NewDawnTz
JF-Expert Member
- Nov 15, 2010
- 1,667
- 362
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA ameonesha ujasiri mkubwa. Anajua matatizo ndani ya chama chake yanayoweza kupelekea chama chake kikapoteza hata kiti kimoja ilichonacho Kigoma.
Amejitokeza wazi kwenye vyombo vya habari na umma kuzungumzia mapungufu ya chama chake, tofauti na viongozi wenzake ndnai ya chama. HUU ni MTAJI tosha wa kuleta reforms ambazo wengi (akiwamo Rev Kishoka na Mwanakijiji) wamekuwa wakipendekeza zifanyike ndani ya chama.
Naamini wakina Rev Kishoka (kama nilivo mimi) ni waamini wazuri wa mabadiliko ya kimfumo (wa uchumi, siasa, kiutawala/uongozi na kijamii) kwenye nchi yetu nje ya CCM. Hivyo mapendekezo haya ni katika kuhakikisha chama kilichojizolea nguvu ya kuleta mabadiliko kinajipanga vema kuweza kufanya hivyo na kuweka vema public image (kupuuzia ufa ni kujenga ukuta)
Kwa nini mtaji huu wa Zitto kufahamu mapungufu ndani ya CHADEMA na kuonesha ujasiri wa kuweza kuyashughulikia usiwe MTAJI wa muhimu kufanya reform ndani ya CHADEMA maana huwezi fanya reform kwa matatizo usiyoyajua wala kuyakiri kuwa unayajua
Kwa mantiki hii, Je ambao tunapenda kuona nchi hii ikiwa nje ya makucha ya CCM na tunaamini CHADEMA ni mbadala sahihi, hatuoni kuwa sasa ni wakati sahihi wa Mh. Zitto Zuberi Kabwe kupewa jahazi la CHADEMA (awe mwenyekiti wa chama)?
Naamini atafaa na nawaomba wadau wote tumuunge mkono na kuwaomba viongozi wa CHADEMA kumpa nafasi hii Zitto aweke chama vema kama ambavyo ametanabaisha kuwa kuna mambo ya kuwekwa sawa ndani ya CHADEMA. Narudia tena, ukipuuzia ufa utajenga ukuta. GHARAMA hiyo
Amejitokeza wazi kwenye vyombo vya habari na umma kuzungumzia mapungufu ya chama chake, tofauti na viongozi wenzake ndnai ya chama. HUU ni MTAJI tosha wa kuleta reforms ambazo wengi (akiwamo Rev Kishoka na Mwanakijiji) wamekuwa wakipendekeza zifanyike ndani ya chama.
Naamini wakina Rev Kishoka (kama nilivo mimi) ni waamini wazuri wa mabadiliko ya kimfumo (wa uchumi, siasa, kiutawala/uongozi na kijamii) kwenye nchi yetu nje ya CCM. Hivyo mapendekezo haya ni katika kuhakikisha chama kilichojizolea nguvu ya kuleta mabadiliko kinajipanga vema kuweza kufanya hivyo na kuweka vema public image (kupuuzia ufa ni kujenga ukuta)
Kwa nini mtaji huu wa Zitto kufahamu mapungufu ndani ya CHADEMA na kuonesha ujasiri wa kuweza kuyashughulikia usiwe MTAJI wa muhimu kufanya reform ndani ya CHADEMA maana huwezi fanya reform kwa matatizo usiyoyajua wala kuyakiri kuwa unayajua
Kwa mantiki hii, Je ambao tunapenda kuona nchi hii ikiwa nje ya makucha ya CCM na tunaamini CHADEMA ni mbadala sahihi, hatuoni kuwa sasa ni wakati sahihi wa Mh. Zitto Zuberi Kabwe kupewa jahazi la CHADEMA (awe mwenyekiti wa chama)?
Naamini atafaa na nawaomba wadau wote tumuunge mkono na kuwaomba viongozi wa CHADEMA kumpa nafasi hii Zitto aweke chama vema kama ambavyo ametanabaisha kuwa kuna mambo ya kuwekwa sawa ndani ya CHADEMA. Narudia tena, ukipuuzia ufa utajenga ukuta. GHARAMA hiyo