CHANZO: GUMZO LA JIJI: Hoja: Je! Mavazi ya Polisi wa Kike yanakidhi matakwa ya Waraka Na 3 wa Mavazi ya Watumishi wa Umma?
Waraka wa Utumishi Na. 1 wa mwaka 1971 unaohusu mavazi ulitokana na mwongozo uliotolewa na Chama cha TANU kuhusu mavazi. Madhumuni ya waraka huo ilikuwa kuimarisha heshima ya Taifa kwa kuhakikisha kuwa watumishi wa Serikali wanavaa mavazi ya heshima wanapowahudumia wananchi. Waraka huo uliainisha baadhi ya mifano ya mavazi ambayo yalionekana hayafai na yale yanayofaa kwa wanawake na wanaume, utengenezaji wa nywele unaofaa na usiofaa na vipodozi visivyokubalika.
Hali ilivyo sasa:
2. Tangu waraka huo ulipotolewa kumekuwepo na mabadiliko makubwa ya mitindo ya mavazi, nywele na vipodozi. Mabadiliko ya mitindo ya mavazi ni jambo lisiloepukika. Hata hivyo baadhi ya mitindo hiyo ya mavazi inashusha heshima na hadhi ya utumishi wa umma kama itaendelea
kuvaliwa na ni kinyume na kifungu cha 2 (e) cha kanuni za Maadili ya utendaji katika utumishi wa umma za mwaka 2005 Hata hivyo kumekuwepo na tatizo la kutokuwepo na tafsiri inayoeleweka juu ya mavazi gani ni ya heshima au yanayokubalika na yasiyokubalika mahali pa kazi.
2
Uamuzi wa Serikali:
Tafsiri ya mavazi ya heshima hutegemea mila na desturi ya jamii husika. Katika utumishi wa umma mavazi ya heshima kwa mtumishi wa umma ni yale ambayo yanazingatia mila na desturi za taifa letu ambayo yanapovaliwa hayaonyeshi sehemu ya maungo ya mwili ambayo hayakuzoeleka kuachwa wazi, hayabani na ambayo hayana michoro au maandishi ya kudhalilisha wengine au yanayoonyesha ushabiki wa kitu fulani. Kwa hiyo waraka huu unatoa ufafanuzi kuhusu mavazi nadhifu yanayopaswa kuvaliwa kazini kwa kutoa mifano michache ya mavazi ambayo siyo ya heshima na ambayo hayakubaliki katika utumishi wa umma kwa jinsi zote mbili.
Utekelezaji:
3. Ufuatao ni ufafanuzi wa mavazi yasiyokubalika mahali pa kazi ambayo pia yameonyeshwa kwa picha kwenye kiambatisho A na B. Nguo kama Jeans na fulana zinaweza kuvaliwa na watumishi ambao wanalazimika kufanya kazi za nje ya ofisi.
3.1 Kwa Wanawake
(i) Baadhi ya mavazi yasiyofaa:
Nguo zinazobana,
Nguo fupi ambazo zinaacha magoti wazi.
Nguo ambazo zinaacha sehemu ya mwili wazi kama
vile kitovu na kifua,
Nguo ambazo zina picha, michoro, na maandishi ambayo hayaendani na shughuli za serikali,
Kaptura aina yoyote ile kama vile pedo na pensi,
Nguo zinazoonyesha maungo ya mwili (transparent).
Suruali za Jeans,
Suruali yoyote iliyoachwa bila kupindwa,
Fulana T-Shirts (Hizi zivaliwe tu wakati wa shughuli maalum inayotambulika),
Nguo ambazo ni za kazi maalum michezo, kazi za nje au burudani. Hizi zivaliwe mahususi wakati wa utekelezaji wa shughuli hizo,
Nguo yenye maandishi ya chama chochote cha siasa au ushabiki wa kitu fulani,
Nguo yeyote inayopingana na maadili ya utumishi wa umma.
(ii) Nywele zisizofaa:
Nywele chafu na ambazo hazikutengenezwa vizuri.
(iv) Viatu visivyofaa
Kandambili,
Viatu vya michezo (isipokuwa wakati wa shughuli
maalum za michezo),
Waraka wa Utumishi Na. 1 wa mwaka 1971 unaohusu mavazi ulitokana na mwongozo uliotolewa na Chama cha TANU kuhusu mavazi. Madhumuni ya waraka huo ilikuwa kuimarisha heshima ya Taifa kwa kuhakikisha kuwa watumishi wa Serikali wanavaa mavazi ya heshima wanapowahudumia wananchi. Waraka huo uliainisha baadhi ya mifano ya mavazi ambayo yalionekana hayafai na yale yanayofaa kwa wanawake na wanaume, utengenezaji wa nywele unaofaa na usiofaa na vipodozi visivyokubalika.
Hali ilivyo sasa:
2. Tangu waraka huo ulipotolewa kumekuwepo na mabadiliko makubwa ya mitindo ya mavazi, nywele na vipodozi. Mabadiliko ya mitindo ya mavazi ni jambo lisiloepukika. Hata hivyo baadhi ya mitindo hiyo ya mavazi inashusha heshima na hadhi ya utumishi wa umma kama itaendelea
kuvaliwa na ni kinyume na kifungu cha 2 (e) cha kanuni za Maadili ya utendaji katika utumishi wa umma za mwaka 2005 Hata hivyo kumekuwepo na tatizo la kutokuwepo na tafsiri inayoeleweka juu ya mavazi gani ni ya heshima au yanayokubalika na yasiyokubalika mahali pa kazi.
2
Uamuzi wa Serikali:
Tafsiri ya mavazi ya heshima hutegemea mila na desturi ya jamii husika. Katika utumishi wa umma mavazi ya heshima kwa mtumishi wa umma ni yale ambayo yanazingatia mila na desturi za taifa letu ambayo yanapovaliwa hayaonyeshi sehemu ya maungo ya mwili ambayo hayakuzoeleka kuachwa wazi, hayabani na ambayo hayana michoro au maandishi ya kudhalilisha wengine au yanayoonyesha ushabiki wa kitu fulani. Kwa hiyo waraka huu unatoa ufafanuzi kuhusu mavazi nadhifu yanayopaswa kuvaliwa kazini kwa kutoa mifano michache ya mavazi ambayo siyo ya heshima na ambayo hayakubaliki katika utumishi wa umma kwa jinsi zote mbili.
Utekelezaji:
3. Ufuatao ni ufafanuzi wa mavazi yasiyokubalika mahali pa kazi ambayo pia yameonyeshwa kwa picha kwenye kiambatisho A na B. Nguo kama Jeans na fulana zinaweza kuvaliwa na watumishi ambao wanalazimika kufanya kazi za nje ya ofisi.
3.1 Kwa Wanawake
(i) Baadhi ya mavazi yasiyofaa:
Nguo zinazobana,
Nguo fupi ambazo zinaacha magoti wazi.
Nguo ambazo zinaacha sehemu ya mwili wazi kama
vile kitovu na kifua,
Nguo ambazo zina picha, michoro, na maandishi ambayo hayaendani na shughuli za serikali,
Kaptura aina yoyote ile kama vile pedo na pensi,
Nguo zinazoonyesha maungo ya mwili (transparent).
Suruali za Jeans,
Suruali yoyote iliyoachwa bila kupindwa,
Fulana T-Shirts (Hizi zivaliwe tu wakati wa shughuli maalum inayotambulika),
Nguo ambazo ni za kazi maalum michezo, kazi za nje au burudani. Hizi zivaliwe mahususi wakati wa utekelezaji wa shughuli hizo,
Nguo yenye maandishi ya chama chochote cha siasa au ushabiki wa kitu fulani,
Nguo yeyote inayopingana na maadili ya utumishi wa umma.
(ii) Nywele zisizofaa:
Nywele chafu na ambazo hazikutengenezwa vizuri.
(iv) Viatu visivyofaa
Kandambili,
Viatu vya michezo (isipokuwa wakati wa shughuli
maalum za michezo),