Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,196
- 25,516
Natoa wito kwa watanzania wenzangu wazalendo kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam kuipokea Taifa Stars itakayorejea kutokea Misri kwenye mashindano ya Mataifa ya Afrika. Ilikuwa mara yetu ya pili kushiriki. Tumejifunza mengi.
Tukiwa kifua mbele, tujazane uwanjani na pembezoni mwa barabara kuilaki timu yetu ya Taifa iliyofungwa mabao manane tu na kufunga mawili kwenye mechi tatu dhidi ya Senegal, Kenya na Algeria. Ushiriki wetu kule Misri uwe funzo kubwa kwetu. Mosi, kutochanganya siasa na michezo. Pili, kutofanya matumizi yasiyo ya lazima kwenye soka letu.
Timu zote za Taifa zenye mafanikio zina maandalizi makubwa. Kuanzia kuwaandaa wachezaji tangu wakiwa makinda; kupata kocha na benchi la ufundi bora; kuwa na mashabiki wenye mshikamano na maelewano na hata hamasa kutoka kwa wadau. Kwetu sisi hatujachelewa. Maandalizi ya timu zetu za taifa yafanywe mapema kwa kila linalopaswa kufanywa badala ya kuendeshwa kwa hisia.
Inapofikia watanzania wenzetu, tena wakiwa hapa hapa Tanzania, wakiiombea Taifa Stars ishindwe, si jambo jema. Ni dalili ya hatari kwenye Umoja na mshikamano wetu kama nchi. Kwangu mimi, naiona sababu ya kuchanganya siasa na soka ikichangia. Soka lilikuwa hatarini kutumika kisiasa kwa maslahi ya vyama vya kisiasa au ya wanasiasa. Hili si jambo la mbolea.
Tutembee vifua mbele, one day YES. We are on the right track!😀
Tukiwa kifua mbele, tujazane uwanjani na pembezoni mwa barabara kuilaki timu yetu ya Taifa iliyofungwa mabao manane tu na kufunga mawili kwenye mechi tatu dhidi ya Senegal, Kenya na Algeria. Ushiriki wetu kule Misri uwe funzo kubwa kwetu. Mosi, kutochanganya siasa na michezo. Pili, kutofanya matumizi yasiyo ya lazima kwenye soka letu.
Timu zote za Taifa zenye mafanikio zina maandalizi makubwa. Kuanzia kuwaandaa wachezaji tangu wakiwa makinda; kupata kocha na benchi la ufundi bora; kuwa na mashabiki wenye mshikamano na maelewano na hata hamasa kutoka kwa wadau. Kwetu sisi hatujachelewa. Maandalizi ya timu zetu za taifa yafanywe mapema kwa kila linalopaswa kufanywa badala ya kuendeshwa kwa hisia.
Inapofikia watanzania wenzetu, tena wakiwa hapa hapa Tanzania, wakiiombea Taifa Stars ishindwe, si jambo jema. Ni dalili ya hatari kwenye Umoja na mshikamano wetu kama nchi. Kwangu mimi, naiona sababu ya kuchanganya siasa na soka ikichangia. Soka lilikuwa hatarini kutumika kisiasa kwa maslahi ya vyama vya kisiasa au ya wanasiasa. Hili si jambo la mbolea.
Tutembee vifua mbele, one day YES. We are on the right track!😀