Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Hoja binafsi ya mbunge wa Mpanda Mjini Said Amour Arfi na ile ya mbunge wa Ubungo John Mnyika zimenyimwa fursa ya kuwasilishwa bungeni. Habari kutoka ofisi ya bunge hoja hizo zimezimwa kwa kuwa zingeibua mijadala mizito yenye kugusa vigogo ndani ya serikali na bunge. Chanzo hicho kimeeleza kuwa tayari bunge lilikuwa katika mivutano kutokana na hoja za posho, sheria ya mabadiliko ya katiba na mgomo wa madaktari hivyo isingewezekana kuingiza hoja nyingine.
Afisa huyo kutoka ofisi ya katibu wa bunge ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa hoja Arfi ingemgusa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu uuzaji wa ardhi ya wananchi Rukwa wakati ile ya Mnyika ingemgusa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa kuhusu Richmond.
Bado kuna kiporo cha utekelezaji wa maazimio ya bunge kuhusu suala la Jairo ambacho kinawagusa viongozi wazito akiwemo aliyekuwa katibu mkuu kiongozi na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, hivyo hatuwezi kuingiza hoja nyingine kwa sasa.
Chanzo hicho kimesema hoja mbili za wabunge Zitto Kabwe na January Makamba ziliingizwa ili kuchukua nafasi ambayo ingetumika kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa serikali kuhusu suala la Jairo na Taarifa ya Kamati ya Huduma za jamii kuhusu mgomo wa madaktari. Awali siku mbili za mwisho za bunge zilipangwa kwa ajili ya hoja binafsi za wabunge, lakini mvutano ndani ya CCM kuhusu muswada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba na kuhusu mgomo wa madaktari zilifanya serikali isogeze mbele hoja zingine. Habari zaidi zinaeleza kuwa baada ya Spika wa Bunge kukabidhi ripoti ya Jairo na kuelezwa yaliyogunduliwa na kamati ya bunge kuhusu mgomo wa madaktari aliona kwamba itaivua nguo serikali hivyo akairudisha tena kwa serikali hali ambayo ililazimu hoja hizo mbili za wabunge kuingizwa katika ratiba ili kuziba pengo.
PM
Afisa huyo kutoka ofisi ya katibu wa bunge ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa hoja Arfi ingemgusa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu uuzaji wa ardhi ya wananchi Rukwa wakati ile ya Mnyika ingemgusa Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa kuhusu Richmond.
Bado kuna kiporo cha utekelezaji wa maazimio ya bunge kuhusu suala la Jairo ambacho kinawagusa viongozi wazito akiwemo aliyekuwa katibu mkuu kiongozi na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, hivyo hatuwezi kuingiza hoja nyingine kwa sasa.
Chanzo hicho kimesema hoja mbili za wabunge Zitto Kabwe na January Makamba ziliingizwa ili kuchukua nafasi ambayo ingetumika kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa serikali kuhusu suala la Jairo na Taarifa ya Kamati ya Huduma za jamii kuhusu mgomo wa madaktari. Awali siku mbili za mwisho za bunge zilipangwa kwa ajili ya hoja binafsi za wabunge, lakini mvutano ndani ya CCM kuhusu muswada wa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba na kuhusu mgomo wa madaktari zilifanya serikali isogeze mbele hoja zingine. Habari zaidi zinaeleza kuwa baada ya Spika wa Bunge kukabidhi ripoti ya Jairo na kuelezwa yaliyogunduliwa na kamati ya bunge kuhusu mgomo wa madaktari aliona kwamba itaivua nguo serikali hivyo akairudisha tena kwa serikali hali ambayo ililazimu hoja hizo mbili za wabunge kuingizwa katika ratiba ili kuziba pengo.
PM