanya kazi Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam, amethibitisha hata Ubalozi wenyewe umeshangazwa na aliyechapisha taarifa hiyo katika mitandao ya kijamii bila kujiridhisha.

Wanahojiana, hivi walishindwa hata kuwapatia Polisi Oysterbay wachunguze? Au hata wale walinzi wa pale FFU au G4S ambao wanalinda Ubalozi wao?

Walishindwa kuwapa JWTZ? walishindwa kuwapa Usalama wa Taifa waseme wanayojua? Je huu sio ujasusi uliopindukia katika nchi za wenzao?

Hayo maswali lazima yawasukume Wamarekani kuwaomba radhi washirika wao katika masuala ya Kiusalama. Kuna Mikataba ya Kimataifa inayowataka kushirikiana na vyombo vya ndani ya nchi husika wanapofuatilia mambo yanayohusu masuala ya ndani ya nchi.

Wamarekani hadi wanatoa kauli, walituma wachunguzi wao Masaki?Je, waliomba kibali Wizara ya Mambo ya Nje Tanzania au hata Umoja wa Mataifa? Wanatumia njia gani kuchunguza mambo nchini Tanzania hadi kutoa kauli ya namna hiyo?

Nani amewathibitishia huko mitaani hizo taarifa hadi kuchapisha katika tovuti yao? Tujiulize sote haya maswali.

Hivi Balozi wa Tanzania nchini Marekani hata akiwa na taarifa yoyote ya nchi hiyo ndio atoke kwa umma pale Washington DC kutangaza anachojua kuhusu Marekani?Sisi watu wa Diplomasia tunahoji, hiyo ni diplomasia ya wapi?

Basi ukiona hivi kuna jambo wanatengeneza kwa makusudi, si vinginevyo. Watanzania tuwe AMKENI.

Marekani, waombeni RADHI Watanzania na lazima mjenge tabia ya kufanya kazi na vyombo vya dola vya Tanzania katika kazi zenu. Umoja wa Mataifa unafuatilia jambo hili kwa karibu
 
Sasa kama 1998 hawakutoa tahadhari na Shambulio likatokea, basi tukio hilo liliwafunza ndio maana sasa hv wametoa tahadhari. Mi nadhani cha muhimu hapa ni kuchukua tahadhari tu basi. Tusijiweke ujuaji saaana hawa wenzetu wanatuzidi mbinu za kupata taarifa.
 
Hivi wewe ukiambiwa ulindwe na askari WA tz au wa marekani utakubali wapi?

Wenzetu hawana siasa kwenye issues zinazowagusa raia wao maana walishang'atwa na nyoka wanajua uchungu wake.

Tushukuru Sana wametoa taarifa mm nimefurahi kumbe tupo salama na kuna zaidi ya ulinzi huu tunaoujua sisi hapa tz.

Hii ndio maana ya USA kuitwa superpower.
Safi Sana.
 
Mdharau mwiba mguu huota tende. Hiyo ni tahadhari unaweza kuifanyia kaz au kuipuuza. Lkn ukipuuza na ikija kutokea utajilaumu mwenyew kwa upu.uzi uliyoufanya, na isipotokea basi maisha yataendelea. Usikimbilie kupingana na hawa wa2 b4 ya kufanya tafiti au uchunguz wa kina kwa hicho walichotahadharisha. Waliulize Kenya na Ethiopia ambao walipuuza kilichokuwa kinatahadharishwa na hawa jamaa nini kiliwatokea baada ya kupuuza tahadhari!
 
Kuna kitu kimoja muhimu sana hapa.

Hizi taarifa zilikuwa na msingi wa ukweli au hazikuwa na msingi huo?

Kama zina msingi wa ukweli, Wamarekani wana wajibu wa kuwataarifu angalau raia wao.

Wamarekani waliingia matatani Kenya kwa kuwaonya raia wao tu kabla ya mashambulizi ya kigaidi Nairobi.

Sasa hapa wametaarifu umma napo wanalaumiwa.

Mmakonde anakwambia "ukichimama nchale, ukikimbia nchale".
 
Back
Top Bottom