Uchaguzi 2020 Hoja binafsi: Jaji Kaijage apongezwe kwa busara zake zilizombeba Tundu Lissu, busara zaidi itumike kuepuka sintofahamu za makusudi kwenye Uchaguzi

Tatizo hapa ni mihemko ndio inatupa shida.
Yaani ccm na matawi yake yote wanavyo hangaika kupata sababu za kuwakata wapinzani wao, halafu wapate sababu lakini wawaache wapite eti kwa busara?

Kama ungesoma vizuri halama za nyakati ungegundua kwamba kila mmoja yupo katika kumtega mwenzake ili apate nafasi yakujiongezea wapiga kura.

Alichokifanya Lissu kilikuwa mtego kwa tume, lakini tume iligundua mtego huo na kuuepuka.
Na hata tweet yao iliandikwa kimtego lakini wewe mleta uzi umeshindwa kugundua mtego huo na umekunasa. Matokeo yake habari nzima uliyoandika haina faida tena kwa sababu hata ushahidi wako wa hiyo tweet ya CDM umekataana na maelezo yako.

Labda nikusaidie mtego wenyewe ulivyo. Tweet yao inasema hivi:
"Kwa ajili ya kusimamia utaratibu wa kisheria, fomu za mgombea urais wa JMT mh Tundu Lissu hazikupita kwa wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi kwa ajili ya zoezi la uhakiki".

Maana yake ni kwamba CDM wanajua kwamba fomu kuhakikiwa na wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi si utaratibu kisheria, ndio maana wamesimamia utaratibu wa kisheria kutopitisha fomu hizo kwa wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi.

Maana kuu hapa ni kwamba CDM walisimama katika sheria ndio maana hawakufuata kanuni kwa sababu wanajua sheria ipo juu ya kila kitu, na kanuni haiwezi kuwa juu ya sheria.

Hivyo ungeipongeza tume kwa kuhepuka mtego wa Lissu na chama chake. Na si busara ya huruma kama unavyotaka kuwaaminisha watu.
Tatizo kubwa hapo ni ujuaji tu mkuu. We unadhani Tume walikuwa wajinga hawajui hiyo sheria hadi wakatoa maelekezo wadhamini wahakikiwe kwenye ofisi za majimbo? Wagombea woote wa vyama vyote kumi nne walikuwa hawajui hiyo sheria Ila ni Lissu tu na CHADEMA ndio wanaojua sana Sheria?
Alafu Kama haitoshi anakuja kulalamika kakarishwa muda mrefu huoni kama ni unafiki huo?

Mkuu penye haki tutetee lakini pia lazima wakati mwingine tuwaambie CHADEMA na Lissu wapunguze ujuaji mwingi.
 
Tatizo kubwa hapo ni ujuaji tu mkuu. hadi wakatoa maelekezo wadhamini wahakikiwe kwenye ofisi za majimbo? Wagombea woote wa vyama vyote kumi nne walikuwa hawajui hiyo sheria Ila ni Lissu tu na CHADEMA ndio wanaojua sana Sheria?
Alafu Kama haitoshi anakuja kulalamika kakarishwa muda mrefu huoni kama ni unafiki huo?

Mkuu penye haki tutetee lakini pia lazima wakati mwingine tuwaambie CHADEMA na Lissu wapunguze ujuaji mwingi.
"We unadhani Tume walikuwa wajinga hawajui hiyo sheria".
Mimi sidhani wala sitaki kuamini kwamba tume ni wajinga. Kiongozi tatizo hapa sio maelekezo ya tume, tatizo ni sheria. Maelekezo ya tume yanatakiwa yaendane na sheria, yasipingane na sheria. Je Lissu na CDM walivunja sheria kutokupeleka fomu kwa wasimamizi wa majimbo ya uchaguzi? Je unadhani kama wamevunja sheria tume ingempitisha Lissu? Na kama imempitisha hali amevunja sheria wagombea wengine wangekubali kugombea na mtu aliepitishwa kienyeji bila kufuata sheria?
 
Jaji Kaijage na team yake ya Tume ya uchaguzi kama si busara zao za kukubali kufanya uhakiki wa wadhamini wa mgombea urais Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA Mhe. Tundu Lissu jambo ambalo kikanuni lilipaswa kufanyika kwenye ofisi za majimbo za Tume ya Uchaguzi basi ni dhahiri Lissu alitakiwa kutopitishwa na Tume.

Ajabu ni kwamba Mhe Tundu Lissu hakufanya hivyo iwezekana hakujua ama alijua Ila tu ni kiburi na kutaka kuonyesha umwamba mbele ya Tume ya Uchaguzi. Kikawaida hapa alitakiwa kukatwa moja kwa moja kwasababu tayari ameshavunja kanuni lakini busara za Tume zimembeba.

Mwanasheria makini msomi na mjuaji kama Tundu Lissu unawezaje kuvunja kanuni muhimu kama hii? Je hapo angakuta baadhi ya wadhamini ni hewa ingekuwaje ?

Hii inatoa picha kuwa kuna tatizo kubwa sana kwa hawa wagombea wa CHADEMA kwenye utaratibu wa ujazaji wa fomu za Ubunge na udiwani. Hawa wagombea wa ccm wanao pita bila kupigwa si kwamba ni mchezo mchafu wa CCM bali ni uzembe unao fanywa na wagombea wenyewe wa CHADEMA.

Kama imewezekana kwa Rais mtarajiwa kufanya kosa la kiufundi kama hili kwa wabunge je haitakuwaje?

Kama Lissu angekatwa na Tume asingekuwepo wa kulaumiwa makosa ni yake mwenyewe.
Kisha CHADEMA bila aibu wanakuja kusema hivi


Kibaya zaidi mhe Tundu Lissu bila kujali busara zilizotumiwa na Tume bado ametoa lawama nyingi kuwa kwanini amekalishwa masaa mengi kwenye uhakika wakati mhe Rais Magufuli alitumia muda mchache Kama ilivyopangwa.
Bila kuwarudisha wagombea wa Upinzani walioondolewa na makada wa ccm ambao wanaitwa Wakurugenzi , mwisho wa Kaijage utakuwa mbaya sana ! atakamatwa
 
Back
Top Bottom