darubin ya mbao
JF-Expert Member
- Aug 3, 2016
- 1,893
- 4,023
Waambie waelewe.Ni kweli. Kuwa na uwezo wa kumudu lugha za kigeni ambazo hukuzaliwa nazo ni ishara ya uwezo mkubwa wa kiakili.
Sio tu Kiingereza, bali lugha yoyote ile.
Maana yake ubongo wako una uwezo mkubwa wa kuchakata taarifa na mawazo katika lugha tofauti tofauti kwa wakati mmoja na ukaweza kuzungumza bila kubabaika ama kuchanganyikiwa.
Ni ufundi. Ukiwa goigoi wa akili huwezi kuzungumza lugha zaidi ya mbili.
Ndio maana wengine mpaka leo hawawezi kutamka Kiswahili kikaeleweka maana bongo zao zimeelemewa na tope zito la lugha mama.