Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
- Thread starter
- #61
Ndio maana nahoji kama kweli aliwashirikisha wabunge wenzie katika kudraft mapendekezo. Ni lazima tukiri kuwa alifanya utafiti mzuri sana lakini tujue kuwa pale wapo katika mchezo wa siasa na sisi wote tupo katika mchezo wa siasa ndio maana tunajadili haya. kwa kuwa hoja hizi huwasilishwa mapema walikwishaikalia hoja ya Mhe Zitto na kumundalia mb unge atakayetumia Kanuni kuipiga knock technical out hoja yake.
kwa ufahamu wangu mambo yote aliyopendekeza Mhe Zitto ni ndoto za mchana kwa watendaji wa serikali ya CCM ambao hukaa kuvizia posho wakati wote.
Sababu ingine iliyofanya haja hiyo kutupwa ni kashafa zilizoko katika ubinafsishaji wa mashamba ya mkonge mojawapo likiwa shamba alilochukua CHAVDA aliyesababisha Mhe Lyatonga Mrema kuondolea katika baraza la mawaziri. Ndio maana Hoja hii ilitakiwa kukaliwa kweli kweli na kuandaliwa makakati wa pamoja kama chama.
Kwa hilo nipo ukurasa mmoja na wewe. Kwa mtazamo wako, nini kifuate? Zitto asubiri hiyo kamati gani sijui imalize kazi yake kama alivyo adhidi Waziri wa Kilimo? Zitto ajipange tena na hoja yake binafsi? Au Zitto na Chadema kwa ujumla wajipange zaidi kwa kuliweka hili katika bajeti yao ya wizara kivuli ya kilimo hapo mwezi Juni?