Hofu Yatanda Wizara ya Afya Wauguzi hawana Amani na Kazi zao, wenye bifu zao sasa wanalipiza kisasi kwa kesi za kufoji na kuwafukuzisha kazi

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Wana JF , umuofia kwenu.

Kumekuwa sintomfahamu katika sekta ya wizara ya afya baada ya wakazi wenye bifu zao na stress za maisha kuwageukia Manesi na kuwabambikia kesi nzito kiasi kwamba hawana pa kutokea kwani hawana watetezi wala wengi hawasikilizwi.

Imekuwa tabia sasa ya kuwaonea kila wakati, kuna uzembe mwingi unafanywa na wagonjwa wenyewe, mwingine unafanywa na serikali.

Mfano ngonjwa anaweza kuficha taarifa muhimu wakati wa kujifungua akapata shida. mgonjwa/mama kijacho anaweza kutengeneza kadi ya taarifa feki kutoka kwa mtu mwenye ufahamu wa mambo hayo, ambapo anaficha kuwa ana UKIMWI hivyo wakunga wakamzalisha kwa njia ya kawaida na mtoto akapata maambukizi, pia hata manesi wanapata maambukizi wakati wa kufua damu na vitu vyenye nchi kali vikimgusa. Wamama wengi wamekuwa na tabia mbaya sana, anapopima akagundulika ana UKIMWI anaweza kuanza matibabu au asianze, wengi kwa kutambua kuwa wenye ukimwi wanazaa, wanaenda kutafuta madume asije akafa bila kuacha watoto, kasumba hii imetokea sana kwa sasa, madada poa wengi wakijihisi wana ukimwi ujibebesha mimba na kuama maeneo au kuama mkoa, huko hutoa taarifa feki akijifanya mzima mpaka anajifungua. Mtoto anapozaliwa anapata maambukizi, mtoto akipata maambukizi hicho kituo cha afya kilichomzalisha wana kesi ya kujibu.

Manesi wengi walikuwa wakitukanwa ovyo na wagonjwa kiasi kamba anapandishwa hasira kwa kukosa uvumilivu na kuanza kujibizana. hii inatokea kwa serikali kukosa kupeleka vifaa kwa wakati, wananchi wanaambiwa dawa zipo, vifaa vya kujifungua vipo, wamama hawa wakienda wakavikosa, matusi kwa mane, wakikosa dawa matusi pia kwa manesi wakiambiwa wao ni wezi wakubwa wengine kutishiwa kuchapwa makofi hadharani...

Serikali chukueni hatua za kiuchunguzi kufuatilia mienendo ya manesi na wateja wao la sivyo atakuja kutokea maafa.makubwa kwani sasa hivi manesi hawaheshimiki ni watu wakunyanyaswa ovyo, daktari anamyanyasa nesi, mkuu wa mkoa ananyanyasa nesi, DED ananyanyasa Nesi. Chama chao cha kuwatetea masirai yao kimekuwa butu, hawana wa kuwasemea kwenye kazi zao, ni watu wa hofu muda wote.

Manesi ni watu wanafanya kazi mgumu na za hatari, magonjwa mbaya uwapata wakiwa kazini, lakini cha kushangaza ndio walio na masirahi kiduchu, angalau wakati wa awamu yanne walikumbukwa kidogo kwa kuongezea mishahara, sasa hivi baada ya serikali kutoa dawa bure wanafanya kazi ngumu wamezidiwa na wagonjwa wakati idadi yao ikiwa ndogo.
 
Hii ni hatari. Kwa nini mama aruhusiwe kujifungua bila kwanza kufanyiwa hiv test?
mtu anakuja ghafla ana hali mbaya huku amebeba, kadi ya clinic yenye taarifa feki juu yake. utaacha kumzalisha kwanza kabla ya kuanza kumhudumia wakati akiwa yupo taabani hajielewi?
 
anayezaa tofauti na
Mbona waliojeruhiwa hata wakiwa hoi kivipi lkn lazima wapate kwanza PF3.
aliyejeruhiwa, huyu ana furaa ya kupata mtoto mpya huyu anatibu majeraha, sasa kama mtu chupa ishapasuka unawezaje kumsubirisha kupata majibu ya HIV?
 
Yawezekana kuna visasi lakini nyie pia MNA mapozi, mnadharau wagonjwa, viburi na mnapenda rushwa, jitengenezieni taswira njema kwa jamii ili mkionewa tuwatetee.
Wana JF , umuofia kwenu.

Kumekuwa sintomfahamu katika sekta ya wizara ya afya baada ya wakazi wenye bifu zao na stress za maisha kuwageukia Manesi na kuwabambikia kesi nzito kiasi kwamba hawana pa kutokea kwani hawana watetezi wala wengi hawasikilizwi.

Imekuwa tabia sasa ya kuwaonea kila wakati, kuna uzembe mwingi unafanywa na wagonjwa wenyewe, mwingine unafanywa na serikali.

Mfano ngonjwa anaweza kuficha taarifa muhimu wakati wa kujifungua akapata shida. mgonjwa/mama kijacho anaweza kutengeneza kadi ya taarifa feki kutoka kwa mtu mwenye ufahamu wa mambo hayo, ambapo anaficha kuwa ana UKIMWI hivyo wakunga wakamzalisha kwa njia ya kawaida na mtoto akapata maambukizi, pia hata manesi wanapata maambukizi wakati wa kufua damu na vitu vyenye nchi kali vikimgusa. Wamama wengi wamekuwa na tabia mbaya sana, anapopima akagundulika ana UKIMWI anaweza kuanza matibabu au asianze, wengi kwa kutambua kuwa wenye ukimwi wanazaa, wanaenda kutafuta madume asije akafa bila kuacha watoto, kasumba hii imetokea sana kwa sasa, madada poa wengi wakijihisi wana ukimwi ujibebesha mimba na kuama maeneo au kuama mkoa, huko hutoa taarifa feki akijifanya mzima mpaka anajifungua. Mtoto anapozaliwa anapata maambukizi, mtoto akipata maambukizi hicho kituo cha afya kilichomzalisha wana kesi ya kujibu.

Manesi wengi walikuwa wakitukanwa ovyo na wagonjwa kiasi kamba anapandishwa hasira kwa kukosa uvumilivu na kuanza kujibizana. hii inatokea kwa serikali kukosa kupeleka vifaa kwa wakati, wananchi wanaambiwa dawa zipo, vifaa vya kujifungua vipo, wamama hawa wakienda wakavikosa, matusi kwa mane, wakikosa dawa matusi pia kwa manesi wakiambiwa wao ni wezi wakubwa wengine kutishiwa kuchapwa makofi hadharani...

Serikali chukueni hatua za kiuchunguzi kufuatilia mienendo ya manesi na wateja wao la sivyo atakuja kutokea maafa.makubwa kwani sasa hivi manesi hawaheshimiki ni watu wakunyanyaswa ovyo, daktari anamyanyasa nesi, mkuu wa mkoa ananyanyasa nesi, DED ananyanyasa Nesi. Chama chao cha kuwatetea masirai yao kimekuwa butu, hawana wa kuwasemea kwenye kazi zao, ni watu wa hofu muda wote.

Manesi ni watu wanafanya kazi mgumu na za hatari, magonjwa mbaya uwapata wakiwa kazini, lakini cha kushangaza ndio walio na masirahi kiduchu, angalau wakati wa awamu yanne walikumbukwa kidogo kwa kuongezea mishahara, sasa hivi baada ya serikali kutoa dawa bure wanafanya kazi ngumu wamezidiwa na wagonjwa wakati idadi yao ikiwa ndogo.
 
Yawezekana kuna visasi lakini nyie pia MNA mapozi, mnadharau wagonjwa, viburi na mnapenda rushwa, jitengenezieni taswira njema kwa jamii ili mkionewa tuwatetee.
Hapo sasa kama kila mtu atakuwa ngangali unafikiri watabaki wangapi?
 
Hii ya daktari kumnyanyasa nesi si kweli kabisa...daktari hawezi fanya kazi bila nesi...tatizo lililoko manesi wengi ni wajuaji na hujiona ni ma Dr...japo wako watiifu na waelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii ya daktari kumnyanyasa nesi si kweli kabisa...daktari hawezi fanya kazi bila nesi...tatizo lililoko manesi wengi ni wajuaji na hujiona ni ma Dr...japo wako watiifu na waelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijasema Nesi ananyanyaswa na DK, bali nimesema mgonjwa anaweza kumstaki nesi kwa daktari na dk akachukua hatua za haraka bila kufanya uchunguzi
 
mtu anakuja ghafla ana hali mbaya huku amebeba, kadi ya clinic yenye taarifa feki juu yake. utaacha kumzalisha kwanza kabla ya kuanza kumhudumia wakati akiwa yupo taabani hajielewi?
Tahadhari anazopewa mwenye maambukizi iwe ndio utaratibu wakuufuata kwa yeyote bila ya kujali ana maambukizi au la. La sivyo wakunga watakuwa wahanga.
Kutukanwa wavumilie,bila ikitokea kupigwa, nao wajitetee. Maneno (matusi) hayamtii mtu kilema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mtu anakuja ghafla ana hali mbaya huku amebeba, kadi ya clinic yenye taarifa feki juu yake. utaacha kumzalisha kwanza kabla ya kuanza kumhudumia wakati akiwa yupo taabani hajielewi?
Wewe una ufahamu mdogo sana wa PMTCT, PPE & IPC. I hope utakuwa sio mtu wa afya
Kwa upande wa kufoji taarifa kwenye RCH card No. 4 inawahusu wauguzi wenyewe. Hapa na maanisha wauguzi ndio wahusika wakuu wa clinic ya Mama, Baba na mtoto.
Wauguzi wasio na maadili ya kiuguzi ndio hujaza hizo taarifa zisizo sahihi kwa ndugu zao, marafiki zao, wao wenyewe au nawaliowapa rushwa ili kuficha ukweli wa hali ya maambukizi
 
nimesoma mada yako naona kama vile hali haiko hivyo kwenye field yenyewe......mtumishi wa afya kitu cha kwanza katika kazi yake popote pale akiwa kazini ni kuhakikisha anajua IPC kama inavyotakiwa.

Suala la mama mjamzito kufika na kedi yenye taarifa feki haimzuii muuguzi mkunga kushindwa kutoa huduma ya uzazi kwa kufuata SOP na hapo ni hasara kwa mama mjamzito wa kutojua umuhimu au faida za yeye kuwasilisha taarifa sahihi...hapo suala la elimu huko PMTCT,PITC na VCT kuhusu taarifa muhimu za HIV

Madaktari na wauguzi wanafanya kazi kwa pamoja na kila mmoja anamtegemea mwenenzake hivyo si rahisi kudharauliana kazini

Serikali inajitahidi kupeleka vifaa tiba na dawa na wewe mtumishi fanya kazi kulingana na uwezo wa kituo chako kutoa huduma na hutakiwi kulazimisha kufanya huduma ambazo kituo chako hakina uwezo nazo na hakuna vitendea kazi...jiongeze na ndiyo maana kuna rufaa.
 
Wewe una ufahamu mdogo sana wa PMTCT, PPE & IPC. I hope utakuwa sio mtu wa afya
Kwa upande wa kufoji taarifa kwenye RCH card No. 4 inawahusu wauguzi wenyewe. Hapa na maanisha wauguzi ndio wahusika wakuu wa clinic ya Mama, Baba na mtoto.
Wauguzi wasio na maadili ya kiuguzi ndio hujaza hizo taarifa zisizo sahihi kwa ndugu zao, marafiki zao, wao wenyewe au nawaliowapa rushwa ili kuficha ukweli wa hali ya maambukizi
Hizo tabia zipo na kuna ushahidi mwingi sana, kwetu kuna manesi wanakutana na kesi nyingi hasa wanapozalisha mtoto akapata ugonjwa kumbe mama yake alificha taarifa sahihi unakuta siku ya kujifungua anakimbizwa hospital nyingine, neda kibaha utakuta kesi nyingi na ndio UKIMWI umetamalaki sana Mkuu
 
Kwa nilichokishuhudia leba nilipokua mahututi nimeshindwa kujifungua kawaida, manesi hasa hawa wakike hawana ubinadamu kabisa
 
Manesi na walimu kwa sasa wote wacheza ngoma moja, poleni sana enyi watumishi wa umma mnaotoa Huduma muhimu kwa jamii lakini hamuheshimiwa hata chembe so serikaki si wateja wenu
 
Hizo tabia zipo na kuna ushahidi mwingi sana, kwetu kuna manesi wanakutana na kesi nyingi hasa wanapozalisha mtoto akapata ugonjwa kumbe mama yake alificha taarifa sahihi unakuta siku ya kujifungua anakimbizwa hospital nyingine, neda kibaha utakuta kesi nyingi na ndio UKIMWI umetamalaki sana Mkuu
"Ndio maana nasema huna uelewa wa PMTCT. Ni kwamba 90% ya wtt wenye maambukizi ya VVU wameambukizwa na mama zao.
Mama anaweza kumuambukiza mtt wake wakati wa ujauzito, wakati wa kujifungua au kipindi cha kunyonyesha(Kipindi hiki ndio cha hatari zaidi kama mama hata zingatia kikamilifu afua za PMTCT)
Kwasasa mama mjamzito anapogundulika kuwa na maambukizi basi huanzishiwa dawa(ART) ambazo atatumia maisha yake yote(PMTCT B+). Hii ni kwaajili ya afya yake na kinga kwa mtt wake
Toka program hii ya Option B+ ianze watoto wengi wanaozaliwa na hawa wamama wamekuwa salama.
Hii ni kwasababu mama akiwa mfuasi mzuri wa ART idadi ya VVU mwilini(Viral load) hupungua sana na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa chance ya kumuambukiza mtt wake.
Tatizo la wauguzi wa nyakati hizi hawazingatii mambo kama haya. Wamesahau maadili yao ya kazi nakufanya kazi kwa mazoea. Kazi wanafanya kwa kulipua na kibaya zaidi waliowengi hawa record hudima wanazo wapatia wateja wao.
Katika mazingira kama hayo kwanini usishtakiwe kwa uzembe? Keep documents, know your clients, adhere medical principles then you will fear nothing.
Hapo haonewi mtu. Nausije kufikiri kwamba kila mteja unaemhudumia ni mpumbavu. Wengine ndugu zao ni wa wauguzi/madaktari kama ninyi na hawa ndio wanao chochea mshtakiwe.
 
Back
Top Bottom