Hofu zingine bwana!!!!hadi vitandani

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
Hofu zingine!

Mwanaume na mwanamke wanapokuwa kitandani (uchi) ni suala kubwa na linaloonesha ukaribu wa hali ya juu sana hata hivyo mwanamke (siyo wote) ndiye ambaye hujikuta yupo wazi kwa hofu kuu mbili ambazo ni:-
Kwanza ni je, mwili wangu utakataliwa au utakubaliwa na kusifiwa?
Pili ni je, mwanaume atakuwa na mtazamo gani kuhusiana na mwili wangu?
Nipo beautiful au ugly?

Turudi kwenye bible tuone mwanaume anayejua kupenda alichukua au alifanya nini kwa mpenzi wake au mke wake kuhusiana na hizi hofu kuu mbili.

Wimbo Ulio Bora 1:1-8
Inaonesha hawa wanandoa walikuwa wanapendana sana na mwanamke alikuwa na hofu kufanya kazi kwenye jua kwani jua lilimfanya aonekane mweusi mweusi.
Hata hivyo mwanaume alichokifanya ni kumwondolea hofu mke wake kwa kumsifia sura nzima (Wimbo Ulio Bora 4: 1 – 16)

Je, kama wewe ni mwanaume umewahi kumsifia mke wako kwa maneno ya kutosha naye akajisikia kweli ana mwanaume anayejali?
 
Back
Top Bottom