Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 17,871
- 33,236
Kama kuna ufujaji wa fedha ambao wananchi wa Tanzani wanabebeshwa basi ni kuwepo kwa Halmashauri za miji Tanzania. Hivi umuhimu wa kuwepo kwa Halmashauri hizi ni upi kama hazikusanyi kodi, zikifanya baadhi ya maamuzi yake yanaweza kutenguliwa na Waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa? Hazimiliki Ardhi, zinaweza kugawanywa wakati wowote bila ya kushauriana nao na Halamshauri hizi zinaendeshwa na wakurugenzi ambao wenye Halmashauri zao hawana sauti ya kuwaajiri ama kuwafukuza kazi.
Ni kitu gani kitapungua kama hizi Halmashauri hazitokuwepo kuliko hivi sasa hata ushuru kidogo wanaokusanya unaishia kuwalipa madiwani ambao ni kama simba wa karatasi kwani kila waliamualo likiwaudhi wenye nchi yao linabatilishwa? Kwa nini tusiache nchi ziongozwe na Wakuu wa wilaya na mikoa?
Ni kitu gani kitapungua kama hizi Halmashauri hazitokuwepo kuliko hivi sasa hata ushuru kidogo wanaokusanya unaishia kuwalipa madiwani ambao ni kama simba wa karatasi kwani kila waliamualo likiwaudhi wenye nchi yao linabatilishwa? Kwa nini tusiache nchi ziongozwe na Wakuu wa wilaya na mikoa?