YAGHAMBA
JF-Expert Member
- Aug 8, 2012
- 545
- 147
Ndugu wanajamvi, salamu.
Kutetereka kwa hali ya amani ya nchi yetu Tanzania kunakotokana na tetesi za uwepo wa vikundi vya kigaidi vya siasa kali za kiislamu vinavyodaiwa kupanga kufanya mashambulizi kwenye makanisa mbalimbali wakati wa sikukuu ya pasaka, makanisa mbalimbali yamewatangazia waumini wao watakaohudhuria misa ya mkesha wa pasaka kuwa misa hizo zitaanza kati ya saa 11 jioni na saa 1 badala ya saa 3 usiku kama ilivyozoeleka miaka yote.
Kanisa katoliki jimbo kuu la Mwanza kupitia mahubiri ya jana jumapili limewaelekeza waumini wake walioko kwenye vigango kuanza misa saa 11 na wale wanaosali parokiani kuanza misa saa 12 ili kufikia saa 3 usiku shughuli ya ibada iwe imekamilka. Pia waumini wametakiwa kuchukua tahadhari kwa kitu au mtu yeyote wanayemtilia mashaka.
Vilevile waumini wa kikristo wametakiwa kufunga kwa siku saba na kuliombea taifa na kwamba silaha pekee ya mkristo awapo kwenye nyakati ngumu za mateso ya kiimani ni kufunga na maombi.MY TAKE; Serikali ya CCM inajisikiaje kwa haya yanayoendelea nchini?, nauliza hivyo kwa kutambua kuwa mbegu hizi za udini na ukabila zimepandwa na wanasiasa wake huku serikali hiyohiyo ikitoa vibali kwa wahubiri wa dini moja kuzunguka nchi nzima kueneza chuki dhidi ya ukristo na baba wa taifa Mwl.
Nyerere huku wakikishambulia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA. Nasema wahubiri hao walipewa kibali kwasababu polisi walikuwa wakilinda mihadhara iliyokuwa ikifanyika viwanja na kumbi za wazi. Miongoni mwa kauli zilizokuwa zikitolewa katika mihadhara hiyo ni hii; " KUFA KUPONA TUTAHAKIKISHA UKATOLIKI UNANG'OKA MIZIZI YAKE TANZANIA".
Ebu fikiria kauli kama hiyo inatolewa mbele ya polisi na usalama wa taifa ndani ukumbi wa Diamond Jubilee halafu watu hao wanaendelea kuzunguka mikoa mingine kueneza hayohayo, serikali haichukui hatua, maana yake ni kuwa tutaamini viongozi wakuu wa chama na serikali inayotawala wapo nyuma mpango wa wahubiri hao na wana baraka zote za mkuu wa nchi na vyombo vya ulinzi na usalama vina taarifa ya kutokuwachukulia hatua zozote wahusika.
Leo tumefika hapa kwa mbegu hizi zilizopandwa chini ya usimamizi wa watawala, na huenda hali ikawa mbaya zaidi kwani watawala hawaonekani kuchukua hatua stahili ingawa ni kweli kuwa hawawezi kuchukua hatua stahili kwa jambo waliloliunda kwa maslahi ambayo mpaka sasa nashindwa kuyatambua.
WITO; CCM na serikali chini ya Jakaya Kikwete, hili jambo mmeliasisi wenyewe kwa malengo mnayoyajua, mlitatue na mlimalize ili nchi yetu ibaki salama. Mungu ibariki Tanzania.
Kutetereka kwa hali ya amani ya nchi yetu Tanzania kunakotokana na tetesi za uwepo wa vikundi vya kigaidi vya siasa kali za kiislamu vinavyodaiwa kupanga kufanya mashambulizi kwenye makanisa mbalimbali wakati wa sikukuu ya pasaka, makanisa mbalimbali yamewatangazia waumini wao watakaohudhuria misa ya mkesha wa pasaka kuwa misa hizo zitaanza kati ya saa 11 jioni na saa 1 badala ya saa 3 usiku kama ilivyozoeleka miaka yote.
Kanisa katoliki jimbo kuu la Mwanza kupitia mahubiri ya jana jumapili limewaelekeza waumini wake walioko kwenye vigango kuanza misa saa 11 na wale wanaosali parokiani kuanza misa saa 12 ili kufikia saa 3 usiku shughuli ya ibada iwe imekamilka. Pia waumini wametakiwa kuchukua tahadhari kwa kitu au mtu yeyote wanayemtilia mashaka.
Vilevile waumini wa kikristo wametakiwa kufunga kwa siku saba na kuliombea taifa na kwamba silaha pekee ya mkristo awapo kwenye nyakati ngumu za mateso ya kiimani ni kufunga na maombi.MY TAKE; Serikali ya CCM inajisikiaje kwa haya yanayoendelea nchini?, nauliza hivyo kwa kutambua kuwa mbegu hizi za udini na ukabila zimepandwa na wanasiasa wake huku serikali hiyohiyo ikitoa vibali kwa wahubiri wa dini moja kuzunguka nchi nzima kueneza chuki dhidi ya ukristo na baba wa taifa Mwl.
Nyerere huku wakikishambulia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA. Nasema wahubiri hao walipewa kibali kwasababu polisi walikuwa wakilinda mihadhara iliyokuwa ikifanyika viwanja na kumbi za wazi. Miongoni mwa kauli zilizokuwa zikitolewa katika mihadhara hiyo ni hii; " KUFA KUPONA TUTAHAKIKISHA UKATOLIKI UNANG'OKA MIZIZI YAKE TANZANIA".
Ebu fikiria kauli kama hiyo inatolewa mbele ya polisi na usalama wa taifa ndani ukumbi wa Diamond Jubilee halafu watu hao wanaendelea kuzunguka mikoa mingine kueneza hayohayo, serikali haichukui hatua, maana yake ni kuwa tutaamini viongozi wakuu wa chama na serikali inayotawala wapo nyuma mpango wa wahubiri hao na wana baraka zote za mkuu wa nchi na vyombo vya ulinzi na usalama vina taarifa ya kutokuwachukulia hatua zozote wahusika.
Leo tumefika hapa kwa mbegu hizi zilizopandwa chini ya usimamizi wa watawala, na huenda hali ikawa mbaya zaidi kwani watawala hawaonekani kuchukua hatua stahili ingawa ni kweli kuwa hawawezi kuchukua hatua stahili kwa jambo waliloliunda kwa maslahi ambayo mpaka sasa nashindwa kuyatambua.
WITO; CCM na serikali chini ya Jakaya Kikwete, hili jambo mmeliasisi wenyewe kwa malengo mnayoyajua, mlitatue na mlimalize ili nchi yetu ibaki salama. Mungu ibariki Tanzania.